Huu ndo Ushahidi wa Nchi za Magharibi zinavyotusaidia. Anayewatukana na kuwasimanga muonee huruma sana!

North Korea waliwekewa vikwazo na kunyimwa misaada, bado wametengeneza mpaka nuclear. Wanamtisha mpaka Mmarekani. Sisi tunalilia kusaidiwa. Labda ubongo wa mtu mweusi uliumbwa kwa mabaki ya material.
China ameshikilia utawala wa North Korea
 
Ukipitisha mkataba mbovu halafu utake kuuvunja kiholela, kwa dunia ya leo, utapigwa tu.
Sio issue ya mkataba, bali ni Nchi inayojinasibu ya Kidemokrasia (Canada) kuitisha nchi ndogo (Tanzania) iwaache Barrick la sivyo wanasitisha misaada, hii inaonesha Fika Misaada inakuja na masharti magumu hata wakiwa wanaiba basi wasishughulikiwe.

 
China ameshikilia utawala wa North Korea
Hata sisi miaka ya 1970 na 1980 tulikuwa marafiki wakubwa wa China, Cuba, Urusi na East Germany kabla haijaungana. Kwa nini bado hata mlo tu unatushinda ? Kwa nini hatujatumia urafiki wa nchi hizo kuwa sawa na North Korea?
 
Kwani anayepereka bakuri si ni wewe? We tulia uone kama watakufuata, walidanganya uchaguzi Zanzibar wakasitisha REA karibu miaka 5, ilirejea tena baada ya kupiga magoti.
 
Lkn hawanyang'anyi
SI mna viongozi wanaosaini hiyo mikataba
 
Its a trap, Nchi nyingi za Ki Africa haziwezi kuishi bila misaada ila haimaanishi kwamba zenyewe ndio zinafaidika.
alafu suala la kuuliwa watu haliwezi kuwa ni mambo ya ndani.tanzania ipo duniani.kila mtu anaona yanayotendeka
 
Hata sisi miaka ya 1970 na 1980 tulikuwa marafiki wakubwa wa China, Cuba, Urusi na East Germany kabla haijaungana. Kwa nini bado hata mlo tu unatushinda ? Kwa nini hatujatumia urafiki wa nchi hizo kuwa sawa na North Korea?
Huwezi fananisha urafiki na ukaribu wa China na North Korea na Watanzania na hayo mataifa.

North Korea ina maslahi makubwa kwa China kama nchi kuanzia usalama na siasa za ukanda ule ikianguka North Korea hasara kubwa mpaka China itapata.

Utofauti mwingine wakorea wana akili IQ kubwa wakati Watanzania akili hazipo
 
Zimbabwe vp
 
Peda ni nyingi sana ila kazi yake naona ni kujenga ccm tu
 
Wewe ni kilaza kama walivyo vilaza wengine na ndio mmejaza Africa, Unategemea nini hapo ? Unajisifia umasikini kwenye nchi ya Ardhi tajiri , nyie wajinga ndio mnaturudisha Nyuma sana .
Alichokisema muanzisha uzi ni rahisi kueleweka. Sijui kwa nini hujaelewa.
Umesema ni kilaza na a ajisifia umaskini.
Kiufupi, ni kama vile ulitaka aseme kama Magufuli alivyokuwa akiwaambia Watanzania watembee vifua mbele kwa vile wao siyo maskini,na nchi yao ni tajiri....,siyo?

Ukitaka mtu awe na fikra za kujitoa katika hali aliyomo,unatakiwa kumuambia ukweli wake. Waambie watanzania ukweli mchungu kwamba wao ni maskini na nchi yao ni maskini sana ili wajiulize ni kwa nini wako katika hali hiyo ,na wafanye nini ili kujitoa katika dimbwi la umaskini.

Katika nyanja ya diplomasia,mwenye nguvu ya kiuchumi ndiye mwenye ushawishi(influence)...hakuna two way traffic hapo.
Tanzania ni nchi maskini ambayo bajeti yake hadi sasa inachangiwa na wahisani,..sasa inapataje ujeuri wa kuwapiga mkwara na kutukana wahisani wake...tena kwa kuzungumzia jambo jema la kufanyika kwa uchunguzi ambalo hata rais mwenyewe alilisemea?

Ni kweli tunatakiwa kuwa na jeuri hiyo ya kupiga mkwara nchi nyingine kwa sababu zenye mashiko na hadi pale tutakapojitoa katika umaskini tulionao.
Kwa taarifa yako tu,kitendo cha rais kusema kwamba atawachongea mabalozi wa nchi za magharibi kwa marais wao kwa vile uamuzi wao ni wa binafsi, kimetuaibisha kama taifa...maana ,kidiplomasia inaeleweka sauti ya balozi ni sauti ya nchi anayowakilisha. Sasa kama rais wetu hajui hata jambo dogo kama hilo,sasa hayo masuala mazito ya kuitoa nchi katika umasikini ataelewaje?
Rais alitakiwa kujua endapo balozi ataongea maneno yake binafsi kinyume na takwa la nchi anayoiwakilisha,nchi husika inamrudisha nyumbani(recalled).

