Huwezi kuchukua nchi bila SYSTEM kuwa upande wako

Huwezi kuchukua nchi bila SYSTEM kuwa upande wako

Chadema mnapofanya siasa zenu tambueni kuwa ni ngumu kuchukua nchi bila kufanya urafiki na vyombo vya ulinzi na usalama. Either mtatumia umwagaji damu, Vyombo vya ulinzi ndio watanzania wenyewe ukiona umekubalika 50% kwa watanzania na ndani ya ulinzi ndio hivyo hivyo, maafisa wa vyombo wanataka kujilidhisha na sera zenu juu yao.

Hivyo wapinzani mnapotaka kufanya siasa msijitenge na vyombo kama Police, TISS na JWTZ ni ushauri wangu tu wa leo kuvishutumu vyombo vya ulinzi mala kwa mala mtajenga kutoaminika kupewa nchi ndio maana wanawasumbua sana maana wanajuwa mkiingia mtawageuka na kuwachukulia hatua. Siasa imebadilika vyombo vya usalama ni muhimu ili kwenda hasa ikulu.

Ili jambo litaponza upinzani miaka mingi sana na tutachelewa kuondoa mfumo mbovu wa taifa endapo upinzani hautabadilika na kuwa upinzani wa sera za mageuzi na sio lawama kwa vyombo vya usalama siasa zetu tuzifanye na kumshutumu Magufuli lakini sio taasisi za ulinzi wa nchi.
Techinically hatuhitaji nguvu ya vyombo vya dola kushinda uchaguzi tunahitaji mazingira sawa na haki ya uchaguzi. Just kwa mfano kama ambavyo ccm inafanya siasa kila siku na Chadema turuhusiwe kwa mipaka hiyo hiyo kufanya siasa.

Uchaguzi ufanyike kwa mazingira sawa. Tutashinda asubuhi na mapema. Lakini vyombo hivyo haviwezi kufanya hivyo kwa kuwa the are corrupts and devil's advocates kama ilivyo ktk nchi zote za kiafrika.
 
Chadema mnapofanya siasa zenu tambueni kuwa ni ngumu kuchukua nchi bila kufanya urafiki na vyombo vya ulinzi na usalama. Either mtatumia umwagaji damu, Vyombo vya ulinzi ndio watanzania wenyewe ukiona umekubalika 50% kwa watanzania na ndani ya ulinzi ndio hivyo hivyo, maafisa wa vyombo wanataka kujilidhisha na sera zenu juu yao.

Hivyo wapinzani mnapotaka kufanya siasa msijitenge na vyombo kama Police, TISS na JWTZ ni ushauri wangu tu wa leo kuvishutumu vyombo vya ulinzi mala kwa mala mtajenga kutoaminika kupewa nchi ndio maana wanawasumbua sana maana wanajuwa mkiingia mtawageuka na kuwachukulia hatua. Siasa imebadilika vyombo vya usalama ni muhimu ili kwenda hasa ikulu.

Ili jambo litaponza upinzani miaka mingi sana na tutachelewa kuondoa mfumo mbovu wa taifa endapo upinzani hautabadilika na kuwa upinzani wa sera za mageuzi na sio lawama kwa vyombo vya usalama siasa zetu tuzifanye na kumshutumu Magufuli lakini sio taasisi za ulinzi wa nchi.
Mawazo potofu ya kijima
 
Wapinzani wanataka ikulu

Wanamabadiliko wanataka nguvu ya kutunga sheria kwani itatupeleka kwenye rule of law and total separation of power

Tz haiwezi badili aina ya uongozi bila kubadili signifances changes in constitution na sheria nyingi mbovu na kandamizi

Tiss move ya benja kuwatoa ikulu ilianza safari ya mabadiliko lkn yameshindwa kuendelezwa mpaka leo bado wako primitive oriented

Police ukibadili sheria yao kidogo kwa kuwa regulatory entity pia ukanabadili criminal procedure act sambamba na kukuza nguvu ya Dpp kila wilaya bila kusahau sheria ya serikali za mitaa ya 1984


Kazi hiyo ni ndogo tukipata wabunge wanamanadiliko 250
 
Tusitaniane kama yaani Tujenge urafiki na tiss inayomlinda rais na mapapai,mafenesi yake ikulu ya chato
 
Ndipo huwa nashangaa wanaposema Lissu kugombea urais!! Huwezi kuwaza urais huku unakashifu viongozi wooote waliopita na waliopo,unaponda tiss,polisi,takukuru,majeshi nk. Huwezi ukapata urais kwa style hiyo kamwe.
Shindana kihoja na wanasiasa wenzio bila kuingiza kila mtu pasi na sababu za msingi
 
Hakuna mazingira sawa ya ushindani
Kama mbunge wa upinzani hata akishinda inakuwa vigumu kutangazwa sasa hili litawezekana lini Mkuu.

