Huku Watanzania tunajisifu ujinga kila mtoto ajipambanie from scratch, kijana wa kisomali miaka 25 anasimamia malori 90 biashara iliyoanzishwa na babu

Huku Watanzania tunajisifu ujinga kila mtoto ajipambanie from scratch, kijana wa kisomali miaka 25 anasimamia malori 90 biashara iliyoanzishwa na babu

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Ubinafsi wa wabantu umekita mizizi mpaka kwenye familia, Baba kapambana kuwa na biashara iliyofanikiwa lakini hashirikishi watoto, akifariki familia haijui lolote kuhusu biashara, umasikini unaanza kuinyemelea familia.

Nimeicheki hii interview ya kijana wa miaka 25, Abdullah Mahmoud

1736171201076.png

Ni boss wa kampuni ya malori 90 yanayosafirisha mafuta Zambia, Congo, Rwanda, n.k.

Yeye ni kizazi cha tatu cha biashara ya familia, biashara ilianzishwa na babu yake, ikarithishwa kwa baba yake na sasa ni yeye kizazi cha tatu anaisimamia.

Alianza kuzoeshwa biashara ya familia akiwa na miaka 6 (sita), kufikia 20 tayari alikuwa kaiva, tayari ana ujuzi wa malori, anavijua vibali husika vya biashara na kujifunza nidhamu ya fedha kwa kujionea jinsi pesa inavyotafutwa.

Inasikitisha kuona waafrika hasa hii asili ya wabantu bado tupo na huu ujinga wa kila mtu ajitafute kivyake, halafu tumekuwa brainwashed na huu utamaduni wa kumuona mtu alierithishwa biashara sio chochote, tunamsifu yule aliejipambana kutoka sifuri, tunapenda kuona mtu aliefanikiwa kwa kupitia mikiki na msoto.

 
Ubinafsi wa wabantu umekita mizizi mpaka kwenye familia, Baba kapambana kuwa na biashara iliyofanikiwa lakini hashirikishi watoto, akifariki watoto hawajui lolot ekwenye biashara, aibu za kufirisika zinaanza...
Shida ni akili zetu tu, tafuta nyuzi huku jukwaani watu wakitoa ushuhuda namna walivyoteketeza mali za urithi kwa kutumbua starehe na totoz na pombe. Nadhani matumizi mabaya ya hizi mali ndio sababu madingi wanawatoa watoto patupu ili watafute zao na hivyo wawe na uchungu na hizo mali.
 
Uchoyo ndiyo jadi yetu
Tunapata ajali ndugu wanatapanya Mali... watoto wanagawiwa kwa ndugu wawalee kwa mateso na masimango
"Baba yako alikuwa na pesa sana lakini hakututazama sisi na wanetu..
Impact of extended family
 
Mtu mweusi usithubutu kumuandalia Mali .

Wewe msomeshe sehemu yoyote hata Jamaica mpeleke.

Kuna watu wamejaribu wameshindwa na kupata hasara.

Mimi Baba Mkubwa wangu Alifanikiwa kupata hela na kufungua kampuni ya kuuza spare za magari na vipuri Ila alichoambulia ni hasara kubwa.

MTU mweusi kaumbwa kuongozwa na sio kuongoza
 
Nimeicheki hii inyerview ya kijana wa miaka 25, Abdullah Mahmoud

Na ni mtanzania kasomeshwa hadi Marekani kisha kaamua kurudi nyumbani Tanzania kushiriki kuendesha kampuni ya familia.

Hongera sana kjana mtanzania na familia kwa kuonesha mifano mizuri. Jamii zetu zingine za kiTanzania watasema ooh kijana badala ya kwenda kuanzisha biashara zake anavizia urithi.

Baadhi ya waTanzania Wanasahau urithi unaweza kuwa majumba, malori, boti za uvuvi, mifugo n.k Lakini utajiri huo hatuuoni tunataka vijana tujiajiri badala ya kushirikishwa katika shughuli za kiuchumi za familia zisonge mbele kizazi hadi kizazi.
 
Shida ni akili zetu tu, tafuta nyuzi huku jukwaani watu wakitoa ushuhuda namna walivyoteketeza mali za urithi kwa kutumbua starehe na totoz na pombe. Nadhani matumizi mabaya ya hizi mali ndio sababu madingi wanawatoa watoto patupu ili watafute zao na hivyo wawe na uchungu na hizo mali.
Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo

Kama mtoto humfunzi nidhamu ya pesa, akiachiwa mali nyingi za urithi atazitapanya.

Wenzetu wanashirikishwa tangu umri mdogo kujionea jinsi pesa inavyotafutwa kwa shida.
 
Back
Top Bottom