Huwezi lazimisha Mwanamke akuheshimu, Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda

Huwezi lazimisha Mwanamke akuheshimu, Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
HUWEZI LAZIMISHA MWANAMKE AKUHESHIMU, MWANAMKE ANAMHESHIMU MWANAUME ANAYEMPENDA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Wanaume wengi hudhani kúmpiga Mwanamke ndio humfanya Mwanamke awe mtiifu na mwenye heshima. Wengine huwafokea na kuwatukana na kuwatolea maneno makali kwa kudhani kufanya hivyo ndio humfanya Mwanamke amheshimu.
Elewa Mwanamke sio mtoto mpaka umpige. Elewa, Mwanamke ni kiumbe pekee chenye kisasi. Elewa Mwanamke hawezi kusahau jambo baya lolote hata moja ambalo umemfanyia hasa ukimpiga àu kumfanyia ushenzi wowote.

Wazee wetu wengi wakifikisha miaka kuanzia hamsini (50+yrs) huanza kupewa kiinua mgongo chao kwa yale yote waliyofanyia Wake zao kipindi cha nyuma.
Sasa kijana anapompiga mkewe, au kumfokea kwa maneno ya kudhalilisha, alafu akaona Mwanamke wake amekaa kimya wanadhani ndio heshima imerudi. Kumbe hawa viumbe wamejiweka kiporo ambacho wanauhakika watakinywea na chai ya moto yenye tangawizi na mdalasini. Wakati huo kiporo ambaye ni wewe utakuwa wabaridi umepoa unakaribia kuchacha.

Asije akakudanganya mtu kuwa kukusanya pesa pekee kutakuondoa na kadhia ya mkeo uliyemnyanyasa. Njia pekee labda ni kupeana talaka. Vinginevyo hata uwe nani, nasema hata uwe nani. Lazima upasuke.

Wengine hufikiria heshima wataipata kwa kutoa pesa, na hiyo hupelekea kutafuta pesa kwa nguvu zote na kuwapa wake zao lakini mwisho wa siku heshima hawapewi.

Taikon Master kama mtaalamu wa saikolojia, falsafa, na mwanasosholojia ninakuambia kuwa kwenye hii dunia Mwanamke hawezi kukuheshîmu kisa unampa pesa, au kukuheshîmu kisa unampiga. Huwezi force heshima ya Mwanamke kwako.

Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda bila kujali mwanaume huyo yupo katika nafasi ipi,

Hata uwe Rais, hata uwe mfalme, hata uwe mkuu majeshi, hata uwe nani. Mwanamke ambaye utamuita mkeo au ambaye utalala naye uchi mkakutana kimwili hawezi kukuheshîmu kisa hicho cheo chako au mapesa yako.

Mwanamke huogopa zaidi kumsaliti mwanaume anayempenda kuliko kitu chochote.
Kuwa mkuu wa majeshi, au Rais au jambazi hakumuogopeshi Mwanamke asiku-cheat.

Elewa Mwanamke woga wake upo katika hisia zake. Mwanamke anaogopa zaidi kupoteza kile kinachompa furaha.
Elewa, Mwanamke anaheshimu kile kinachompa furaha. Na mtu anayempenda raha ndiye anayempa raha.

Ukiona upo kwenye kundi la wale wanaume wanaodhani wanawake hawatoi pesa zao kwa wanaume jua huyo Mwanamke uliyenaye hakupendi. Na kama hakundi automatically hakuheshimu wala kukutii ila anakuigizia.

Ukiona upo na mwanamke ambaye chake ni chake lakini chako ni Chenu be aware, huyo hakupendi na automatically hakuheshimu ila anachokifanya ni unafiki.

Mtu anayesema Mwanamke hapendi lakini anapaswa awe mtiifu anashindwa kuelewa kuwa Utiifu ni matokeo ya upendo uliopitiliza.
Kumaanisha Mwanamke anatakiwa akupende sana ili awe mtiifu kwako. Huwezi mtii mtu usiyempenda. Kama unamtii mtu usiyempenda tafsiri yake ni kuwa unamwogopa.
Kuna heshima au Utiifu na kuja hofu au Woga.