Kuza uchumi wako kwanza ndipo uwe na jeuri ya kupiga mkwara wengine....,vinginevyo kaa kimya.
 
Nakupinga 100%. Kinachotokea ni kuwa kila mmoja anasaidia sisi masikini (in Dkt Samia and Dkt Kikwete Voices), kulingana na repatriation strategy yake. Mfano, US kwenye afya akishaileta hiyo hela anaichukua kupitia kuuza madawa, watalaamu, na washauri ambao ni wa USA, tena wana masharti magumu sana kushinda tenda zao. Same kwa Mchina, anasaidia kulingana na uwezekano wa kurudisha hela kwao. Mfano kwenye maujenzi ana mtaji mkubwa hivyo anaweza kushindana na mara zote anafanya lobbying kwa serikali ili apate kazi na mwisho wa siku hizo hela zinarudi kwake. In short kiuchumi ukingalia equation ya GDP utaona kabisa kuna component ya hela inayorudi kwao ina imarisha uchumi wao, na ndiyo maana kiuchumi inafahamika kuwa nchi inayotoa msaada ndiyo huwa inafaidika kuliko inayopokea. In conclusion, usiandike na kushadadia mambo usiyoyajua, Dkt Magufuli ndiyo alikuwa sahihi ktk ujenzi wa uchumi ambao ni more sustainable kuliko Dkt Samia ambaye anaamini ktk kukopa na misaada kwa sababu eti sisi ni masikini. Kama anauona huu uzi awaulize wachumi wake akina Dkt Blandina kuhusu misaada na maendeleo labda wamdanganye, ila ukweli huwezi kuendelea kwa mikopo nje ya nchi na misaada, ni mpaka uimarishe ukusanyaji wa mapato ya ndani na kufanya more of government expenditure, simple like that. Mengine haya ya factors of production huwa yanakuja menyewe kwa sababu wanasema kila taifa lina own endowment ndiyo maana mwarabu hajasomesha ila anaajili wageni etc.
 
Ukivunja kiholela mkataba ulioingia mwenyewe utapigwa tu, na hata kama utapigwa kwa kuonewa, wewe mwenyewe utakuwa umejiwekea mazingira ya kupigwa na kutetewa kwako kuwe kugumu.

Laumu aliyeingia mkataba mbovu. Laumu aliyevunja mkataba kiholela. Utalaumu vipi wafanyabiashara wajanja waliojiwekea mazingira ya kushinda, pamoja na nchi zao zinazowatetea kwa kufuata mifumo ya sheria?

Unaliangalia tatizo kutoka upande usio sahihi. Hapa wa kulaumiwa ni viongozi wa Tanzania. Kuanzia walioingia mkataba mpaka Magufuli. Si Barrick wala serikali ya Canada.

Anayekupa msaada ana uhuru wa kukuwekea masharti yoyote anayoyataka na kusitisha msaada wake kwa sababu zake zozote, si msaada anatoa yeye, unataka kumpangia jinsi ya kutoa msaada?
 
Ukweli ni kwamba hizi nchi hazitusaidii, naweza kusema zinatuchezea mchezo fulani hivi ili miaka nenda rudi tubaki tumeganda tu katika eneo ilo ilo.

Ukweli mwingine ni kwamba hatuna uwezo, mbinu wala mikakati ya kujinasua katika mchezo wanaotuchezea.

Kufikiri kwamba wanatusaidia au kuwaletea jeuri haitatusaidia chochote.
 
Unamsujudia vipi mtu ambae ukoo wake ,uliwabaka, uliwatesa, uliwaua ukoo wako na kuwaletea magonjwa yote unayoyajua kwenye vitabu??

Malaria, Gono, mpox, Kaswende n.k

Na bado wanaendelea kuigiliba Afrika.
 
Huyo toka ile mada yake kuhusu Mama Samia anaonekana anayapima mambo kiutoto utoto sana.
Kwenye hiyo misaada kuna ukoloni mambo leo wa kuyashikilia mataifa kisiasa na kiuchumi.
Ila huyu sidhani kama analijua hili.
Anadhani hiyo misaada inakuja hivi hivi tu.
 
Mbona unajitungia comment na kujijibu badala ya Kujibu hoja yangu?

Serikali ya Canada ni Mahakama? Misaada wanayotupa ni Hakimu?

Hakuna alievunja mkataba, bali Barrick walipewa kesi ya kukwepa kodi, iwe ni kweli ama si kweli Mahakama ingeamua, ila kutishia Nchi kwamba tunakatisha misaada sababu umeidai kampuni yetu Kodi huoni kama wanatumia hio misaada ku suppress maamuzi ya Nchi ndogo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…