Huduma mbovu za Mtandao wa TTCL: Malalamiko ya wananchi

Huduma mbovu za Mtandao wa TTCL: Malalamiko ya wananchi

Sio siri ngoja niende kwenya mada moja kwa moja.

Huu mtandao una matatizo mengi sana kama yafuatayo:

1. Huduma ya T PESA
Aisee huu mtandao kama utatuma hela siku ya Ijumaa usiku ghafla litokee tatizo wallah utakuja kuhudumiwa siku ya Jumatatu.

Hili tatuzo limenipata juzi hapa Ijumaa tarehe 7 yaani nilitamani kulia wallah.

2. Vifurushi
Hawa majamaa ukitaka uende nao sawa kwenye masuala ya MBs nakushauri tafuta kitambulisho cha chuo.

Aisee yaani GB 5 kwa Tsh 5000 mwezi mzima.

3. Vocha
Asikwambie mtu, TTCL hawana vocha aisee. Jana nimeenda pale Makao Makuu niliulizia vocha ya 500 hakuna wanasema zipo za 1,000.

Aisee ukienda kuulizia madukani yaani muuzaji anaweza akashangaa maana hiyo vocha ya TTCL ndiyo kwanza anaisikia kwako.

Kilichonipata jana
Nilijiapiza nikaonane na Afisa Masoko pale Makao Makuu pale Posta ili nimshauri kitu kimoja tu. Yaani nikafika mapokezi nikaonana na mama ana sura ngumu.

Yule mama wa mapokezi aliongea sana mpaka wakati naondoka nikamtukana kwa sauti ya chini. Maana shida yangu nilitaka kuonana na Afisa Masoko au CEO wao.

Nilichotaka kumwambia afisa masoko
Nilitaka nimwambie kama vocha mtaani ni ngumu basi katika option ya kununua bando mteja achague alipe upitia T PESA au salio la kawaida.
mgTeam.png
 
Huku ndo rudi nyumbani kumenoga!

Hebu imagine nakaa katikati ya mjini centre napata mateso sana na huu mtandao.

Ushauri wa bure kama wewe ni mtu ambaye unafanya mishe zako mtandao au majukumu mbalimbali ambayo yanaitaji mtandao au unahitajika kila muda fulani uwe mtandaoni kwa muda muafaka usitumie TTCL.

Mtandao wao umekuwa wa ajabu sana unarudi na kupotea.

Kibaya ni kuna siku unaamka unakuta inasoma E tu na 3G yenye x hapo hata text za Whatsapp haziendi.

Tatizo limekuwa sugu na linajirudia kila siku yaani inamlazimu mtu kuwa na bando la ziada la mtandao mwengine maana wao hawaaminiki saa yoyote wanapotea na kuzingua mpaka masaa 6.

Customer care yao ndo jangaa unasubiri simu dakika 45 ndo wanapokea wanaboa kinyama.

Nimepata hasara sana kazi nyingi zinakuwa pending mtandaoni mtu anasema nafanya kusudi.

Wewe fikiria ndo nimejiunga bando la buku 5 kwa week halafu kutokana na mtandao wao kupotea potea nalazimika kuwa na bando jingine la mtandao mwingine ila wakipotea nitumie huko.

Hili ni bando la mwisho nikimaliza natupa line yao chooni hawana tofauti na continental decoder king'amuzi HD lakini no signal kila saa.

Screenshot_20200215-001603.jpeg
Screenshot_20200215-001638.jpeg
Screenshot_20200215-001648.jpeg
Screenshot_20200215-001704.jpeg
Screenshot_20200215-001726.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simu ina gb 8 ram itakuwa 1:mkuu tatizo ni simu sio TTCL Kwa storage hiyo lazma ije E . ...MAPS GO....GOOGLE GO ogopa hizo simu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom