Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Unapewa ubalozi huridhiki, unamwona aiyekuteua ni bwege, unaacha ubalozi ili uje umshugulikie, ukiwa ma paund 60,000 za kummaliza, akikugeuzia kibao eti dicteta. Mlitaka nchi iwe kama Somalia ili mradi tu Jamaa zenu waitwe marais
 
Kuna kitabu cha Historia kilichochapishwa 1965 kinaitwa "The Making of Tanganyika". Mwandishi ni Judith Listowel. Kina facts nyingi kuhusu mambo yanazungumzwa hapa. Nilikisoma kama miaka thelathini iliyopita. Judith Listowel alikuwa jikoni na alifahamu michango ya akina Kambona na maasi ya 1964 kwa undani. Kitafuteni hicho kitabu kwenye maktaba.

Nilihudhuria semina ya kwanza ya kuhusu vyama vingi, baada tu ya vyama vingi kuruhusiwa tena. Ilifanyika IPS building (I am trying to remember). Kasanga Tumbo, Mapalala, na Mabere Marandu walihutubia.
 
Tatizo kuu la MWALIMU hakutaka kuruhusu mawazo mbadala kwa kujiona anajua kila kitu angemsikiliza Kambona mambo yasingeharibika sana.Alikuwa na chuki na matajiri kwa kuamini umasikini ni fahari kwa kukumbatia Sera za ujamaa, ikiwemo vita feki ya uhujumu uchumi kwa kufirisi watu mali hata walizopata kihalali. Akasababisha watu wawe na tabia ya ulevi na uzinzi kwa kuoa wake wengi kwa maana ukikutwa na mali nyingi ni kosa na huwezi weka bank nyingi utafatiliwa,hivo ukizipata sababu ya nafasi yako ni kuzitumbua tu.Ye ndo msababishi wa wazee wetu wengi kufa masikini hali nafasi walikuwa nayo. Kwa mazuri mengi tumpongeze,mfano kuifanya ardhi kuwa Mali ya umma, kuwaunganisha watz wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmm, sasa huu uzi unakuja vizuri, kama kuna mwanahabari makini achukue mambo hapa, awatafute wazee waliobakia na kuoanisha hizi taarifa, ili tuboreshe historia yetu. Swali je kwa nini vyama vingi vilifutwa Tanganyika? Vilikuwa vingapi? Na viongozi wake walikuwa ni nani?

Nakumbuka siku ile tulipokua ikulu tukizungumzia mustakabali wa vyama vingi Tanganyika, mara Mtemvu na Julius walipokwidana. Mmoja akisema "By the way did you call me another Shombe in Afrika" Mkutano ukavunjika na vyama vingi vikalwakatariwa. Chipaka sijui bado anakumbuka? maana ndio alikuwa muamuzi wa mechi.
Ndo tunataka turudi kulekule wakati ni ukuta watashindwa,kashindwa MWALIMU wataweza wao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wakongwe wanasema historia ya nchi hii imechakachuliwa sana, hata mimi ukiniuliza sijui lolote zaidi ya hitoria ya mwalimu tu ndiyo iliyoandikwa kwenye vitabu vingi, wengine hamna kitu - hata sasa ukiniambia nimuelezee Oscar Kambona, siwezi zaidi ya kukwambia akikuwa katibu mkuu wa Tanu (tena hii nimesimuliwa tu) kisha akatimkia uingeleza kufanya nini na kwa nini mimi hapo sijui kitu.
Kuupata ukweli halisi wa history ya Tanganyika nje ya MWALIMU ni ngumu nyingi zimembeba MWALIMU kuliko wengine nadhani sababu kubwa ni ya yeye kuweza kumiliki kila kitu ikiwemo watu.Ndo maana mashuleni alisomwa yeye zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna historia ya Tanzania imefunikwa!Kuna akina Tumbo ,Mapalala etc.
Ningefurahi mtu siku moja aandike kitabu kuhusu wapinzaniwa kwanza wa udikteta wa Nyerere(Chama kimoja).

Wengi nasikia waliwekwa kizuizini ama Kilwa au huwezi kutoka kijijini kwako.

Kama unajua hiyo story ya hawa waliowekwa kizuizini hasa kisiwani ,labda mlikuwa majirani au watoto.
Akina Kasela Bantu,Tumbo ,Chief Makwaia wote wamesahaulika kabisa.

