Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Hivi waliompa paundi 60,000 ili ampindue Mwl. walihitaji nini kama mrejesho endapo angefanikiwa
 
Hivi waliompa paundi 60,000 ili ampindue Mwl. walihitaji nini kama mrejesho endapo angefanikiwa
Huyo mwalimu wenu kisingizio Cha kuficha ukatili na tamaa ya madaraja huwa ni kupinduliwa tu!?..kambona,titi Mohammed,kasanga tumbo,kasela bantu,fundikira nk
 
Huyo mwalimu wenu kisingizio Cha kuficha ukatili na tamaa ya madaraja huwa ni kupinduliwa tu!?..kambona,titi Mohammed,kasanga tumbo,kasela bantu,fundikira nk
Mtoa mada anasema kuwa Christopher Kassanga Tumbo mwenyewe alisema kuwa alipewa kiasi hicho cha pesa ili ampindue mwalimu. Je waliompa pesa walitaka wafaidike nini kupitia pesa walizotoa ?
 
Mtoa mada anasema kuwa Christopher Kassanga Tumbo mwenyewe alisema kuwa alipewa kiasi hicho cha pesa ili ampindue mwalimu. Je waliompa pesa walitaka wafaidike nini kupitia pesa walizotoa ?
Porojo hizo
 
nafikiri baadaye ikawa order arudi kwao kijijini, na ndiyo maana anakarudi ipole; ni kweli alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa na hakuwa na marafiki pale kijijini, alikuwa mpweke sana na muda wa kuongea na wanakijiji ulikuwa ni wakati wa misiba tu. Na kila utakapomwona lazima awe na radio yake ndogo maskioni na mara nyingi tulikuwa tukisogelea tunasikia habari za kiingeleza, nafikiri alikuwa nasikiliza BBC

Mzee huyu alikuwa anachunga ngombe kutwa nzima juani, mavazi duni sana, kiujumla hali ya miasha yake ilikuwa vigumu kuielezea.
Dah!...taifa letu limepitia mengi sana.
 
H
Wakurugenzi,

Nilibahatika kuzaliwa kijiji kimoja na Chritopher Kasangatumbo, alikuwa si mbinafsi mjamaa wa kweli, nilibahatika kumjua nikiwa kijana mdogo sana pale kijijini kwetu ipole, alikuwa mzee mpole na kwenye hekma sana; kwenye misiba alikuwa anatumia muda mwingi kutuelimisha, nakumbuka alituambia mambo ya demokrasia na dhana nzima ya vyama vingi kipindi nipo darasa la tatu; sikuielewa philosophy yake hadi nilipofika kidato cha sita na kukutana na kitu kinaitwa vyama vingi (1995) hapo ndipo nikafungua macho na kujua ni nini hasa Kasangatumbo alimaanisha those days.

Kuna tetesi kwamba wale wote waliohoji au kwenda tofauti na mawazo ya mwalimu walipata ban; yule mzee Kasangatumbo alifanyiwa visa vingi sana hadi kufikia kuibiwa ngombe zake zote, Pamoja na kuishi uingeleza lakini hakuwa na mali yoyote ile mbali ya ngombe zisizozidi therathin alizorithi kutoka kwa wazazi wake. Nilibahatika kusoma na watoto wake, nakumbuka hata viatu hawakuwa navyo; tulienda shuleni pekupeku pamoja ingawa wenzangu waliyaonja maisha ya Uingeleza.

Mzee alikuwa mjamaa wa kweli na hilo halina ubishi, tatizo ni kwamba je alikorofishana vipi na mwalimu? Mimi na wewe hatujui, kuishi kijijini ilikuwa ni moja ya adhabu alizopewa toka juu. Kuna kipindi pale Tabora mjini Bendera ya taifa ilikuwa inashushwa, yeye hakusimama, akakamatwa kupelekwa kituo kikuu, pale kituoni akawaambia mapolice kwamba hawezi kuongea ya yeyote yule pale isipokuwa mwalimu tu. Police hawakumpa nafasi hiyo bali wakamsweka ndani - habari zikamfikia mwalimu ikulu na mara moja akawaambia wamfungulie aende zake - hizo zilikuwa moja ya story zake tukiwa kwenye misiba pale kijijini kwetu.

Kuna siku nilikuwa nimepanga foleni kwa ajiri ya kupata vitu adimu (sukari, sabuni), kwa wale mnaokumbuka yale maduka ya RTC basi watoto tuliambiwa twende mapema ili wakati duka linafunguliwa saa 9 basi tupate vitu hivyo; mida ya saa kumi duka linafunguliwa foleni ikiwa ndefu sana, nikamwona Kasangatumbo anafika eneo la duka, akatuambia tumsikilze dk tano, pale nakumbuka alituambia tutapanga foleni hizo hadi tutakapoamua kuwa na demokrasia ya vyama vingi - pale sikuelewa kitu kwamba hiyo demokrasia ndiyo italeta maduka mengi? I was young by age anyway. (9)

Inaendelea post #2 chini...

cc Ngongo, JingalaFalsafa, Mzee Mwanakijiji, Ogah, Mohamed Said, Nguruvi3, Mchambuzi, WOWOWO, Mkandara, Jasusi, Gembe, Phillemon Mikael, Mwanagenzi, Rutashubanyuma, Augustine Moshi, Pasco,
Hakuna Mjamaa anayehubiri Demokrasia, ukikutana naye wa hivyo basi tambua kuwa huyo ni Mamluki, ni Kibaraka na mshenga wa wakoloni.
 