Elewa kuwa hakuna pesa yoyote ya kununua upendo wa Mwanamke, asije akakudanganya mtu yeyote.
Utapigwa na kitu kizito. Upendo haununuliwi.

Elewa, Wanawake huipata pesa kipaombele baada ya ku - disappontiwa, kuumizwa na kusalitiwa na wanaume wanaowapenda.
Mwanamke yeyote aliyeumizwa na mwanaume aliyempenda sana hubadilika kwa kiwango cha juu.

Elewa huwezi fanya lolote kumpa furaha Mwanamke ambaye hana furaha. Furaha ya Mwanamke ipo kwa mwanaume anayempenda.

Usijesema sikukwambia. Hivyo ndivyo utakavyoishi ña Wanawake Mwanangu

Robèrt Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Hapa nakuunga mkono ila kwenye ile mada ya kumruhusu mwanamke aende semina ya wiki3 kisa yuko kazini hapana siwezi kuunga mkono!

Mwanamke kama anakupenda hilo sio tatizo

Tatizo linakuja wengi huoa na kuunda familia na wanawake ambao wanajua kabisa hawawapendi. Na ndio hayo ya kumzuia asiende kwa hofu ya kuchapiwa.

Mwanamke anayesaliti anakusaliti akiwa nyumbani kwako moyoni. Mwilini anapoenda kuchapwa ni matokeo ya usaliti uliopo moyoni mwake ambao upo hata úkimfungia ndani.
 
# ROCA FELLA

MWANAMKE AMEUMBWA NA MADHAIFU MENGI KULIKO MWANAUME INGAWAJE WANA WA ADAMU WOTE TUNA MADHAIFU YETU, MWANDISHI AMEELEZA NA KUFAFANUA MADA KAMA IPASAVYO PONGEZI KWAKE.

USHAURI ZAIDI, KWA SASA DUNIA INAZIDI KWENDA KASI KILA KITU KINABADILIKA HASA UPANDE WA MAPENZI IMEKUWA NI MWIBA KWA WAPENZI NA WANA NDOA WENGI WANAPITIA CHANGAMOTO NYINGI LAKINI MSICHOKE KUMWOMBA MOLA MLEZI YEYE NI MLEZI WA WOTE KILA MWENYE KUHITAJI HURUMA YAKE.
 
Dhana ya upendo na kusaliti itazame vizuri si kinadharia si kivitendo kusaliti kuna sababu nyingi sana kupenda sio ishu ya kuzaliwa kuhusu mpendwa na matokeo ya safarini Duniani, vysnzo vingi ushawishi, umaskini, tamaa, hulka na mengine mengi, upime upendo na kusaliti kwa benchmarking na uwepo wa sababu za usaliti na nguvu ya hizo sababu katika kuushinda moyo wa upendo, pia yapo mazingira ya kiu na upweke itazame vizuri hio hoja.

Sijamaanisha umekosea ila ipo haja ya kuexploit hio expansive thinking na analysis ya hio kitu kuna vitu ni inherent na kuna vitu kuhusu externalities
 
# ROCA FELLA

MWANAMKE AMEUMBWA NA MADHAIFU MENGI KULIKO MWANAUME INGAWAJE WANA WA ADAMU WOTE TUNA MADHAIFU YETU, MWANDISHI AMEELEZA NA KUFAFANUA MADA KAMA IPASAVYO PONGEZI KWAKE.

USHAURI ZAIDI, KWA SASA DUNIA INAZIDI KWENDA KASI KILA KITU KINABADILIKA HASA UPANDE WA MAPENZI IMEKUWA NI MWIBA KWA WAPENZI NA WANA NDOA WENGI WANAPITIA CHANGAMOTO NYINGI LAKINI MSICHOKE KUMWOMBA MOLA MLEZI YEYE NI MLEZI WA WOTE KILA MWENYE KUHITAJI HURUMA YAKE.

