Huku Zanzibar kuna mambo ya ajabu sana

Huku Zanzibar kuna mambo ya ajabu sana

Wabongo watu wa ajabu sana, badala ya kuwashangaa Wasukuma na kiswahili chao cha ajabu ajabu(maana hata hawajui matumizi ya R na L) eti wanataka kusema Zanzibar hawajui kiwahili! Aguju!!! Kwa taarifa tu kule kiswahili ndio lugha mama. Kama mtu ataongea lugha nyingine basi hiyo ni yakujifunza
Kwahiyo ninyi hamna lugha za makabila?
 
Sardine sio dagaa mchele chief.
Dagaa mchele kule wanaitwa - tonge kwa tonge!
Haha kuna soko fulani nilipita mkoa fulani nikasikia horn speaker ikinadi dagaa moja wapo ni hiyo tonge kwa tonge, sikujua wanamaanisha aina ya dagaa.
 
Huko ndio kwenye kiswahili sio kwenye mnakomix R na L
Yaani mtu hata R.I.P wanaandika L.I.P
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji377][emoji377][emoji377][emoji2445][emoji2445][emoji2445]
Lakini mbona nimewasikia wa zanzibar wanaomix pia R na L?
 
Kabisa yani. Imagine pale mjini tu kuna vitu hauelewi halafu unaambiwa bora wa mjini kule shamba ndiyo kabisa hauelewi kitu.
Sidhani kama hicho wanachoongea huko vijijini ni kiswahili, huenda ndio kikabila Chao kilichopapaswa kidogo na misamiati ya kiswahili.
 
Kwasababu huko ndiko wanapoongea kiswahili, mixer lahaja, mixer krioli mixer isimu, mixer tamathali za semi. Sasa wasiojua kiswahili wataelewa vipi?!
Hiyo sio standard swahili, sababu hata mengi ya maneno yao hayapo kwenye dictionary, halafu nani kasema zanzibar ndio yenye mandate ya kuclaim lugha ya kiswahili? Yapo maneno kibao toka kwenye lugha zetu za makabila zipo kwenye kiswahili.
 
-Hela zinatwa PESA

-Nyanya zinaitwa TUNGULE

-Watu watokao bara wote wanaitwa WANYAMWEZI

-Umeme huku haukatwi isipokuwa UNAZIMWA

-Mvua huku hainyeshi bali INAKUNYA

-Viazi vinaitwa MBATATA

-Daftari linaitwa BUKU

-Kalamu inaitwa PENI.....nk,nk,nk,

Tanganyika na Zanzibar ni nchi mbilitafauti,Lugha,mila,desturi na Utamaduni tafauti

If you don't know now you know

Fanya haraka uondoke Kabla hawaja Ku......
Itapendeza sana siku Muungano unavunjika sababu naona mnatulemea sana, Zanzibar ni kaeneo kadogo sana lakini uwakilishi wake hauakisi ukubwa wake geographically, hizo gharama za kuwahudumia ni kodi zetu, fikiria idadi yenu pale bungeni na kwenye taasisi za Muungano tunaenda sambamba wakati watu wa tatu tu wangetosha kukiwakilisha kaeneo kenu.
 
Siwezi kuchukia ujinga, ila ni vizuri kama kitu hujui uliza. Mfano mzuri neno mchamba wimba, angalia kwenye post zake alivyolidadavua, je ndivyo ilivyokuwa hadi kupatikana kwa jina la eneo hilo?
Kwani we nani mpaka tafsiri yako tuiamini yake tuikatae? Kuna kipi cha tofauti labda hapo? Sababu naona wote ni wanaJF tu hamna cha ziada, yeye pia anauwezo wa kusema wewe ndio mpotoshaji na tikamuamini.
 
Hivi wanaongea kikabila hao?
Nilimsikia mtu akisema hawana makabila ila pia nilisikia history kwamba wote hao wametokea bara haswa Mtwara na Lindi lakini Ukiwasikia lugha wanayo ongea huko vijijini sio standard swahili kilichopo kwenye dictionary

Nipo interested kuwajua zaidi.
 
Itapendeza sana siku Muungano unavunjika sababu naona mnatulemea sana, Zanzibar ni kaeneo kadogo sana lakini uwakilishi wake hauakisi ukubwa wake geographically, hizo gharama za kuwahudumia ni kodi zetu, fikiria idadi yenu pale bungeni na kwenye taasisi za Muungano tunaenda sambamba wakati watu wa tatu tu wangetosha kukiwakilisha kaeneo kenu.

mara zote wanodai kuvunjika muungano huwa na maslahi yao nje ya wananchi wa zanzibar.

raia wa kawaida ukimwambia muungano uvunjike,anakushangaa.anagalia walivyojaa kkoo,ilala nk kote huko wanafanya biashara zao kama nyumbani.
 
Back
Top Bottom