Huwezi nishawishi Nyerere alikuwa Rais bora

Huwezi nishawishi Nyerere alikuwa Rais bora

Baadhi ya mabaya au ubovu wa Mwl. Nyerere:-
1. Kuiga, Kuanzisha na kuendeleza Sera na Itikadi Mbaya kabisa ya Siasa za Ukomunisti/Ujamaa hapa Tanzania.

Huu ndio ulikuwa mwanzo wa Kujenga Msingi mbovu wa Taifa la hovyo kabisa lililopo hivi sasa.
Itikadi na Sera ya Ukomunisti/Ujamaa ikaja kushindwa vibaya Sana huku yeye mwenyewe akishuhudia kwa macho yake kushindwa kwa itikadi yake aliyoileta hapa Tanzania kutoka kwa marafiki zake wa China, Urusi na Cuba.

2. Kutengeneza Taifa la Watu waoga, Wanyonge, dhaifu wa fikra wasiojitambua na Wala wasioweza kuhoji. Taifa la watu 'misukule'.

3. Kutengeneza au kuunda nchi isiyokuwa na Mipango-miji, hususani kupitia kwenye Sera yake mbaya kabisa ya ujamaa/Ukomunisti. Sera au Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti ndio ilikuwa chanzo Cha Kuanzishwa kwa Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, the Worse Operation that completely destroyed the Country and Town Planning process within the Country.
Arusha Declaration and Operation Vijiji also led to the Death of Real Estate Industry and its development.

Kupitia Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti, Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, Watu wengi sana walinyang'anywa Ardhi zao pamoja na majumba yao waliyokuwa wakimiliki. Nyumba nyingi sana za Watu zilitaifishwa, Leo hii nyumba hizo zinamilikiwa na Shirika la Nyumba (NHC).

4. Kutuletea Katiba ya nchi ambayo ni mbaya kabisa, isiyofaa na ambayo imesababisha na inaendelea kusababisha madhara makubwa sana kwa Raia. Katiba mbaya ambayo imewatengeneza Watawala wa nchi hii kuwa 'Miungu Watu.'
Vyote unavyoviona ni vibaya ni kwa sababu unavitazama katika mtazamo wa 2024, yeye Mwalimu na wasaidizi wake waliitazama dunia ya mwaka 1980 kurudi nyuma.

Tangu ameaga dunia ni miaka 25 robo karne, sisi tulioachwa duniani tumefanya nini kuubadili huo ubaya ili uwe ni uzuri?.
 
Vijana wenye hofu ni wale wa zamani, sio hawa watoto wa 2000.

Vijana wa sasa wanatembea na dunia nzima viganjani mwao kwa kutumia simu za kupangusa hawana sababu yoyote ya kuhofia chochote.
Hapana aisee, hawa wa sasa ndio wa hovyo na waoga kupita, aheri ya hao wa zamani

Hizo simu kutwa ni kuangalia ngono na kubeti na umbea umbea tu
 
Ikiwa huwa unapata wasaa wa kupita pita kwenye vijiwe vya kahawa kupoteza muda wanamokaa wazee aged 65+ ambao wengi wakati wa Mwl Nyerere walikuwa vijana lazima wakujaze ujinga.

Huyu mzee ililala hekima kubwa sana kichwani mwake japokuwa kwa wakati wake kuna ambao hawakutaka azitumie lakini alizilazimisha ndiyo maana mpaka sasa unaona tulivyo bora japo siyo bora wa kuringia ila at least tuna kitu.

View attachment 3089392
NB;Kipande kifupi cha hotuba yake tumia muda kidogo tu ukisikilize uelewe ilipo tofauti yake na wengine unaohisi wangekuwa bora kuliko yeye.
Nyerere alikuwa mdini kuliko kiongozi yeyote tangu uhuru, ndio maana alihubiri sana udini. Ukitaka kuamini, angalia leo hii Watanzania wamebeba sana udini kuliko mataifa mengine yote.
 
You're completely wrong and out of point.
1. (a) Endapo kama Ukomunisti lilikuwa wazo zuri kama unavyodai, Je, inawezekana vipi wazo liwe zuri halafu lishindwe kutekelezeka? How comes? Uzuri wake ni upi Basi?
(b) China Wana sera mseto, hawana utawala wenye itikadi Moja tu ya siasa za ukomunisti, Bali wamechanganya itikadi mbalimbali kama vile Ukomunisti, Ubepari. China walisha-adopt sera ya Ubepari tangu mwanzoni mwa miaka ya 1960 hata Urusi nao wapo hivyo hivyo, that's why ndani ya China au Urusi kuna makampuni makubwa Sana ya kutoka nchi za kibepari hususani nchi za Magharibi, e.g. Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Canada, Australia, n.k.
Aidha, hata kwenye hizo nchi za Magharibi nako pia kuna Makampuni makubwa Sana ya biashara kutoka China na Urusi. Na biashara kwenye makampuni hayo zinafanyika chini ya misingi ya siasa za kibepari, Wala siyo kwa misingi ya Ukomunisti. Sera za kibepari chini ya taasisi za kimataifa kama vile WB, IMF, WTO, n.k ndizo zinazotumika katika kuendesha biashara Kati ya mataifa hayo.
(c) Nchi za Afrika ya Kusini, Nigeria, Morocco, na Misri zilizopo barani Afrika ndizo baadhi ya nchi ambazo zinefanikiwa zaidi kutokana na Sera za Siasa za Ubepari. South Africa ni mfano mzuri zaidi kati ya hizo kwani Utawaka wa Makaburu uli-adopt Ubepari tangu mwishoni mwa miaka ya 1800's, hususani kuhusiana na suala zima la biashara ya madini ya Vito.
2. Ukomunisti huwafanya Watu kuwa dhaifu kifikra, hujenga raia waoga kwa watawala wao, husababisha raia kuwa wanafiki, wasioweza kuhoji, raia-misukule, n.k.
Aidha, South Africa siyo nchi ya kikomunisti.
3. Sera ya kuwaweka Watu pamoja aliyofanya Mwl. Nyerere chini ya Siasa za kikomunisti/ujamaa kamwe haikuwa na lengo zuri kwani iliua kabisa Real Estate Industry katika nchi hii.
Endapo kama Sera hiyo ingefanyika kwa kuzingatia misingi imara ya ubepari, basi sera hiyo ingetoa matokeo mazuri zaidi, na tena ingeing'arisha nchi kwa kuwa na Mipango-miji Bora katika bara hili.

4. Nyerere anastahili kubeba lawama nyingi zaidi kwa kuifanya nchi hii kuwa na misingi mibovu karibia kwenye kila nyanya za maisha ya Watu, ukianzia na kutunga Katiba ya nchi ambayo ni mbaya na isiyofaa.
Unaujuaji mwingi acha tukuache maana wewe unajua kilakitu
 
Utaamini vipi km alikuwa bora wakati wewe umeanza kuijua Tanganyika enzi za jiwe.
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
ulikuepo kipindi cha Tanganyika??? ubora wake unaanzia hapo sasa, alafu mtu kama wewe huwezi kuona ubora wake maana umesimuliwa mengi ya nyerere kuliko kuyaona
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Labda wewe ndio msukule!
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Nchi hii ina watu million 60, sio muhimu kukushawishi wewe
 
Back
Top Bottom