Uchaguzi 2020 Huenda CCM na Dkt. Magufuli hawakujiandaa kwa upinzani huu

Uchaguzi 2020 Huenda CCM na Dkt. Magufuli hawakujiandaa kwa upinzani huu

Kitu pekee ninacho kipenda CCM wana mikakati ya kudumu na endelevu.

Mfano: kabla hata rais kutoka madarakani huwa kuna kijana anaandaliwa zaidi ya miaka mitano a kuwa mgombea wa urais miaka ijayo.
Na hii ndio hufanya CCM kuwa stable kila Mwaka.

Lakini hili kimbilio la wapotevu "CHADEMA" hawajawahi kuwa na long plan yeyote ili kusaidia chama chao.
Bali wao hujikuta tu anayetaka kuwa mgombea wao wa urais anajichagua tu kama mnaada vile.

Angali mh. Lowassa katoka zake CCM kaenda mnadani CHADEMA akasema nataka kuwa rais WAKAMKUBALIA..akakosa urais akaamua kusepa zake "Wakabaki midomo wazi" hahaha 😂
Maghufuli naye aliandaliwa? Unaandika kitu usichokijua
 
Wanajamvi Salam,

Zikiwa zimebaki siku kumi na nne (14) tu kwenda kushuhudia historia ikiandikwa Tanzania, kwa ama wananchi kuendelea kuchagua ccm ambayo kiukweli imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili watanzania walio wengi au wananchi kwenda kuchagua Uhuru Haki na Maendeleo yao kwa kufanya mabadiliko ya uongozi hasa katika nafasi nyeti ya uraisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

Kampeni za vyama vyote shindani zinaendelea na huku wadadisi na wachambuzi wa kisiasa wakipima upepo wa kisiasa hasa kwa kuangalia Sera za vyama vyote na idadi ya watu wanaohudhuria katika mikutano ya kampeni kwa vyama tofauti. Hali imekuwa si shwari kwa chama tawala, imekuwa kana kwamba wanapumulia mashine. Kampeni zao zimekuwa zikiratibiwa kwa kiasi kikubwa nje ya chama, hapa nikimaanisha kwa kutumia vyombo vya Dora pamoja na wasanii. Huku upande wa chama kikuu Cha upinzani CHADEMA Mambo ni bul bul. Hali hii imekuja baada ya ccm kukosea hapa

1. Wamefanya siasa kwa miaka mitano peke yao, hivyo ni Kama vile wananchi wamewachoka, wananchi wanataka kusikia mawazo mapya. Wanataka kusikia kile ambacho walikuwa wanafichwa kuambiwa kwa miaka mitano huku ccm wakisema peke yao. Ndiyo maana unaona kwenye mikutano ya chama kikuu Cha upinzani wananchi wanajazana pasi na aina yoyote ya ushawishi wa wasanii. Kwenye hili ccm imewakinaisha wananchi hivyo wanataka mawazo mapya.

2. Kizazi kilichokuwa ccm kufa na kuzikana kinazidi kuisha. Wale wazee waliokuwa 60+ mwaka 2015 wakati Magufuli anaingia madarakani wamezidi kuisha, hivyo kuja damu mpya ambayo bado haioni hayo maendeleo ambayo ccm wanajivuna kuwaletea wananchi zaidi ya maumivu makali kila uchwao.

3. Ccm wanecheza karata mbaya kwa Bernard Kamiliud Membe. Najua hii ndiyo ilikuwa kete pekee ya ccm kwenye uchaguzi huu. Maandalizi makubwa waliyafanya hapa kwa kumuweka Membe kuwa Kama kibaraka kwa wapinzani, lakini CHADEMA waliliona hilo wakaruka kihunzi hicho. Rejea maneno ya Membe baada ya kikao maalumu Cha kuhojiwa na kamati ya nidhamu ya chama. " Tumeongea Mambo mazuri kwa mustakabari wa taifa letu na chama chetu." Lakini pia wanaccm waliokuwa wakimshinikiza Membe kwenda upinzani walikuwa ni wengi kuliko upinzani wenyewe. Hii maana yake walijipanga kwenye hili.

