Rweye
JF-Expert Member
- Mar 16, 2011
- 17,057
- 7,611
Kuna taarifa zisizo rasmi kwamba kutokana na ujenzi wa miradi mikubwa mikubwa hapa Tanzania na miradi hiyo ikiwa chini ya wachina basi inasadikika jamaa hawa kutoka Asia wameamua kufanya yao ili wasisumbuke na ujenzi.
Nimejikuta najiuliza mengi na nikajiuliza sasa maisha yetu yanakwenda kuwaje. Joto limezidi kila kona, ardhi imekauka na mazao yamekaukia mashambani. Kwingineko magonjwa pia yamechachamaa mno kwasababu miili imechemka kupita kiasi
Kama hii kweli ni wachina ndo wanahusika basi hawa watu watatuletea majanga makubwa. Wanatakiwa kujua kwamba nchi yetu iko katika ukanda wa joto kali la tropic ambako kwa kiasi kikubwa kutofautiana na ile ya china, kama kwao wanafanya hivyo ni sawa lakini kwa Tz si sehemu sahihi kwani kijiografia tayari sie tuko kwenye tanuru na hatuitaji tena kuchochewa kuni na mkaa
Tuiombee nchi yetu watanzania, asubuhi njema!
Nimejikuta najiuliza mengi na nikajiuliza sasa maisha yetu yanakwenda kuwaje. Joto limezidi kila kona, ardhi imekauka na mazao yamekaukia mashambani. Kwingineko magonjwa pia yamechachamaa mno kwasababu miili imechemka kupita kiasi
Kama hii kweli ni wachina ndo wanahusika basi hawa watu watatuletea majanga makubwa. Wanatakiwa kujua kwamba nchi yetu iko katika ukanda wa joto kali la tropic ambako kwa kiasi kikubwa kutofautiana na ile ya china, kama kwao wanafanya hivyo ni sawa lakini kwa Tz si sehemu sahihi kwani kijiografia tayari sie tuko kwenye tanuru na hatuitaji tena kuchochewa kuni na mkaa
Tuiombee nchi yetu watanzania, asubuhi njema!