CCM inavyofanya sasa ni matokeo ya ukoministi wa chama kimoja!Rafiki zetu wa China mpaka sasa wana chama kimoja,
uhuru wa magazeti hakuna.Hata kuabudu!Falun Gong wanapata tabu huko.
Ila Wachina kama utaiibia serikali ,utakipata cha moto.Drug dealersni kupigwa risasi.

Hakuna EPA ,Richmond etc
Udikteta una asili ya Kanda ya ziwa,angalia Uganda, Rwanda,Burundi, awamu ya kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kinachosikisha ni namna treatment ilifanyika kwa wapinzani wa wakati huo; walionekana ni maadui wakubwa - its just the same what is happening now.

Watu wenye mawazo badala katika uongozi wa taifa lao ni watu muhimu sana; kazi yao kubwa ni kuonyesha watawala the 2nd option to rulling the nation; sasa kuwakandamiza hawa ni kuliua taifa. Hili ndilo lilifanyka enzi hizo na ndilo linafanyika sasa. Killing opposition.
True alikuwa aambiliki anajua kila kitu akutaka kupokea mawazo mbadala ya kujenga kama ilivo asili ya Kanda ya ziwa.Matokeo yake akafail kwenye uchumi, kabla ya Uhuru dola moja ilikuwa ni shilingi 10 ya Tz.Mfumo wa ujamaa kwa mwafrica haufai maana asili yetu ni uvivu bila mboko au kutengenezewa mfumo wa kujituma hatuendi.Mjerumani alijenga nchi kwa viboko kitu ambacho kilikuwa ni sahihi sababu iweje usipalilie SHAMBA lako likaota magugu utalishwa na nani.Alionywa na Kambona kuhusu kukumbatia ujamaa akayaona matokeo yake mashirika na mali za umma watu wakalamba yote.Amekuja kuelewa akiwa keshachelewa kwa kuharibu uchumi, ndo kinachokuja wataelewa kumbe kukaza vyuma kusomesha no ili kuwakomoa watu sio tija na tutaathirika wote.Kwa maana hakuna kiingiacho ziwa kuu,tuliowakopa wanataka chao,hatukopesheki tena tumefika mwisho.Miradi hailipi tena sababu purchasing power hakuna,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kafa maskini kazikwa kienyeji; kaburi la udongo; just thinking kama wanafamilia watanikubalia basi nitalijengea. Huyu ndie balozi wetu wa kwanza nchini ui geleza baada tu ya uhuru wa nchi yetu 1961.Sidhani kama watanzania wengi wanajua h5istiria hii.
Ni history nzuri iifadhiwe waombe familia watakubali ulijenge kaburi lake lisipotee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila kujua falsafa ya Kasanga & Kambona na wangineo waliompa.ushauri mwalimu kuhusu namna ya kuijenga Tanganyika mpya; basi hata wewe utasema jamaa walikuwa ni wahaini tu sababu hujui content za maudhui yao.

Jiulize toka 1961 hadi 1985 je taifa limesogea juu ya wale maadui watatu ( Ujinga, Maradhi na Umaskini)? Je toka 1985 hadi 2018 taifa limesogea kuwamaliza maadui hawa? Kushangilia ununuzi wa ndege moja kama sikukuu ya kitaifa; is that you call it nation achievement.
Kaongezeka mmoja ufisadi, hatuwezi songa hakuna viashiria vya kusonga,hela inaenda kwa visivozalisha wala tija ya kujenga productivity mfano kuhamia dodoma,Marudio ya chaguzi za kuifurahisha kijani,itakuwa kila siku ni kurudia uchaguzi hadi 2025,ni kiasi gani tutapoteza.Zingetupwa kuwajengea uwezo wa kuzalisha vijana mfano kuwapa elimu ya Kilimo,ufundi,nk wakazalisha tungeweza kukuza pato La ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fuso,
Napenda niseme machache kuhusu Kassanga Tumbo.

Mwaka wa 1955 babu yangu Salum Abdalah alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa
Tanganyika Railway African Union (TRAU) na Kassanga Tumbo akiwa Katibu.

TRAU si kwa bahati mbaya kuwa ilifuatana na TANU katika kuuundwa kwani huyu
Mwenyekiti wake alikuwa na historia ndefu ya siasa kuanzia African Association.