4. Magufuli amechagua timu mbovu ya kampeni ambayo haina uzoefu na masuala haya ya pilika pilika. Watu wengi ikiwemo Mimi, tulitarajia kwenye timu ya kampeni ya ccm mwaka huu wangeweka full mkoko. Pale Kuna Nape, Makamba, Mzee Mangula pamoja na viongozi wengine wabobezi ndanibya chama. Lakini uwepo wa watu Kama Polepole na Bashiru kumefanya timu ya kampeni kupwaya sana ndani ya CCM. Angalia hata upangaji wa ratiba tu unawacost.

Sioni wapi CCM watashinda iwapo uchaguzi huu utafanywa kwa kufuata misingi ya Sheria ambazo wao wenyewe ndiyo wameziweka. Iwapo tume watakuwa tayari kumtangaza hata wasiyempenda, sioni CCM watashinda vipi.

Asalam Alleykum
Kajifunze kwanza kujenga hoja,!! Mbavu kabsa
 
Maghufuli naye aliandaliwa? Unaandika kitu usichokijua
Nikiwa kama miongoni wa viongozi tuliotekeleza hili jambo. So,this is not hearsay!

Swali: Chadema mlishawahi kumuandaa mgombea yeyote?? Ndio maana Dkt.Slaa alisema alichokisema kuwakejeli😂
 
Wanajamvi Salam,

Zikiwa zimebaki siku kumi na nne (14) tu kwenda kushuhudia historia ikiandikwa Tanzania, kwa ama wananchi kuendelea kuchagua ccm ambayo kiukweli imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili watanzania walio wengi au wananchi kwenda kuchagua Uhuru Haki na Maendeleo yao kwa kufanya mabadiliko ya uongozi hasa katika nafasi nyeti ya uraisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

Kampeni za vyama vyote shindani zinaendelea na huku wadadisi na wachambuzi wa kisiasa wakipima upepo wa kisiasa hasa kwa kuangalia Sera za vyama vyote na idadi ya watu wanaohudhuria katika mikutano ya kampeni kwa vyama tofauti. Hali imekuwa si shwari kwa chama tawala, imekuwa kana kwamba wanapumulia mashine. Kampeni zao zimekuwa zikiratibiwa kwa kiasi kikubwa nje ya chama, hapa nikimaanisha kwa kutumia vyombo vya Dora pamoja na wasanii. Huku upande wa chama kikuu Cha upinzani CHADEMA Mambo ni bul bul. Hali hii imekuja baada ya ccm kukosea hapa

1. Wamefanya siasa kwa miaka mitano peke yao, hivyo ni Kama vile wananchi wamewachoka, wananchi wanataka kusikia mawazo mapya. Wanataka kusikia kile ambacho walikuwa wanafichwa kuambiwa kwa miaka mitano huku ccm wakisema peke yao. Ndiyo maana unaona kwenye mikutano ya chama kikuu Cha upinzani wananchi wanajazana pasi na aina yoyote ya ushawishi wa wasanii. Kwenye hili ccm imewakinaisha wananchi hivyo wanataka mawazo mapya.

2. Kizazi kilichokuwa ccm kufa na kuzikana kinazidi kuisha. Wale wazee waliokuwa 60+ mwaka 2015 wakati Magufuli anaingia madarakani wamezidi kuisha, hivyo kuja damu mpya ambayo bado haioni hayo maendeleo ambayo ccm wanajivuna kuwaletea wananchi zaidi ya maumivu makali kila uchwao.

3. Ccm wanecheza karata mbaya kwa Bernard Kamiliud Membe. Najua hii ndiyo ilikuwa kete pekee ya ccm kwenye uchaguzi huu. Maandalizi makubwa waliyafanya hapa kwa kumuweka Membe kuwa Kama kibaraka kwa wapinzani, lakini CHADEMA waliliona hilo wakaruka kihunzi hicho. Rejea maneno ya Membe baada ya kikao maalumu Cha kuhojiwa na kamati ya nidhamu ya chama. " Tumeongea Mambo mazuri kwa mustakabari wa taifa letu na chama chetu." Lakini pia wanaccm waliokuwa wakimshinikiza Membe kwenda upinzani walikuwa ni wengi kuliko upinzani wenyewe. Hii maana yake walijipanga kwenye hili.

