Huwezi nishawishi Nyerere alikuwa Rais bora

Huwezi nishawishi Nyerere alikuwa Rais bora

Babu yako alifeli, baba yako kafeli, wewe umekuwa mtu mzima bado upo pale pale huna mbele wala nyuma, hapo mjinga ni nani wewe au babu yako? Kuendelea kumlalamikia mtu aliyetoka madarakani over 30yrs ago ni ufinyu wa fikra na ujinga wa hali ya juu. Mlitaka Nyerere asolve matatizo yenu yote ya mbele ili nyie mfanye nini?
Hawa wajinga ndiyo wanafanya nchi yetu inadharauliwa. Sasa Nyerere kwa mfano alikataa kuchimba madini hadi tusome. Mkapa kaanza kuchimba 1998 na akina Kikwette hadi Samia waliendelea. Utamlaumuje Nyerere kwa umaskini wetu wakati na madini alitutunzia?

Haya Nyerere kaanzisha mashirika ya umma 400, watanzania aliowaamini wakayafilisi hadi ikabidi yauzwe, still hawa wajinga bado wanamlaumu
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Kama umezaliwa 2000, hata sura tu unaona picha. Tuliosoma bure bila kubagua dini, tena akapora shule za WAKRISTO ili wote wasome, kutibuwa bure, mpaka scholarship ulaya bure, uhuru kuanzia, Angola, Namibia, Msumbiji, SA, Zimbabwe, Zambia nk inatosha kujua ubora wake. Wewe peke yako una uhuru wa mawazo kuona hafai.
 
Babu yako alifeli, baba yako kafeli, wewe umekuwa mtu mzima bado upo pale pale huna mbele wala nyuma, hapo mjinga ni nani wewe au babu yako? Kuendelea kumlalamikia mtu aliyetoka madarakani over 30yrs ago ni ufinyu wa fikra na ujinga wa hali ya juu. Mlitaka Nyerere asolve matatizo yenu yote ya mbele ili nyie mfanye nini?

Wezi wa mali za Nchi hawawezi kumkubali Nyerere kuwa alikuwa Rais bora !
 
Hawa wajinga ndiyo wanafanya nchi yetu inadharauliwa. Sasa Nyerere kwa mfano alikataa kuchimba madini hadi tusome. Mkapa kaanza kuchimba 1998 na akina Kikwette hadi Samia waliendelea. Utamlaumuje Nyerere kwa umaskini wetu wakati na madini alitutunzia?

Haya Nyerere kaanzisha mashirika ya umma 400, watanzania aliowaamini wakayafilisi hadi ikabidi yauzwe, still hawa wajinga bado wanamlaumu

Uko sahihi kabisa 💯 🙏
 
Hawa wajinga ndiyo wanafanya nchi yetu inadharauliwa. Sasa Nyerere kwa mfano alikataa kuchimba madini hadi tusome. Mkapa kaanza kuchimba 1998 na akina Kikwette hadi Samia waliendelea. Utamlaumuje Nyerere kwa umaskini wetu wakati na madini alitutunzia?

Haya Nyerere kaanzisha mashirika ya umma 400, watanzania aliowaamini wakayafilisi hadi ikabidi yauzwe, still hawa wajinga bado wanamlaumu

Bado hawajui changamoto ambazo utawala wa Nyerere ulipitia kama vita na Uganda. Alirudisha over 10M pounds kwa kusapoti uhuru wa Western Sahara nk.

Kwa mambo aliyofanya Nyerere angekuwa wakati huu wakati donor countries ni nyingi na wataalaam ndani na nje ni wengi angekuwa mbali sana.
 
Lawama zote hizi ukifuatilia sana ni kwasababu za kidini tu. Tunawajua walioamua kum-discredit na kum-demonize Nyerere.
Tuoe hizo sababu za "kidini".

Mbona huzitaji, tukuamini vipi hujatupa hata mfano mmoja?
 
Bado hawajui changamoto ambazo utawala wa Nyerere ulipitia kama vita na Uganda. Alirudisha over 10M pounds kwa kusapoti uhuru wa Western Sahara nk.

Kwa mambo aliyofanya Nyerere angekuwa wakati huu wakati donor countries ni nyingi na wataalaam ndani na nje ni wengi angekuwa mbali sana.
Lini Tanganyika au Tanzania ilijitosheleza bajeti yake bila hao donors?
 
Hata Mwenye ulimwengu wapo wasiosadiki kuwa yu mwema.
Badala ya kulalamika hovyo tenda wewe mema mengi mpaka Dunia ikujue badala ya blah! blah!
Watu walalamishi hivi ukichunguza hata familia zao tuu zimewashinda😭
 
Nyerere Kama binadamu mwingine yoyote yule, alikuwa ana mazuri yake lakini pia alikuwa ana mabaya yake, ingawaje kwa kiasi kikubwa mapungufu yake mengi yalikuwa yanavumilika ukimlinganisha na wenzake wengine wote waliomfutia.


Baadhi ya mabaya au ubovu wa Mwl. Nyerere:-
1. Kuiga, Kuanzisha na kuendeleza Sera na Itikadi Mbaya kabisa ya Siasa za Ukomunisti/Ujamaa hapa Tanzania.

Huu ndio ulikuwa mwanzo wa Kujenga Msingi mbovu wa Taifa la hovyo kabisa lililopo hivi sasa.
Itikadi na Sera ya Ukomunisti/Ujamaa ikaja kushindwa vibaya Sana huku yeye mwenyewe akishuhudia kwa macho yake kushindwa kwa itikadi yake aliyoileta hapa Tanzania kutoka kwa marafiki zake wa China, Urusi na Cuba.

2. Kutengeneza Taifa la Watu waoga, Wanyonge, dhaifu wa fikra wasiojitambua na Wala wasioweza kuhoji. Taifa la watu 'misukule'.

3. Kutengeneza au kuunda nchi isiyokuwa na Mipango-miji, hususani kupitia kwenye Sera yake mbaya kabisa ya ujamaa/Ukomunisti. Sera au Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti ndio ilikuwa chanzo Cha Kuanzishwa kwa Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, the Worse Operation that completely destroyed the Country and Town Planning process within the Country.
Arusha Declaration and Operation Vijiji also led to the Death of Real Estate Industry and its development.

Kupitia Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti, Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, Watu wengi sana walinyang'anywa Ardhi zao pamoja na majumba yao waliyokuwa wakimiliki. Nyumba nyingi sana za Watu zilitaifishwa, Leo hii nyumba hizo zinamilikiwa na Shirika la Nyumba (NHC).

4. Kutuletea Katiba ya nchi ambayo ni mbaya kabisa, isiyofaa na ambayo imesababisha na inaendelea kusababisha madhara makubwa sana kwa Raia. Katiba mbaya ambayo imewatengeneza Watawala wa nchi hii kuwa 'Miungu Watu.'
1.)Ukomunisti lilikuwa wazo zuri ila lisilotekelezeka badala ya kulialia tungejifunza china mbona wao wana maendeleona sio waoga? Urusi pia?
Tupe nchi ya afrika ilofanikiwa saana kwasababu ya ubepari!!
2.)Ukomunisti ulileta uoga? Mbona china,Cuba,urusi si waoga? Kama ni uoga basi South Afrika ndowangekuwa waoga haswa. Mwalimu mmoja anawezaje kufanya nchi iogope
Tatizo nihao watu...
3.)sera ya kuweka watu pamoja lengolilikuwa zuri (ili wapate huduma kirahosi) ila ilikosewa kiutendaji kama vile binadamu tunavyokosea mambo kadhaa ktk maisha.
Hakuna kiongozi ni malaika so kukosea ni ubinadamu labda uwe muoga kujaribu mambo mapya
4.) Ni upumbafu mtupu kumlaumu rais wa kwanza kuhusu katiba. Vijana amkeni mdai katiba mpya msilaletake mletewe kitandani!!
Poor minds hulaumu kwanini hawajapewa vitu vizuri alakini best minds huvitafuta na kuvipambamia vilivyo vizuri...
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Unafikiri ni bora angekuwa Fisadi na kuua wapinzani wake wote. Kenya, DRC makabila, dini zinapingana. Ulitaka muwe kama DRC?
Ladda usingeweza kuandika hivi, ungeshaliwa kichwa.
 
