Huku mtaani kwa sasa hakuna mwanasiasa maarufu kuliko Makonda

Huku mtaani kwa sasa hakuna mwanasiasa maarufu kuliko Makonda

Wanafanya vizuri sababu wanakibomoa chama Chao Kwa kuifanya Serikali nzima ionekane Si kitu mbele ya Mwenezi.

Wananchi tunafurahia move hii kama tu itasababisha chama kuangukia pua 2025.
CCM haitegemei kura yako, ina NEC Fake na polisi
 
CCM haitegemei kura yako, ina NEC Fake na polisi
Kama haitegemei kura za wananchi,

Kwanini wanatumia nguvu kubwa kuigiza kuwa wanakubalika?

Ingekuwa ni Kweli isemayo, wangeweka nne na wasijihangaishe na chochote wakiamini polisi na Jeshi kama usemavyo!!
 
Kama haitegemei kura za wananchi,

Kwanini wanatumia nguvu kubwa kuigiza kuwa wanakubalika?

Ingekuwa ni Kweli isemayo, wangeweka nne na wasijihangaishe na chochote wakiamini polisi na Jeshi kama usemavyo!!
Kwahiyo unaamini CCM huwa inashinda kihalali?
 
Mheshimiwa Paul Makonda ndiye mtetezi wa wanyonge ndiye Sauti ya watanzania,kinywa cha Mh Makonda kinazungumza kwa niaba ya mamilioni ya watanzania. Mh makonda ndiye aliyebeba matumaini ya vijana na watanzania ambao wameamua kumpeleka ikulu kwa kishindo ifikapo mwaka 2030.
UMASHUHURI WA MAKONDA NI WA MUDA TU UTAPOROMOKA PALE TU ATAKAPOSHINDWA KUWATETEA HAO WANYONGE KWA KILE WALICHOAMINI WATAWAPA KUPITIA YEYE NI SUALA LA MUDA TU

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Tatizo watanzania wanamuona Jpm kwa Makonda. Na sio uongo Jpm anawafuasi wengi sana
T
JPM hakupendwa kwa Madaraja wala kwa Barabara alizojenga alipendwa kwa KUTUMBUA😁.

Nakuapia leo hii afufuke arudi Ikulu halafu akae KIMYA asiwafilisi Matajiri na Wafanyabiashara ASITUMBUE asiongee kwa Ukali aongee kama Mbalawa halafu uone😄

Utasikia huyu Magufuli Feki huyu🤣😆

Hii Nchi ilishalaaniwaga zamani.
 
Naomba thread za wajinga wanaolipwa kumsifia Makonda huku ndani zipelekwe kwenye vichekesho… au waende huko instagram
 
Huku Mtaani Walalahoi wanafuatilia kwa makini sana BIFU la Bashe na Makonda Walalahoi wamesahau hata kama wanashindia mlo mmoja au hata nusu mlo lakini wameanza KUBETI wengine wanasema BASHE anatumbuliwa wengine wanasema Makonda ndie ATAKAEUFYATA Mkia😁

Kwa Mtu anaehangaika kumjua Mtanzania au labda unataka KUMKOMBOA Mtanzania😆 zaidi ni kupoteza muda tu.
 
Makonda ana akili za kuzaliwa, ni mzalendo na mchapa kazi. Mungu ambariki sana Makonda wetu.
Labda akili za Makonda ziko kwenye msambwanda, ila kama ni kichwani nakataa, hakuna kitu. Yaani ZEROBRAIN
Screenshot_20231111_190308_Google.jpg
 
Ikiwa 90% ni wajinga basi nawe ni miongoni mwa hao wajinga kwa sababu nilichoandika hata hujakielewa sio ajabu imetoa maelezo marefu yasiyohusiana na uzi


Wapi nimesema wananchi wanasikilizwa? Hivi unajua kusoma kwa ufahamu au unasoma kama upo kwenye mashindano ya kusoma imla kwa haraka haraka kama kasuku?

Soma tena uzi alafu uelewe uzi Unazungumzia jambo gani.


Hapa sio Kanisani au msikitini kwamba useme ninaamini au siamini. Mimi nimeeleza ninachokiona na kukisikia mtaani. Sio Masuala ya imani kama hadithi za NONDO mla Watu.


Sasa kama unajua nchi inahitaji strong institution Kwa uelewa wako Unafikiri hiyo taasisi yenye nguvu inajengwa na nani kama sio kiongozi mmoja


Kwa kukurahisishia ni kuwa mada ilikuwa inasema Mpaka sasa Makonda ndiye mwanasiasa maarufu kuliko wote.
Labda umaarufu wa Makonda ni mkubwa kuliko wanasiasa wengine kwa kigezo cha mtaani kwako. Huyu ni mfungwa mtarajiwa tu baada ya awamu ya 6. Mark this post
 
Makonda ni ushahidi tosha huko CCM wananchi wana-miss aina ya uongozi kipindi cha Magufuli. Hawana mtu wa kumlilia shida.