Tume huru ya uchaguzi inatosha
Hata Mnyika anaweza kumshinda Magu kama kuna Tume huru ya uchaguzi asubihi na mapema

Mfumo wa siasa za Tanzania mpaka hautoi Nafasi kabisa ya upinzani kushinda udiwani ubunge na uraisi zaidi ya kuwa kandamiza tu .hicho ndio kilichobaki kwa sasa .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapinzani wanataka ikulu

Wanamabadiliko wanataka nguvu ya kutunga sheria kwani itatupeleka kwenye rule of law and total separation of power

Tz haiwezi badili aina ya uongozi bila kubadili signifances changes in constitution na sheria nyingi mbovu na kandamizi

Tiss move ya benja kuwatoa ikulu ilianza safari ya mabadiliko lkn yameshindwa kuendelezwa mpaka leo bado wako primitive oriented

Police ukibadili sheria yao kidogo kwa kuwa regulatory entity pia ukanabadili criminal procedure act sambamba na kukuza nguvu ya Dpp kila wilaya bila kusahau sheria ya serikali za mitaa ya 1984


Kazi hiyo ni ndogo tukipata wabunge wanamanadiliko 250

..Jumla ya Wabunge ni 393.

..Wabunge wa majimbo ni 264.

..Viti maalum ni 113.

..toka baraza la wawakilishi 5.

..wa kuteuliwa na Raisi 10.

..Mwanasheria Mkuu 1.

..kama unataka wabunge 250 naamini hawa ni wa majimbo + viti maalum.

..250 ni zaidi ya asilimia 66% ya wabunge wa majimbo + viti maalum.

..mimi kwa observation yangu, mgombea Uraisi huwa anachangia sana kupata wabunge wa majimboni.

..vyama vya upinzani vikiweza kupata mgombea ambaye ana mvuto, hata kama atashindwa ktk kura za Uraisi, anaweza kuwasaidia kupata wabunge wengi.

..Na process hiyo inatakiwa kuwa endelevu kwamba kila uchaguzi lazima waongeze kura zao za Uraisi na idadi ya wabunge mpaka pale watakapoweza kuwa na quorum ya kuwa na turufu ktk kubadilisha sheria.
 
..nadhani unazungumzia kwa nafasi ya URAISI.

..vyama vya upinzani havijawahi kuwazidi ccm ktk kampeni za Uraisi.

..mara zote wameweka wagombea ambao ni weaker compared to mgombea wa ccm.

..pia mara zote wamekuwa out-campaigned na out-organized na ccm.

..ccm wamekuwa wakifanya kampeni kwa nguvu zaidi kuwashinda wapinzani.

..ccm pia wamekuwa wakifanya kampeni ambazo ziko more organized kuzidi kampeni za ccm.

..Kuna mambo matatu ya msingi. La kwanza MGOMBEA. La pili CAMPAIGN / UJUMBE. La tatu ORGANIZATION.

..Wapinzani wajitahidi washinde mambo mawili kati ya hayo matatu na hakutakuwa na kisingizio cha system kuwazuia.

cc Kalamu1, Nguruvi3
Mkuu JokaKuu,

Kwanza nianze kwa kukataa hoja ya mleta mada; pamoja na kwamba sijasoma aliyowasilisha ndani ya mada yake. Nakataa nadharia yake kutokana na kichwa cha habari aliyowasilisha.

Lakini hili siyo lililonivuta kuja hapa na kuitikia wito wako.

Nimekusoma kwa haya uliyojadili hapo juu, na mimi nikaona nidandie hapo hapo kuweka yale ambayo nimekuwa nikiyawaza kwa muda mrefu kidogo kuhusu siasa zetu hizi za Tanzania.

