Humphrey polepole na King msukuma figisu zenu za kumhujumu Rais Samia hazitawafikisha popote

Humphrey polepole na King msukuma figisu zenu za kumhujumu Rais Samia hazitawafikisha popote

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Humphrey polepole na King msukuma hakuna asiyejua kuwa nyie ni miongoni mwa waliokuwa wanufaika wakuu wa utawala wa hayati Magufuli.

Ni katika kipindi hicho ambapo vijana tulipokuwa tukihoji masuala ya ajira mnatukebehi kwa maneno yaliyojaa kejeli na dharau kubwa

Nakumbuka wakati humphrey polepole ukiwa bado ni katibu mwenezi ulipoulizwa kuhusu suala la ajira ulisema serikali haiwezi kufanya kazi ya kuajiri tu hivyo vijana wajiajiri hata kwa kulima matikiti na nyanya.

Jambo la kushangaza baada ya Rais Samia kuingia madarakani ukapokonywa ukatibu mwenezi badala ya kujiajiri kwenye kilimo cha matikiti kama ulivyohamasisha vijana, unafanya harakati za kumpinga mheshimiwa Rais kwa sababu ya uchu wako wa madaraka. Mbaya zaidi vijana wale wale uliowaambia wajiajiri kwenye kilimo cha nyanya na matikiti ndio hao hao unataka wakuunge mkono kwenye hizo harakati zako uchwara za kumpinga Rais Samia. Je, unafikiri hili litawezekana au unapoteza muda wako bure tu?

Tukirudi kwa King Msukuma, huyu mara zote amekuwa ni adui wa wasomi hakuna asiyejua. kipindi chote cha hayati magufuli, Msukuma alikuwa na kazi ya kutukana wasomi tu hasa vijana walipokuwa wakiiomba serikali iwaajiri.

Lakini juzi kwenye sakata la RC Makalla na machinga, Msukuma huyu huyu anayetukana na kudharau wasomi anatoka na kujifanya kana kwamba anawatetea vijana wenye digrii waliojiajiri kwenye umachinga. Hapa ndipo najiuliza, hii huruma anayoionyesha Msukuma kwa vijana imeanza lini?. Sio unafiki huu?. Mbona wakati wa magufuli hakuwatetea zaidi ya kuwatukana na kuwafedhehesha?..

Hata hivyo vijana wanajitambua, hivyo humphrey na king msukuma kama mnafikiri mnaweza kuwatumia vijana hawa hawa mliowadhalilisha kipindi cha awamu ya tano kama madaraja ya kufanikisha maslahi yenu binafsi ya uchu wa madaraka kwa kumkwamisha na kumfitinisha Rais Samia tambueni kwamba mnapoteza muda wenu bure kwani hakuna kijana mwenye akili timilifu atawaunga mkono. Hivyo basi, kubalini kwamba zama zenu za kula mema ya nchi zimeshapita, mwacheni Rais afanye kazi yake maana fitina zenu kwake hazitawafikisha popote.
 
Kuna vitu huvijui ndio maana umeangalia harakati zao kwa upande mmoja ukafika hitimisho,

Kijana mwenzetu, hii nchi ni ngumu (ina hardness level sawa na diamond).

Ilipaswa uwaunge mkono.
 
Karibu kwenye darasa la uongozi kila jumamosi, upate maarifa ya ya kumshauri mama yako kipenzi namna Bora ya kuliongoza Taifa letu.

Usipuuze, huyo mama Naye anafuatilia kwa makini Sana ila naamini kwa huu Uzi wako inaonesha dhahiri nawe ni mfuatiliaji mzuri wa darasa la uongozi ndugu yetu komredi Humphrey Polepole
 
Vyote ongeeni ila Pole pole ni Kinyonga wa hali hali ya juu sana. Take reference Kwenye katiba mpya nyakat zile.pili Angalieni Siasa chafu ya kununua wanasiasa!!

HUYU MTU WENGINE TULISHAMPUUZA KITAMBO..NI NJAA HUA ZNAONGEA SIO yeyeee!!Mama apige kazi kadri ya utashi wake mana niwakati wake!!
 
Mbona wakati wa magufuli alikuwa kimya hatukusikia akitoa mawazo hayo mawazo tofauti au kwakuwa alikuwa anatembelea V8?
Whether alikua kimia ama alisema haimzuii yeye kusema.

Wewe sikiliza ujumbe, achana na mambo mengine.
 
Duuuh kila mwenye mawazo chanya ni mfitini Basi poa acha tukae kimya
Polepole na msukuma hawana mawazo chanya yoyote. Zaidi, wanatumiwa na genge fulani kwa minajiri ya kusaka madaraka ya kiti cha Urais kwa kupandikiza chuki kwa wananchi dhidi ya Rais Samia na bahati nzuri wote wanaowatuma na genge lao tunawafahamu
 
Kuna vitu huvijui ndio maana umeangalia harakati zao kwa upande mmoja ukafika hitimisho,

Kijana mwenzetu, hii nchi ni ngumu (ina hardness level sawa na diamond).

Ilipaswa uwaunge mkono.
Niunge mkono uhaini?

Nop! I can't do that
 
Kwa bahati mbaya ccm wote hawana ushawishi kwa umma, hiyo vita yao ya madaraka watamalizana wenyewe, lakini hawana ushawishi wowote kwa umma. Sio msukuma na Polepole, wala huyo mama Samia.
tu huLvijui ndio maana umeangalia harakati zao kwa upande mmoja ukafika hitimisho,

Kijana mwenzetu, hii nchi ni ngumu (ina hardness level sawa na diamond).

Ilipaswa uwaunge mkono.
 
Kwa hiyo wanaotakiwa kuongea kwa sasa ni kina nani, tuwekeeni orodha mpya ya waongeaji tuanze kuwasikiliza hao maana hata mwanaharakati huru siku hizi simsikii tena.......
 
Wazo chanya kutoka kwa msukuma?!
NB:samahani kama nitakukwaza.
Pengine huyo msukuma ni bora sana kuliko wewe unae jiona mjuaji wakati umejificha nyuma ya kibodi.
huyo unae mdharau kumbuka ana nafasi kwenye bunge la jamuhuri., na anashiriki kutengeneza sheria na utazifuata tu utake ustake, mfamo tozo.
sidhani kama ni ujanja kumdharau mtu anae fahamika na jamii na pengine anakuzidi kila kitu.
 
Mbona wakati wa magufuli alikuwa kimya hatukusikia akitoa mawazo hayo mawazo tofauti au kwakuwa alikuwa anatembelea V8?

Sasa hapa ndio ujiulizwe vizuri kwanini sasa na sio wakati ule...

Hakikisha unatengeneza hoja(majibu) zaidi ya moja arafu kwenye hizo hoja chagua hoja(jibu) moja iliyo sahihi zaidi, using'ang'anie upande mmoja.

Niunge mkono uhaini?

Nop! I can't do that
 
Back
Top Bottom