Hotuba za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Hotuba za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Kauli ya Mwalimu Nyerere Kuhusu Lowassa: NEC
Dodoma 1995
"Hapa hatuchagui mtu maarufu, tunachagua mtu
safi na huyu si safi. Kama unapenda sura yake
basi nenda kanywe naye chai. Wengine mnasema
aaah ni tuhuma tu. Samuel (Sitta)! Yusuf
(Makamba)! Mnasimama hapa mnasema ni
tuhuma tuhuma tu! Lakini mtakumbuka mke wa
Kaisari alipotuhumiwa kwa ugoni Kaisari akaagiza
uchunguzi ufanyike. Uchunguzi ukafanyika na
ikabainika kwamba sio kweli. Lakini Kaisari bado
akamuacha, akasema mke wa Kaisari hapaswi
hata kutuhumiwa. Na sisi hapa Mgombea wetu
hapaswi hata kutuhumiwa wakati wapo wengine
safi ambao hawana tuhuma. Kama mkimteua
huyo mimi sitapiga kampeni. Siko tayari
kumsafisha mtu matope halafu ndio nimuombee
kura. Hapana kabisa. Huyu mimi najua si msafi
na nchi nzima inajua si msafi. Hafai kuwa
mgombea wetu." - Mwl. Julius Nyerere, NEC
Dodoma, Juni 1995
MYTAKE
JE TUNA MUASISI MWL NYERERE AU TUNAMPINGA? THINK CRICTICALLY.[/QUOTEmwl,Hivi kumbe kwa ccm kumuenzi mwalimu ni kumkataa lowasa?kuyauza mashirika ya umma,kuwauwa tembo,kuiba kupitia escrow,epa,meremeta,na kuingiza madawa ya kulevya havihusiani na kumuenzi mwalimu nyerere?wacha kujiaibisha na kutumia vibaya jina la mwl,leo hii ccm mnarithishana vyeo kwa watoto wenu na familia zenu mbona nyerere hakuwahi kufanya hayo mambo?
 
Ma ccm mtahangaika sana mwaka huu,ila ukweli unabakia pale pale kuwa lowasa ndiye RAIS WA JMT,baada ya november 2015.
 
Mwaka huu mtateseka sana. Lakini imani tulokua nayo juu yake.... Sidhani kama mtaweza kutuondolea kwa majungu yenu.

Cha msingi fanyeni yenu na sisi tubaki na mtu wetu. Mwisho wa siku kura zitaamua.
 
Kauli ya Mwalimu Nyerere Kuhusu Lowassa: NEC
Dodoma 1995
"Hapa hatuchagui mtu maarufu, tunachagua mtu
safi na huyu si safi. Kama unapenda sura yake
basi nenda kanywe naye chai. Wengine mnasema
aaah ni tuhuma tu. Samuel (Sitta)! Yusuf
(Makamba)! Mnasimama hapa mnasema ni
tuhuma tuhuma tu! Lakini mtakumbuka mke wa
Kaisari alipotuhumiwa kwa ugoni Kaisari akaagiza
uchunguzi ufanyike. Uchunguzi ukafanyika na
ikabainika kwamba sio kweli. Lakini Kaisari bado
akamuacha, akasema mke wa Kaisari hapaswi
hata kutuhumiwa. Na sisi hapa Mgombea wetu
hapaswi hata kutuhumiwa wakati wapo wengine
safi ambao hawana tuhuma. Kama mkimteua
huyo mimi sitapiga kampeni. Siko tayari
kumsafisha mtu matope halafu ndio nimuombee
kura. Hapana kabisa. Huyu mimi najua si msafi
na nchi nzima inajua si msafi. Hafai kuwa
mgombea wetu." - Mwl. Julius Nyerere, NEC
Dodoma, Juni 1995
MYTAKE
JE TUNA MUASISI MWL NYERERE AU TUNAMPINGA? THINK CRICTICALLY.

mmmh haipo hiyo lowassa ndio rais wetu
 
Mwalimu hakuwa mungu kwamba kila alilosema halibadiliki, alikuwa na utwshi wa binadamu wa kawaida akimpenda au kutompenda mtu kwa sababu za kibinadamu ndo maana hata alie mpendekeza ktk awamu ya tatu tunajua alichotufanyia.
 
Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni"
***********************


'Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa mawazo, ni umaskini mbaya sana' 01/5/1995

***********************


'Mtu mwenye akili akikuambia neno la kipumbavu -ukalikubali, anakudharau!' 01/5/1995

***********************


“Siku inakuja ambapo watu watachagua kifo kuliko fedheha na ole wao wale watakoiona siku hiyo! Na ole wao wale watakaoifanya siku hiyo isiepukike. Natumaini na kusali kuwa siku hiyo kamwe haitofika” –MwalimuNyerere (Januari, 1966)

***********************


"Rushwa ni adui wa haki. Tunamtaka rais ambaye atalitambua hilo na ataichukia rushwa hata ukimuangalia anaonyesha kweli anaiichukia rushwa, sio rais ambaye anayesema kweli rushwa ni adui wa haki....lakini ukimuangalia usoni unashangaa na kusema.... aaaah kweli huyu?

