Huu ndio ukweli: Hakuna kiongozi mteule anayemuogopa Rais Samia

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
•Wangekuwa wanamwogopa huu mgao wa umeme wangeudhibiti mapema.

•Wangekuwa wanamwogopa wale mafisadi aliowawaambia wampishe baada ya madudu ya ripoti ya CAG wangempisha haraka lakini hakuna hata mmoja aliyempisha.

Kwa tafsiri ya Maandiko matakatifu kuogopa maana yake ni kuheshimu.

Hivyo nichelee kusema viongozi hawamuheshimu Rais aliyewateua.

Rais anaonekana ana nia njema ya kuwafikisha mbali Watanzania lakini hatoweza katu kama hatasimama kama amiri jeshi mkuu wa Majeshi yote .
 
Hivi ukiteuliwa ni lazima kumuogopa aliyekuteua?

Unateuliwa kumsaidia majukumu aliyokupatia.

Tuseme wazi kwamba, wanamuangusha kwa sababu ni mwanamke na CCM haipendi habari ya kuongozwa na mwanamke
 
•Wangekuwa wanamwogopa huu mgao wa umeme wangeudhibiti mapema...
Rais hatakiwi kuogopwa, rais anatakiwa kuheshimiwa.

Ukimuogopa rais ndiyo mwanzo wa kuogopa kumshauri ushauri sahihi, kwa kuogopa kwamba hataupenda huo ushauri.
 
Hivi ukiteuliwa ni lazima kumuogopa aliyekuteua?
Unateuliwa kumsaidia majukumu aliyokupatia.

Tuseme wazi kwamba, wanamuangusha kwa sababu ni mwanamke na CCM haipendi habari ya kuongozwa na mwanamke
Nimeedit content.
Soma tena, nimetoa maana ya neno kuogopa.
 
Rais hatakiwi kuogopwa, rais anatakiwa kuheshimiwa.

Ukimuogopa rais ndiyo mwanzo wa kuogopa kumshauri ushauri sahihi, kwa kuogopa kwamba hataupenda huo ushauri.
Nimeedit content na kutoa maana ya neno KUOGOPA
 

Sisi wanafunzi wa vyuoni tunasubiri mabadiliko kwa huyu , maana badru duh!
 
Nimeedit content na kutoa maana ya neno KUOGOPA
Kuogopa si kuheshimu.

Habari za "kwa tafsiri ya maadiko matakatifu" zinabeba logical fallacies angalau tatu.

1. Argument from dictionary.
2. Argument from tradition.
3. Argument from authority.
 
Makonda kwa sasa anaogopewa kuliko bosi wake.
Kila mtu anafanya lake so long as asimguse Makonda.
Makonda baada ya kumchamba Mwanasheria mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni nani sasa aliye juu yake?
 
Hawa mheshimu wala hawamuoni kama Kiongozi sababu hana sifa za uongozi.
 
fact!
 
Makonda ndivyo alivyo hatishwi kirahisi hivyo hata wakati wa Magufuli akiwa Mkuu wa Mkoa wa wa dsm ni hivyo hivyo tu
 
True.

Bora viongozi wamuogope Samia halafu watende kwa hofu ya kuogopa kutumbuliwa, kuliko kumheshimu huku wakifanya kazi kwa mazoea yanayolelekea kuwaumiza watanzania.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kwa ufupi Dkt Samia kazungukwa. Kujinasua sasa ni ngumu sana. Awavumilie tu waendelee kuiba ili ya Dkt Magufuli na Kijazi yasimkute
 
Makonda kwa sasa anaogopewa kuliko bosi wake.
Kila mtu anafanya lake so long as asimguse Makonda.
Makonda baada ya kumchamba Mwanasheria mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni nani sasa aliye juu yake?
Hahahaha Makonda ni msemaji wa Chama hahaha ila mpaka raha mno. Unajua Dkt Nchimbi alianza kusema eti sijui kudhalilisha viongozi hahaha na yeye alichambwa na Makonda live hahaha, Bashe naye akajileta naye akala mapigo hayo hayo sasa sijui nani ataibuka hahaha, ila nadhani viongozi wengi hawaelewi maana ya siasa ya hiki kizazi wanadhani ni wa enzi za Mwl Nyerere, au Mwinyi. Sasa hivi kila kitu watu wanahoji! Makonda piga kazi
 
Sasa kama wanajua waliteuliwa Msoga unadhani itakuwaje ?
 
Nimekupa "like" kwa hizo aya za nne za mwanzo, lakini kwa hiyo aya ya mwisho ni bonge la noooooooooo.
 
Heheheee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…