Nimekuwa nikiwaza mawazo haya niyaanzishe mada yake pembeni, lakini nimekuwa nikisita.

Nitatumia nafasi hii kuyaweka hapa na wewe pamoja na wasomaji wengine pengine mkiona yanastahili mjadala mkubwa, basi, utakuwa ni mwanzo wa kuyaeneza.

Tumekuwa na vyama vya upinzani kwa muda mrefu sasa, tokea 1995, na tokea hapo takribani vyama vyote vilivyotaka kushiriki vimekuwa huru kushiriki kwenye chaguzi mbali mbali na Chaguzi Kuu za Rais na Wabunge.

Mara zote hizi CCM ndio imekuwa mshindi, kwa kura nyingi kwa Rais, na kupata wabunge wengi. Ni mara chache sana, sikumbuki uchaguzi uliofanyika CCM ikakosa kupata wabunge zaidi ya nusu Bungeni.

Imekuwa hivyo nyakati zote, kiasi cha kwamba, nadhani yamekuwa ni mazoea kwa watu kutegemea CCM ishinde na kupata wabunge wengi.
Nasema imekuwa mazoea, kwa sababu hakuna anayeuliza kwa nini iwe hivyo kila mara?

Vyama vya upinzani, naona kwa sababu nisizozielewa, hili haliwasumbui, kwa sababu huwa sisikii wakilijadili wala kulisemea kwenye kampeni ili watu walijue. Mara zote, nasisitiza, kwa sababu sina ushahidi tofauti ya haya ninayoyaandika, mara zote, wapinzani lengo lao ni kushinda urais na wabunge wengi bungeni kama anavyofanya CCM. Hilo ndilo huwa wanalisisitiza mara zote.

Sasa najiuliza, kwa nini iwe hivyo? Na hasa baada ya Rais Magufuli kuonyesha wazi anavyopenda na kufaidika na ushindi wa asili mia. Ule wa serikali za mitaa bado hakuridhika na asili mia tisini na tisa; atafurahi safari hii Oktoba akipata 100%!

Baada ya kuona aliyofanya tokea 2015, kwa nini waTanzania wasielezwe; hapana, wasikumbushwe athari ya mazoea yao ya kuchagua CCM na wabunge karibu wote Bungeni kuwa wa CCM?

WaTanzania wanahitaji kukumbushwa na kutahadharishwa waache hii tabia ya kuchagua chama kimoja na kukirundikia madaraka yote.

Magufuli na Ndugai wametuonyesha waziwazi bila ya kificho chochote ubovu wa tabia hii.

Hata kama waTanzania bado wanayo mashaka ya vyama vya upinzani kuwa na uwezo wa kutawala, ni kuwaweka wengi wao zaidi bungeni ili wapate huo uzoefu wanaoutaka, mbali ya kuwa na sababu mhimu zaidi ya kumzuia Magufuli na Ndugai kumiliki kila kitu.

Nisirefushe sana mawazo haya, nadhani ninachotaka kukieleza, hata kama sikukinyoosha kitakuwa kimeeleweka.

WaTanzania wahimizwe na waache tabia ya kurundika bungeni wabunge wengi toka chama kimoja, hasa hiki chama cha CCM.
WaTanzania wawapeleke wabunge wengi toka upinzani Bungeni, angalao hata wafikie nusu ya wabunge waliomo humo.

Naomba nieleweke vizuri. Sijaandika mahala popote kwamba Magufuli ni lazima ashinde kura hapo Oktoba. Lakini kama akilazimisha kushinda, hata hao wabunge wengi atalazimisha wananchi wakubali?

(Sikuhariri).
 
Chadema mnapofanya siasa zenu tambueni kuwa ni ngumu kuchukua nchi bila kufanya urafiki na vyombo vya ulinzi na usalama. Either mtatumia umwagaji damu, Vyombo vya ulinzi ndio watanzania wenyewe ukiona umekubalika 50% kwa watanzania na ndani ya ulinzi ndio hivyo hivyo, maafisa wa vyombo wanataka kujilidhisha na sera zenu juu yao.

