Huwezi lazimisha Mwanamke akuheshimu, Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda

Huwezi lazimisha Mwanamke akuheshimu, Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda

Ni wapi Mungu alilazimisha upendo kiongozi?

By the way
Kuna mwanamke nilikuwa nae tukawa tunaishi maisha ya ligi sana kutukanana
Siku moja nikamkusanya.

longtime nilishajua huyu sitawezana nae na mwisho wangu na yeye utakuwa ni wa visasi ni yule mwanamke ukikaa nae anazungumzis yale mabaya tu hana nzuri analoweza kuzungumza
nilizaa nae mtoto mmoja.

Niliona bora tu tuachane.

Soma kwenye Torati utaona vile Yehova alivyokuwa analazimisha Watu waheshimu maagizo yake lakini iliishia wapi?

Tena huyo anayezungumzia mabaya yako mbele yako ni mzuri kuliko yule mkimya ambaye mabaya yako yapo kwa mashoga zake au huko mtañdaoni kwa utambulisho wa anonymous
 
Nashauri uwe elastic kwenye hili la upendo na usaliti, mwanamke Hana nafsi ya kupenda na hata akiitumia ni kwa muda tu, mwanamke kaumbiwa kumheshimu na anaheshimu anaemzidi na anaetimiza matarajio yake ya Nafsi na mwili, ndiomana mwanamke huyo huyo akiwa na Mali hupunguza heshima na huona umuhimu wa yeye kuwa kichwa na kuishi peke yake.

Mwanamke anapenda kama ilivyo mwanaume. Tena anapenda zaidi ya mwanaume ndio maana huwa mtiifu.
Huwezi kumtii mtu usiyempenda.

Pesa haibadili moyo wa mtu akiwepo hiyo Mwanamke.
Pesa inampa uhuru mtu wa kuonyesha hulka yake halisi.

Mwanamke kama alikuwa hakupendi akiwa na pesa ndio wakati wa kuonyesha kile ambacho ulikuwa hukioni.

Pia elewa, hata ukizeeka au ukiishiwa au kufilisika ndio wakati ambao Mwanamke atakuwa huru kuonyesha yaliyomoyoni mwake. Kama alikuwa hakupendi ndio utajua lakini kuna kulipa kisasi.

Hata wanaume sisi tulipata hizo pesa mbona wengi tunaanzisha mahusiano mengine na kuwa na MICHEPUKO au kuoa kabisa wanawake wengine?
Sio kwamba pesa ndio zimetubadilisha, ila pesa zimetupa uhuru wa kujionyesha dhahiri sisi ni watu wa aina gani.

Mwanamke anapenda. Sema wengi hawapati bahari ya kuolewa na wanaume wanaowapenda ndio maana unasema ulichokisema
 
Mapenzi ya dhati yanaendana na kutimiza majukumu ipasavyo, mwanamke asipokuwa na stress upendo wake kwako utaongezeka, na hata kama ikitokea mara moja moja umekosa hawezi kuwa na shida.

Tatizo linakuja pale utaposhindwa kutimiza majukumu ipasavyo, akachoka kukuvumilia hata kama alikuwa anakuoenda kwa dhati, ukamlazimu mwanamke aanze kujichanganya kwa ajili ya kuihudumia familia, akishaanza kukutana na watu tofauti huku akiwa na akili ya kutafuta, penda usipende upendo wake kwako na heshima vitaanza kupungua.

Umeandika uzi wako kama vile upendo na heshima vya mwanamke kwa mwanaume ampendae ni constant, havipungui, no way, hivyo vyote lazima ujue namna ya kuvitunza kwa ajili ya manufaa yako.
 
Mapenzi ya dhati yanaendana na kutimiza majukumu ipasavyo, mwanamket asipokuwa na stress upendo wake kwako utaongezeka, na hata kama ikitokea mara moja moja umekosa hawezi kuwa na shida.

Tatizo linakuja pale utaposhindwa kutimiza majukumu ipasavyo, ukamlazimu mwanamke aanze kujichanganya kwa ajili ya kuihudumia familia, akishaanza kukutana na watu tofauti huku akiwa na akili ya kutafuta, penda usipende upendo wake kwako na heshima vitaanza kupungua.

Umeandika uzi wako kama vile upendo na heshima vya mwanamke kwa mwanaume ampendae ni constant, havipungui, no way, hivyo vyote lazima ujue namna ya kuvitunza kwa ajili ya manufaa yako.

Upo sahihi Mkuu.

