Huku mtaani kwa sasa hakuna mwanasiasa maarufu kuliko Makonda

Kuna kaukweli kidogo hapo !
Sio kidogo hiyo ndio hulka ya Mtanzania AKA Mnyonge AKA Mlalahoi.

Mimi hapa Mtaani nilinunua ISUZU tani tatu nikaanza kununiwa na kuitwa "Zungu la Unga", this is Bongo bhana😁... na hawa watu wakipata Dikteta kama Mobutu anaweza kuwatawala milele mpaka ajifie kwenye Ikulu trust me.

Mimi hunidanganyi kuhusu "Mbongo nuksi" hata siku moja, hawa wa Pwani hadi Dodoma kwa wale Wagogo.

Wabongo makini wako Nyanda za juu Kilimanjaro Arusha Kagera nk.
 
Hapa ndio CCM inapowapiga magoli kuchukulia swala la kuungwa mkono na wananchi poa.

Hata dictatorship za wazi kama China, Russia na North Korea; zinahitaji public support na wanatumia hela nyingi kwenye nationalism propaganda.

Nyie CCM kutafuta public support mnawaona mafala na hao wananchi wanaojaza mikutano yao mnawaona mazuzu badala ya kujiuliza why wanajazana.

Makonda ni katibu mwenezi watatu chini ya uraisi wa Samia; ushajiuliza mbona wananchi walikuwa awajai hivyo kwenye mikutano ya Shaka, Sophia Mjema. Iweje kwa Makonda wanajazana.

Mbona walikuwa hawajai ivyo kwenye mikutano ya Chongolo au Kinana; why kwa Makonda.

Kama nilivyokwambia awali siasa pia inahitaji kufanya research (similar to that of marketing). You don’t get support kwa kuamini wewe unauelewa mpana (even if it were true) so wananchi wanatakiwa wakuamini utakachowaeleza. It doesn’t work that way it is the other way around unatakiwa uelewe wananchi wanataka nini and exploit that.

Kwenda huko vijijini kuwaambia habari za katiba mpya, sijui sheria ya uchaguzi. Wakati mkulima ana ugomvi locally na afisa kilimo, body ya kununua mazao yake, mtu kaporwa ardhi etc halafu hayo mambo hayo uongelei unadhani ukitoka hapo watakuelewa.

Jifunzeni kwa Makonda akienda huko mikoani apigi porojo za umeme, sijui kupanda kwa bei ya chakula. Kwa sababu hizo sio local issues kila sehemu anatumia muda mwingi ku-address local challenges anazoletewa na hiyo ndio inamfanya kila anapoenda kukuta umati unaongezeka kwa sababu wanajua anaenda kuongea local politics.

Hiyo inakwambia kuna watanzania wanashida luluki all they care ni mtu ambae anaweza pambana na changamoto zao, they don’t care kuhusu hadithi za kutunga za watu kukutwa kwenye viroba, sijui kuzuia media and other national issues wakati wao wenyewe wana matatizo luluki yamewazunguka locally hawana wa kuwasaidia.

CCM hawachukulii local politics poa kwa sababu wanaelewa umuhimu wa support atakama kushindwa uchaguzi ni hadithi. Halafu upinzani ambao hata hizo chance za kushinda uchaguzi ni almost zero halafu hawa 70% ya watanzania wanaoenda kwenye mikutano ya Makonda wanawaona mazuzu.

What you need to understand Magufuli changed the political landscape ya Tanzania kwa wananchi on how they define value kwa value kiongozi. Sasa uhutaji kumtaja Magufuli but you can’t ignore what people want, it’s for the opposition to figure out how best to package that info to suit their narrative as an alternative.

Siasa ni science
 
Ni kweli kabisa !
 
Makonda yeye anachokifanya anatumia Magufuli style ambayo watanzania wengi(nazungumzia kajamba nani) ndio wanapenda
Nakuelewa sana. Watu masikini ni hatari sana. Umasikii umefunika kabisa ufahamu wao ,wala hawana uwezo ya kubaini ulaghai uliojificha katika siasa za huyu jamaa.
 