Lakini kwenye muungano, na kuwafukuza wazungu na kuwaachia wale waliozaluwa humu eti hawajui kiswahili kina kanjibahi
 
Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.
Kwa nini unataka ushawishiwe na wengine; wewe huna akili za kujitosheleza mwenyewe; au unataka na wengine nao wawe na akili pungufu kama zako?
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.

Kizazi cha vijana waoga na machawa wote hakikuwepo wakati wa Mwalimu Nyerere .
Kizazi cha mwalimu kimeishia kwa kina Jenerali Ulimwengu.
Kikwete ,Kinana, Padri Kitima ,Askofu Bagonza, Askofu Shoo n.k.,Dr. Mwakyembe n.k . Pombe Magufuli n.k.
Hiki kizazi kingine ni kizazi cha kina , Mwinyi kizazi cha kupenda fedha ,Mkapa kizazi cha 10%, Kikwete Kizazi cha mafisadi , JPM kizazi cha ubabe, Samia kizazi cha kila mtu kula kwa urefu wa Kamba yake .
Wanasiasa Waliotengeneza vijana waliopo leo ni akina :- Mbowe, Maalim Seif,Lipumba , Slaa , Zito Kabwe, Akina Msigwa ,Sugu, Mnyika , Tundu Lisu, Lema , Makonda ,Magufuli , Kikwete Chalamila , Sabaya , Tulia Aksoni n.k. Hawa ndio Kioo cha siasa za kizazi hiki kilichojaa usanii na woga kila sehemu. Kwa hiyo kila mtoto au kijana mdogo alimuita mwanasiasa aliyempenda na wengine hawakupenda siasa wakapenda miziki ,mpira , ushoga ,usagaji ,kujipendekeza pendekeza n.k alimradi apate chakula .
Lakini Pia Tanganyika ilikua na maadili yake na miiiko yake na mila yake .
Tanganyika dira yake ni ya Kijamaa kutokana na uwepo wa dini tofauti tofauti na makabila tofauti huku pakiwa na rasilimali kila mkoa jambo ambalo lingeweza kujenga ubaguzi mkubwa sana. Zanzibar inamfumo wa Kisultani na kifalme unaopelekea wetu wachache au mmoja kumiliki RASILIMALI ZOTE NA WENGINE KUWA KAMA Watoto wake tu wa kupewa kila kitu.Mfumo wa Zanzibar ni mfumo unaofanana na mifumo ya nchi za kiarabu.
Sasa tumekosa dira kutokana na kuwa na nchi mbili zenye Muungano wa kinafiki zaidi kwani moja haikua inataka kupoteza nchi yake ili kujenga dira moja. Kutokana na ukweli kuwa waasisi wake walilenga siasa na usalama wa nchi kwa wakati huo dhidi ya wakoloni waliokua wanaipenda sana Tanganyika na pia Zanzibar kutokana na rasilimali nyingi zilizopo zinazoifanya Tanganyika kuwa kama shamba la bibi la kuchota tu.
Nyerere alijenga vijana wa waliokua na Elimu kiasi lakini wenye uwezo mkubwa sana na wazalendo sana.
