Huu mwaka 2023 kuna watu bado wanamsikiliza Issa Shivji?

Umesema vitu jumuishi bila kurejea vifungu alizosema Shivji...wewe utakuwa mnufaika wa DPW
Kakopi sehemu hilo andiko, nimesoma kwa paragraph kadhaa sioni mahali anaandika kuainisha mjadara wa Prof. Shivji.

Although kapewa au kakopi aweke hapa JF.
 
Haya, kuanzia na 1 hadi 3, fafanua sababu za kubinafsisha na faida au hasara za kufanya hivyo ili niendelee kuwa kwenye jahazi lako la fikra
Mbona THE BOSS ameelewa na kujibu mkuu,. Jiongeze wewe, mimi nimesema wewe zikubali au zikate kwa maelezo ujuayo.
 
Kak Huna taarifa kuwa ktk kitabu Cha mkapa binafsi alikiri kuwa alifanya makosa ktk ubinafisishaji wa mashirika ya umma leo umekuja Tena unataka bandari apewe muarabu
 
Hayo anayojutia Mkapa kwenye kitabu chake haudhani kwamba we're repeating he same mistakes? Kwamba kwa huu uwekezaji Samia in the near future hawezi kuja na same stories?
Mkuu mimi sio mwanasheria ila Nina uzoefu na Bandari kwenye kampuni Binafsi, hata zilipokuja Habari za Ticts kuondolewa hata kabla ya mambo ya Dpworld kuja nilishauri watafute mtu mwengine mbadala wa Ticts.

Bandari sio madini kwamba utaibiwa ama Bandari itaisha, uendeshaji wake ni wa Ki pekee. Leo Dp akija akachimba kina kirefu cha bandari siku wakiondoka hawezi kuondoka na Kina chake ataacha vile vile, akijenga miundombinu vile vile.

Bandari Wakusanya mapato ni wale wale Tra, Dp haji kukusanya mapato,

Na Dp kwa interest zao ili wapate mapato zaidi inabidi meli nyingi zaidi zije, zipakuliwe haraka zaidi, Jinsi makontena mengi yanavyopita kwao ndio jinsi watakavyopata hela nyingi, hii interest yao inakuwa neema pia kwetu jinsi makontena mengi yatakavyopita ndio jinsi Ushuru mwingi na kodi utakavyokusanywa.

Turudi kwa Mkapa Alichojutia kikubwa kwenye Kitabu chake ni Hicho wawekezaji kung'oa miundombinu ya viwanda ama Uwekezaji wao na kwenda kutumia kwa maslahi yao Binafsi badala ya maslahi ya Taifa kwa ujumla, Hebu tu relate kwa Dp world, Wakija Kuna Risk ya kutoa crane zetu kuu kuu na kuziiba? Ama wataleta zao za Kisasa?

Kwanini tunawaogopa? Kama ni Bandari ilibinafaishwa toka mwaka 2000 kwa Ticts kampuni ya kina Karamagi, kuna nini Dp world Wakija wataharibu na Ticts walikua wakifanya Vyema?
 
Hii ID ya mwanzisha mada imegeuka kituko sana. Ni moja ya ID iliyokuwa inaheshimika sana kumbe issues huwa ni ugali tu sio uzalendo.
 
TimuYaWananchi!watu 10 out of 60 milioni raia.

10/60000000=1/6000000=0.0000166666%.

Ni ujinga kuamini kwamba watu asilimia 0.00001667 ya raia wote,ndiyo watushawishi kukataa makubaliano ya uwekezaji yaliyopitishwa na raia takribani asilimia 99.9999 huko,wakiwakilishwa na wabunge na serikali yao!?.
Endeleeni kupiga kelele za chura.
 
Kwa hiyo mtoa mada unashauri tumsikilize/tuwasikilize akina nani? Tuwasikilize akina Joseph Kasheku Msukuma, au!!!!

Majibu tafadhali.
Msikilize Msukuma!Msukuma ana akili kuliko hao waliojaza vichwani vya kukariri darasani.
Einstein alitafasiri Akili kuwa"Nikile kinachobaki kichwani baada ya kuondoa yote uliyoingiziwa darasani".
 
[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Hii ID ya mwanzisha mada imegeuka kituko sana. Ni moja ya ID iliyokuwa inaheshimika sana kumbe issues huwa ni ugali tu sio uzalendo.
Mjibu tu hoja zake... Hayo mengine sio pahala pake hapa...,😊
 
Unajishushia heshima
Anajishushia heshima kwa kuwakosoa nyinyi mafisadi? Mbona hamjibu hoja za terms za mkataba ambazo huyo mama amesaini hata bila kuzielewa? Nobody is against private investments ,it is the terms of their investments that the Wananchi are questioning. Ni ujinga ulioje kumpa muwekezaji mkataba usiokuwa na ukomo ; na ujinga huu hauhusianai na dini ya mtu bali ni mapungufu ya mtu husika!
 
Chawa wa mama bwana, Sisi tunataka ujadili issues na siyo mtu
 
wasiomsikiliza shivji ni watu ambao ubongo wao upo kwenye masaburi tu. kwa mtu mwenye akili timamu anajua kuwa anachoongea shivji ni cha faida kwa taifa na yeye hana maslahi yeyote kama watetezi walivyo.

Mkapa hakuwa sahihi to ignore Shivji kwasababu baadae, baada ya Kustaafu alikili kuwa alifanya makasa jinsi alivyotekeleza sera ya ubinafsishaji!!! Hao wakina Rostam walinunua viwanda vya ngozi kwa bei ya che ambavyo baadae hawakuviendeleza kama mikataba ilivyotaka wafanye; leo wanasimama kutetea uwekezaji wa masharti ya kijinga ili wanufaike tena!!
 
Chawa wa mama bwana, Sisi tunataka ujadili issues na siyo mtu
Huyu sio Boss ninaemfahamu humu siku nyingi unless his ID has been hacked ; he is not the one to advance such shallow arguments!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
team makasuku wanahaha wamefika hatua hadi kama wanaona aibu kuendelea

imagine darasa la 7 b wanashindana na maprofesa..... wataweza kweli?????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…