Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Let's hope MISS MUMBAI 2008 atakuwa Kokushubirwa Somebody kutoka Haneti, Kondoa!
 
wewe ndio umetumia neno wazawa.. so wewe ulidefine! ili nijue unazungumzia nini. Mmetoka kwenye rangi, mnaenda kwenye kupachikwa... si mseme tu hakuzaliwa TAnzania tujue! na wazazi wake siyo raia!

Bubu, hujaniambia Richa amekosea nini? WEwe umeng'ang'ania wahindi hivi wahindi vile.. je we unaendaga kwenye misiba yao!? Unaendaga kwenye harusi zao? HIvi kuna mtu humu ambaye anarafiki wa kihindi na aliwaalika kwenye harusi au sherehe fulani na hawakutokea?

- akina nani hao waliotoka kwenye rangi kwenda kwenye kupachikwa ? i stand by myself, for myself katika hoja zooote !

- still having a hard time understanding unajaribu kuniweka mie na watu wa kundi gani sijui

- Na kama wewe MWANAKIJIJI unadhani wahindi wanapaswa kupewa nafasi za taifa pale tanzania, basi kuanzia leo ufunge mdomo wako na mikono yako kutoandika chochote sijui RA, sijui Manji sijui nani !

kama umeshindwa kutafuta maana ya hilo neno, kalime kijiji kama jina lako linavyoelewa, lol !
 
Tena mmenikumbusha, kulikuwa na mwalimu fulani Mwanza alikuwa anaitwa Mwalimu Mbiti, mweusi, (watu wa Mlimani, Bugando/Pamba primary wanaweza kumjua), yeye mbona alioa mhindi?

mmh! mbona wengi tu. hebu nendeni pale kariakoo junction ya mtaa livingstone na narung'ombe kuna mchaga kamchanganya mtoto wa kihindi mpaka kahama kwao!

nakubaliana kuwa waTZ wenye asili ya afrika hatujui kusomesha style ya kuwafanya wadosi waingie!
 
Na kama wewe MWANAKIJIJI unadhani wahindi wanapaswa kupewa nafasi za taifa pale tanzania, basi kuanzia leo ufunge mdomo wako na mikono yako kutoandika chochote sijui RA, sijui Manji sijui nani!

Kada mbona havina uhusiano??

Anyway Mwnakjj nakupa tano, sioni tofauti sana kati yako na watu kama martin L King, Mz madiba, mahatma gandh na Mwalimu JK.
 
kiingereza,kifaransa nk isiwe kigezo hata kidogo cha ushindi.ufahamu wa mtu ndio unaotakiwa.tena huyo richa angefanya la maana zaidi huko aendako akajibu maswali yote kwa lugha yetu ya taifa ili awakilishe zaidi utanzania wake.
 
Nasikitika kwamba mijadala ambayo inahitaji uchambuzi wa kina tunaijadili kwa mitizamo ya ki layman mno.Mada hii imeanzia kwenye makala ya mwanakijiji, ukiisoma vizuri mbali ya kuwa alilenga kujadili suala la Ms tz, kajenga hoja kwa mifano mingi ambayo kimsingi ina rise maswali magumu kuliko majibu.Nina hakika hata yeye kuna mambo mle ukimstukiza hawezi kukujibu kwa haraka. We need to think beyond the horizon, suala la uyu dada halina ubishi ni mtanzania na ana haki zote za kutuwakilisha. Tunaweza lakini kwenda mbali ya hapo na kujadili mambo mapana zaidi kuhusu ili suala nje kabisa ya huyu dada. kwa kizungu naweza sema 'we take the topic in broad context and discuss it objectively'' si suala la ubaguzi kabisa hilo ila kujielimisha zaidi, mimi napenda kutumia msemo wa 'think big' Msinifanye niamini JF ni mahala pa 'kupiga soga tu'(quote from http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=66652#post66652) au kutafute easy answers to hard questions,we can do more than that wazee.