Tulianza kupotea kama taifa kisiasa ,kijamii na kiutamaduni baada ya Mwinyi kuruhusu kila kitu kifanyike bila utaratibu kutokana na woga wa kupinduliwa maana Hata Polisi na jeshi yalikua na maisha magumu. Ujambazi ulikua mkubwa sana . Mpaka Treni walikua wanaweka magogo ili ipinduke na watu waibe mali za abiria. Mabasi yalikua yanatekwa mita chache kutoka kituo cha polisi na watu wenye silaha za Kivita na waliovaa sare zinazofanana na za majeshi mengine huko kwenye nchi zinazofanana na za kwetu. Magendo yalikua yanapita kila boda bila ushuru ,viwanda vya ndani vikafa. Rushwa ikawa kubwa sana ,uhalifu mkubwa sana na hali ikawa ni ngumu sana kwa watumishi wa umma na mabanki kama NBC ikawa ni shamba la bibi la wafanyabiashara kukopa kwa dhamana feki na kutokomea ,watu waliaminishwa kuwa ili uwe tajiri ni lazima udhulumu ,uibe, ufanye biashara za magendo ,ukwepe kodi.
Kwenye Jeshi la Kule Burundi kuna kambi zilikua ni kiwanda cha kutengeneza Pombe haramu ya Gongo maana wanajeshi wa Burundi walikua na maisha magumu sana na mishahara wakati mwingine walikua wanakopa kwa mfanyabiashara wa ngano na sembe n. k. Polisi wa Burundi na wanajeshi walikua na uhasama mkubwa sana kutokana na kuwa kamba za polisi kula zilikua ndefu sana mpaka kwa wauza gongo ambao walikua kwenye Makambi ya jeshi kule Bujumbura .
Hali hiyo ya Kikolombia iliibua matajiri wengi wenye asili ya Kiasia na wachache watanganyika walioamua kuwa mabeduli,majambazi , waporaji ,wakwepa kodi n.k . Wakaibuka wanaharakati wa kidini na maandamano ya kidini kudai haki za dini fulani fulani ikiwemo kuibuka kwa madhehebu yenye imani kali za kilokole na Pia upande wa kiislam kudai kujiunga na OIC ,wengine kudai haki ya elimu eti walidhulumiwa kusoma , wakaanza kudai kuvaa nguo zinazoashiria imani za kidini kwa lengo la kujuana .Misaada ikawa inakuja kinyemela kufadhili shughuli za kidini kama Kareti kwenye nyumba za ibada. Chuki za kidini zikaanza chini chini . Kama kawaida ya siasa za nchi za Kiafrika Lawama zikaangushiwa Rais aliyetangulia baada ya aliyepo kukosa mikakati mipya ya kulinda uchumi imara ,kulinda kuporomoka kwa thamani ya pesa ,kudhibiti mfumuko wa bei . Pakaanza kuibuka nyaraka za kanisa , huku zikiibiwa na wanaharakati wa dini zingine kuitetea serikali kwa maslahi ya wanasiasa wanaowafaddhili na au kuwatafutia wafadhili toka nje . Hapo ndipo paliipoibuka kitu kinachodaiwa kuwa Tanzania inaendeshwa kwa mfumo Kristo hivyo waislam wakandamizaji . Matatizo ya wananchi hayakuwa yanashughulikiwa tena kitaifa bali kidini na kwa hisia za kidini. Yaani harufu ya Udini inakua kwa kasi sana . Maandamano ya kudai mfumo wa vyama vingi yakawa yanafukuta vyuo vikuu wakati huo wasomi walikua wa chache wanyeuwezo wa kufikiri wenyewe bila kufikiriwa na hapakua na machawa kwani wote walikua na Kadi ya CCM lakini walikua wanahoji serikali na kuandamana na migomo mpaka kwenye mashule ya sekondari.
Pakawa na Mihadhara ya kukashifu dini nyingine . Watanganyika wakaletewa utamaduni wa Kubaguana kutokana na dini. Mfumo wa vyama vingi ukaanzishwa wakati ambapo nchi ilikua imeshaparaganyika hasa kidini . Pakaibuka siasa za kudai haki za kidini kwa kusema kuwa serikali inapendelea dini moja huku lawama ikitupiwa kwa Nyerere kwa sababu aliyekuwepo alikua ni wa dini tofauti na ya kwake . Sasa lengo likawa kama vile aliyepo ndiye anabalance dini zote kumbe ni kutokana na hulka aliyoizoea kule Zanzibar kutokana na serikali ya kule kuwa na watu wa dini moja tuu. Sasa walipofika huku wanakutana na watu mchanganyiko matokeo yake wanashangaa mbona kama kila mahali kuna misalaba shingoni . Basi huku inaelekea wa dini nyingine wamezidiwa . Kumbe ni ile hali ya kuchangamana na kule hawakuzoea hali hiyo kabisa . Wakawa wanajaribu kumchanganya mara OIC mara elimu ,mara teuzi zifuate dini mara ,Bucha ,mara ,kitimoto . Seikali ikasema Ruksa kila mtu kufanya anachotaka .
Likaibuka azimio linalofeva hulka za ubinafsi na kuua umoja ,uzalendo,utu na siasa za kuamini kiwa cheo ni dhamana.
Badala yake cheo ni Fursa ya kujilimbikizia mali.
Kweli wakafanikiwa kulimbikiza mali nyingi . Pakaibuka Kundi la wanasiasa matajiri wanaofadhili michakato ya chaguzi ndani ya CCM na hata vyama vingine kama UDP. Hili kundi likawa linatumia fedha wakati wa uchaguzi . Huna pesa hupati uongozi . Madiwani wa CCM wakaiba mali za vyama vya ushirika huko vijiji na kuzigeuza kuwa mali zao binafsi .Uongozi ukawa unanunuliwa kila idara pakawa na biashara kubwa ya kuuza mitihani mashuleni kwenye vyuo na kila mahali. Polisi wachache walioshirikiana na wahalifu wamegeuka kuwa mabilionea . Wale waadilifu wa kizazi cha Nyerere wakawa wanakopa tu kwenye maduka ya watu kwani mabenki hayakuwa na uwezo wa kukopesha wafanyakazi kutokana seikali kuwa mufilisi kabisa na pesa zimehamia kwa mifumo isiyo rasmi ikiwemo watu kutorosha dhahabu na mke wa mkubwa alituhumiwa kufanya hiyo biashara wakati Nyerere hakuruhusu .
Sasa hali hiyo imebadili kabisa dira ya nchi na kupoteza kabisa moyo wa kulitumikia taifa kuanzia kisiasa ,kiuchumi na kiutamaduni
.
Kifupi Nyerere ukurasa wake ulifungwa siku aliyokua anastaafu na kufunguliwa dira na mrengo tofauti kabisa .Hii ni kutokana na Mamlaka makubwa anayokuwa nayo Rais aliyekua madarakani. Kwani anaweza kubadili chochote anachotaka bila kuzuiliwa au kuulizwa na yeyote .
Mfano Rais aliyepo leo ameamua tu kujenga taifa la vijana machawa na wabinafsi wanaowaza mambo yao binafsi tuu ,starehe ,mpira ,mziki na Pombe kiasi kwamba wamekua kama nyumbu mpaka mtu anashushwa kwenye gari na kuuawa wao wanaangalia tu.Kisa hayo hayaruhusu. Watawala wao wameletewa chakula mezani na katiba lakini wanawadanganya watu kuwa Katiba achaneni nayo haiwezi kuwaletea chakula mezani huku wao wakiwa wana magodown ya chakula kutokana na katiba 😆😆😆
 
