Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
HUMPHREY POLEPOLE UPEPO WA KISASI UNAKUANDAMA. CHUNGA SANA. MUNGU ANAKULIPA.
Kwa Mkono wa Robert Heriel
Kisasi kisasi! Ni Jambo la hatari ambalo linaweza kuzuilika lakini ni ngumu kuzuilika.
Miaka kadhaa iliyopita wakati wengine wakifungwa midomo wasiikosoe serikali Ndugu yangu POLEPOLE alikuwa kimya, Hakuwa anapiga kelele Kwa sababu alikuwa sehemu ya Mfumo. Kama POLEPOLE angekuwa Mpenzi na Muumini wa Haki basi hizi kelele zake tungezisikia tangu awamu ya tano ambapo hakuna ubishi kuwa ilikuwa awamu iliyogubikwa na kuziba watu midomo.
Kama POLEPOLE angekuwa mkweli hivi leo kila mtu angeungana na yeye kuwa ni mwenye Haki kwani Hana Double Standard. Lakini POLEPOLE sio mwenye Haki, sio msema kweli Kama anavyojitanabaisha mbele ya Kamera.
Unajua hata watu Wabaya wanajua Fulani ni mwenye Haki Mwema.
Lakini ukishakuwa Double Standard hata waovu wanaona kuwa wewe ni Muovu Kama wao tuu. Hivyo hawaoni shida kukufanyia Uovu wao.
Kinachomtesa Polepole kwa sasa ni UPEPO mbaya wa kisasi unaozunguka katika mfumo wake wa maisha.
Ninachomuomba awe mjanja, awe makini ikiwezekana atambue kuwa kinachotaka kutokea ni muda wa malipizi.
Wakati miaka iliyopita walioikosoa serikali wakivamiwa na watu wasiojulikana, wakitekwa huku wengine wakipotea kusikojulikana mpaka hivi leo, POLEPOLE hakuwahi kusema kitu, Hakuwa kupinga Uovu huo. Aliona ni SAWA,
Leo anashangaa, anabweka anapozuiwa kuongea, anapozibwa mdomo asiongee mawazo yake. Polepole hapa unachokitafuta hukijui; kuna kisasi kinakutafuta ulipwe Sawasawa na Wale waliofanyiwa wakati ule ukiwa sehemu ya utawala upande wa CCM.
Ujasiri ulionao usiizidi Akili yako, huo ujasiri lazima ujue chimbuko lake ni lipi hasa, je mi ujasiri utokanao na HAKI? Hilo nalipinga Kwa sababu nilishasema kuwa ungekuwa mtu wa haki ungepinga tangu awamu ya tano.
Je, mi ujasiri utokanao na KISASI kinachokutafuta kukuangamiza ili uwe fundisho Kwa kizazi hiki na kijacho? Jibu ni ndio.
Hao wanaokuambia ukae kimya wanakuona unawakosea Kwa sababu mbona wakati wa awamu ya tano hukuwahi kuipinga SERIKALI wala kuikosoa?
Kimsingi wanayohoja alafu wewe hauna hoja ya kuwaelewesha kuwa iweje awamu ya tano iliyojaa ukandamizaji wa Uhuru wa kutoa maoni ulikaa kimya alafu leo hii kujifanya unaongea.
Hoja zako hazijibiwi Kwa sababu hawaoni sababu ya kukujibu na hawaoni kuwa hoja hizo unastahili kuzianzisha wewe mnafiki uliyenyamaza awamu ya tano.
Hata ningekuwa Mimi nisikubali nikujibu hoja zako na wala nisingekuruhusu uzitoe.
Yaani wakati unakunywa Castle Lite ulikaa kimya kusema ni pombe. Alafu Mimi wakati wangu nikinywa Serengeti unanyanyua mdomo wako kuwa niache kunywa pombe wakati hata Castle Lite nayo ni pombe labda kiwango tuu cha ulevi kilichopo.
Mwisho; jichunge Sana, ujasiri ulionao ni matokeo ya kisasi kinachokutafuta kukuangamiza ili kuwalipia wale walioumizwa wakati ule wewe ukiwa kiongozi.