Its sad to see members reducing/lowering JF to the status of a chat room.It leaves me wondering at times what are all the intelligent people doing arguing with fools.Its a thankless job trying to educate those who are so narrow minded and shortsighted that they cant see beyond their noses.
Somebody with the rules and conditions for paticipants in this Miss Tz kindly post them here so we can figureout whether Richa ( Rachael )qualified to take part and more importantly WIN.
Had the award been a bicycle I dont think the question of her origin or colour would be a matter for discussion/argument today,I can assure you.
 
Mimi nilivyoelewa ni kwamba hawa ndugu zetu wanapitia njia nyingi ili kuweza kuonesha ubora wao katika mwafrika na kuonesha kwamba kwa kusoma katika shule za maana, kuandaliwa kwa mbinu mbalimbali na mengine, bado wataendelea kutumia mgongo wa mtanzania asilia kufanikiwa katika mambo yao.

Hili suala ni zito na linahitaji uchambuzi yakinifu kama alivyoainisha bwana Mjengwa.

Kwa kuongezea ni kwamba ni lazima kuanzishwe vijikampuni vingine vya kushindanisha mabinti na bwana Lundenga ili tuweka ushindani katika sekta hii inayoonekana ina ulaji.

Wizara husika pia iwe inatumia macho mambo kama haya yanoyogusa jamii kubwa ya watanzania ambayo ni vijana.

Pia nafikiri huyu dada alikuwa ashinde ndio maana amepoozwa kwa zawadi ingine angalau kutua roho.

Mambo Bongo ni mazito!
 
Hili suala la Richa, uhindi na utanzania limezushwa na watu ima kwa makusudi au kwa kutojua, kuelezea mawazo yao kuhusu fani fulani kabla au bila ya kufanya utafiti kuhusiana na fani husika. Naamini watu walipaswa kuuliza au kuulizana kuhusu vigezo, sheria na mazingira yahusuyo masuala ya ulimbwende na kanuni za msingi zitumiwazo na kamati inayohusika na maandalizi ya hayo mashindano.
Ni vema kujichunga na maoni ambayo hatimaye tutatamani kuyameza! Tujadili jambo hili kwa misingi ya utamaduni uliotawala mwenendo mzima wa Miss Tz na maana na maslahi yake kwa jamii na taifa. Tujitahidi kuepuka ufinyu wa fikra na kujongeza zaidi hoja zenye upana wa maoni na kina cha hekima.
Asanteni!
 
Juzi juzi tu tulikuwa na msiba wa dada yetu Amina Chifupa, pamoja na kuwa alikuwa na umaarufu mkubwa lakini hao 'dada zako na kaka zako' hatukuwaona kwenye msiba huo hilo wewe hulioni. Angalieni vizuri mjue ni nani mbaguzi!

Huyu Shyrose Banji utamiita naani ?? Get a life man.
 
Kwenye hili mstari umechorwa, na pande mbili ziko dhahiri. Kuna wale ambao wamekubali na wanatetea ubaguzi wa rangi Tanzania kwa kisingizio chochote kile na wale ambao wanatetea usawa, uhuru, na nafasi sawa kwa kila Mtanzania bila kudali rangi, dini, nasaba, au mahali au asili ya Utaifa. Katika pande hizi mbili wapo wale wanaotaka kumhukumu Richa kwa rangi na asili yake na si kwa LOLOTE ambalo yeye alifanya au ametuhumiwa kufanya. Hakuna ambaye amekuwa na ujasiri wa kusema Richa amefanya hiki au kile ambacho kinamfamfanya asistahili kuwa Miss Tanzania. Tatizo ni kile ambacho hana uwezo nacho! Ni bora tuwe na Miss Tanzania ambaye amejitahidi kufikia pale kuliko kupewa Miss Tanzania ati kwa vile ni mweusi tu! Wabaguzi endeleeni kubagua, na sisi tutaendelea kuwaonesha kuwa ninyi ni wabaguzi, hakuna cha uzalendo wala utaifa mnaotetea!
 
