Huu ndio Mtihani kwa ACT-Wazalendo: Kukubali maridhiano na kuunda Serikali

Huu ndio Mtihani kwa ACT-Wazalendo: Kukubali maridhiano na kuunda Serikali

Raha ya kuwa mwanaccm, unaweza kumtukana au kumkashifu aliyekuzidi umri mradi yuko upinzani, maneno hayohayo akiyatoa upinzani yanakuwa matusi!
Mkuu elvischirwa , ujinga sio tusi ni hali, na kumuita mtu mjinga sio tusi. Tofauti kufanya ujinga na kumuita mtu mjinga. Mwaalimu Nyerere alitumia sana hili neno, mjinga, wajinga, ya kijinga, ujinga, etc. Ila pia naungana na wewe, inapotokea mtu amekuzidi umri, akafanya mambo ya kijinga, ni kweli sio ustaarabu kumtukana mjinga, na mimi sijamtukana mtu mjinga ila nimeuzungumzia ujinga uliofanyika.

Its very unfortunate, mimi ni mtu wa Nyerere, alikuwa hapendi ujinga, hivyo na mimi pia sipendi ujinga, na kuna ujinga mwingi nimekemea kwenye uchaguzi, japo mimi ni kada, lakini chama changu kikitufanyia ujinga tunakemea, ule uchaguzi mdogo wa Kinondoni kiukweli ulikuwa ni ujinga, sisi makada wazalendo tukakemea ujinga ule, 2020 chama chetu kikajirekebisha kikatuondolea ujinga ule
P
 
Kama Maalim Seif atakubali kuunda serikal ya Umoja wa kitaifa kwa matukio hovyo yaliyojitokeza basi Atakuwa nae ni Mchumia tumbo tu na kwa upande wang hakuna Mwanasiasa wa upinzani nitakayemuamin tena katika nchi ya TANZANIA kwan watakuwa wanatuyumbisha sisi wafuasi wao!.
 
Yes, tena ni ujinga mkubwa sana ambao mpaka leo, anaufidia.
P
Bro Mayalla unayumba haukuwa hivyo kabisa,nakufuatilia sana ww ni mwandish wa habar mzur sana na unajengaga hoja zur sana ktk kuleta maendelea ya nchi yetu,lakini tangu siku ile ulivyouliza swali zur na matata sana pale ikulu na ukajibiwa ndivyo sivyo mpaka leo sikusikii tena,umeamua kuegemea upande mmoja kwa maslah yako na familia yako!,any way sisi wote ni watanzania na tutaishi kwa woga kama wewe lakin ipo siku woga utaisha!
 
Kama Maalim seif atakubali kuunda serikal ya Umoja wa kitaifa kwa matukio hovyo yaliyojitokeza basi Atakuwa nae ni Mchumia tumbo tu na kwa upande wang hakuna Mwanasiasa wa upinzani nitakayemuamin tena katika nchi ya TANZANIA kwan watakuwa wanatuyumbisha sisi wafuasi wao!.
Sidhani kama Maalim na chama chake watakubali hili jambo, ikiwa tayari alishatoa kauli hii hapa...

"Uchaguzi ulitekwa na vyombo vya dola. Ikiwa kulikuwa hakuna uchaguzi vipi nitamkubali aliyetangazwa?, hakuwekwa madarakani na wananchi kama Katiba inavyotaka, amewekwa madarakani isivyo halali"
 
Hilo sahauni na halitatokea abadan abadan ,wala msilipigie chapua,ili mpate afweni yaguju,mnalo jiti ni mapambano kwa usiku na mchana kwa muda wa miaka mitano.
 
Mkuu elvischirwa , ujinga sio tusi ni hali, na kumuita mtu mjinga sio tusi. Tofauti kufanya ujinga na kumuita mtu mjinga. Mwaalimu Nyerere alitumia sana hili neno, mjinga, wajinga, ya kijinga, ujinga, etc. Ila pia naungana na wewe, inapotokea mtu amekuzidi umri, akafanya mambo ya kijinga, ni kweli sio ustaarabu kumtukana mjinga, na mimi sijamtukana mtu mjinga ila nimeuzungumzia ujinga uliofanyika.

