James Hadley Chase
JF-Expert Member
- Mar 25, 2020
- 1,984
- 3,695
Sijajua, ila ujenzi unaendelea ili kuunganisha mikoa ya Njombe, Morogoro na RubumaZinafika Km ngapi kutoka hapo Moro Hadi pale Lumecha pachani?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sijajua, ila ujenzi unaendelea ili kuunganisha mikoa ya Njombe, Morogoro na RubumaZinafika Km ngapi kutoka hapo Moro Hadi pale Lumecha pachani?
Hilo daraja la chuma limetutesa sana wakazi wa Ifakara. Ilikuwa ni mwendo tu wa kusubiriana. Gari za upande wa pili kuzisubiri gari nyingine zipite kwanza.Muonekano wa Daraja la Ruaha Mkuu lenye urefu wa mita 133 katika barabara ya Mikumi- Kidatu - Ifakara sehemu ya Kidatu - Ifakara kilometa 66.9 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami Mkoani Morogoro.
Daraja hilo limejengwa na Mkandarasi Reynolds Construction Company - RCC ya Nigeria na Mhandisi Mshauri kutoka Kitengo cha Uhandisi (TANROADS Engineering Consulting Unit - TECU).
Usanifu na maandalizi ya nyaraka za zabuni ulifanywa na Kampuni ya kihandisi ya Crown-Tech Ltd ya Tanzania.
Ujenzi wa Daraja la Ruaha Mkuu limejengwa sambamba na barabara ya Kidatu - Ifakara kwa kiwango cha lami, Ujenzi ulianza 02 Oktoba 2017 na kukamilika 30 Juni, 2024 kwa gharama ya Shilingi Billion 157.15, ikihusisha ujenzi wa barabara, daraja, usimamizi na fidia ya mali zilizoathiriwa na mradi.
Barabara ya Kidatu - Ifakara na Daraja la Ruaha Mkuu imefunguliwa rasmi leo Agosti 04, 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
#WajinGaSiSi.Mradi ulianza 2017 wanasema, ukakamilika 2024! Umbali ni km 67 nadhani, daraja likiwa na mita 133.
Gharama ni 157bn, eti wamelipa fidia pia.
Tunajenga km 70 kwa miaka 7? Wastani wa 10km kwa miezi 12?
Tunajenga km 1 kwa 2.25bn?
Mkuu hawa vijana wanadai ni kazi ya samia wakati ni magufuliHilo daraja la chuma limetutesa sana wakazi wa Ifakara. Ilikuwa ni mwendo tu wa kusubiriana. Gari za upande wa pili kuzisubiri gari nyingine zipite kwanza.
Ahueni ndugu zangu wa Ifakara, lami imewafikia.
Kumbe mbali hivyo , almost dar shinyanga ?Umeandikaje? labda ngeli imekuchenga ila wanasema ni 805km
Bora kupita lindiHapo sawa so Ni kama masaa 11 hivi kwa basi .
Unatoka zako Songea kabla jua halijazama upo DSM au unashuka Moro unaingia kwenye SGR
Unabishi nn?..mm nipo nasafirisha Tv yangu hisense inchi 55...nimepakata sijui kama ntafika nayo haijavunjika roho juu tu....ni masaa 12 na zaidi kufika malinyi huko mbeleKumbe mbali hivyo , almost dar shinyanga ?
Sidhani kama ni kweli
Unaenda wapi?Unabishi nn?..mm nipo nasafirisha Tv yangu hisense inchi 55...nimepakata sijui kama ntafika nayo haijavunjika roho juu tu....ni masaa 12 na zaidi kufika malinyi huko mbele
Hiyo Ndo njia wazee wetu zamani walikuwa wanaenda kwa mganga Binti Kalembwani!!Inawezekana. Maana ya kutokea Namtumbo inaanzia Malinyi huko. Hiyo ni kuelekea Ifakara. Mbele ya Ifakara ndo kuna ya kwenda Namtumbo.
Hapo pembeni ya daraja kulikuwa na imani ya kuwepo chunusi. Enzi nipo K1 (Kilombero Sugar), daraja lilikuwa la kuvuka gari moja, mnafanya kusubiriana. Atakayewahi ndo anapita. Mbele hapo kulikuwa na stendi ya Mkamba
Hii si pale Tanesco Kidatu, ukiwa unaelekea Kiwanda Kingine cha Kilombero? Anyway sijaenda siku nyingi sana kule
Ndiyo enyewee!!!Hii road ndo itakuja Hadi huku Namtumbo??