Huu utaratibu wa kuhubiri injili kwenye magari ya abiria ni kero kubwa, LATRA muingilie kati

### muhisika
 

Mathayo 24:14

Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.

Kama kanisani huendi , msikitini huendi, chaneli za dini husikilizi wala kuangalia, bora injili ikufuate hukohuko.
 
Bidhaa zao zote hazina majina.
 
Ukiona neno la Mungu linakukera ujue una tatizo la kiroho.
 
Kimsingi neno la Mungu siyo kelele, wapo wanaotamani wasikie kelele ila hawakubahatika kuwa na masikio yenye uwezo huo, jambo ninaloafikiana nawe ni huo mchezo wa kuwaibia watu kwa kisingizio cha sadaka
 
Umeshawahi kukutana na wale wenye speaker
 
Ikitokea ajali mbaya ikakugusa huenda ukatambua uwepo wa Mungu regardless ni muslim au christian anahubiri, zamani zile nakumbuka baadhi ya mabasi yalianza safari baada ya kufanya sala, na hata baadhi walifanya sala walipofika maeneo ajali ziliyopoteza ndugu wengi [Hili nililiona sana kwenye Mombasa Raha wasafiri tulipofika eneo la Sekenke]
 
Waislam mna matatizo sana
Hebu vuta picha wangekuwa waislamu au waislamu na wao wafanye kama hivyo tungepata utulivu kweli. Ibada inatakiwa ifanyike sehemu maalumu ambayo imeshatengwa (msikitini, kanisani) at least wanaojenga majukwaa mitaani ,sio hao wengine kila Kona wanahubiri tu inakuwa sasa kama wamekosa namna ya huwavuta watu kwenye dini wanaamua kulazimisha
 
unaona Neno la Mungu kero? subiri kuna siku utalitafuta na hautalipata. acha kiburi cha uzima.
 
Kuna wale wanaouza madawa na bidhaa mbalimbali kwenye mabasi ni kero tupu.
 
Mbona wanafanya sana mkuu.
 
Mungu ni kila kitu jamani, ingekua kheri kumtukuza Mungu kila pahala. Mtu asiyependa mahubiri ana mapepo ya kutosha, injili kwake ni kero!
Kama kwako unaona unahitaji kupumzika, Mungu naye apumzishe Pumzi yake kwa wakati huo au aondoe macho yako kwa wakati huo - kisha tuone kama ungekataa mahubiri. Mungu ni Yote katika Yote.
Tena nakushauri umpokee huyo YESU maana bila YESU ni ubatili na kujilisha upepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…