Well said!
Kusema fulani anacopy bila kusema ancopy wapi ni unafki na inaprove vile mtu anaweza kua first class hater for no reason!
By the way, uandishi unahitaji research ambapo research ni lazima ihusishe literature review ili ujue waandishi wengine walisemaje kuhusu topic unayoiandikia!
Watanzania tunapenda mafanikio, ila tunawachukia waliofanikiwa!
Peace be upon you!
Kaka upo sahihi kabisa na wewe ni mtu wa pili nakuunga mkono hoja.
Katika uandishi pia kuna kuchunga amana kama ilivyo kuchunga amana katika mambo mengine.
Uandishi umegawanyika. Kuna uandishi wa kubuni na kuna ule ambao ni kinyume chake uandishi huu wa pili ni uandishi wa kielimu uandishi wa ukweli,uadilifu na haki,uandishi huu unahitaji umakini sana na kuchunga kutokuwadhulumu watu haki zao.
Hakuna jipya sana katika uandishi hasa huu wa pili,ku nakili hakuepukiki sababu sisi tunasoma kwa wale walio tutangulia na sisis si wa mwanzo. Cha msingi unapo nakili jambo au kauli kutoka sehemu fulani,lazima itoe marejeo ya wapi ulipotoa maandishi au nukuu hiyo au hata kuashiria huku ndio kuchunga amana za watu.