4. Magufuli amechagua timu mbovu ya kampeni ambayo haina uzoefu na masuala haya ya pilika pilika. Watu wengi ikiwemo Mimi, tulitarajia kwenye timu ya kampeni ya ccm mwaka huu wangeweka full mkoko. Pale Kuna Nape, Makamba, Mzee Mangula pamoja na viongozi wengine wabobezi ndanibya chama. Lakini uwepo wa watu Kama Polepole na Bashiru kumefanya timu ya kampeni kupwaya sana ndani ya CCM. Angalia hata upangaji wa ratiba tu unawacost.

Sioni wapi CCM watashinda iwapo uchaguzi huu utafanywa kwa kufuata misingi ya Sheria ambazo wao wenyewe ndiyo wameziweka. Iwapo tume watakuwa tayari kumtangaza hata wasiyempenda, sioni CCM watashinda vipi.

Asalam Alleykum
Nape Nnauye kampeni zake za kum support Magufuli anafanyia Twitter kwa kuweka meme za mafumbo ya hapa na pale.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nguvu ya upinzani wameitengeneza na wanaendelea kuitengeneza wao wenyewe na hiyo ndiyo itakayo waangamiza.sii mbali Bali kesho kutwa Oct.28.Watanzania ni wakati wetu was kuwaangamiza ccm.Chama kisichowapenda Watanzani .
Ccm inapinga kampeni ya miaka 100 ijayo,sio ya huyo beberu
 
Tume ndio mchawi aliye baki, bila hivyo sisiemu inahali ngumu.
 

Tendwa: CCM hii inaweza kuanguka​

Sunday April 3 2016​

Tangu mwaka 1995 vyama vya upinzani vimekuwa vikisimamisha wagombea urais katika Uchaguzi Mkuu bila ya mafanikio, lakini John Tendwa anawataka wasikate tamaa kwa kuwa CCM inaweza kuanguka.

ccm..jpg
Aliyekuwa Msajili wa vyama vya siasa nchini, John Tendwa akizungumza na waandishishi wa gazeti hili, jijini, Dar es Salaam hivi karibuni. Picha na Said Khamis
BY Fidelis Butahe, Mwananchi gazeti

IN SUMMARY​

Tangu mwaka 1995 vyama vya upinzani vimekuwa vikisimamisha wagombea urais katika Uchaguzi Mkuu bila ya mafanikio, lakini John Tendwa anawataka wasikate tamaa kwa kuwa CCM inaweza kuanguka.
Advertisement

Dar es Salaam. Tangu mwaka 1995 vyama vya upinzani vimekuwa vikisimamisha wagombea urais katika Uchaguzi Mkuu bila ya mafanikio, lakini John Tendwa anawataka wasikate tamaa kwa kuwa CCM inaweza kuanguka.

Tendwa, ambaye alikuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, amesema demokrasia nchini inakuwa kwa kasi na hivyo kuna siku upinzani unaweza kushinda lakini itategemea na mahitaji ya wakati huo sambamba na kuibuka na hoja ambazo CCM watakuwa wameshindwa kuzitekeleza.

Mwanasheria huyo, ambaye alistaafu Agosti mwaka 2013, alitoa kauli hiyo katika mahojiano maalumu na waandishi wa gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

“Niwambieni ukweli kama CCM isingekuwa na mgombea mzuri anayeweza kujieleza na wasingekuwa na ilani nzuri ambayo wameweza kuiuza, huwezi kujua pengine Ukawa ingeweza kuchukua madaraka,” alisema Tendwa ambaye alishikilia nafasi ya Msajili wa Vyama kwa miaka 13.

Katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana, CCM ilimsimamisha Dk John Magufuli kugombea urais akipambana vikali na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa wa Chadema ambaye aliungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa.

Katika uchaguzi huo uliokuwa na msisimko mkubwa, Dk Magufuli alishinda kwa kupata kura milioni 8.8 (asilimia 58.47), akifuatiwa na Lowassa aliyepata kura milioni 6.07 (asilimia 39.97), zikiwa ni zaidi ya mara mbili ya kura ambazo wapinzani wamewahi kupata tangu uchaguzi wa vyama vingi urejeshwe mwaka 1995.

“Kama unataka kuzingatia demokrasia hakuna nchi duniani ambayo unakuta chama kinaongoza milele. Mfano Marekani kuna vyama vya siasa zaidi ya 53 ila vikubwa ni Democratic na Republican ambavyo licha ya kuungwa mkono na vyama vidogo, pia vyama hivyo vinapokezana kuongoza nchi,” alisema Tendwa.

