Huyu Meneja wa TRA Tanga kuipongeza CCM Kumteua Rais Samia kugombea Urais 2025 inaruhusiwa katika Sheria za Utumishi wa Umma na ni rukhsa Kikatiba?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kwa wale Wote ambao leo Asubuhi tulitizama Jambo Tanzania na TBC1 nadhani tulimuona Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga alipokuwa akimpongeza Rais Samia kwa Siku yake ya Kuzaliwa leo na baadae akaenda mbele na kusema kuwa anakipongeza Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa Kumpitisha Rais Samia kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Haya GENTAMYCINE nawaomba wale Watetezi Chawa Mambumbumbu (WCM) mniambie je, Kisheria (hasa kwa Sheria za Utumishi wa Umma) na katika Katiba pia ya nchi inaruhusiwa kwa Mfanyakazi wa Serikali (tena kutoka TRA) kusema alichokisema huyu Meneja TRA Mkoa wa Tanga? Na kama inaruhisiwa kwa Sheria za Utumishi wa Umma mbona hakuwasifia pia CHADEMA kwa Kumchagua Tundu Lissu kuwa Mwenyekiti CHADEMA Taifa na ACT pia?
 
Machawa hayanaga wala hayaoni sheria

Ki ukweli ni kinyume na ethics/maadili ya kazi
 
Kwa namna nchi inavyoendeshwa, wala sio ajabu kuona upumbavu wa namna hiyo unafanywa na watumishi wa umma, tena waandamizi.
Tina taifa la hovyo sana!
 
ni mwananchi na mtanzania km wewe
 
Ukiona hivyo ujue huyo meneja hakusanyi vizuri maduhuli huko Tanga. Hizo ni mbinu za porini za kubakia kwenye vyeo.
 
Huko hakuna noma, mpongeze lissu na ni mtumishi uone kazi inavyokuwa ngumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…