Hujaoa/Hujaolewa alafu unatumia Tsh 10,000 au zaidi kwa siku kwa ajili ya chakula tu! Ni anasa hizo

Hujaoa/Hujaolewa alafu unatumia Tsh 10,000 au zaidi kwa siku kwa ajili ya chakula tu! Ni anasa hizo

sijaoa na kwa siku natumia elfu 20: 2000 nauli kwenda na kurudi kazini, chai 1500, lunch 3500, dinner 3000, maji ya kunywa chpa 3 kwa siku 1600, vocha 2000, bia 3 jioni elfu 6, shemeji yako vocha 1000, ushuru wa taka nyumbani 500, dobi wa kunifulia 2000, kubet 1500, mpelelezi wangu wa kunipa umbea wa mtaani 500 kwa cku, gym membership 3000 kwa siku, soda/juice 1000, matunda ya njiani kv chungwa/tiktiki 200-500, movie kwa jamaa wa kukodisha movie 1000. UPO?
 
Kuna msemo alikua anautumiaga sana babu yngu mungu amiweke pahala pema pepon. Alikua anasema "kula hakumfilisi mtu"
 
Asubuhi 3000-3500 (mtori au supu ya mbuzi) + maji 1500
Mchana 3500 - 5000
Usiku nyumbani au kama nikila nje basi pale etina makange ya kuku/samaki/firigisi 10,000/=

Kuliko nile chakula cha elfu moja ni bora nisile kabisa, ninashukuru nilishavuka huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila mtu na aina ya maisha yake mzee!
Kuna watu hiyo 10k hata chai haitoshi.
Kama wewe unaleta ubahili kwa hela unayoihangaikia basi endelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi na binti Yangu wa miaka 3.5 tunatumia 10000 kwa siku tunapika

don't invest in a woman
 
Yaani mkuu kila nikiona username yako huwa najikuta nachaka tu. Huwa najiuliza huyu mtu alikuwa anawaza nini wakati anaandika hii username?
Mkuu kama mimi yani alafu hakuna gepu kwamba jina la baba au mtoto.

Daaaahhuyujamaaanomaa
Ila ninachohisi itakuwa hili jina lake limetokana na kisa fulanii


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nusu ya nyama ya kitimoto siku hizi imepanda mpaka TSh. 4000 /= katika buku kumi inabaki buku sita, hujanunua nyanya tufanye za mia tano, bado kitunguu, mchele /Unga n. k

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Kusema kweli nawashangaa watu wengi sana.

Mtu unaishi peke yako, alafu unatumia Tsh 10,000 nzima kwa ajili ya msosi tu. Tena kwa ajili yako wewe mwenyewe.

Hiyo ni anasa na ufujaji wa pesa!!

Maximum kwa siku tumia 5000/- kwa siku kwa ajili ya msosi.

Buku chai, buku jero lunch, buku jero dinner, buku maji na matunda...

Tuachane na anasa, pika mwenyewe nyumbani. Na gharama haitozidi elfu 5 kwa siku kwa ajili ya kula tu.


Niite,

Mjina Mrefu
Dadadeq


Sent using Jamii Forums mobile app
Da !! Kweli aisee hii ilnikuta juz Kat had kichwa kiliniuma Kama tu ntakuwa nakula kwa kupka mwenyewe gharama zimekuwa kichele hadi raha agree with your suggestions🔚
 
Back
Top Bottom