“Kwa nini Dar es Salaam wabunge wengi wa CCM wameshindwa? Kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa miaka 23 iliyopita, Jiji limekwenda upinzani na hivi karibuni Naibu Meya atachaguliwa na huenda akawa wa upinzani kwa sababu wana wapigakura wengi labda kuwe na ushirikiano.”

“Kama huo ndiyo mwanzo, nini kitafuata baadaye?” alihoji na kusisitiza kuwa ushindi huo wa upinzani katika jiji hilo ni somo tosha.

Tendwa alisema hayo wakati Rais Magufuli anaonekana kutekeleza mambo mengi ambayo wapinzani walikuwa wakipigia kelele kwenye serikali zilizopita, kama kuboresha bandari, kubana matumizi kwa punguza safari za nje za viongozi na kupambana na rushwa na uzembe kazini.

Hata hivyo, mbinu zake za kutekeleza hayo zimekuwa zikikosolewa, hasa utumbuaji majipu ambao wapinzani wamekuwa wakieleza kuwa haufuati taratibu, kubana matumizi kwa kufuta safari za nje na kupunguza mishahara ya vigogo wa taasisi kubwa za Serikali.

Pia, uamuzi wa hivi karibuni wa Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) kuinyima Tanzania mkataba wa miradi ya maendeleo kutokana na kuamini kuwa uchaguzi wa Zanzibar haukuwa shirikishi, umechukuliwa na wapinzani kama Serikali kushindwa kusimamia demokrasia.

Tendwa hakuacha kugusia sakata la uchaguzi wa meya wa Dar es Salaam ulioahirishwa mara tatu kabla ya Rais Magufuli kuingilia kati, akitaka CCM na Ukawa kutoendelea kuyumbisha na kushauri kila upande kuwa tayari kukubali matokeo.

“Ilikuwa vizuri rais kuingilia maana hii ni nchi yetu na hili ni jiji letu. Kama upinzani wamepita waache, wapite na tukubali kuwa hiyo ndiyo demokrasia. Kama CCM imeshindwa, mkubali,” alisema huku akibainisha kuwa CCM ndiyo chama chake.

Alisema baada ya Meya wa Jiji, Isaya Mwita kupatikana ni wazi kuwa Dar imepata meno na kuvitaka vyama vya siasa kuachana na dhana kuwa Serikali iliyopo madarakani ni ya CCM.

“Kila chama kina wajibu wa kushirikiana na wananchi katika kusukuma maendeleo na wasibweteke kwamba CCM wapo peke yao kwa kuwa upinzani kuna viongozi pia,” alisema Tendwa.

“Kwa sasa Jiji lipo upinzani hivyo wafanye kazi maana hii ndiyo serikali yao ya kwanza na waonyeshe umahili ili wakienda katika uchaguzi wawe na sera ya kusema.”

Alipoulizwa kuhusu viongozi kuhama vyama kama ilivyokuwa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015, Tendwa alisema: “Kuhama chama ni afya katika demokrasia. Nchi ya Marekani haina wanachama waanzilishi wa vyama na ndiyo nchi inayosifika kwa demokrasia duniani.”

Alisema watu wanabadilika kutokana na mambo wanayooona kuwa na manufaa kwao kwa wakati husika huku akitoa mfano wa vyama vikubwa viwili vya nchi hiyo.

Alikitoa mfano wa mbunge wa Bunda, Ester Bulaya aliyeihama CCM na kujiunga na Chadema, Tendwa alisema wanasiasa waliohama wameongeza ushindani wa kisiasa.

“Ni wakati wake (Bulaya) wa kufanya yale aliyokuwa akiyakosoa yaonekane kwamba ni sahihi na kweli wapigakura waseme kuwa ameyatekeleza,” alisema.