Hivyo wapinzani mnapotaka kufanya siasa msijitenge na vyombo kama Police, TISS na JWTZ ni ushauri wangu tu wa leo kuvishutumu vyombo vya ulinzi mala kwa mala mtajenga kutoaminika kupewa nchi ndio maana wanawasumbua sana maana wanajuwa mkiingia mtawageuka na kuwachukulia hatua. Siasa imebadilika vyombo vya usalama ni muhimu ili kwenda hasa ikulu.

Ili jambo litaponza upinzani miaka mingi sana na tutachelewa kuondoa mfumo mbovu wa taifa endapo upinzani hautabadilika na kuwa upinzani wa sera za mageuzi na sio lawama kwa vyombo vya usalama siasa zetu tuzifanye na kumshutumu Magufuli lakini sio taasisi za ulinzi wa nchi.
Hii mada yako inayo matatizo.

Vyama vya siasa (upinzani) haiwalazimu kusifu maofisa wa serikali na hao polisi kama wanafanya uhalifu kwa kuogopa wasipendelewe, au iwasaidie kuingia kwenya madaraka.

Vyama vya upinzani haiwalazimishi kunyamazia uvunjaji wa sheria yoyote, eti wasihatarishe nafasi yao ya kupata ushindi.

La mhimu hapa, ni vyama vya siasa kukemea maovu yote, uvunjifu wote wa sheria kila unapotokea bila kujali ni nani anahusika na makosa hayo.

Haya ninayoandika hapa, sio kwamba hivi vyama havihitaji kuwa na urafiki na maelewano na hivyo vyombo vyote vinavyohusika.
Hawa ni waTanzania kama tulivyo sote. Kama sera na uongozi mzuri unaonekana huko kwenye upinzani, hata hawa waTanzania watayaona hayo mazuri na kuyaunga mkono.
 
.vyama vya upinzani vikiweza kupata mgombea ambaye ana mvuto, hata kama atashindwa ktk kura za Uraisi, anaweza kuwasaidia kupata wabunge wengi.
Mfano wa Ngoyayi na CHADEMA, 2015?

Safari hii inaweza ikawa tofauti kidogo, hasa kutokana na tuliyoyaona kwa mgombea wa CCM.
Hii ni kazi wanayotakiwa kuisisitiza vyama vya upinzani kwa wananchi ili waelewe.
 
Mfano wa Ngoyayi na CHADEMA, 2015?

Safari hii inaweza ikawa tofauti kidogo, hasa kutokana na tuliyoyaona kwa mgombea wa CCM.
Hii ni kazi wanayotakiwa kuisisitiza vyama vya upinzani kwa wananchi ili waelewe.

..Lowassa afya yake haikuwa nzuri, and he did not put up any fight.

..pia kampeni yake ilikuwa out of sync na kampeni za wabunge wa ukawa.

..zaidi mgombea wa ccm, Magufuli, alifanya mikutano mingi ya kampeni kuliko mgombea wa ukawa, Lowassa.

..vilevile kulikuwa na media blackout kwa mgombea uraisi wa ukawa na wagombea ubunge.

..lakini pia Lowassa alipata kura nyingi ambazo hazi-reflect udhaifu wa kampeni aliyofanya.
 
Mkuu JokaKuu,

Kwanza nianze kwa kukataa hoja ya mleta mada; pamoja na kwamba sijasoma aliyowasilisha ndani ya mada yake. Nakataa nadharia yake kutokana na kichwa cha habari aliyowasilisha.

Lakini hili siyo lililonivuta kuja hapa na kuitikia wito wako.

Nimekusoma kwa haya uliyojadili hapo juu, na mimi nikaona nidandie hapo hapo kuweka yale ambayo nimekuwa nikiyawaza kwa muda mrefu kidogo kuhusu siasa zetu hizi za Tanzania.

Nimekuwa nikiwaza mawazo haya niyaanzishe mada yake pembeni, lakini nimekuwa nikisita.

Nitatumia nafasi hii kuyaweka hapa na wewe pamoja na wasomaji wengine pengine mkiona yanastahili mjadala mkubwa, basi, utakuwa ni mwanzo wa kuyaeneza.

Tumekuwa na vyama vya upinzani kwa muda mrefu sasa, tokea 1995, na tokea hapo takribani vyama vyote vilivyotaka kushiriki vimekuwa huru kushiriki kwenye chaguzi mbali mbali na Chaguzi Kuu za Rais na Wabunge.