Mmm, sasa huu uzi unakuja vizuri, kama kuna mwanahabari makini achukue mambo hapa, awatafute wazee waliobakia na kuoanisha hizi taarifa, ili tuboreshe historia yetu. Swali je kwa nini vyama vingi vilifutwa Tanganyika? Vilikuwa vingapi? Na viongozi wake walikuwa ni nani?

Nakumbuka siku ile tulipokua ikulu tukizungumzia mustakabali wa vyama vingi Tanganyika, mara Mtemvu na Julius walipokwidana. Mmoja akisema "By the way did you call me another Shombe in Afrika" Mkutano ukavunjika na vyama vingi vikalwakatariwa. Chipaka sijui bado anakumbuka? maana ndio alikuwa muamuzi wa mechi.
Kama vile amenikumbusha enzi za campaign ya kudai Uhuru WA Tanganyika miaka ya 1950 hadi 1960,Historia ya Kasanga Tumbo na akina Chief Fundikila WA pale Itetemya Kipalapala iko wazi,MWL.Nyerere hakutaka malumbano ya vyama Bali waungane kupambana ukoloni,mkutano WA Tabora WA Tanu,wimbo unaosema Ehe Sasi jabela mitwe haaa !
Umenikumbusha kitu kwenye wimbo huo "TANU jabela mitwe" wengine wakidai TANU imewahi kufanya mauaji ya waasi wake kwa kuwakata vichwa, kuna ukweli wowote? Wimbo huo ulimaanisha nini?
 
Yeah, lakini historia ya nchi imemuweka pembeni kabisa same as Kambona.
Fuso,
Namjua Kassanga Tumbo kwani yeye na babu yangu Salum Abdallah wameacha historia ya pekee katika historia ya vyama vya wafanyakazi Tanganyika.

Babu yangu Salum Abdallah mwaka wa 1947 aliongoza ''General Strike,'' (mgomo) Tanganyika nzima dhidi ya Waingereza.

Akafanya hivyo tena mwaka wa 1949 na mwaka wa 1960 wakati huo akiwa Chairman wa Tanganyika Railway African Union (TRAU) Katibu akiwa Christopher Kassanga Tumbo na wote ndiyo waasisi wa chama hicho cha wafanyakazi wa reli 1955.

Mwaka wa 1960 TRAU chini ya uongozi wao waliitisha mgomo uliovunja rekodi kwani ulidumu kwa siku 82.

Mgomo wa ulioitishwa na Makhan Singh, Kenya ulidumu kwa siku 62.
Angalia picha hapo chini:

Kulia ni Christopher Kassanga Tumbo na anaefuatia ni babu yangu Salum Abdallah
siku hiyo wanachama wa TRAU walimvisha huo mgogolole kama alama ya jemedari
anaongoza majeshi katika vita dhidi ya ukoloni hii ni miaka ya katikati 1950s.

Harakati hizi TRAU walifanya bega kwa bega na TANU na babu yangu ni katika waasisi wa TANU Tabora na alikuwa mjumbe katika kamati ya siri ya kuasisi TANU.

Mwaka wa 1964 babu yangu na Kassanga Tumo pamoja na viongozi wengine wa vyama vya wafanyakazi kama Victor Mkello waliwekwa kizuizini baada ya maasi ya wanajeshi.

1685215174122.png
 
H
Hakuna Mjamaa anayehubiri Demokrasia, ukikutana naye wa hivyo basi tambua kuwa huyo ni Mamluki, ni Kibaraka na mshenga wa wakoloni.
Uko sahihi kwa maana halisi ya mjamaa ambayo tafsiri yake hasa ni mkomunisti. Ukomunisti hauendani na demokrasia. Ni socialists ndio wanatambua na kuzingatia demokrasia. Bila shaka, Tumbo alikuwa socialist. (huwa inachanganywa na ujamaa).

Nyerere aligoma hata kutoa tafsiri ya “ujamaa” kwa marafiki zake wa Mashariki na Magharibi walipotaka kujua endapo ujamaa ni socialism au communism. Yeye alidai ujamaa ni mfumo wa kipekee wa maisha wa kiafrika; hauna tafsiri nyingine!

Kwa jinsi ilivyojionyesha kwamba anafuata zaidi modeli ya China (PRC), hakukuwa na shaka kwamba ujamaa ni ukomunisti wenye sifa kuu zifuatazo: Mfumo wa chama kimoja cha siasa kilichoshikamanishwa kikamilifu na dola. Chama kushika hatamu kwenye mihimili na taasisi zote za umma ikiwa ni pamoja na za kiraia/kibinafsi. Uchumi kudhibitiwa na dola (command economy). Kutaifisha mali za mabepari (watu binafsi) bila fidia, kudhibiti/kuondoa sekta binafsi, kukusanya wananchi katika makazi na shughuli za uchumi za pamoja (vijiji vya ujamaa/collectivization), n.k.
 
Chumvi za waleta story..pound maana yake alipewa na waingereza, waingereza wampindue Nyerere ili iweje wakati alikua mtu wao!!?
Na ukizingatia baada ya kunusurika kupinduli na jeshi la nchi na kulivunja,aliikabidhi nchi chini ya jeshi la Uingereza kwa karibu mwaka mzima wakati ikiundwa JWTZ.
 
Back
Top Bottom