Kwahiyo unaamini CCM huwa inashinda kihalali?
Kwa Mfano, CDM wakagomea uchaguzi na vyama vyote vya upinzani,

CCM wakajitokeza Wachache kwenye uchaguzi,

Patakuwa na ushindi wa halali? Ili ushinde, ni sharti ushindane na mpinzani wako na ushinde.

Ogopa sana kitu inaitwa uchaguzi, Serikali Huwa hailali USINGIZI.
 
Unakoroma sana
 
akina Heche naona wanakuja na nitoke vipi kupitia makonda
 
Ndugu yangu usipoteze muda kunipa aina hiyo ya elimu. Mimi sina interest na mikakati ya power politics za vyama vya siasa. Siko huko kabisa.

CONCERN YANGU KUBWA ni jinsi Tanzania itakavyopata mfumo na muundo makini wa uongozi wa kisiasa utakaopelekea utendaji bora na ufanisi katika uchumi na huduma za jamii nchini. Mfumo utakaohakikisha rasilimali za taifa zinatumika kwa weledi na ufanisi mkubwa kuliletea taifa maendeleo sahihi. Sio hii make-believe ya Makonda and his mentor.

Ubingwa wa vyama vya siasa katika mikakati yenye lengo la kudumu madarakani TU by hooks and crooks ni ANATHEMA kwangu. Ni chukizo kubwa.

Ni aibu kubwa sana na uhaini kwa taifa kwa CCM, chama dola tangu tupate uhuru KUISHIA kufikiria mikakati ya kudumu madarakani kwa janja janja, ulaghai, wizi wa kura/chaguzi na hujuma dhidi ya vyama na wanasiasa wa upinzani.

Hata CHADEMA, kwa mfano, wakiamua kwenda na mikakati ya janja janja kama CCM ili kuingia na kubaki madarakani, sitaona sawa.

Hii nchi sasa hivi ina analogy kubwa na BANANA REPUBLIC. Tunahitaji uongozi utakaotuondoa kwenye muelekeo huo na kutuelekeza kwenye misingi ya utawala bora.
 
Hata humu JF Makonda ni maarufu kuliko mwanasiasa yeyote.
Angalia mada zake zinazoandikwa zilivyo nyingi kisha zilivyo na wachangiaji wengi.

Hapa ningemtaja mwanasiasa mwingine hata wewe usingekuja kutoa maoni yako
So pointi yako ni umaarufu tu au pointi yako ni nini? Mbona hata piere liquid ni maarufu pia?
 
Hata sijakuelewa
 
Kwa umaarufu ndio hoja
Kesi ya uhalifu ni ishu nyingine Mkuu.
Kwa nini hutaki kukubali ukweli maana ukweli wako mimi nimekubali
Ukweli kwako siyo ukweli kwangu. Vigezo ulivyovitumia ni dhaifu.

Mwanasiasa maarufu kumzidi Tundu Lissu au Mbowe?
 
Lkn kwa nn yeye anathubutu. Wengine wamezubaa.

Hapo naelewa kundi ambalo halimuelewi ni public employee maana yeye ni kama chambo
 
Hata wasiojulikana walikuwa maarufu sana, mfano kwangu Mimi bashite ni maarufu sana kwakuwa natafakari mtu aliyestahili adhabu ya kunyongwa lakini Leo ana cheo kikubwa tena ndani ya nchi ileile alotakiwa kuhukumiwa.
 
Umeona, wanaokuja kumsikiliza? Ni wale tunaoita "wretched of the earth" Apeche alolo! Choka mbaya, wanaoambiwa "raisi anataka wawe na furaha! Na, wao, wanashangilia, wakati watoto hawana hakika ya kupata elimu Bora, ajira, mishahara minono, chakula, huduma Bora za, afya,sheria na, haki, upuuzi mtupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…