Mara zote hizi CCM ndio imekuwa mshindi, kwa kura nyingi kwa Rais, na kupata wabunge wengi. Ni mara chache sana, sikumbuki uchaguzi uliofanyika CCM ikakosa kupata wabunge zaidi ya nusu Bungeni.

Imekuwa hivyo nyakati zote, kiasi cha kwamba, nadhani yamekuwa ni mazoea kwa watu kutegemea CCM ishinde na kupata wabunge wengi.
Nasema imekuwa mazoea, kwa sababu hakuna anayeuliza kwa nini iwe hivyo kila mara?

Vyama vya upinzani, naona kwa sababu nisizozielewa, hili haliwasumbui, kwa sababu huwa sisikii wakilijadili wala kulisemea kwenye kampeni ili watu walijue. Mara zote, nasisitiza, kwa sababu sina ushahidi tofauti ya haya ninayoyaandika, mara zote, wapinzani lengo lao ni kushinda urais na wabunge wengi bungeni kama anavyofanya CCM. Hilo ndilo huwa wanalisisitiza mara zote.

Sasa najiuliza, kwa nini iwe hivyo? Na hasa baada ya Rais Magufuli kuonyesha wazi anavyopenda na kufaidika na ushindi wa asili mia. Ule wa serikali za mitaa bado hakuridhika na asili mia tisini na tisa; atafurahi safari hii Oktoba akipata 100%!

Baada ya kuona aliyofanya tokea 2015, kwa nini waTanzania wasielezwe; hapana, wasikumbushwe athari ya mazoea yao ya kuchagua CCM na wabunge karibu wote Bungeni kuwa wa CCM?

WaTanzania wanahitaji kukumbushwa na kutahadharishwa waache hii tabia ya kuchagua chama kimoja na kukirundikia madaraka yote.

Magufuli na Ndugai wametuonyesha waziwazi bila ya kificho chochote ubovu wa tabia hii.

Hata kama waTanzania bado wanayo mashaka ya vyama vya upinzani kuwa na uwezo wa kutawala, ni kuwaweka wengi wao zaidi bungeni ili wapate huo uzoefu wanaoutaka, mbali ya kuwa na sababu mhimu zaidi ya kumzuia Magufuli na Ndugai kumiliki kila kitu.

Nisirefushe sana mawazo haya, nadhani ninachotaka kukieleza, hata kama sikukinyoosha kitakuwa kimeeleweka.

WaTanzania wahimizwe na waache tabia ya kurundika bungeni wabunge wengi toka chama kimoja, hasa hiki chama cha CCM.
WaTanzania wawapeleke wabunge wengi toka upinzani Bungeni, angalao hata wafikie nusu ya wabunge waliomo humo.

Naomba nieleweke vizuri. Sijaandika mahala popote kwamba Magufuli ni lazima ashinde kura hapo Oktoba. Lakini kama akilazimisha kushinda, hata hao wabunge wengi atalazimisha wananchi wakubali?

(Sikuhariri).

..Mkuu asante sana.

..umeweza kueleza kwa ufasaha mkubwa kile nilichokuwa najaribu kukieleza.

..natumaini wapinzani watarekebisha makosa ya 2015. Na baadhi yao wanakiri mapungufu ya kampeni yao ya 2015.
 
leo umewaza mbali sana kuleta wazo kma hili, ila siyo lazima viwe upande wako pale ambapo kuna demokrasia ya kweli, kumbuka Ivory Coast, jamaa alikuwa na vyombo vya usalama pmja na jeshi lote nyuma yake, lakini wananchi waliamua...Tunisia, Misri ni mifano tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Alupishana na system ikambwga
 
Chadema mnapofanya siasa zenu tambueni kuwa ni ngumu kuchukua nchi bila kufanya urafiki na vyombo vya ulinzi na usalama. Either mtatumia umwagaji damu, Vyombo vya ulinzi ndio watanzania wenyewe ukiona umekubalika 50% kwa watanzania na ndani ya ulinzi ndio hivyo hivyo, maafisa wa vyombo wanataka kujilidhisha na sera zenu juu yao.