Hao wapinzani wakati CCM inaachana na style ya uongozi badala ya wao kuziba gap kwa faida ya kisiasa ndio kwanza wakipata wasaa kwenye media yule mtu alikuwa hafai. Leo wamebaki kujitekenya na kucheka wenyewe wakijiaminisha wana support yenye nguvu nchini.

Watanzania hawana trust tena na uongozi wa upinzani na Makonda ndio anaenda kuudhofisha kabisa.

Siku Makonda anatangazwa katibu mwenyezi wengine tulishaiona hii move ya kisayansi inalenga nini na si ajabu msingi wake ni use of ‘big data’.
Mkuu, tuweke umaarufu (populism) pembeni. Hii “style ya uongozi” ya Makonda unaamini ndiyo itakayowezesha serikali kuongeza utendaji (performance) wake? Kwamba ufanisi utaongezeka kwenye utatuzi wa matatizo ya wananchi na utekelezaji wa majukumu yake kwa ujumla?

Sio kwamba serikali ya CCM inatafuta “kupendwa” na wananchi kwa kuwalaghai (hoodwinking) na hizo populism gimmicks za Makonda? Eti kutatua matatizo hadharani, mubashara mbele ya vyombo vya habari! Yaani baada ya kushindwa kutimiza majukumu na wajibu wake kwenye taasisi zake sasa serikali imehamia kwenye propaganda za kilaghai mitaani.

Ndio tunatarajia wapinzani nao washindane na serikali ya CCM kwa siasa za kilaghai kama hizi ili waipate “trust” ya wananchi? That’s really sad.
 
Wanasiasa na viongozi wote na sisi pia tunajua haki huwa haitendeki kwa asilimia kubwa sana
Kila mmoja anajua Tz ingeendelea kama hakuna wizi na uongo na kubebana
Sasa huyu jamaa anapiga mule mule ingawa kwa nchi masikini ni nguvu za soda kwani hata anaemuiga alipita humo humo ila tatizo alikuwa peke yake

Nchi ukiona masikini sio kwa upumbavu bali walioko juu ndio wanakula asilimia yote
Kila mahali kuna ulaji na viongozi wanalijua hilo na wao wanakula humo na maisha ya wizi na dhulma ni kawaida

Mpaka Mawaziri wote waungane na wakurugenzi kukataa tabia hizi basi tutabakia masikini tu
Hata huyu Makonda anajua fika baada ya Uchaguzi tunarudi kule kule
 
Kwema Wakuu!

Sijui anatumia uchawi gani.
Sijui anatumia mbinu gani za kimedani.
Lakini huyu jamaa kwa sasa hakuna mwanasiasa yoyote ambaye anamsogelea kwa umaarufu hata kwa kilometa mia moja.

Kama ni riadha za siasa tunasema Makonda angeshatangazwa ndiye Mshindi kwa sababu tangu aingie kwenye riadha amewaweka wenzake wote pembeni na sio tuu pembeni bali mbali huko.

Jana kwenye Malumbano ya Hoja, ITV Makonda mbele.
Sokoni huko Makonda.
Bodaboda nao Makonda.
Kwenye Daladala Makonda.

Kwani Makonda kafanyaje?
Nilipofuatilia zaidi wengi wa washangiliaji wake wanasema kuwa Makonda ndiye Mtetezi wao, Makonda ndiye Magufuli wao.
Kwamba kwa nchi hii Watanzania waliowengi wanamchukulia Magufuli ndiye Masihi na sasa mrithi wake ni Makonda. Hayo ni mawazo na mtazamo wa watanzania hasa wa hali ya chini ambao ni zaidi ya asilimia 80 hivi.

Sio Chadema, sio ccm, sio Act hakuna mwanasiasa mashuhuri na mwenye ushawishi kwa Tanzania kumzidi Makonda. Hii inamaanisha nini? Kama hali itaendelea hivi basi Watu wataanza kumpenda na upendo siku zote uko na nguvu kuliko Mauti.

Ingawaje mimi sio mfuasi wa siasa za Makonda lakini nikiri kwa ukweli kuwa yeye ndiye amebeba kwa sasa siasa za nchi yetu. Jina lake likiwa kubwa na lenye kuandikwa na kusemwa na waliowengi.

Wasalamu

Punguza uchawa. Unamwita maarufu na hujui kafanya Nini?.
 
Labda umaarufu wa Makonda ni mkubwa kuliko wanasiasa wengine kwa kigezo cha mtaani kwako. Huyu ni mfungwa mtarajiwa tu baada ya awamu ya 6. Mark this post

Kwa umaarufu ndio hoja
Kesi ya uhalifu ni ishu nyingine Mkuu.
Kwa nini hutaki kukubali ukweli maana ukweli wako mimi nimekubali
 
Back
Top Bottom