Hatari sana
 
Dhana ya upendo na kusaliti itazame vizuri si kinadharia si kivitendo kusaliti kuna sababu nyingi sana kupenda sio ishu ya kuzaliwa kuhusu mpendwa na matokeo ya safarini Duniani, vysnzo vingi ushawishi, umaskini, tamaa, hulka na mengine mengi, upime upendo na kusaliti kwa benchmarking na uwepo wa sababu za usaliti na nguvu ya hizo sababu katika kuushinda moyo wa upendo, pia yapo mazingira ya kiu na upweke itazame vizuri hio hoja.

Sijamaanisha umekosea ila ipo haja ya kuexploit hio expansive thinking na analysis ya hio kitu kuna vitu ni inherent na kuna vitu kuhusu externalities

MTU anayekupenda ni ngumu kukusaliti Mkuu

Ingawaje mazingira ya usaliti hutokea kwa namna inayoanzia ndani zaidi kuliko nje.
Usaliti huanzia ndani sio nje.
Ndio maana wasaliti hawasamehewi kwa sababu kuu ni kuwa usaliti haupo nje, usaliti upo ndani ya mtu. Mtu kama hakupendi kukusaliti ni matokeo tuu.
Usaliti ndio tafsiri halisi ya kutokuwa na upendo wa kweli.

Vinginevyo useme ule usaliti wa kushikiwa bunduki kwa lazima ambao kwa tafsiri sahihi hauitwi usaliti
 
Ndio maana hata Mungu alikuwa analazimisha aheshímiwe kinguvu. Iliishia wapi?
Ni wapi Mungu alilazimisha upendo kiongozi?

By the way
Kuna mwanamke nilikuwa nae tukawa tunaishi maisha ya ligi sana kutukanana
Siku moja nikamkusanya.

longtime nilishajua huyu sitawezana nae na mwisho wangu na yeye utakuwa ni wa visasi ni yule mwanamke ukikaa nae anazungumzis yale mabaya tu hana nzuri analoweza kuzungumza
nilizaa nae mtoto mmoja.

Niliona bora tu tuachane.
 
MTU anayekupenda ni ngumu kukusaliti Mkuu

Ingawaje mazingira ya usaliti hutokea kwa namna inayoanzia ndani zaidi kuliko nje.
Usaliti huanzia ndani sio nje.
Ndio maana wasaliti hawasamehewi kwa sababu kuu ni kuwa usaliti haupo nje, usaliti upo ndani ya mtu. Mtu kama hakupendi kukusaliti ni matokeo tuu.
Usaliti ndio tafsiri halisi ya kutokuwa na upendo wa kweli.

Vinginevyo useme ule usaliti wa kushikiwa bunduki kwa lazima ambao kwa tafsiri sahihi hauitwi usaliti
Taikoni, uko sahihi hakuna usaliti wa bahati mbaya usaliti hupangwa
 
MTU anayekupenda ni ngumu kukusaliti Mkuu

Ingawaje mazingira ya usaliti hutokea kwa namna inayoanzia ndani zaidi kuliko nje.
Usaliti huanzia ndani sio nje.
Ndio maana wasaliti hawasamehewi kwa sababu kuu ni kuwa usaliti haupo nje, usaliti upo ndani ya mtu. Mtu kama hakupendi kukusaliti ni matokeo tuu.
Usaliti ndio tafsiri halisi ya kutokuwa na upendo wa kweli.

Vinginevyo useme ule usaliti wa kushikiwa bunduki kwa lazima ambao kwa tafsiri sahihi hauitwi usaliti
Nashauri uwe elastic kwenye hili la upendo na usaliti, mwanamke Hana nafsi ya kupenda na hata akiitumia ni kwa muda tu, mwanamke kaumbiwa kumheshimu na anaheshimu anaemzidi na anaetimiza matarajio yake ya Nafsi na mwili, ndiomana mwanamke huyo huyo akiwa na Mali hupunguza heshima na huona umuhimu wa yeye kuwa kichwa na kuishi peke yake.
 
Back
Top Bottom