TRAU na TANU ilipigana bega kwa bega dhidi ya ukoloni wa Muingereza na kwa
hali hii Salum Abdallah na Kassanga Tumbo walikuwa pamoja.

Mwaka wa 1960 Salum Abdallah na Kassanga Tumbo waliongoza mgomo wa
wafanyakazi wa reli uliodumu kwa siku 82.

Mgomo huu ulisimamisha kila shughuli za reli kuanzia gari moshi, mabasi na meli.
Mgomo ulifanikiwa sana na mwishowe serikali ya kikoloni ilikubali madai yote ya
TRAU.

Baada ya uhuru mwaka wa 1961 Mwalimu Nyerere alimteua Kassanga Tumbo kuwa
Balozi wa Tanganyika Uingereza.

Kassanga Tumbo hakukaa Uingereza akajiuzulu ubalozi akarejea Tanganyika na kuunda
chama cha siasa, Tanganyika Democratic Party, (TDP).

Mwaka wa 1958 kutokana na Uchaguzi wa Kura Tatu baadhi ya wanachama wa TANU
wakajitenga na kuanzisha chama cha Kiislam, All Muslim National Union of Tanganyika,
(AMNUT).

Waislam walikikataa chama hiki kwa iyo hakikupata nguvu.

Wakati Kassanga Tumbo anarudi Tanganyika kutoka Uingereza baada ya kujiuzulu
ubalozi, Kassanga Tumbo aliingia mazungumzo ya kuunganisha chama chake TDP
na AMNUT.

Hii ilikuwa mwaka wa 1963.

Mwaka 1964 askari wa Tanganyika Rifles waliasi na na baada ya Waingereza kumaliza
uasi ule ikapita kamata kamata na Salum Abdallah na Kassanga Tumbo walikamatwa
na kuwekwa kizuizini pamoja na viongozi wengine wa vyama vya wafanyakazi.

Huu ukawa ndiyo mwisho wa TRAU na vyama vingine vya wafanyakazi ikaundwa NUTA.
Yako mengi lakini kwa sasa naomba kusimama hapa.
History kama hizo yafaa mziweke wazi watu wapate history kamili ya Tanganyika sio ile ya upande mmoja.Inatakiwa watu wajue mchango wa Bibi Titi,Kambona, nk kwenye history ya nchi hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
heee!!! kumbe alikua anatumika Kwa maslahi ya watu Fulani?! tuachane na hayo nyerere alikua kiongozi mwenye akili sana si jambo dogo kutupatia Uhuru kutoka kwa watu waliokuahawapo tayari kuachia dhahabu,almasi,shaba,ndovu,na mengine mengiiii haikua kazi rahisi aisee...
Si kweli kwamba tuliwaondoa wakoloni, ni wao waliona ni hasara na gharama kubwa sana kutawala hivo wakaona ni vyema warudi kwao kwa kusimika vibaraka wao ( wakoloni weusi) ili waendelee kuinyonya Africa indirect. Maana tulitegemea kuuza mazao,madini,na raslimali zote kwao,na wao walitupangia bei, tishio kubwa kwao ni China ambae kajipenyeza Africa kwa uwekezaji wa dola billion 10,lkn ye akiwa ni mnufaika mkuu 80% ya uwekezaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani kwenye majadiliano tu ya vyama vingi vita ikatokea !!! Nyerere bado alikua sahihi kuvifuta muda ulikua bado na hatukua tayari tumejiandaa na vyama vingi...sipingi ila najaribu kuangalia alichokiona Mwl nyerere by then kwenye upande Wa pili Wa shillingi je tulijiandaa wakati huo?!
Alivipinga si kwamba hatukujiandaa,bali aliogopa changamoto, vyama vingi vimekuwepo hata kabla ya uhuru,soma history. Alivipiga marufuku hakutaka kupingwa kwa maana alikuwa anaamini kwa wakati ule kuwa anajua kila kitu,na aliwaogopa wasomi mfano tuntemeke SANGA,Kambona, Nk.Kwa sababu ya kujua kila kitu akafail kwenye uchumi, akaja kuelewa umuhimu wa kukosolewa akiwa keshachelewa kila kitu kimeharibika,mashirika,viwanda, Mashamba,miradi yote imekufa.Hata haya uyaonayo sasa yafanywayo na ccm ni sababu ya Presha za upinzani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapewa ubalozi huridhiki, unamwona aiyekuteua ni bwege, unaacha ubalozi ili uje umshugulikie, ukiwa ma paund 60,000 za kummaliza, akikugeuzia kibao eti dicteta. Mlitaka nchi iwe kama Somalia ili mradi tu Jamaa zenu waitwe marais
Sio wote tumbo kwanza, wengine watu kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngongo,
Inawezekana hujaona mchango wangu humu.
Kwa nini mimi nikulazimishe wewe kuhusu historia ya wazee wangu?

