Huwezi nishawishi Nyerere alikuwa Rais bora

Huwezi nishawishi Nyerere alikuwa Rais bora

Nyerere ni raisi bora. Mwinyi akawa bora zaidi katika kuifungua nchi kiuchumi amabopo ilikua inaelekea kaburini. Mkapa akawa bora kwenye kuanzisha taasisi za kusimamia mambo muhimu ya nchi kama kodi n.k. Ila ni katika kipindi cha mkapa na kuendelea pesa za umma zikaanza kuibwa waziwazi kufadhili kampeni za chama. Baadae wakazaliwa mafisadi wanaodumu hadi kesho.
 
Nyerere ni the best, binafsi yangu sijaona taifa Africa ningependa niwe raia tofauti na Tanzania na hii imechangiwa na misingi aliyoiacha. Sema pia ni ujinga sana kuamini kwamba kila maamuzi yake yalikuwa sahihi.
 
Mimi nafikiri Nyerere si wa kulaumiwa. Tunamlaumu kwa uongozi wake wa miaka 24/25.
Tangu atoke madarakani ni miaka 40, tangu amekufa ni miaka 25. Kile alichokosea kwa miaka hiyo tumeshindwa kurekebisha kwa muda wote tangu ametoka madarakani.
Wa kulaumiwa ni sisi tulioachiwa nchi
Anapaswa kulaumiwa kwa sababu ameanzisha kujenga Msingi mbovu wa Uongozi katika Taifa hili.
Kumbuka: Nyumba imara huanza na ujenzi wa Msingi imara na ulio Bora.
 
Mkuu 'Stevo', napita tu na kujikumbusha.
Hayo maneno ndani ya mstari huo najuwa yametukoroga sana wewe na mimi; pamoja na kwamba naelewa unacho kisema hapa.
Kwangu, hayo ni maneno ya kisingizio tu cha rahisi rahisi tunapo tafuta njia za mkato kueleza kushindwa kwa viongozi wetu kuongoza wananchi wake.
Nilisha sema mara kadhaa, katika majibishano yetu humu. Hakuna nchi hata moja duniani isiyo kuwa na watu wenye tabia kama hizi zetu. Ubinafsi, ufisadi, majungu tele, n.k., Tofauti pekee kati ya baadhi ya nchi na nyingine ni uongozi unao amua kuwa na mwelekeo tofauti na tabia hizo mbovu tunazo semekana sisi tunazo.

Wachina ni wezi sana; kama tunavyo wajuwa sasa baada yao kuwa miongoni mwetu. Lakini nenda China uchunguze tabia hiyo ya wizi waliyo nayo na jinsi inavyo zimwa humo nchini mwao. Kuna baaddhi ya nchi ambazo tume aminishwa wao hawana tabia za hovyo hovyo, kutokana na imani zao za kidini. Lakini pamoja na kuwa na imani hizo tabia hizo mbovu zinazimwa kutokana na sheria na adhabu zilizopo zinazotishia hadi uhai wa watu hao wenye tabia mbovu.
Kwa nini sisi hapa tunataka watu wetu wawe kama malaika wakati hakuna juhudi na mikakati ya kuwaondolea ushawishi wa kufanya maovu?

Huo ni mfano mmoja tu wa tabia za kifisadi/wizi/ukwapuzi.
Hali ni hiyo hiyo hata katika kukosa wajibu wa kusimamia shughuli zao za kimaendeleo. Siyo kwamba ni wavivu, la hasha uongozi wetu haujaweka jitihada za kuwafanya waTanzania waweke juhudi zaidi katika ufanisi wa kazi zao, iwe maofisini, au hata kazi binafsi
Hakuna nchi ambayo haikuwa na wavivu, watu wasiopenda kujibidisha zaidi ya kuwa na chakula cha milo michache; lakini uongozi wa nchi unapambana na kuibadili hali hiyo.