Mimi nilivyoelewa ni kwamba hawa ndugu zetu wanapitia njia nyingi ili kuweza kuonesha ubora wao katika mwafrika na kuonesha kwamba kwa kusoma katika shule za maana, kuandaliwa kwa mbinu mbalimbali na mengine, bado wataendelea kutumia mgongo wa mtanzania asilia kufanikiwa katika mambo yao.

Richa amefanya yapi kati ya hayo? Na hawa Watanzania Asilia ni wapi?

Kama nilivyomuuliza mtu mwingine hapo juu niwaulize hivi Mtanzania Asilia = Mtanzania Mzawa?

Hili suala ni zito na linahitaji uchambuzi yakinifu kama alivyoainisha bwana Mjengwa.

Kwa kuongezea ni kwamba ni lazima kuanzishwe vijikampuni vingine vya kushindanisha mabinti na bwana Lundenga ili tuweka ushindani katika sekta hii inayoonekana ina ulaji.

Wizara husika pia iwe inatumia macho mambo kama haya yanoyogusa jamii kubwa ya watanzania ambayo ni vijana.

Pia nafikiri huyu dada alikuwa ashinde ndio maana amepoozwa kwa zawadi ingine angalau kutua roho.

Mambo Bongo ni mazito!

hizi zote ni Bla Bla Bla... Miye nashauri huyu Binti ajiuzulu ili wampe mtu mweusi!
 
Mie nimeuliza huko nyuma, kwamba sawa tunasema mtanzania tuache ubaguzi, je itakuwa sawa RA akiwa raisi wa awamu ya tano Bongo?
 
Rwabugiri, Katiba ya Tanzania inatoa sifa za nani anaweza kuwa Rais, je Rostam anatimiza sifa hizo? Kama hatimizi basi hawezi na hastahili kuwa Rais, kama anatimiza why not?
 
Rwabugiri, Katiba ya Tanzania inatoa sifa za nani anaweza kuwa Rais, je Rostam anatimiza sifa hizo? Kama hatimizi basi hawezi na hastahili kuwa Rais, kama anatimiza why not?

Kweli kama umeiva kiasi hicho nakupongeza sana. kwa upande wangu siku RA akiwa raisi wetu wa awamu ya tano, Alkaeda watakuwa wamepata new member 'I' kwikwikwi..
 
ubaguzi ni silka na hulka ya binadam yeyote yule. Awe mzungu, muhindi, mchina etc. Hata kama Miss tanzania angetoka Kilimanjaro, bado watu wangelalamika...mbona kilimanjaro ndio inatoa ma-miss tu? upo hapo??
 
Its sad to see members reducing/lowering JF to the status of a chat room.It leaves me wondering at times what are all the intelligent people doing arguing with fools.Its a thankless job trying to educate those who are so narrow minded and shortsighted that they cant see beyond their noses.
Somebody with the rules and conditions for paticipants in this Miss Tz kindly post them here so we can figureout whether Richa ( Rachael )qualified to take part and more importantly WIN.
Had the award been a bicycle I dont think the question of her origin or colour would be a matter for discussion/argument today,I can assure you.
naona sasa ubinadamu wako ndio umekamilika, manake bila kutumia hiyo lugha wewe bado ni nusu mtu..........
 
Richa amefanya yapi kati ya hayo? Na hawa Watanzania Asilia ni wapi?

Kama nilivyomuuliza mtu mwingine hapo juu niwaulize hivi Mtanzania Asilia = Mtanzania Mzawa?



hizi zote ni Bla Bla Bla... Miye nashauri huyu Binti ajiuzulu ili wampe mtu mweusi!

Mheshimiwa mwanakijiji,

Mimi nafahamu unaelewa tofauti ya mtanzania asilia na yule mzawa.

Richa ni mtanzania mwenye asili ya Asia lakini kazaliwa Tanzania(uki-trace babu zake wako Asia) na mwingine anajulikana bila ubishi ni mtanzania wa kuzaliwa na kwa asili (uki-trace babu zake asili ni Tanzania).

