Huku mtaani kwa sasa hakuna mwanasiasa maarufu kuliko Makonda

Huku mtaani kwa sasa hakuna mwanasiasa maarufu kuliko Makonda

Hata mimi nilitaka nimuulize makonda ni maarufu kwa jambo lipi
Tanzania standard zetu za mambo mengi zipo chini sana
Nakuomba uset standards kaka na uzitume hapa!! Maana hutaki kukubali tu kuwa jamaa ndo anatrend kuliko yeyote nchini!
 
Makonda ni kina kirefu nyumbu watazama
 
Mheshimiwa Paul Makonda ndiye mtetezi wa wanyonge ndiye Sauti ya watanzania,kinywa cha Mh Makonda kinazungumza kwa niaba ya mamilioni ya watanzania. Mh makonda ndiye aliyebeba matumaini ya vijana na watanzania ambao wameamua kumpeleka ikulu kwa kishindo ifikapo mwaka 2030.
We Jamaa umejaa misifa ya kijinga sana...Unaboa
 
Kwa umaarufu ndio hoja
Kesi ya uhalifu ni ishu nyingine Mkuu.
Kwa nini hutaki kukubali ukweli maana ukweli wako mimi nimekubali
Umaarufu wa nini na je huo umaarufu umekua na manufaa gani kwa mwananchi wa kawaida anaye nunua sukari 4500, na kuendelea, umeme unaokatika mara kwa mara
 
Labda una obsession na Makonda tu kama walivyo watanzania wengi zaidi ya 90% ambao ni wajinga.

Je ni kweli wananchi Wanasikilizwa ? Hilo pekee siyo suluhisho.

Hakuna mtu aliyeyatuliwa shida yake na Makonda mpaka sasa toka aanze ziara zake

Ukiamini katika uliyoyaandika unanithibitishia kuwa mfumo wa utendaji na utoa huduma wa Serikali umekufa.

Barack Obama alipotembelea Ghana Julai 11, 2009 alisema "Africa doesn't need strongmen, it needs strong institutions,”

Kwa kuwa strong men watakufa ila strong institutions zitadumu milele.

Na hiyo ambayo Barack Obama alikuwa anaiponda ndiyo "Magufulism". Nchi inamtegemea mtu mmoja kwa maguvu yake na akili zake, akifa na mfumo umekufa.

Kama unasema unasema Makonda ni mouthpiece ya prez, then the prez has shown weakness. Unawateua watendaji wewe mwenyewe, je unashindwaje kuwawajibisha hadi "mwenezi" ndiyo awafokee. ??
Strong institutions zinajengwa na watu.

Ambacho kwa afrika watu hao hawapo.
 
Kumbe ni maarufu, nilidhani ni mwanasiasa Bora. Umaarufu wake umesababisha umeme wa uhakika kupatikana, bei ya sukari imeshuka, treni ya mwendokasi imeanza juzi mwezi wa January. Unaweza kuwa maarufu kwa mambo ya kijinga, wenye akili zetu tunapima ubora na sio kiki.
Kumbe sukari zimepanda?

Kumbe hauna umeme?


Kwani Magufuli bado yuko hai?
 
Samia hakuwa mjinga kumleta Makonda
 
Kwema Wakuu!

Sijui anatumia uchawi gani.
Sijui anatumia mbinu gani za kimedani.
Lakini huyu jamaa kwa sasa hakuna mwanasiasa yoyote ambaye anamsogelea kwa umaarufu hata kwa kilometa mia moja.

Kama ni riadha za siasa tunasema Makonda angeshatangazwa ndiye Mshindi kwa sababu tangu aingie kwenye riadha amewaweka wenzake wote pembeni na sio tuu pembeni bali mbali huko.

Jana kwenye Malumbano ya Hoja, ITV Makonda mbele.
Sokoni huko Makonda.
Bodaboda nao Makonda.
Kwenye Daladala Makonda.

Kwani Makonda kafanyaje?
Nilipofuatilia zaidi wengi wa washangiliaji wake wanasema kuwa Makonda ndiye Mtetezi wao, Makonda ndiye Magufuli wao.
Kwamba kwa nchi hii Watanzania waliowengi wanamchukulia Magufuli ndiye Masihi na sasa mrithi wake ni Makonda. Hayo ni mawazo na mtazamo wa watanzania hasa wa hali ya chini ambao ni zaidi ya asilimia 80 hivi.

Sio Chadema, sio ccm, sio Act hakuna mwanasiasa mashuhuri na mwenye ushawishi kwa Tanzania kumzidi Makonda. Hii inamaanisha nini? Kama hali itaendelea hivi basi Watu wataanza kumpenda na upendo siku zote uko na nguvu kuliko Mauti.

Ingawaje mimi sio mfuasi wa siasa za Makonda lakini nikiri kwa ukweli kuwa yeye ndiye amebeba kwa sasa siasa za nchi yetu. Jina lake likiwa kubwa na lenye kuandikwa na kusemwa na waliowengi.

Wasalamu
Labda mtaa wa makuwadi us dpworld.
 
Kumbe sukari zimepanda?

Kumbe hauna umeme?


Kwani Magufuli bado yuko hai?

