Huu ndio Muonekano wa Daraja la Ruaha Mkuu (Mita 133) katika barabara ya Mikumi- Kidatu - Ifakara

Huu ndio Muonekano wa Daraja la Ruaha Mkuu (Mita 133) katika barabara ya Mikumi- Kidatu - Ifakara

Muonekano wa Daraja la Ruaha Mkuu lenye urefu wa mita 133 katika barabara ya Mikumi- Kidatu - Ifakara sehemu ya Kidatu - Ifakara kilometa 66.9 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami Mkoani Morogoro.

Daraja hilo limejengwa na Mkandarasi Reynolds Construction Company - RCC ya Nigeria na Mhandisi Mshauri kutoka Kitengo cha Uhandisi (TANROADS Engineering Consulting Unit - TECU).

Usanifu na maandalizi ya nyaraka za zabuni ulifanywa na Kampuni ya kihandisi ya Crown-Tech Ltd ya Tanzania.


Ujenzi wa Daraja la Ruaha Mkuu limejengwa sambamba na barabara ya Kidatu - Ifakara kwa kiwango cha lami, Ujenzi ulianza 02 Oktoba 2017 na kukamilika 30 Juni, 2024 kwa gharama ya Shilingi Billion 157.15, ikihusisha ujenzi wa barabara, daraja, usimamizi na fidia ya mali zilizoathiriwa na mradi.

Barabara ya Kidatu - Ifakara na Daraja la Ruaha Mkuu imefunguliwa rasmi leo Agosti 04, 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Daraja hili halina hata taa za barabarani Wala deflectors kwa pembeni?? Designing process ilikuwaje Hadi wamesahau kuweka vitu hivi muhimu???
 
Daraja hili halina hata taa za barabarani Wala deflectors kwa pembeni?? Designing process ilikuwaje Hadi wamesahau kuweka vitu hivi muhimu???
Mradi ulianza 2017 wanasema, ukakamilika 2024! Umbali ni km 67 nadhani, daraja likiwa na mita 133.

Gharama ni 157bn, eti wamelipa fidia pia.

Tunajenga km 70 kwa miaka 7? Wastani wa 10km kwa miezi 12?
Tunajenga km 1 kwa 2.25bn?
 
Zinafika Km ngapi kutoka hapo Moro Hadi pale Lumecha pachani?
Nimefanya utafiti wangu nimebaini umbali wake ni kama hivi ifuatavyo:-
1. Umbali wa kutoka Morogoro Mjini Hadi Mikumi ni 120 km.
2. Mikumi Hadi Kidatu ni 35 km.
3. Kidatu-Ifakara-Lupiro-Malinyi - Lumecha Namtumbo ni 486 km

Hivyo basi, JUMLA ya Umbali wa kutoka Morogoro Mjini-Mikumi-Ifalara-Malinyi hadi Lumecha Namtumbo ni Kilomita 641.

Aidha, umbali wa kutoka Dsm hadi Morogoro ni 196 km.

Hivyo, umbali wa kutoka Dsm- Morogoro-Mikumi-Ifakara-Malinyi-Lumecha Namtumbo ni Kilomita 837.
 
Nimefanya utafiti wangu nimebaini umbali wake ni kama hivi ifuatavyo:-
1. Umbali wa kutoka Morogoro Mjini Hadi Mikumi ni 120 km.
2. Mikumi Hadi Kidatu ni 35 km.
3. Kidatu-Ifakara-Lupiro-Malinyi - Lumecha Namtumbo ni 486 km

Hivyo basi, JUMLA ya Umbali wa kutoka Morogoro Mjini-Mikumi-Ifalara-Malinyi hadi Lumecha Namtumbo ni Kilomita 641.

Aidha, umbali wa kutoka Dsm hadi Morogoro ni 196 km.

Hivyo, umbali wa kutoka Dsm- Morogoro-Mikumi-Ifakara-Malinyi-Lumecha Namtumbo ni Kilomita 837.
Hapo sawa so Ni kama masaa 11 hivi kwa basi .
Unatoka zako Songea kabla jua halijazama upo DSM au unashuka Moro unaingia kwenye SGR
 
Kweli kasimamia, maana pesa ya ujenzi walitoa israel toka mwaka 2017 ndio barabara imekamilika leo
Huo mradi wa jiwe kwani umesahau lijualikali alipiga mpaka magoti akiomba hiyo rami ijengwe jiwe akapiga simu ujenzi ukaanza hapo hapo
 
Hii road ndo itakuja Hadi huku Namtumbo??
Inawezekana. Maana ya kutokea Namtumbo inaanzia Malinyi huko. Hiyo ni kuelekea Ifakara. Mbele ya Ifakara ndo kuna ya kwenda Namtumbo.

Hapo pembeni ya daraja kulikuwa na imani ya kuwepo chunusi. Enzi nipo K1 (Kilombero Sugar), daraja lilikuwa la kuvuka gari moja, mnafanya kusubiriana. Atakayewahi ndo anapita. Mbele hapo kulikuwa na stendi ya Mkamba
 
Back
Top Bottom