Maswali ni yale yale mawili aliyobainisha ndugu Mjengwa nafikiri umesoma maoni yake.

Kwa nilivyosoma taarifa mbalimbali kuhusu jambo hili,nimeona kulikuwa na majaji watanzania pamoja na majaji watanzania wenye asili ya Asia akiwemo mwenyekiti wa majaji Agbani Darego na wenzie mratibu Rameshi Shah na jaji mwingine Prashanti Patel.

Mimi pi nawafahamu hawa wenzetu nimeishi nao na kufanya kazi nao kila siku huku majuu katika miji yao mbalimbali kama Leicester na Birmingham na hata wewe unawafahamu huko uliko, hio haiitaji kueleza saana.

Pia kama hujui ni kwamba hawa wenzetu wengi "waliwahi" kuja majuu kwa kutumia pasi ya Tanzania huko nyuma na leo ndio wamerudi au wanarudi Tanzania wakiwa na makampuni yote unayoyaona hapo Bongoland. Na wanafanya biashara zote ambazo wewe unaota kuzifanya.

Hawa ndugu zetu umeeleza mwenyewe hapo kabla kuhusu mahusiano yao na sisi kama watanzania waafrika.

Hawa watu ni wabaguzi namba moja mkubwa wangu mwanakijiji, na sasa wametumia nafasi hii kwa sababu ambazo wanazijua wao na wewe hutazijua.

Sasa nini cha kufanya?

1. Akina Jacline Ntuyabaliwe ambae nae alikuwa ni jaji ni lazima waende benki na "business plan" ya kuanzisha kampuni yao ya "events management and entertainment" kama hizi badala ya kumtegemea au kudandia kwa Lundenga na kupata hela ya kula ugali tu.

2. Kwa kuwa fani hii imeingiliwa na wasanii wengi tu wakiwemo hawa "wenzetu" basi serikali kupitia mzee Bendera waweke "tight regulations" kwenye kampuni hizi zilizopo (kama inawezekana) ili mshindi apatikane kwa haki na watu wote waridhike.

3. Fani hii ya Miss Tanzania kwa sasa inaonekana inaingiza mheshimiwa mwanakijiji, kwa hio ndio hivo tena!

Mimi nimeishia hapa naomba kutoa hoja.
 
Huyu Shyrose Banji utamiita naani ?? Get a life man.

Yaani kundi la wahindi waliopo Tanzania kuja huyo mhindi mmoja basi umeshaona wanashiriki kwenye misiba yetu! Hivi kuna msiba gani mwingine wa mmatumbi aliohudhuria usiokuwa wa mkubwa? I have a life and a good life for that matter. Please watch your language we can debate all day and all night long but I am not ready to be intimidated by you. If you want to go there, I am ready for you.
 
Kwenye hili mstari umechorwa, na pande mbili ziko dhahiri. Kuna wale ambao wamekubali na wanatetea ubaguzi wa rangi Tanzania kwa kisingizio chochote kile na wale ambao wanatetea usawa, uhuru, na nafasi sawa kwa kila Mtanzania bila kudali rangi, dini, nasaba, au mahali au asili ya Utaifa. Katika pande hizi mbili wapo wale wanaotaka kumhukumu Richa kwa rangi na asili yake na si kwa LOLOTE ambalo yeye alifanya au ametuhumiwa kufanya. Hakuna ambaye amekuwa na ujasiri wa kusema Richa amefanya hiki au kile ambacho kinamfamfanya asistahili kuwa Miss Tanzania. Tatizo ni kile ambacho hana uwezo nacho! Ni bora tuwe na Miss Tanzania ambaye amejitahidi kufikia pale kuliko kupewa Miss Tanzania ati kwa vile ni mweusi tu! Wabaguzi endeleeni kubagua, na sisi tutaendelea kuwaonesha kuwa ninyi ni wabaguzi, hakuna cha uzalendo wala utaifa mnaotetea!

