Huku Watanzania tunajisifu ujinga kila mtoto ajipambanie from scratch, kijana wa kisomali miaka 25 anasimamia malori 90 biashara iliyoanzishwa na babu

Pombe, ngono, starehe
 
Hapa Tz, wazazi hawaandai chochote kwaajiri ya watoto. Urithi wako ni elimu bwashee!
Elimu inatosha kama wazaz ni maskinii utakiwi ku complain kuhusu wazaz wako jaribu na wew kutengeneza utajiri ukiweza sawa ukishindwa sawa watoto wako pia watakulaumu pia
 
Yani mmenikumbusha mjomba wangu alipogeuka " Uncle" ghafla kupitia pensheni ya bibi alitumbua mali hata ukimpa tabasamu tu anakupiga elfu kumi, kuchukua costa nzima mkalewe na kesho yake mnapigwa supu kawaida sasa hivi hali yake mpaka huruma karudi kuwa mjomba
 
Hahaha
 
Waafrika hasa wabantu tuache ubinafsi, wazazi waandae watoto kusimamia biashara
Unazungumzia wote au baadhi?
Mbona watoto wa Mengi (kwa mfano) wanaendesha biashara alizoacha baba ,yao?
 
Sisi NI masikini mideset zetu NI umaskini...manji alikabidhi biashara kwa mwanae alipofikisha imri wa 40+ sisi Sasa mtoto akifika 20 anataka agaiwe uridhi na mzazi hataki kumpa wakti mzazi akimtumikisha mtoto kwenye shughuli zake alisema nawatafutia nyinyi...wanapokuwa anawaambia kila MTU atafute vya kwake...kizingumkuti kinaanzia hapo...mzazi mtoto akikaa kwake MDA mrefu anamfukuza anaona anamwibia au kumnyonya...
 
Deep sana hii.
 
Kwa hiyo Nini kifanyike kuondo mindset hii mbovu?

Kusema wanaume waombes kuishi umri mrefu, Hilo ni jambo la bahati na sibu sana hasa Kwa kizazi Cha wanawake mliopo Sasa.
 
Kwa hiyo Nini kifanyike kuondo mindset hii mbovu?

Kusema wanaume waombes kuishi umri mrefu, Hilo ni jambo la bahati na sibu sana hasa Kwa kizazi Cha wanawake mliopo Sasa.
Basi,tuishi humo
 
Hicho ndio kitu kinatufanya tuanze mwanzo kila siku muda ambao race zingine zinaendelea walipo ishia wazazi wao
.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…