Huu Ndo Ukweli kuhusu Mkoa wa Mara

Huu Ndo Ukweli kuhusu Mkoa wa Mara

acha uongo wewe ..mara ni mara tu ....Mme kumkata panga mkewe kitu cha kawaida Sana acha kupotosha.. ndio maana mji hauendelei maana mtu anaogopa kufungua biashara zake za maana...maana ukipewa 10000 mtamchinja tu ....bila woga...

mnahitaji Maombi ya ukombozi ili mfunguliwe na maroho ya mauaji na kukatana bila hata woga....khaaa acha kucheza na kina muraaa bana!....

watu wanakuja tu sababu ya ajira....na wanapangiwa 19 wanaripoti 4 khaaa nyie Sio kabisa.....maana mtu akija kwenu aombe Sana Mungu kila iitwapo Leo....maana nyie Sio.
Sio kweli huku wageni wengi na wanaishi kwa amani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jamaa moja alikwenda Tarime, akiwa amekaa bar anakunywa bia yake akaja jamaa ana panga na rungu halafu ana makovu kibao usoni
Akamsalia huyo mgeni: hujambo mrembo? jamaa akabaki anamsahangaa tu.
Akarudia hujambo mrembo? Jamaa kwa uoga akaitikia sijambo!
Akamwambia yule jamaa - ole wako usinge itikia ungejua mi nina, shenzi we mwanaume gani huna kovu? Halafu huyoo akasepa, huyo mgeni akabaki anatetemeke tu asijue la kufanya.
Hiyo ndy tarime.
[emoji1] [emoji1] [emoji1] hii itakuwa ni kichekesho tu mkuu sio kweli
 
Tuhuma za kujichanjana au kupiga wanawake hiyo ni hulka ya mtu...mfano mwaka juzi kuna sehemu nilipanga na nyumba moja na mchagga mmoja alikuwa anamshushia kipigo cha mbwa mweusi mke wake na huku yule Dada alibadilisha dini ili aolewe na huyo mchagga hadi yule mdada alikimbia na mtoto wake je huyo nae katoka Mara??
MOROGORO huko kuna jamaa alimchoma mkuki mfugaji sijui mkulima mkuki hadi ukatokeza upande wa pili je huyo nae anatoka mkoa wa Mara? Binafsi mm nimezaliwa huko nikakulia huko nikasoma O_level nikaenda nyanda za juu kusini nikajifunza mengi na leo hapa dar nashangaa mengi lakini kuna mambo yanayotokea dar hapa kule mara hatuwezi vumilia...mfano inshu ya panya road kule MARA wala tusingehangaisha jeshi la polisi wangekufa wote ,inshu ya scorpion tusingemchekea ,hapa dar mtu anakabwa mchana kweupe watu wanaangalia tu,mtu anapiga nduru kuomba msaada watu wanaangalia tu au wanajifungia ndani kitu ambacho watu wa Mara bila kujali kabila tunaushirikiano sana bila kujali kabila wala dini ila walegevu wakija lazima tuwatoe upepo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbna kule ni kawaida na wa2 wako poa kabisa
Ata dsm kuna hayo mambo lkn mara ndo inatangazwa vibaya sana
Insue ni usiibe wake za wa2 au mali za wa2 baass
Na usiguse binti wa kikurya ambaye hajaolewa, hapo unajitafutia majanga. Kiufupi Wakurya ni wakarimu na ndo wanatajwa sana kwa ukatili. Mtoa mada anajichanganya kwa kudhani mkoa mzima wa Mara ni wakurya tu. Kuna makabila zaidi ya 10 na mengi yao ni watu wazuri sana ukiacha wakurya ambao tulikuwa na misuguano ya koo na haswa akutokana nakuibiana mifugo na kugombea mipaka. Ukiwa Tarime na ukaishi kistaarabu hakuna atakayekugusa. Mambo ya kuzingatia ni kuwa mbali na wake na mabinti za watu, hapo utaenjoy sana kuwa Tarime. Ukileta mambo ya uswahilini kuvizia mali za watu hutopona hakika.
 
Hii ilisababishwa na mapigano hasa wizi wa ng'ombe kutoka nchi jirani ila shukrani kwa kanda maalum wizi wa ng'ombe umekomeshwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Ng'ombe wenyewe washaisha, matukio ya kupigana yamepungua sana na wakurya huwaheshimu sana wageni wanajieshimu. Tunao wachaga kibao na wanafanya biashara zao vizuri tu kwani wanajua wasichopaswa kufanya.
 
Back
Top Bottom