Ha ha ha Wabaguzi sisi kwa kusema jamo kama tunavyoliona. Kwamba pamoja na wahindi kuzaliwa Tanzania na kuishi miaka mingi wengi wao hawaoni umuhimu wa kukijua kiswahili maana kwao wao ni lugha ya washenzi. Pamoja na kuishi Tanzania miaka chungu nzima bado wanajitenga katika maeneo maalum 'uhindini' na kamwe hawataki kujichanganya na sisi washenzi, pamoja na kuishi Tanzania miaka chungu nzima bado wanajiona wao ni bora kuliko sisi na hawako tayari kwa intermarriages kati yao na wamatumbi washenzi! lakini hili la huyo mhindi kutokuwa na sifa zozote za kupewa Umiss India...Ooops! Miss Tanzania na watu kusema ukweli wanavyoona wewe unaona ni ubaguzi! Mwe! Kazi kweli kweli na safari bado ni ndefu sana!

Pia unataka walioshiriki wamsupport huyo mhindi, kwa nini hasa alichokifanya hata wamsupport? kwa kupewa ushindi ambao washiriki wote wanajua hakustahili!? Hao wahindi lini walisimama na kuwasupport Miss Tanzania wa miaka ya nyuma? au kwa kuwa wao ni bora kuliko sisi hivyo hawana haja ya kufanya hivyo!? Acha hizo!
 
asalamu alaykum.

mjadala wa miss tanzania ni mtamu sana lakini hakuna haja ya kumuonea Richa kutokana na maksoa ya jamii yake ni kweli wazazi wa kihindi miaka ya nyuma walikuwa wabaguzi lakini sasa wanaonekana kubadilika kidogo kidogo na kama hamuamini hivyo kujitokeza Richa na kuungana na wenzake kambini na kufika hadi kushiriki basi ni sababu moja tosha ya kuwa wahindi sasa wanabadilika na ndio maana wanashiriki katika mambo kadhaa hapa tanzania ikiwemo masuala ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

kwa hapa visiwani zanzibar hatuna tatizo kubwa sana la kubaguana na watoto wa kihindi wanakaa pamoja sana na watoto wa kiswahili na hata suala la ndoa ziko nyingi sana ambazo nyengine ni watu mashuhuri. mfano mmoja mfanyabiashara mashuhuri ambaye ni ndugu yake mohammed raza anaitwa naushad ameowa mswahili tena mswahili hasa sio wa mjini wa shamba kabisa tena miaka mingi tu na anaye hadi leo. mwengine mfanyabishara maafuru Salum Turky mkewe mswahili, Bombay Bazaar mkewe mswahili, Ismail Jussa mama yake amewahi kuolewa na kuishi miaka mingi sana na Ali Haji Pandu ambaye ni mmakunduchi hao niliowataja ni watu wazima na wengine wameshajukuu, mwengine mwandishi wa ITV Farouk Karim ameowa mswahili wa makunduchi, mwengine Ibrahim Sanya mbunge wa mji mkongwe naye ameowa mweusi na wengi tu. na hata kushirikiana kwenye misiba, sherehe za harusi nk watu wanashirikiana kisawasawa hakuna tatizo kubwa sana. kwa hivyo haya mambo yalikuwepo zamani sana na kila siku yanabadilika kidogo kidogo watanzania walipaswa kumpa moyo Richa na kumpongeza kushiriki kwake na kuchanganyika na waswahili na sio kusema yeye ni mhindi ikiwa mhindi so what? tatizo ni wivu tu unakawabili hawa watoto. hakuna lolote. kwanza huyo Hoyce alisema mhindi then amebadilisha maneno amesema yeye hasemi hafai Richa kutokana na uhindi wake eti hana sifa, Hoyce anataka sifa gani? abandike nywele za bandia kama wao ndio atafaa? na ndio atakuwa ana vigezo? nafuu zanzibar yalivyopigwa marufuku yaho mashindano maana naona hayana mpango wowote.
 
Back
Top Bottom