***********************


"Poverty is not the real problem of the modern world. For we have the knowledge and resources which could enable us to overcome poverty. The real problem--the thing which causes misery, wars, and hatred among men--is the division of mankind into rich and poor."

***********************


Not So Sure kama kweli alisema haya na wapi…. lakini inasemekana Source inapatikana kwenye hiki kitabu
Reflections On Leadership in Africa' VUB University Press, 2000.

Amini nawaambieni enyi Waswahili wachache mnaotawala; mnategemea kweli kuwa mtawaongoza Watanzania kwa lazima wakati wamepoteza matumaini, na mtegemee kuwa watasalia wamekaa kimya kwa amani na utulivu?

***********************

Amani ni zao la matumaini, pindi matumaini yatakapotoweka kutakuwa na vurugu katika jamii.

***********************

Wakati wengi wa wananchi wanapopoteza matumaini unajenga volcano. Volcano hii italipuka siku moja. Labda kama watu hawa ni wajinga.

***********************


Kukubali kukandamizwa namna hiyo wakati wanayo nguvu inayotokana na wingi wao, ni kwa sababu ni wajinga tu.

***********************


Hivyo basi Watanzania watakuwa ni wajinga na mataahira, kama watakubali kuendelea kukandamizwa na watu wachache (viongozi) katika nchi yao wenyewe....

***********************


Na hakutakuwa na watu wa kizazi hiki na karne hii ambao watatakiwa kujitoa muhanga kwa ajili ya maisha bora katika siku zijazo wakakubali, wakati wanawaona watu wachache wakiendelea kuneemeka machoni pao bila kujali wakati ujao, wakati wao (wananchi) na watoto wao wakiendelea kuishi katika maisha duni na dhalili.

***********************
Tafadhali Ongeza na za Kwako!!

 
Tumenyanyaswa kiasi cha kutosha,tumedharauliwa kiasi cha kutosha,tumepumbazwa kiasi cha kutosha,ni ujinga wetu uliotufikisha hapa na kutupitisha kwenye yoote hayo.
Sasa tunasema baaaaaaaasi"
 
Mkuu ukipata zingine rusha, asante sana.
Hotuba ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere mara tu baada ya kuwa Waziri Mkuu kufuatia ushindi wa TANU ambao ulikipa ridhaa chama hicho kuunda Baraza la Kwanza la Mawaziri wa Serikali ya Tanganyika mwaka 1961.

HOTUBA YA KWANZA YA MWALIMU NYERERE



Gazeti-Mtanzania; Ijumaa Oktoba 14, 2005.
 
Huyu alikuwa binadamu tu ndo maana alimpgania mkapa ambaye ndiye huyo aliyeuza viwanda na kuua mashirika ya serikali;
na huyo huyo anatuhumiwa kumrestisha in peace

TUMSIKILIZE VP TENA?Kuna ya kusikilza na mengne unaongeza zako
 
KAULI YA Mwalimu Nyerere Kuhusu Mgombea mchafu!
NEC Dodoma 1995..
Hapa hatuchagui mtu maarufu, tunachagua mtu
safi na huyu siyo msafi. Kama unapenda sura yake
basi nenda kanywe nae chai.
Wengine wanasem aah ni tuhuma tu..
Samuel { SITA } Yussuf {Makamba }! Mnasimama
hapa mnasema ni tuhuma tu.!
Lakini mtakumbuka mke wa Kaisar mke wa
Kaisari alipotuhumiwa kwa ugoni, Kaisari akaagiza
uchunguzi ufanyike.
Uchunguzi ukafanyika na ikabainika siyo kweli.
Lakini Kaisari bado akamuacha mkewe, akasema
mke wa Kaisari hapaswi hata kutuhumiwa...
Nasisi hapa wetu hapaswi hata kutuhumiwa.g
Wakati safi ambao hawana
tuhuma.. Kama mkiteua huyo mimi sitapiga
kampeni. Siko tayari kumsafisha mtu matope halafu
ndiyo nimuombee kura.. Hapana kabisa.
Huyu mimi najua si msafi na nchi nzima inajua si
msafi. Hafai kuwa mgombea wetu..
Mwlm Julius Nyerere.
NEC Dodoma Juni 1995..
 
Kwasababu ya uchafu wake hata Kubenea ndiyo maana alidiriki kuandika kuwa hasafishiki. Nami namalizia, hafai kuwa raisi.
 
Hafai kuwa kiongzi wa taifa hili amekuwa mtu msahaulifu mpaka wa maneno yake mwwnyewe asitudanganye wananchi
 
kwa style hiyo hata magufuli hatufai maana ana tuhuma nyingi na haijajibiwa hata moja
 
Back
Top Bottom