Yaani dhalimu aendelee kuoza hadi mifupa. Kama Ili bei ya sukari ishuke na umeme uwepo ni lazima dhalimu awepo, basi acha visiwepo kabisa.
 
Mkuu, tuweke umaarufu (populism) pembeni. Hii “style ya uongozi” ya Makonda unaamini ndiyo itakayowezesha serikali kuongeza utendaji (performance) wake? Kwamba ufanisi utaongezeka kwenye utatuzi wa matatizo ya wananchi na utekelezaji wa majukumu yake kwa ujumla?

Sio kwamba serikali ya CCM inatafuta “kupendwa” na wananchi kwa kuwalaghai (hoodwinking) na hizo populism gimmicks za Makonda? Eti kutatua matatizo hadharani, mubashara mbele ya vyombo vya habari! Yaani baada ya kushindwa kutimiza majukumu na wajibu wake kwenye taasisi zake sasa serikali imehamia kwenye propaganda za kilaghai mitaani.

Ndio tunatarajia wapinzani nao washindane na serikali ya CCM kwa siasa za kilaghai kama hizi ili waipate “trust” ya wananchi? That’s really sad.
Hiyo ndio science ya uchaguzi ‘trust’ you are able to sort their problems. The trick is in how you package that message.

Anachofanya Makonda kwenye ziara yake inaweza isiwe mvuto kwa mtu mwenye middle income au mfanyabiashara mdogo ambae shida zake ni umeme wa uhakika, kodi, hasara za mafuriko, bima ya afya na mengineo. Huyu inabidi umetengezee message nyingine na kumwaminisha una uwezo kweli wa kuzitatua hizo shida ukipewa nafasi.

Vita mbinu sio porojo tu na kuongea vitu unavyodhani wewe mwanasiasa wananchi wanataka kusikia, la hasha ongea vitu ambavyo wao wanataka kusikia.

Uwezi ukawa kila siku unaponda symbol (Magufuli) ambayo wananchi wengi wanao hudhuria mikutano ya Makonda, hiyo symbol ina connotation ya haki kwenye macho yao (hata kama upendi ndio khali) tembeles huo upepo.

Siasa ni science sio hisia za mtu. Ndio maana watu wanafurika kwenye mikutano ya Makonda na kuchunia maandamano ya CDM hakuna trust anymore.
 
Umemsifia na kuvuka mipaka,utakuwa huna nia njema na Makonda.
 
Hiyo ndio science ya uchaguzi ‘trust’ you are able to sort their problems. The trick is in how you package that message.

Anachofanya Makonda kwenye ziara yake inaweza isiwe mvuto kwa mtu mwenye middle income au mfanyabiashara mdogo ambae shida zake ni umeme wa uhakika, kodi, hasara za mafuriko, bima ya afya na mengineo. Huyu inabidi umetengezee message nyingine na kumwaminisha una uwezo kweli wa kuzitatua hizo shida ukipewa nafasi.

Vita mbinu sio porojo tu na kuongea vitu unavyodhani wewe mwanasiasa wananchi wanataka kusikia, la hasha ongea vitu ambavyo wao wanataka kusikia.

Uwezi ukawa kila siku unaponda symbol (Magufuli) ambayo wananchi wengi wanao hudhuria mikutano ya Makonda, hiyo symbol ina connotation ya haki kwenye macho yao (hata kama upendi ndio khali) tembeles huo upepo.

Siasa ni science sio hisia za mtu. Ndio maana watu wanafurika kwenye mikutano ya Makonda na kuchunia maandamano ya CDM hakuna trust anymore.
Nimeona maandamano ya CHADEMA yakiwa na watu wengi tofauti na unavyoelezea hapa. Anyway, kama ni suala la janja ya kushinda uchaguzi, sawa ingawa inaonyesha ujinga mkubwa ulioenea kwenye jamii ya Watanzania kuchukuliwa na cheap propaganda za chama tawala.

Kwa upande mwingine tunajua CCM ipendwe, isipendwe lazima iingie madarakani kwa nafasi inazotaka. Na hawajawahi kukubali kuweka mazingira ya uchaguzi huru na wa haki hata wakati wa Magufuli - anayedaiwa kuwa kiongozi maarufu sana. So, why the desperate propaganda? Bado wanatumainia muujiza wa kupendwa na wananchi?

CHADEMA kumponda Magufuli si kitu cha kushangaza. Huyu ni Rais aliyeazimia kuua upinzani hasa CHADEMA literally, by any means katika kipindi chake. Uchaguzi wa 2019 na 2020 ni ushahidi tosha. Haiyumkiniki uchaguzi wa 2020 CHADEMA kupata mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa! Na mengine mengi aliyowafanyia. Halafu unatarajia CHADEMA walione jina la Magufuli kuwa “kete muhimu ya uchaguzi” na kuliimbia mapambio? That would be insane for sure!
 
Makonda atumbuliwe Jukwaani na Maza uone Vigelegele vitakavyolipuka Kitaa, Watanzania wanapenda kuona aliyejuu anashushwa chini.

Mfano mwingine Maza akimfilisi Mo Dewji Jukwaani Popularity yake itapanda mara dufu.
Hao ndio WATANZANIA halisi.

Hayo mengine ni mbwembwe tu.
Kuna kaukweli kidogo hapo !
 
Back
Top Bottom