Its very unfortunate, mimi ni mtu wa Nyerere, alikuwa hapendi ujinga, hivyo na mimi pia sipendi ujinga, na kuna ujinga mwingi nimekemea kwenye uchaguzi, japo mimi ni kada, lakini chama changu kikitufanyia ujinga tunakemea, ule uchaguzi mdogo wa Kinondoni kiukweli ulikuwa ni ujinga, sisi makada wazalendo tukakemea ujinga ule, 2020 chama chetu kikajirekebisha kikatuondolea ujinga ule
P
Ungetumia neno busara ingependeza zaidi, siamini mkeo au mwanao alipotenda kosa la kijinga! Kama ulithubutu kumuita mjinga, hata Nyerere ninaamini maisha yake yote hakuwahi kumuita yeyote kwenye familia yake mjinga, anyway the choice is yours, ila nakuomba usipende kutumia neno baya kwa sababu fulani alipenda kulitumia. Maalim Seif si mjinga ila huenda hakutumia busara kwenye uamuzi wake, huu ni mtazamo wangu na si lazima nawe uufuate.
North Pole and South Pole will never meet because they hate each other, same to CCM members hate opposition members and they have their motto Hii nchi inawenyewe na wenyewe ni wanaccm.
 
Ungetumia neno busara ingependeza zaidi, siamini mkeo au mwanao alipotenda kosa la kijinga! Kama ulithubutu kumuita mjinga, hata Nyerere ninaamini maisha yake yote hakuwahi kumuita yeyote kwenye familia yake mjinga, anyway the choice is yours, ila nakuomba usipende kutumia neno baya kwa sababu fulani alipenda kulitumia. Maalim Seif si mjinga ila huenda hakutumia busara kwenye uamuzi wake, huu ni mtazamo wangu na si lazima nawe uufuate.
North Pole and South Pole will never meet because they hate each other, same to CCM members hate opposition members and they have their motto Hii nchi inawenyewe na wenyewe ni wanaccm.
Mkuu elvischirwa , asante kwa ushauri huu, ni ukweli sometimes ninakuwa too arrogant kwasababu nakerwa sana na hii tabia ya kususa, nililishauri sana kwa kuwauliza, what do they wish to achieve?, na hadi Maalim Seif nilimuuliza face to face. Anyway asante kunikumbusha, tuige mazuri ya viongozi wetu na sio kuiga yote kwasababu hata hao viongozi sio malaika!. Asante tena kunirudisha kwenye humility!.

Umenikumbusha hata nilipowaambia hivi Chadema,
Kiliwaka
Nikaomba msamaha

Hivyo hata hili naliombea msamaha.
Paskali
 
Hawezi kupewa kwakua hajafikia 10% hata ule uchaguzi was marudio was March 2016 baada ya jecha kuweka Moira kwapani pia hakufikia 10% japokua alishiriki ndomaana akaishia kupewa uwazir was Afya tu
waampe tu kwani ccm wafuata katiba si ubabe tu nchi yakwao wafanya watakavyo
 
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P

Hemu toa vigezo vya maana ya neno ujinga? Unataka aende as low as you do na hiyo ndo busara?
 
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P


Uhuru wa. ZANZIBAR kwanza mengine hatutaki kusikia
 
Tafsiri kupitia tamko la Rais mteule wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi, baada ya kutangazwa mshindi, inaweza kujenga taswira kuwa kiongozi huyo anaweza kuwa na dhamira ya kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Hata hivyo, mtihani upo kwa mpinzani wake, Maalim Seif Sharif Hamad na chama chake cha ACT-Wazalendo kutoa uamuzi ndani ya siku saba baada ya Rais kuapishwa.

Akizungumza baada ya kutangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jaji mstaafu Hamid Mahmoud Hamid kuwa Rais mteule wa Zanzibar, Dk Mwinyi alisema ataendeleza maridhiano yaliyopo kikatiba

Alisema atadumisha amani iliyopo kwa kushirikiana na wapinzani kwa sababu wao ni nyenzo muhimu katika kukuza demokrasia nchini.

“Nipo tayari kuyaendeleza maridhiano yaliyopo katika katiba yetu, kwani Zanzibar ni kubwa na muhimu kuliko tofauti zetu, nitashirikiana nanyi kujenga Zanzibar mpya,” alisema Dkt. Mwinyi

Akiwa ameshinda kwa zaidi ya asilimia 76.2 alisema kuwa amepokea ushindi kwa mikono miwili na akaahidi kuijenga Zanzibar kwa ushirikiano na Wazanzibari wote bila kujali itikadi

Hata hivyo, kwa mwongozo wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010, ACT-Wazalendo wanapaswa kuketi na Dk Mwinyi ndani ya siku saba kisha kumpa jina la mtu wanayempendekeza kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, vilevile kufanya mashauriano kuhusu muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa

Kauli hiyo ya Dk Mwinyi, pamoja na ile nyingine kwamba “Zanzibar ni kubwa na muhimu kuliko tofauti za kisiasa”, inaweza kujenga picha ya utayari wake wa kushirikiana na wapinzani wake kuunda Serikali

Mtihani ni Seif ambaye awali alitangaza hatamtambua aliyetangazwa kama Rais wa Zanzibar, vilevile uchaguzi uliompa ushindi