Upendo na furaha hulindwa. Majukumu na wajibu ni sehemu ya kuvilinda.
Ningeeléza kila kitu uzi ungekuwa mrefu alafu waja wangekuja
 
HUWEZI LAZIMISHA MWANAMKE AKUHESHIMU, MWANAMKE ANAMHESHIMU MWANAUME ANAYEMPENDA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Wanaume wengi hudhani kúmpiga Mwanamke ndio humfanya Mwanamke awe mtiifu na mwenye heshima. Wengine huwafokea na kuwatukana na kuwatolea maneno makali kwa kudhani kufanya hivyo ndio humfanya Mwanamke amheshimu.
Elewa Mwanamke sio mtoto mpaka umpige. Elewa, Mwanamke ni kiumbe pekee chenye kisasi. Elewa Mwanamke hawezi kusahau jambo baya lolote hata moja ambalo umemfanyia hasa ukimpiga àu kumfanyia ushenzi wowote.

Wazee wetu wengi wakifikisha miaka kuanzia hamsini (50+yrs) huanza kupewa kiinua mgongo chao kwa yale yote waliyofanyia Wake zao kipindi cha nyuma.
Sasa kijana anapompiga mkewe, au kumfokea kwa maneno ya kudhalilisha, alafu akaona Mwanamke wake amekaa kimya wanadhani ndio heshima imerudi. Kumbe hawa viumbe wamejiweka kiporo ambacho wanauhakika watakinywea na chai ya moto yenye tangawizi na mdalasini. Wakati huo kiporo ambaye ni wewe utakuwa wabaridi umepoa unakaribia kuchacha.

Asije akakudanganya mtu kuwa kukusanya pesa pekee kutakuondoa na kadhia ya mkeo uliyemnyanyasa. Njia pekee labda ni kupeana talaka. Vinginevyo hata uwe nani, nasema hata uwe nani. Lazima upasuke.

Wengine hufikiria heshima wataipata kwa kutoa pesa, na hiyo hupelekea kutafuta pesa kwa nguvu zote na kuwapa wake zao lakini mwisho wa siku heshima hawapewi.

Taikon Master kama mtaalamu wa saikolojia, falsafa, na mwanasosholojia ninakuambia kuwa kwenye hii dunia Mwanamke hawezi kukuheshîmu kisa unampa pesa, au kukuheshîmu kisa unampiga. Huwezi force heshima ya Mwanamke kwako.

Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda bila kujali mwanaume huyo yupo katika nafasi ipi,

Hata uwe Rais, hata uwe mfalme, hata uwe mkuu majeshi, hata uwe nani. Mwanamke ambaye utamuita mkeo au ambaye utalala naye uchi mkakutana kimwili hawezi kukuheshîmu kisa hicho cheo chako au mapesa yako.

Mwanamke huogopa zaidi kumsaliti mwanaume anayempenda kuliko kitu chochote.
Kuwa mkuu wa majeshi, au Rais au jambazi hakumuogopeshi Mwanamke asiku-cheat.

Elewa Mwanamke woga wake upo katika hisia zake. Mwanamke anaogopa zaidi kupoteza kile kinachompa furaha.
Elewa, Mwanamke anaheshimu kile kinachompa furaha. Na mtu anayempenda raha ndiye anayempa raha.

Ukiona upo kwenye kundi la wale wanaume wanaodhani wanawake hawatoi pesa zao kwa wanaume jua huyo Mwanamke uliyenaye hakupendi. Na kama hakundi automatically hakuheshimu wala kukutii ila anakuigizia.

Ukiona upo na mwanamke ambaye chake ni chake lakini chako ni Chenu be aware, huyo hakupendi na automatically hakuheshimu ila anachokifanya ni unafiki.

Mtu anayesema Mwanamke hapendi lakini anapaswa awe mtiifu anashindwa kuelewa kuwa Utiifu ni matokeo ya upendo uliopitiliza.
Kumaanisha Mwanamke anatakiwa akupende sana ili awe mtiifu kwako. Huwezi mtii mtu usiyempenda. Kama unamtii mtu usiyempenda tafsiri yake ni kuwa unamwogopa.
Kuna heshima au Utiifu na kuja hofu au Woga.

Elewa kuwa hakuna pesa yoyote ya kununua upendo wa Mwanamke, asije akakudanganya mtu yeyote.
Utapigwa na kitu kizito. Upendo haununuliwi.

Elewa, Wanawake huipata pesa kipaombele baada ya ku - disappontiwa, kuumizwa na kusalitiwa na wanaume wanaowapenda.
Mwanamke yeyote aliyeumizwa na mwanaume aliyempenda sana hubadilika kwa kiwango cha juu.

Elewa huwezi fanya lolote kumpa furaha Mwanamke ambaye hana furaha. Furaha ya Mwanamke ipo kwa mwanaume anayempenda.

Usijesema sikukwambia. Hivyo ndivyo utakavyoishi ña Wanawake Mwanangu

Robèrt Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
1717910656112.png
 
Mapenzi ya dhati yanaendana na kutimiza majukumu ipasavyo, mwanamket asipokuwa na stress upendo wake kwako utaongezeka, na hata kama ikitokea mara moja moja umekosa hawezi kuwa na shida.

