Lema katika kampeni zake amerekodi sauti ya Rais Magufuli wakati anamtumbua Mrisho Gambo na anawasikilizisha wananchi huku akiwashawishi kuwa Gambo hafai kuwa Mbunge.
Halima Mdee naye kwenye gari lake la matangazo ya kampeni anarusha sauti ya askofu Gwajima akiponda vyeo vya uwaziri na ubunge na kutishia kuhujumu madrasa.
Binafsi nauchukulia utaratibu huu kama siyo wa halali na ninaiomba NEC na msajili wa vyama kufuatilia na kuchukua hatua.
Maendeleo hayana vyama!