Usinielewe vibaya. Sisemi kila mtu ndani ya nchi atakuwa sawa na mwingine, la hasha, lakini kimwelekeo wa jumla, nchi inakuwa na mwelekeo wa kufanya vizuri na siyo hao wavivu, majizi ndio wawe mifano ya kuigwa kama inavyo elekea kuwa kwetu hapa.

Nimekusoma toka mwanzo wa mada hii, na nina hakika kuwa kimsingi tunakubaliana kwa sehemu kubwa. Tatzo letu lilipo sasa nalielewa vizuri zaidi.

Nimekwisha sema leo na jana mara kadhaa kwamba tumemalizana; lakini nashangaa kujikuta nikirudi kuendelea na maongezi haya baina yetu. Lakini kwa vile nina ufahamu mpana kidogo juu yako sasa, nadhani yale maneno ya kichokonozi "upuuzi, mpumbavu, huna akili" yatapumzika sasa!

Lakini naomba usinichokoze tena, kwa kuwadharau waTanzania. Lawama zielekezwe mahali zinapo stahili kuelekezwa; hata kama ni kwa viongozi tunao waheshimu sana wakishindwa kutimiza wajibu wao wa kuongoza.
Inasemekana aliyepewa tenda ya ujenzi wa uwanja wa Taifa kwa upande wa China aliporudi kwao na kugundulika kaiba huku Tanzania serikali yao ilimnyonga. Lakini mtanzania aliyeshirikiana nae wizi huo katika michakato ya ujenzi mpaka leo yupo hai.

Hiyo ni tofauti ya China na Tanzania, nidhamu zetu hazifanani hata kidogo.
 
Kimsingi alikuwa wa hovyoo kabisa yaani watu alitujegea hofu, alituharibia mfumo mzuri wa Elimu Kwa kuondoka mtaala wa Cambridge,aliamini katika umaskini,alipora mali za watu,alitutoa relini kabisa watanzania wanaomaliza vyuo vikuu vyetu ni kiwango cha kata, hawana fulsa ya kuajiriwa popote Duniani,leo hii Kila mwanafunzi aliyeko chuo kikuu wala hazingatii kusoma anawaza apate cheti Kwa vyovyote vile,avae nguo za kijani awe chawa Ili apate teuzi basi inasikitisha sana
 
Kama watu kama Sinde wakiweka ukweli bila kumumunya maneno wangeongea mengi ila kakazania muungano tu
Wakati tunapewa uhuru kumbuka kukikuwa na hela nyingi sana yaani million za dollars na zilikuwa za serikali wakiwepo wazungu wakamwachia PM Nyerere
Viwanda vilikuwa vipya na vinafanya kazi
Hela zote zilienda wapi?
Baada ya miaka kadhaa tukaingizwa vitani kwa maneno ya kuwa Uwezo tunao
Hela zikaisha zote
Mpaka dawa za mswaki zikawa magendo
Halafu ikaja Uhujumu uchumi kwa sisi ilikuwa mengine
Ila vijana hawajui haya
Mkuu waafrica na watanzania mna low IQ
kama ndo ivo mbona ndege mmeshindwa kuendesha
Bandari mmeshindwa mmempa muarabu
Umeme bado hoe hae
Nipo mwanza kutoka ninapo ishi had ziwani km2 tu lakini mtaani hamna maji.

Singida dodoma kuna ukame lakini kila kona mmezungukwa na ukame ziwa tanganyika nyasa na victoria


Itoshe kusema Hata uachiwe Tirion ngap kama akili huna huna tu vitapukuchika kama vumbi.
Nyerere alikua geniuous kwene nchi ya mapopoma
 
Kimsingi alikuwa wa hovyoo kabisa yaani watu alitujegea hofu, alituharibia mfumo mzuri wa Elimu Kwa kuondoka mtaala wa Cambridge,aliamini katika umaskini,alipora mali za watu,alitutoa relini kabisa watanzania wanaomaliza vyuo vikuu vyetu ni kiwango cha kata, hawana fulsa ya kuajiriwa popote Duniani,leo hii Kila mwanafunzi aliyeko chuo kikuu wala hazingatii kusoma anawaza apate cheti Kwa vyovyote vile,avae nguo za kijani awe chawa Ili apate teuzi basi inasikitisha sana
Absolutely true.
 