Fast forward 2020
13 October 2020
Maoni ya John Tendwa uchaguzi 2020


John Tendwa msajili mstaafu wa vyama vya siasa Tanzania atoa maoni kuhusu kampeni za 2020

Source : wakili tv
 
Wanajamvi Salam,

Zikiwa zimebaki siku kumi na nne (14) tu kwenda kushuhudia historia ikiandikwa Tanzania, kwa ama wananchi kuendelea kuchagua ccm ambayo kiukweli imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili watanzania walio wengi au wananchi kwenda kuchagua Uhuru Haki na Maendeleo yao kwa kufanya mabadiliko ya uongozi hasa katika nafasi nyeti ya uraisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

Kampeni za vyama vyote shindani zinaendelea na huku wadadisi na wachambuzi wa kisiasa wakipima upepo wa kisiasa hasa kwa kuangalia Sera za vyama vyote na idadi ya watu wanaohudhuria katika mikutano ya kampeni kwa vyama tofauti. Hali imekuwa si shwari kwa chama tawala, imekuwa kana kwamba wanapumulia mashine. Kampeni zao zimekuwa zikiratibiwa kwa kiasi kikubwa nje ya chama, hapa nikimaanisha kwa kutumia vyombo vya Dora pamoja na wasanii. Huku upande wa chama kikuu Cha upinzani CHADEMA Mambo ni bul bul. Hali hii imekuja baada ya ccm kukosea hapa

1. Wamefanya siasa kwa miaka mitano peke yao, hivyo ni Kama vile wananchi wamewachoka, wananchi wanataka kusikia mawazo mapya. Wanataka kusikia kile ambacho walikuwa wanafichwa kuambiwa kwa miaka mitano huku ccm wakisema peke yao. Ndiyo maana unaona kwenye mikutano ya chama kikuu Cha upinzani wananchi wanajazana pasi na aina yoyote ya ushawishi wa wasanii. Kwenye hili ccm imewakinaisha wananchi hivyo wanataka mawazo mapya.

2. Kizazi kilichokuwa ccm kufa na kuzikana kinazidi kuisha. Wale wazee waliokuwa 60+ mwaka 2015 wakati Magufuli anaingia madarakani wamezidi kuisha, hivyo kuja damu mpya ambayo bado haioni hayo maendeleo ambayo ccm wanajivuna kuwaletea wananchi zaidi ya maumivu makali kila uchwao.

3. Ccm wanecheza karata mbaya kwa Bernard Kamiliud Membe. Najua hii ndiyo ilikuwa kete pekee ya ccm kwenye uchaguzi huu. Maandalizi makubwa waliyafanya hapa kwa kumuweka Membe kuwa Kama kibaraka kwa wapinzani, lakini CHADEMA waliliona hilo wakaruka kihunzi hicho. Rejea maneno ya Membe baada ya kikao maalumu Cha kuhojiwa na kamati ya nidhamu ya chama. " Tumeongea Mambo mazuri kwa mustakabari wa taifa letu na chama chetu." Lakini pia wanaccm waliokuwa wakimshinikiza Membe kwenda upinzani walikuwa ni wengi kuliko upinzani wenyewe. Hii maana yake walijipanga kwenye hili.

4. Magufuli amechagua timu mbovu ya kampeni ambayo haina uzoefu na masuala haya ya pilika pilika. Watu wengi ikiwemo Mimi, tulitarajia kwenye timu ya kampeni ya ccm mwaka huu wangeweka full mkoko. Pale Kuna Nape, Makamba, Mzee Mangula pamoja na viongozi wengine wabobezi ndanibya chama. Lakini uwepo wa watu Kama Polepole na Bashiru kumefanya timu ya kampeni kupwaya sana ndani ya CCM. Angalia hata upangaji wa ratiba tu unawacost.

Sioni wapi CCM watashinda iwapo uchaguzi huu utafanywa kwa kufuata misingi ya Sheria ambazo wao wenyewe ndiyo wameziweka. Iwapo tume watakuwa tayari kumtangaza hata wasiyempenda, sioni CCM watashinda vipi.

Asalam Alleykum
Sahihi
 
Busega, Simiyu
Tanzania

Wanajeshi wastaafu JWTZ wazungumzia Uchaguzi Mkuu 2020
Wanajeshi wastaafu wa JWTZ watoa rai kuwa Mgombea atakayeshinda kihalali atangazwe na kuongeza kuwa chama chochote kitakacho shinda ni cha waTanzania hivyo wananchi tukubali matokeo
 
Ccm hii siyo kwa ajili ya watanzania bali kwa ajili ya kwatisha watanzania wasijue haki zao
 
Back
Top Bottom