Ni Yule Mtibeli
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa Mkono wa Robert Heriel
Kisasi kisasi! Ni Jambo la hatari ambalo linaweza kuzuilika lakini ni ngumu kuzuilika.
Miaka kadhaa iliyopita wakati wengine wakifungwa midomo wasiikosoe serikali Ndugu yangu POLEPOLE alikuwa kimya, Hakuwa anapiga kelele Kwa sababu alikuwa sehemu ya Mfumo. Kama POLEPOLE angekuwa Mpenzi na Muumini wa Haki basi hizi kelele zake tungezisikia tangu awamu ya tano ambapo hakuna ubishi kuwa ilikuwa awamu iliyogubikwa na kuziba watu midomo.
Kama POLEPOLE angekuwa mkweli hivi leo kila mtu angeungana na yeye kuwa ni mwenye Haki kwani Hana Double Standard. Lakini POLEPOLE sio mwenye Haki, sio msema kweli Kama anavyojitanabaisha mbele ya Kamera.
Unajua hata watu Wabaya wanajua Fulani ni mwenye Haki Mwema.
Lakini ukishakuwa Double Standard hata waovu wanaona kuwa wewe ni Muovu Kama wao tuu. Hivyo hawaoni shida kukufanyia Uovu wao.
Kinachomtesa Polepole kwa sasa ni UPEPO mbaya wa kisasi unaozunguka katika mfumo wake wa maisha.
Ninachomuomba awe mjanja, awe makini ikiwezekana atambue kuwa kinachotaka kutokea ni muda wa malipizi.
Wakati miaka iliyopita walioikosoa serikali wakivamiwa na watu wasiojulikana, wakitekwa huku wengine wakipotea kusikojulikana mpaka hivi leo, POLEPOLE hakuwahi kusema kitu, Hakuwa kupinga Uovu huo. Aliona ni SAWA,
Leo anashangaa, anabweka anapozuiwa kuongea, anapozibwa mdomo asiongee mawazo yake. Polepole hapa unachokitafuta hukijui; kuna kisasi kinakutafuta ulipwe Sawasawa na Wale waliofanyiwa wakati ule ukiwa sehemu ya utawala upande wa CCM.
Ujasiri ulionao usiizidi Akili yako, huo ujasiri lazima ujue chimbuko lake ni lipi hasa, je mi ujasiri utokanao na HAKI? Hilo nalipinga Kwa sababu nilishasema kuwa ungekuwa mtu wa haki ungepinga tangu awamu ya tano.
Je, mi ujasiri utokanao na KISASI kinachokutafuta kukuangamiza ili uwe fundisho Kwa kizazi hiki na kijacho? Jibu ni ndio.
Hao wanaokuambia ukae kimya wanakuona unawakosea Kwa sababu mbona wakati wa awamu ya tano hukuwahi kuipinga SERIKALI wala kuikosoa?
Kimsingi wanayohoja alafu wewe hauna hoja ya kuwaelewesha kuwa iweje awamu ya tano iliyojaa ukandamizaji wa Uhuru wa kutoa maoni ulikaa kimya alafu leo hii kujifanya unaongea.
Hoja zako hazijibiwi Kwa sababu hawaoni sababu ya kukujibu na hawaoni kuwa hoja hizo unastahili kuzianzisha wewe mnafiki uliyenyamaza awamu ya tano.
Hata ningekuwa Mimi nisikubali nikujibu hoja zako na wala nisingekuruhusu uzitoe.
Yaani wakati unakunywa Castle Lite ulikaa kimya kusema ni pombe. Alafu Mimi wakati wangu nikinywa Serengeti unanyanyua mdomo wako kuwa niache kunywa pombe wakati hata Castle Lite nayo ni pombe labda kiwango tuu cha ulevi kilichopo.
Mwisho; jichunge Sana, ujasiri ulionao ni matokeo ya kisasi kinachokutafuta kukuangamiza ili kuwalipia wale walioumizwa wakati ule wewe ukiwa kiongozi.
Ni Yule Mtibeli
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam