Huu Mwaka nimekutana na Mwanamke wa ajabu sana. Hii dunia tuwe makini

Huu Mwaka nimekutana na Mwanamke wa ajabu sana. Hii dunia tuwe makini

Kila mwanaume anakutana na mwanamke wa ajabu Maishani mwake..

huyo ni Clasic. Na ashajua uko vyema.
Na anakulia timing. Sasa Ww subiria tu, kizinga chake ni 50+ Mill huko, ndio utaona bora zile laki laki unazoombwa...

NB: mada hii chai ila ni angalizo tu kuwa sometimes mwanamke anakuvuta ujae then akupe jukumu zito
Ni chai kabisa mkuu
 
Ni swala la muda tu, lazima uchezee kizinga. Hakuna mwanamke asiyeomba pesa.
Tena kizinga kizito. Na atajisemesha “huyu hajawahi niomba hela na wakati mwingine hata mimi natumia zake, leo hadi ameniomba ni kweli ana shida. Ngoja nimpe”.
Hapo bidada anarudisha hela zake zote alizowahi kulipia bills na zinabaki hela nyingi tu.
 
Nakuelewa dada yangu. Najua KUPEANA NI KIKOA. lazima tupeane. Nachosema ukingalia malalamiko yangu kwenye nyuzi nyingi ni mianamke ile migugumaji ambayo ukijuana naye some days tu anaanza tangaza shida zake. Huyu nlianza na kuwa nampa zawadi ndogo ndogo kumwona reaction yake. Akawa anapokea kwa furaha na upendo akithamini. So zawadi nampa naye ananipa. Na kwa kweli sijampa za malakhi mengi. Sometimes nampelekea ice cream ya tsh 2000 tu nimwone atapokeaje...you know.
Mbona Ata bigbom wengine tunapokea mlipata tu wafanya biashara 😹😹
 
Haina haja ya salamu watu tupo busy.

Mwaka huu sehemu flani katika mizunguko yangu nilikutana na dada mmoja mzuri sana kwa sura na figure. actually nilikutana naye kwenye Dispensary yake yeye ni Daktari Hosp moja kubwa hapa nchini. kisha akafanikiwa kuanzisha Disp yake.

Ni mdada mrembo na kichwani ana kitu huyu akili anazo kumbuka ni dkt bingwa.

tukaanza urafiki na mimi cares kama zote mwishoo eeeeeh.... nikaanza tukionana tunakumbatiana, tunakisiana nakadhalika. bila kumwambia nampenda tumekuwa wapenzi. sikumtongoza wala nini... tumejikuta tu tumependana.

huyu dada alichonishangaza siku zote hizi. hajawahi kuniomba pesa wala fedha. yaani hapo ndo nikasema ngoja kwa kweli nidumu naye maana mwezi wa 3 huu hajaomba pesa. just imagine hajapatwa na shida ya kuhitaji pesa. si kawaida kwa wanawake wengi wa kisasa. huwa wakikuvumilia sana ni week. kinyume na hapo wanaanza kutanganza shida na matatizo yao. huyu hapana kwa kweli anajiamini ana tumia perfume ya ukweli hasa. zile za 600,000 mpaka million plus huko.

nikasema hii imenifundisha kitu sitaki kabisa mimi kudate wadada wenye njaa. huyu dada ana mapenzi ya dhati yaani nikimgusa tu anavyoshtuka shtuka.... nikimkumbatia kwa namna flani analegea kabisa. yaani yupo ......daaaaah sijui nisemeje. kwa kweli nimeona kila nikija kukaa tz nitakuwa na enjoy sana naye maana nilikuwa nakuwa bored sana nikija TZ na kuanza hangaika na Minunga yembe.

ushauri wangu vijana achaneni na wanawake wenye njaa. mtu unataka mahusiano siyo unataka kwenda hudumia njaa za mtu. siku mbili tatu tu...mama yake mgonjwa, ada imepungua, anaumwa typhoid, simu imeharibika, amefiwa, ana msongo wa mawazo sababu ya madeni n.k huyo achana naye. abaki na uchu wake na wewe ubaki na vitu vyako. utampata mwenye kufanana nawe kiakili.

huyu si mwanamke wa kawaida . toleo kama hili liliisha miaka mingi sana. sielewi imekuaje nimelipata toleo hili. nimeshangaa sana. najiuliza hivi ni kweli ama naota? miezi mitatu hajapata jambo la kuniombea pesa? na sometimes ananiita kunialika some places analipia bills? hili najua wanaume wengi litawaumiza hasa wanaoliwa pesa na kusema si sawa ,sijui mwanaume lazima uhonge. kuonga kwa nyoko. nenda zako misurupwete wewe. wewe honga sisi tule.unahitajika umakini dunia hii kupata mwanamke wa hivi. si mwanamke wa kawaida.
Inamaana umekuja kutusema sisi tunaokutana na madunga yembe😂😂dah hii imeniumiza sana
 
Back
Top Bottom