Huyu ndiye Kiongozi na Mwanadamu anayependwa, kukubalika na mwenye ushawishi zaidi kwa sasa hapa nchini

Huyu ndiye Kiongozi na Mwanadamu anayependwa, kukubalika na mwenye ushawishi zaidi kwa sasa hapa nchini

Siyo tu Mzumbe bali ni kutoka vyuo mbalimbali.Na ikumbukwe vyuo vingi sana vina mpango wa kumpatia heshima hiyo kutokana na uchapakazi wake uliogusa Maisha ya mamilioni ya watanzania pamoja na kuleta mageuzi makubwa sana hapa Nchini kisiasa,kijamii , kiuchumi n.k.
Umesema vyuo vingine vina mpango wa kumpatia PhD,waombe wale pause angalao rais wetu apate muda wa kupumzika.
 
Unatafuta ugali wako wa kila siku!😂
Wewe umesoma ila elimu yako haikusaidii chochote, ndo nyie wote fani mlizo nazo mlichaguliwa na wazazi/walezi saivi umeshindwa kuibadilisha kua pesa umeamua kuwa comedian jf😥
Ugali sitafutii hapa jukwaani
 
Ndugu Luka, punguza kidogo. Sifa zingine hazifai.
Mtu mcha Mungu anajulikana na Mungu mwenyewe tu.
Wacha Mungu utawajua kwa matendo yao kama ilivyo kwa Rais wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.Ambaye amekuwa na hofu ya Mungu kwa matendo na kauli zake.
 
Kazi ngumu sana hii. Usiitamani hata kidogo maana utakosana na jamii.
Hivi kwa akili zako unafikili kuna mtu anatamani kuwa kama uyu baba🤔
Na jambo la kushukuru kajikita kwenye mambo ya siasa akihamia kwenye dini atawaambukiza ujinga watanzania wengi mnoo
 
Mungu pekee ndiye mwenye hiyo mizani.
Na Mungu alishatuambia kuwa tutawajua kwa Matendo yao mema kama ilivyo kwa Rais wetu Mpendwa na kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia.Mama mwenye upendo, huruma,utu , uungwana,ukarimu na mwenye kugusa Maisha ya watanzania
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kuna mwanadamu mmoja na Raia mmoja ambaye kwa sasa ndiye anayependwa , kukubalika,kuungwa mkono na mwenye ushawishi wa hali ya juu sana hapa Nchini.Ndiye Binadamu ambaye asipoonekana hata kwa siku moja tu hadharani watu wanaanza kumtafuta kama Pesa.Ni kiongozi ambaye anapendwa na watu wa makundi yote na mwenye kuheshimika sana hapa Nchini.

Huyu ndiye kiongozi na Mtu ambaye maneno yake tu huwafanya wagonjwa waliolazwa wodini na mahospitalini kupata tabasamu na nafuu na kujihisi wamepona wamuonapo mbele ya nyuso zao .ndiye kiongozi mwenye uwezo wa kuwapa faraja watu wenye majeraha mioyoni mwao.ndiye kiongozi ambaye kwa sasa ameteka mioyo ya mamilioni ya watanzania. Ndiye kiongozi pekee mwenye uwezo wa kuzungumza na kusikilizwa na kuaminika na kuaminiwa kwa jambo lolote lile.

Ndiye kiongozi ambaye amebeba matumaini na hatima ya maisha ya mamilioni ya watanzania mikononi mwake,ndiye kiongozi ambaye watu wote humtizama yeye kama nyota ya asubuhi kwa wavuvi.ndiye mtu ambaye watu wana imani ya kutimiza ndoto zao kupitia yeye.ndiye kiongozi ambaye amefanya mioyo na vifua vya watanzania kujawa na furaha ,amani, utulivu, matumaini na matarajio makubwa sana.

Anapendwa , kukubalika,kuungwa mkono ,kuaminika na kuwa na ushawishi Hapa Nchini kwa sababu Maisha yake hapa Duniani yamefanyika kuwa baraka kwa mamilioni ya watu .kwa sababu amegusa mioyo na Maisha ya mamilioni ya watanzania,kwa sababu ameleta tabasamu na matumaini kwa watu,kwa sababu ameleta nuru katikati ya Giza ya maisha ya watu,kwa sababu ameonyesha njia ya matumaini kwa watu waliokuwa wapo njia panda.kwa sababu amewezesha wengi kutimiza ndoto zao,kwa sababu kila uchao umekuwa bora kuliko jana kwa watanzania.

Huyu ni Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge.huyu ndiye mboni ya Taifa letu .ndiye aliyebeba na kushikilia furaha ya mamilioni ya watanzania.kwahakika Mama huyu jasiri , shupavu, imara, hodari na madhubuti ataendelea kuwa nguzo ya Amani ya Taifa letu kwa ulimi wake,matendo yake na uchapakazi wake utakuwa msingi wa ustawi wa Taifa letu na watanzania wote kwa ujumla wake.

Huyu Mama ni kama Maji tu usipoyanywa utayaoga tuuu utake usitake. Huwezi kumkwepa wala kumchafua wala kumpaka matope.Maana kibali alichopewa na Mungu kuongoza Taifa hili hakiwezi kunyang'anywa na Mwanadamu wala kuharibiwa na mtu mbele za watanzaniaView attachment 3160299View attachment 3160300

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Sasa kama anapendwa kulingana uharo wako inakuwaje mitutu ya bunduki kila kona na kuokotwa watu wametangulizwa kwa Sir.God?.Mtu anayependwa huwa anajali utawala wa sheria na uhuru wa watu kutoa maoni.Yaani,unawafunga miguu na mikono washindani wako afu unawambia mshindane kukimbia mita mia! Huo ni ukichaa.
 
Sasa kama anapendwa kulingana uharo wako inakuwaje mitutu ya bunduki kila kona na kuokotwa watu wametangulizwa kwa Sir.God?.Mtu anayependwa huwa anajali utawala wa sheria na uhuru wa watu kutoa maoni.Yaani,unawafunga miguu na mikono washindani wako afu unawambia mshindane kukimbia mita mia! Huo ni ukichaa.
Rais wetu Mpendwa amekuwa akijali na kuendesha Nchi kwa kuzingatia misingi ya kisheria na utawala bora.ndio Maana unaona hata vyama vya siasa kwa sasa vipi huru kufanya siasa kwa uhuru kabisa bila bughudha pale vinapozingatia sheria.
 
Back
Top Bottom