Hivyo wapinzani mnapotaka kufanya siasa msijitenge na vyombo kama Police, TISS na JWTZ ni ushauri wangu tu wa leo kuvishutumu vyombo vya ulinzi mala kwa mala mtajenga kutoaminika kupewa nchi ndio maana wanawasumbua sana maana wanajuwa mkiingia mtawageuka na kuwachukulia hatua. Siasa imebadilika vyombo vya usalama ni muhimu ili kwenda hasa ikulu.

Ili jambo litaponza upinzani miaka mingi sana na tutachelewa kuondoa mfumo mbovu wa taifa endapo upinzani hautabadilika na kuwa upinzani wa sera za mageuzi na sio lawama kwa vyombo vya usalama siasa zetu tuzifanye na kumshutumu Magufuli lakini sio taasisi za ulinzi wa nchi.
Nguvu za Umma. Enough

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna msemaji mmoja aliwah sema"Dawaamul haal minal muhaal "Mambo hayawezikuwa ktk hali moja daima ipo cku yatabadilika hata kama itachukuwa karne
umma upi?
kumbuka maandamano ya nchi nzima mliringishiwa polisi kidoogo mkatepeta hata road hamjaingia.maneno matupu tu kama kipigo cha mbwa koko,mtapigwa mchakae.mkaogopa.
hayo mambo ya umma sio tanzania.watanzania ni wapole wa kupitiliza.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
system ilimkubali magufuri?
kama ilimkubali na swali lingine kwako
System ilimkubali Magufuli baada ya kuona kuwa wananchi walio wengi wamechoka na ufisadi uliokuwa ukiendelea serikali ambao ulihatarisha usalama Wa nchi kuwa nchi ingeweza ingia kwenye machafuko na mapinduzi kutokana na hasira za wananchi zilivyokuwa Kali ndio maana System ikampiga chini fisadi lowasa ndani ya CCM na ikampiga chini alipogombea kupitia chadema TISS ikampeleka Kipilimba tume ya Uchaguzi akasimamie uhesabu kura kwenye kitengo cha IT kuhakikisha fisadi Lowasa hapiti

Kiuhalisia dola ni vyombo vyombo vya dola kushindana navyo na kutokuwa na uhusiano mzuri so rahisi kufikia malengo ya kushika dola.Kushika dola ni kushika vyombo vya dola unavishikaje wakati huivi navyo utaishia tu kupigwa marungu mitaani

Na mwanasiasa bora ni yule anayehakikisha anakubalika kwenye makundi yote ikiwemo vyombo vya dola sababu pia ni wapiga kura wake na pia wana maamuzi ya kuamua ashinde uraisi au la kupitia systems zao

Mleta mada uko sahihi chadema wanahitaji system kushika nchi na walianza kuwa nayo kipindi cha DR Slaa System ndio walikuwa wakimpa zile takwimu nyeti za mafisadi kuanzia Richmond nk chadema wakatibua mwishoni walipomchukua Lowasa ambaye systems ilikuwa haimtaki kwa ufisadi ndio.maana wajua inside information ya hil DR Slaa na Profesa lipumba wakaamua kujiondoa UKAWA kuungana na System kumpinga Lowasa Fisadi na Seif alipiungana na Lowasa UKAWA system ikahamishia mashambulizi uchaguzi mkuu Wa Zanzibar kuhakikisha Seif hapati uraisi walala mbunge wala mjumbe Wa baraza la wawakilishi na wakaendelea kunshughulikia hadi akanyanganywa chama cha CUF wakampa Profesa Lipumba sasa hivi Seif yuko ICU ACT wazalendo anapumulia mashine ya kisiasa na System imemshughulikia Lowasa barabara ndani ya chadema karudi CCM anachechemea kwa kutenguliwa kiuno cha kisiasa akiwa humo humo ndani ya chadema!!

CUF baada ya Profesa Lipumba kushika uenyekiti ikajitoa UKAWA na Karibuni tu system imekamilisha kazi ya kuhakikisha NCCR inajitoa UKAWA sasa hivi hakuna UKAWA!!!! Na bado mission not yet accomplished!!! Chadema endeleeni tu kuchezea sharubu za simba vyombo vya dola mtapata majibu
Mleta mada yuko sahihi kwa asilimia mia moja
 
Back
Top Bottom