View attachment 3089373Ni ngumu kunishawishi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi bora ngumu sana.

Mtu aliyetengeneza taifa la misukule kamwe hawezi kuwa kiongozi bora.

Propaganda kubwa imefanyika kumchora Nyerere mtakatifu na genius Taifa halijawahi kupata mtu wa hivyo.

Indoctrination imefanyika toka utotoni Nyerere kuonekana bora kila upande.

Jinsi watanzania tulivyo ni masikitiko akili zimeoza.

Huwezi kuwa bora kama unageuza watu wako misukule ili uwatawale vyema.
Tunajua kinachokusukuma kunena hayo ni Falsafa za Mwalimu wako mtoto wa kariakoo ambaye wazazi wake walikatiliwa mbali na Mwalimu.
Kwako aliye bora ni hawa wauzao bandari na rasilmali zetu?
 
Lawama zote hizi ukifuatilia sana ni kwasababu za kidini tu. Tunawajua walioamua kum-discredit na kum-demonize Nyerere.
Na kumpumzisha ili wagawane nchi vizuri .
Walitafuta sababu ya kuchukua mali za umma na kupeana viwanda kiholela .

Yaani watu walichukua nyumba zote za maeneo muhimu mpaka zile zilizopo karibu na ikulu wakajiuzia kwa bei ya chini ya nyumba iliyoko Mbagala halafu wanamlaumu Nyerere .
 
Ujinga wetu mwingi chanzo ni ubinafsi wa kila mtu haswa anapopata nafasi katika taasisi au shirika fulani
Mkuu 'Stevo', napita tu na kujikumbusha.
Hayo maneno ndani ya mstari huo najuwa yametukoroga sana wewe na mimi; pamoja na kwamba naelewa unacho kisema hapa.
Kwangu, hayo ni maneno ya kisingizio tu cha rahisi rahisi tunapo tafuta njia za mkato kueleza kushindwa kwa viongozi wetu kuongoza wananchi wake.
Nilisha sema mara kadhaa, katika majibishano yetu humu. Hakuna nchi hata moja duniani isiyo kuwa na watu wenye tabia kama hizi zetu. Ubinafsi, ufisadi, majungu tele, n.k., Tofauti pekee kati ya baadhi ya nchi na nyingine ni uongozi unao amua kuwa na mwelekeo tofauti na tabia hizo mbovu tunazo semekana sisi tunazo.

Wachina ni wezi sana; kama tunavyo wajuwa sasa baada yao kuwa miongoni mwetu. Lakini nenda China uchunguze tabia hiyo ya wizi waliyo nayo na jinsi inavyo zimwa humo nchini mwao. Kuna baaddhi ya nchi ambazo tume aminishwa wao hawana tabia za hovyo hovyo, kutokana na imani zao za kidini. Lakini pamoja na kuwa na imani hizo tabia hizo mbovu zinazimwa kutokana na sheria na adhabu zilizopo zinazotishia hadi uhai wa watu hao wenye tabia mbovu.
Kwa nini sisi hapa tunataka watu wetu wawe kama malaika wakati hakuna juhudi na mikakati ya kuwaondolea ushawishi wa kufanya maovu?

Huo ni mfano mmoja tu wa tabia za kifisadi/wizi/ukwapuzi.
Hali ni hiyo hiyo hata katika kukosa wajibu wa kusimamia shughuli zao za kimaendeleo. Siyo kwamba ni wavivu, la hasha uongozi wetu haujaweka jitihada za kuwafanya waTanzania waweke juhudi zaidi katika ufanisi wa kazi zao, iwe maofisini, au hata kazi binafsi
Hakuna nchi ambayo haikuwa na wavivu, watu wasiopenda kujibidisha zaidi ya kuwa na chakula cha milo michache; lakini uongozi wa nchi unapambana na kuibadili hali hiyo.

Usinielewe vibaya. Sisemi kila mtu ndani ya nchi atakuwa sawa na mwingine, la hasha, lakini kimwelekeo wa jumla, nchi inakuwa na mwelekeo wa kufanya vizuri na siyo hao wavivu, majizi ndio wawe mifano ya kuigwa kama inavyo elekea kuwa kwetu hapa.

Nimekusoma toka mwanzo wa mada hii, na nina hakika kuwa kimsingi tunakubaliana kwa sehemu kubwa. Tatzo letu lilipo sasa nalielewa vizuri zaidi.

Nimekwisha sema leo na jana mara kadhaa kwamba tumemalizana; lakini nashangaa kujikuta nikirudi kuendelea na maongezi haya baina yetu. Lakini kwa vile nina ufahamu mpana kidogo juu yako sasa, nadhani yale maneno ya kichokonozi "upuuzi, mpumbavu, huna akili" yatapumzika sasa!

Lakini naomba usinichokoze tena, kwa kuwadharau waTanzania. Lawama zielekezwe mahali zinapo stahili kuelekezwa; hata kama ni kwa viongozi tunao waheshimu sana wakishindwa kutimiza wajibu wao wa kuongoza.
 
Back
Top Bottom