Tatizo linakuja pale utaposhindwa kutimiza majukumu ipasavyo, akachoka kukuvumilia hata kama alikuwa anakuoenda kwa dhati, ukamlazimu mwanamke aanze kujichanganya kwa ajili ya kuihudumia familia, akishaanza kukutana na watu tofauti huku akiwa na akili ya kutafuta, penda usipende upendo wake kwako na heshima vitaanza kupungua.

Umeandika uzi wako kama vile upendo na heshima vya mwanamke kwa mwanaume ampendae ni constant, havipungui, no way, hivyo vyote lazima ujue namna ya kuvitunza kwa ajili ya manufaa yako.


Hili neno "nakuvumilia -namvumilia " ni neno la kisiasa Sana.

Hakuna binadamu anayemvumilia mwenzake ikiwa unamuhudumia mwanamke au yeye anakuhudumia hakuna anayemvumilia mwenzake hapo.

Ni tafsiri mbaya Sana kusema nakuvumilia .
 
Nashauri uwe elastic kwenye hili la upendo na usaliti, mwanamke Hana nafsi ya kupenda na hata akiitumia ni kwa muda tu, mwanamke kaumbiwa kumheshimu na anaheshimu anaemzidi na anaetimiza matarajio yake ya Nafsi na mwili, ndiomana mwanamke huyo huyo akiwa na Mali hupunguza heshima na huona umuhimu wa yeye kuwa kichwa na kuishi peke yake.
Hujielewi
 
YAANI TAIKONI HUJAWAHI KUKOSEA SIJAWAHI KUKUPINGA UNAPIGAGA KWENYE MSHONO AISEE 🔥🔥
 
Mapenzi ya dhati yanaendana na kutimiza majukumu ipasavyo, mwanamket asipokuwa na stress upendo wake kwako utaongezeka, na hata kama ikitokea mara moja moja umekosa hawezi kuwa na shida.

Stress inategemea chanzo chake ni nini? Hata sisi wanaume tupo vivyohivyo
Tatizo linakuja pale utaposhindwa kutimiza majukumu ipasavyo, akachoka kukuvumilia hata kama alikuwa anakuoenda kwa dhati, ukamlazimu mwanamke aanze kujichanganya kwa ajili ya kuihudumia familia, akishaanza kukutana na watu tofauti huku akiwa na akili ya kutafuta, penda usipende upendo wake kwako na heshima vitaanza kupungua.
Mwanamke lazima aweze kuihudumia familia yake. Iwe yupo ndoani au hayupo. Mwanamke ni mtu kama alivyo mwanaume.
Na Mwanamke mtafutaji ndiye mwenye upendo wa dhati tofauti na yule ambaye anahudumiwa tuu nyumbani ambaye ndiye unayemuelezea hapo.

Umeandika uzi wako kama vile upendo na heshima vya mwanamke kwa mwanaume ampendae ni constant, havipungui, no way, hivyo vyote lazima ujue namna ya kuvitunza kwa ajili ya manufaa yako.
 
Bila shaka wewe ni mwanafalsafa na unaongozwa na hekima ,haki na upendo .

Iko hivyo.
Kuna vitu havilazimishwi hasa vitu vya asili ambavyo Mungu ameviumba. Vitu artificial vinaweza vikalazimishwa.

Kwa mfano mtu anaweza kulazimisha kujenga bondeni kwa kujaza kifusi lakini kiasili eneo lile ni bonde. Hivyo ipo siku isiyo na jina lazima mafuriko au madhara yatokee
 
Hili neno "nakuvumilia -namvumilia " ni neno la kisiasa Sana.

Hakuna binadamu anayemvumilia mwenzake ikiwa unamuhudumia mwanamke au yeye anakuhudumia hakuna anayemvumilia mwenzake hapo.

Ni tafsiri mbaya Sana kusema nakuvumilia .
Inategemea na muktadha, kweli kuvumiliana endlessly kunaweza kuwa kugumu, lakini kama pillars za upendo zipo kati yenu, basi upendo wenu hauwezi kuyumba.

Ndio maana huwa naamini sio kila mwanaume anayechupuka hampendi mke wake, anayechepuka huku akitimiza mahitaji yote ya familia yake kwangu anajielewa zaidi ya yule anayechupa huku akiwa haijali familia yake.
 
Wanawake ni kuwaacha kama walivyo, ila ukisema Unataka kudili na kilichomo ndani ya moyo wa mwanamke ni uwongozi. Ukiangalia hata kiimani ndiye kiumbe aliyeumbwa baada ya mwanaume lakini alikuja kuwa na nguvu hadi ya ushawishi ana na nyoka naku sababisha usaliti. Wanaume msijikite zaidi kuwafurahisha wanawake, hawatabiriki. We tenda mema ondoka zako vinginevyo natafuta magonjwa ya moyo na kesi za mauwaji.
 
Back
Top Bottom