Kimsingi alikuwa wa hovyoo kabisa yaani watu alitujegea hofu, alituharibia mfumo mzuri wa Elimu Kwa kuondoka mtaala wa Cambridge,aliamini katika umaskini,alipora mali za watu,alitutoa relini kabisa watanzania wanaomaliza vyuo vikuu vyetu ni kiwango cha kata, hawana fulsa ya kuajiriwa popote Duniani,leo hii Kila mwanafunzi aliyeko chuo kikuu wala hazingatii kusoma anawaza apate cheti Kwa vyovyote vile,avae nguo za kijani awe chawa Ili apate teuzi basi inasikitisha sana
Kuamini mtaala wa mzungu ni bora na kushindwa kudevelop mitaala yenu ni uwezo duni wa kufikiri.
We ulichobakiza ni kuolewa tu maana hata vitu inavobidi ujitengenezee unamuwaza mzungu
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Kwa Afrika viongozi bora wote hawakudumu.
 
Kuamini mtaala wa mzungu ni bora na kushindwa kudevelop mitaala yenu ni uwezo duni wa kufikiri.
We ulichobakiza ni kuolewa tu maana hata vitu inavobidi ujitengenezee unamuwaza mzungu
Wakati tunapata uhuru tulikuwa na wataalamu wa kutosha kudevelop mitaala?wewe vipi? Kenya na Uganda iliwasaidia ndiyo maana wapo hapo.Mzungu hauwezi kumkwepa tunanini tulichonacho siyo Cha mzungu?hapo sisi tulipo Kwa Africa mashariki hatuuziki popote pale tumebaki kusifia sifia tu choka mbaya sana na bado tutatoka wenyewe bara barani Muda ukifika
 
Mbona hata ss hatuna mpango wa kukushawishi baki na mawazo yako na sie tubaki na yakwetu
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Kupenda au kuuchukia uongozi wa mtu ni relative.
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Unapingaje ubora wa Nyerere bila kuainisha mapungufu yake yanayokufanya usimuone bora Mzee?
 
Mkuu waafrica na watanzania mna low IQ
kama ndo ivo mbona ndege mmeshindwa kuendesha
Bandari mmeshindwa mmempa muarabu
Umeme bado hoe hae
Nipo mwanza kutoka ninapo ishi had ziwani km2 tu lakini mtaani hamna maji.

Singida dodoma kuna ukame lakini kila kona mmezungukwa na ukame ziwa tanganyika nyasa na victoria


Itoshe kusema Hata uachiwe Tirion ngap kama akili huna huna tu vitapukuchika kama vumbi.
Nyerere alikua geniuous kwene nchi ya mapopoma
Yaani nawe pia mmoja wao aisee
Unaishi mwanza karibu na ziwa kama una akili basi ungekuwa na meli na kiwanda cha samaki
Bora mimi niliondoka miaka ya 70 baada ya kuona hapaeleweki
Usikariri kuona nimechangia ukadhani niko Kasulu
Ulikuwepo miaka ya 70 wakati alileta uhujumu na kudhulumu watu mpaka radio?
 
Hakuna na bado Nyerere alirudisha hela zao kwa misimamo yake. Huyu mpiga mwingi anaweza?
Kasgindwa nyetrere atawea yeye, angekuwa nyerere karudisha pesa zao ingeshikwa ndege afrika kusini? Au umesahau kwanini ilishikwa?
 
Hakuna umoja wala nini

NI UOGA TU tumejazwa na huyo mwalimu
Vizazi na vizazi leo bado vinarithi uwoga na khofu
Na hii si afya kwa maendeleo
Vijana wenye hofu ni wale wa zamani, sio hawa watoto wa 2000.

Vijana wa sasa wanatembea na dunia nzima viganjani mwao kwa kutumia simu za kupangusa hawana sababu yoyote ya kuhofia chochote.
 
Back
Top Bottom