Seif alisema uchaguzi wa Zanzibar uliofanyika Oktoba 27 na 28, haukuwa uchaguzi, bali zoezi la kijeshi. “Uchaguzi ulitekwa na vyombo vya dola. Ikiwa kulikuwa hakuna uchaguzi vipi nitamkubali aliyetangazwa?, hakuwekwa madarakani na wananchi kama Katiba inavyotaka. Amewekwa madarakani isivyo halali,”alisema

Pamoja na msimamo wake huo, bado Seif jana alipozungumza na Mwananchi kwa simu kuhusiana na msimamo wake juu ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa, alirejesha mpira kwa chama chake kwamba ndicho kitakachokuwa na uamuzi wa mwisho

“Kwanza itategemea huyo aliyetangazwa! Akiamua kuunda GNU na kutaka kutushirikisha sisi itategemea maamuzi ya Chama. Si maamuzi yangu,” alisema

Kauli hiyo ya Seif, imeshabihiana na ile ya Mkuu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo, Salim Bimani aliyesema: “Chama kitakaa na kutoa tamko la pamoja kuhusu vurugu zote hizi za uchaguzi. Kwa sasa hatuwezi kuzungumzia ushiriki wetu kwenye hiyo Serikali ya Umoja wa Kitaifa”

Kwa mujibu wa Ibara ya 39 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010, uteuzi wa Makamu wa Kwanza wa Rais kutoka chama kilichoshika nafasi ya pili kwenye uchaguzi wa Rais, si hiari kwa Rais aliyeshinda, bali ni lazima pale mshindi wa pili anapopata kura za urais asilimia 10 au zaidi

Katika matokeo ya urais Zanzibar yaliyotangazwa Oktoba 29, mwaka huu na Jaji Hamid, Seif aliyegombea urais kupitia ACT-Wazalendo, amepata asilimia 19.87, ambayo ni karibu mara mbili ya asilimia zinazohitajika ili chama kilichoshika nafasi ya pili kitoe Makamu wa Kwanza wa Rais na kushiriki kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa

Ibara hiyo inaeleza bila kutaja idadi, kuwa endapo mshindi wa kiti cha urais hakuwa na mpinzani, basi Makamu wa Kwanza wa Rais atapatikana kupitia chama kitakachoshika nafasi ya pili kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

Hadi sasa, kabla ya kupitisha majina ya viti maalumu, CCM ina viti 49 na ACT-Wazalendo kimoja
Kwa ufafanuzi huo wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010, mantiki yake ni kuwa ACT-Wazalendo ndiyo wenye kutakiwa kutoa majibu ya mtihani wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, ama wakubali au wakatae

Na kwa mujibu wa Katibu, wanapaswa kuwa na majibu ndani ya siku saba kutoka siku ambayo Dk Mwinyi ataapishwa.
Kingine kinachoweza kuwapa mtihani ACT-Wazalendo kuingia kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa ni idadi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

Mpaka sasa wana mjumbe mmoja ambaye ndiye pekee ana sifa ya kuteuliwa kabla ya kungoja viti maalum au hisani ya uteuzi katika viti 10 vya Rais wa Zanzibar.



Source: citizen


Hizi pumba za wavamizi peleka Lumumba , ZANZIBAR inapigania uhuru wake tumechoka kuuliwa

ZANZIBAR freedom first.
 
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P
Kwani katiba ya Zanziba inataja makubaliano ya SUK ktk upinzani ni Maalim Seif tu? Mfano kwa sasa CUF pia imepata viti Pemba, hakuna uwezekano kwa mgombea wa CUF au Chama kingine kuingia ktk SUK?
 
Hamad Rashid hakuwa mwanaa CCM yet ali-serve kama Waziri wa Afya kwenye serikali aliyomaliza muda wake.

Bila shaka SuK inawezekana. Na ni vema Malim akubali kutumikia Wazenji kwa siku zake za uzeeni na wenzie wenye damu changa walau wapate fursa ya kukua kisiasa kwa kufanya majukumu
 
Hahaha ni ujinga kukubali kuwa mkia kila siku, kwani wakikataa watapungukiwa nini?!

Ningekuwa mshauri wao ningewashauri waachane na ujinga wa maridhiano, maana hakuna tofauti na kugeuzwa Colgate.

Mliishi bila kuwepo huko serikalini, mtaishi bila kuwepo huko serikalini.

Wameshinda wao waachieni watawale!
Wananchi ndio wamefanya maamuzi ya kuwafanya mkia..unamlaumu Nani hapo..na mkizidi hata huo mkia watawaondolea..subiri
 
Back
Top Bottom