Huyu ndiye Giriki, Dereva aliyetoka na basi Dar saa 12 asubuhi, akaingia Mbeya saa saba mchana

Yuko kanunu
Okay mkuu,tena nakumbuka kwenye huo msafara kulikuwa na land cruiser ambulance iliondoka saa kumi na mbili kasoro kyela tulikuja ikuta vigwaza imepaki dereva anasema amechoka,hesabu yangu(timer) ilianzia uyole japo tulitoka kyela saa tatu na nusu,kwa kweli yule jamaa ni noma.Utingo wa coaster alimsaidia jamaa wa ambulance hadi ubungo.
 
Hiyo dereva wa ambulance angeambiwa apeleke gari Ngara angefia njiani kwa uchovu
 
Magari ya zamani yalikuwa ni malori modified. Lory la kubeba tani 30 libebe abiria 65, giant box high na low, diff imechezewa, bodi limebalance. Utaipenda Scania
Una kumbukumbu sana. Uko sahihi kabisa. Watu hawaamini basi li aweza kwenda 160 kph. Hata kama dashboard inaishia 140 mshale ulikuwa unazidi.
 
Una kumbukumbu sana. Uko sahihi kabisa. Watu hawaamini basi li aweza kwenda 160 kph. Hata kama dashboard inaishia 140 mshale ulikuwa unazidi.
Hapana mabasi ya zamani mengi yalikuwa scania na scania hata lori haziwahi kuvuka speed 125km/h kwenye dashboard japo speed sidhani kama ikifika hiyo 125km/h haiongezeki.
 
Ina maana hizi tochi za usalama hazimuliki? Mwendo mkali unakaribisha kifo.
 
Siku hizi magari hayakimbii. Zamani Embakassy lilikuwa ni basi lisilokimbia kabisa, la kupanda wazee na wagonjwa. Likitoka Dar saa 12 asubuhi Mbeya linaingia saa 10.30 jioni sio saa nne usiku
Nilikuwa nikitoka Mbeya Asubuhi na Skanlink derava Juma au Shaibu nafika Dar mapema nafunga mzigo K koo na kesho nageuza leo gali linalosifiwa linafika Mbeya saa moja na nusu usiku badala ya saa nane au tisa

Kina marehemu Kaberege/Masia wakifufuka wakisikia hii watashangaa
 
Sio kamba kaka hata Marehemu Kaberege aliwahi kufika Uyole saa Saba akiwa na Masia
Na mpaka sasa akuna alievunja rekodi ya Giriki aliingia Songea saa tisa akiwa na Tawaqal enzi hizoooo
 
Kaberege alifariki 😥😭 sikuwa na habari.
 
Kiswele ilikuwa ni basi ya songea dar , haikuwahi kwenda mbeya
Zimewahi Mkuu derava wake alikuwa babu hivi anaupara alikuwa na mbwembwe nyingi (alikuwa anachomekea soksi) kwa sasa ni marehemu alikuwa na matatizo ya miguu
 
Huyo hakuwa giriki , ila lawama alipata yeye, , Giriki kwanza njia yake kubwa ilikuwa ni Dar Mbeya , Songea alikuwa anaenda mara chache chache
Alikuwa Giriki Giriki alikuwa mbele na Tawaqal na Shabiby ilikuwa nyuma ikimfukuzia kwa kasi pale kwenye kona za mpakani Iringa/Ruvuma wakati huo derava wa Shabiby kona ilimshinda akaenda kuvamia gema alikukufa hapo hapo akiwa ametoa macho kwa mshangao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…