Huyu ndio mtoto mwenye akili nyingi kuliko wote Tanzania 2024

Hayo aliyo kariri kwa umri wake ilikua bado. Umeona hata hesabu anafanya bila kuhesabu.
 
Hilo tu la kumsubua mtoto kumkaririsha vitabu na matakataka mengine ya kumjazia ubongo wake utoton ndiyo anakuwa na akili kuliko watanzania wote. Au akili ninini labda?
 
Kuna vitoto vya madurasa vimekariri Qoran nzima na hadithi sijui za Ibn Omar!

Sasa, hiyo siyo akili. Kuwakaririsha watoto mavitabu ya kishamba kama bibilia na Kuruani ni kuendeleza ujinga na ujima katika jamii.

Watoto wafundishwe vitu vya maana.
Ni umri gani mlete hapa. Huyo anafanya hadi hesabu hadi siasa anajua. Ana miaka 4.
 
Akili ni nini!?

Je kuhifadhi kwa wepesi, kuhifadhi jambo kwa muda mrefu, kuwa na kumbukumbu nzuri? Ama uwezo wa kutatua mambo katika namna tofauti tofauti.

Hapo dogo kaonesha ana uwezo wa kumeza, ila sio ana akili nyingi.
Tukifundishwa 1 jumlisha 1 ni 2, 3+2 ni 5 na tukafundishwa imepatiknaje kisha tukapewa swali maandazi ma5 ukipewa na vitumbua vitatu na chapati sifuri, utakuwa na vitafunwa vingapi.
Ule uwezo wa kuchanganua hilo swali, kujua linahitaji kujumlisha japo hakuna sehemu imesemwa jumlisha, kwangu mimi huyu ndio mwenye akili.
Na si lazima iwe kwenye hesabu tu, hata mazingira
Hayo aliyo kariri kwa umri wake ilikua bado. Umeona hata hesabu anafanya bila kuhesabu.
Ewa sasa hapo 1 jumlisha 1 kasema 2, naamini kakariri, akiuliza 7+3, 5+2,4+5, n.k hapo sasa angeluwa katumia sehemu nyimgine ya ubongo nje ya kumbukumbu
 
Watoto wenye uwezo wa kukariri siyo lazima wawe wana akili sana. Tulio kwenye mitandao kwa muda mrefu tumeshakutana na visa vingi vya aiana hii na hao watoto walipokuwa watu wazima hawakuwa na chochote cha zaidi.
 
Ni umri gani mlete hapa. Huyo anafanya hadi hesabu hadi siasa anajua. Ana miaka 4.
Ajibu maswali ya siasa na hesabu angalau.

Hayo mavitabu ya Biblia kwanza yanabishaniwa, wengine wanasema sabini na mbili wengine sitini na sita, wengine wanasema wamakabayo ilitolewa wengine wanataka irudishwe,

Wengine wanasema injili Yuda haipo wengine kitabu cha Enock.

Ni upogo mkubwa kumpima mtoto akili kwa kutumia mavitabu ya kufikirika tu ya kiimani yaliyotungwa sijui na wayunani.
 
Waambie wa google kuhusu Bethuel Mbugua wa Kenya , mtoto aliyekuwa anatoa lecture vyuo vikuu akiwa na miaka 6. Mambo ya human anatomy alikuwa anayajua kama mtu mzima.

 
Watoto wenye uwezo wa kukariri siyo lazima wawe wana akili sana. Tulio kwenye mitandao kwa muda mrefu tumeshakutana na visa vingi vya aiana hii na hao watoto walipokuwa watu wazima hawakuwa na chochote cha zaidi.
Kukariri haimaanishi uwezo wa kiakili, infact kukariri siyo akili kabisa.

Kukariri ni matokeo ya kutokuelewa.

Akili siyo kujua idadi ya vitabu vya biblia, akili ni kujua kwa nini biblia iliandikwa.

Mleta mada abadili kichwa cha habari.

Aandike MTOTO MWENYE UWEZO WA KUKARIRI.
 
anaonekana ana akili nyingi kwa sababu yupo pia mwenye ujinga mwingi
 
Huu ni mtazamo wako
 
Mleta mada umetumia san emotion and not your head kutoa maoni yako kuhusiana ni hio video. Hio ni script mtoto kamezeshwa akarili.
 
Alimeza meza anatomy. Watu kuja kumoa iq test akaonekana hana u GENIUS huo.
 
Pamoja na hayo, basi tukubaliane kwamba memory capacity ya mtoto Ni Kubwa kuliko watoto wengi walio na umri sawa na yeye.

Kakaririshwa sawa, lakini uwezo wa kukumbuka ulichokaririshwa ndiyo jambo la msingi.
Mleta mada umetumia san emotion and not your head kutoa maoni yako kuhusiana ni hio video. Hio ni script mtoto kamezeshwa akarili.
Napingana na wale wanaosema kakaririshwa ujinga (kisa: Aina ya content mtoto anayotiririka). ELIMU zipo za Aina nyingi: dini, sayansi, arts, fedha, n.k. Mtoto kakaririshwa elimu ya dini, watu wanaponda, eti ni ujinga. Loh! Wangependa kusikia Mtoto anatiririka Archemedes Principle, anatomy, atom, molecular biology, etc. ndipo wangefurahi, na wangeamini kweli mtoto anaupekee. Ila kwa kuwa Ni Elimu ya dini wanahitimisha kwamba "Hana lolote".
 
Swali la kujiuliza.
Alikaririshwa kwa muda gani?
Hata hivyo mtoto ana kumbukumbu nzuri, itamsaidia shuleni.
 
Upo sahihi tatizo ni mleta mada kuandika " huyu ndio mtoto mwenye akili nyingi kuliko wote Tanzania'
Kwa haraka haraka wana JF wanategemea labda kavumbua kitu kumbe ni ishu ya kukarlli script
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…