Humphrey Polepole: Mambo ya machifu hayana msaada kwa taifa, yanaweza kuleta ukabila na mgawanyiko, yanapaswa kupingwa

Humphrey Polepole: Mambo ya machifu hayana msaada kwa taifa, yanaweza kuleta ukabila na mgawanyiko, yanapaswa kupingwa

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Humphrey Polepole amesema kuwa

"Mambo ya Machifu yanatusaidia nini kama taifa?nasema jambo hili sio jema,naliona linadhoofisha Utanzania wetu,likiendelea bila kukemewa litaibua tuliyoyazika ya hisia za ukabila, usisi na uwao, Mwalimu Nyerere aliona mbali kukataa haya mambo kwani yataligawa taifa"

"Yapo maeneo uchifu ulishaondoka,haupo. Tulishakubaliana uchifu ni ukoo wenu, mna kiongozi wa ukoo mnazungumza mambo yenu binafsi ya kifamilia leo serikali ikizungumzia uchifu hawa nao wataomba kiongozi wao (wa ukoo) atambulike na apate nafasi huko serikalini"

"Mwalimu Nyerere alikataa jambo hili (uchifu), lina faida gani. Uchifu unataka kutuibulia zile hisia kwamba tuna ukabila kama hakuna wazee wataliona hili jambo, basi mawe yataona"

"Nchi yetu ina wakristo na waislamu, ikitokea mvua imechelewa kiongozi wa serikali huwa anawaomba wakristo kanisani wakaombe na waislamu msikitini wakaombe mvue zinyeshe, lakini huwezi kusikia kiongozi wa serikali akiwaomba washirikina eti wafanye namna mvua inyeshe"

"Kwenye shughuli za serikali ushawahi kuona tunawaita wanaoabudu miti waje kuomba kabla ya shughuli? sasa uchifu wa nini?. Hawa machifu walishafutwa kisheria, tunapowarudisha tunapanda nini?"

"Nenda pale Kilimanjaro, utasema Mareale ndio chifu wao, hapana wako wengi. Kwa hiyo nao wafanye uchaguzi kisha waje kumpata chifu wao wa wote. Kweli tunaenda hivi katika maendeleo"


IMG_20220202_081110.jpg
 
Huyu jamaa ni boya sana ana very low IQ.

Ni fact ya wazi kwamba ma-chief walikuwepo kabla ya Tanzania na bado wapo. Hatuwezi kukataa ukweli kwa uoga wa mambo tusiyoyajua. Iko bayana relevance yao sasa ipo kwenye kuifadhi na kudumisha mila na tamaduni zetu nzuri.
 
Hivi Tanzania mtu pekee aliyekuwa na akili timamu ni mwalimu pekee?
Hua nashangaa sana wao muona kama malaika kwanza sera zake za ujamaa zimeharibu sana hili taifa kutuletea katiba ya hovyo iliyozaa wanafiki na kujipendekeza iliyoleta mzigo katika nchi uliona wapi muungano wa serikali 2 moja ikiwa kupe.

Kimsingi alifanya mazuri ila kuna mengi pia alifeli sana.

Ndio maana aliacha nchi ipo hohehahe.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa ni boya sana ana very low IQ.

Ni fact ya wazi kwamba ma-chief walikuwepo kabla ya Tanzania na bado wapo. Hatuwezi kukataa ukweli kwa uoga wa mambo tusiyoyajua. Iko bayana relevance yao sasa ipo kwenye kuifadhi na kudumisha mila na tamaduni zetu nzuri.
Chief anachaguliwa au Anateuliwa na Nani?
 
Hua nashangaa sana wao muona kama malaika kwanza sera zake za ujamaa zimeharibu sana hili taifa..kutuletea katiba ya hovyo..iliyozaa wanafiki na kujipendekeza..iliyoleta mzigo katika nchi uliona wapi muungano wa serikali 2..moja ikiwa kupe.

Kimsingi alifanya mazuri ila kuna mengi pia alifeli sana.

Ndio maana aliacha nchi ipo hohehahe.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani huwa sielewi wanaomsifu kumbe kaacha nyumba za tembe tupu
 
Mlipandikiza sasa huko Arusha Mkoani wameongeza na UDINI .....

Mwenye USUKANI kiongozi pale juu hasikilizwi....
 
Back
Top Bottom