Nikulazimshe kwa kisa gani na ndiyo iwe nini?
Historia ya Gerezani katika uhuru wa Tanganyika ni ya pekee sana.

Mimi simlazimishi mtu yeyote wao wenyewe wanaposikia niko uwanjani
wanafika kwa khiyari zao kwani wanajua kuna kitu cha maana watajifunza.

Kama hivi wewe ulivyonkaribisha mimi hapa kwenye jamvi.
Je, kuna mtu kakulazimisha kuniita?

Umeniita kwa kuwa ndani ya nafsi yako unajua kuwa mimi najua.

Na hakika Alhamdulilah naijua historia ya wazee wangu na wengi wamethibitisha
hili.

Uzi huu nimeuona na nimeeleza niyajuayo kuhusu Kassanga Tumbo.

Kassanga Tumbo ana nafasi ya pekee kwangu kwani yeye na babu yangu Salum
Abdallah
ndiyo walikuwa waasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU)
mwaka wa 1955.

Pekua utaona mchango wangu.
Hii ni ziada kwako kukuthibitishia kuwa hii historia iko ndani kwetu.

Mtaa wa Kanoni Tabora Isevya mwisho wa mtaa unaelekea Kachoma katika miaka
ya mwanzoni 1960 kulikuwa na nyumba mbili nzuri sana zinatazamana.

Nyumba hizi zilikuwa moja ya babu yangu na nyingine ya Kassanga Tumbo.

Kadoda,
Katika lugha ya Kiswahii kudoda ni kuharibika.
Mathalan unga ukiingia maji na hauwezi kusongwa ugali tunasema ''umedoda,''

Unasema natokwa na ''povu.''
Povu linitoke mdomoni kwa kisa gani?

Hapa katika mchango wangu kuhusu Kassanga Tumbo nimeeleza pamoja
na historia ya babu yangu Salum Abdallah.

Je, lipo povu?
Naetokwa ni mishipa ya shingo si mimi.

Mtafute na jiangalie wewe binafsi.
Mohamed Said: GEREZANI NA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA SIASA KATIKA MJI WA DAR ES SALAAM MIAKA YA 1950
Ni history nzuri sana japo zimefichwa,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Informer,
Naikumbuka hii sana. Tuliposoma kwenye magazeti kuwa Kassanga Tumbo amesema amelipwa hela na Uingereza kumpindua Nyerere tulijua huyu jamaa ataishia detention. Na kweli muda haukupita akawekwa detention. Mimi nadhani tatizo la watu kama marehemu Tumbo ni kwamba alikuwa na akili sana na alijiona kuwa na akili sana na watu aina hii mara nyingi wana matatizo ya kutojua kitu cha kusema hadharani. Kuna mwingine yule aliyemfuata Mwalimu baada ya masomo na kusema kazi anayostahili kupewa ni ile aliyo nayo Mwalimu, sasa mtu kama huyu kweli utasema ana akili timamu?
Tuntemeke Sanga
 
Ukweli ni kwamba histori ya Tanganyika imechakachuliwa sana na Baba CCM yaani Tanu, yapo mengi kama haya. Na miaka 20 ijayo yanaweza yasipatikane tena. Maana wale wazee waliokuwepo wakati huo wanaishia. Namkumbuka Zuberi Mtemvu, Michael Sanga, Patric Kunambi, Kasela bantu, Lifa Chipaka, Kassim Hanga, Oscar Kambona, Aboud Jumbe, Mwamwindi the Great, NK. Ni vizuri kujua upande wa pili wa historia.


Kama tarehe ya uhuru iko hivi historia wazee itakuwaje?
 
Back
Top Bottom