Huyu ndiye Padri Privatus Mutekanga Karugendo (1956-2021)

Huyu ndiye Padri Privatus Mutekanga Karugendo (1956-2021)

Tubuni mkasafishwe na Damu ya Yesu ili muokolewe
Halafu usikute unasali kwa Gwajima! Halafu unahubiri kuokolewa! Hapo ulipo unajifanya huna dhambi! Kwenu nyinyi dhambi ni pombe tu! Na kwa sababu mnatambua fika Wakatoliki wengi wanakunywa! Tena wakati fulani bila hata kificho.

Kugongana nyinyi kwa nyinyi, wala siyo dhambi, tena kwa kisingizio cha kufanya maombi ya usiku! Mkigongwa na Mkatoliki, ndiyo dhambi!!
 
Tangu mwaka 1990 nilipokuwa kidato cha tatu katika Seminari ya Katoke (Biharamulo) hadi leo nimemfahamu Hayati Privatus Mutekanga Karugendo (65) kama mwanateolojia, mwanafalsafa, mchambuzi wa masuala mtambuka, mtafiti, mwandishi, mume na mzazi.

Naandika tanzia hii kuonyesha mafanikio na changamoto zake ninazozifahamu ili viwe somo kwa waombolezaji tuliobaki hai.

Privatus amefariki dunia jioni ya 24 Juni 2021, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam, kutokana na changamoto ya upumuaji aliyokutana nayo ndani ya masaa 12.

Changamoto hii ilitanguliwa na homa ya siku tatu ikiambatana na kushuka ghafla kwa kiwango cha sukari mwilini. Kwa kuwa hati ya kifo bado haijatoka hatujui chanzo cha changamoto hii. Ameacha mke mmoja, Dk. Rose Katesigwa, na mtoto mmoja, Yesigwe.

Kwa mujibu wa mkewe, Dk. Rose Katesigwa, niliyeongea naye leo, mazishi ya Privatus yatafanyika Jumatatu ya 28 Juni 2021, katika Makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Kwa sasa msiba uko nyumbani kwake, eneo la Tabata, Dar es Salaam.

Kuzaliwa

Kwa mujibu wa maandiko yake mwenyewe, Privatus ni mmoja wa watoto wa kiume sita katika familia ya Karugendo. Wengine ni Primus, Pacificus, Pascrates, Princhipius, na Prudence. Tayari Princhipius na Prudence wametangulia katika haki.

Privatus alizaliwa 14 Januari 1956, katika Jimbo la Bukoba. Lakini maisha yake yote ya upadre yamekuwa ni Jimboni Rulenge, kwenye wilaya za Ngara, Biharamulo, Karagwe na Kyerwa.

Elimu ya juu na utumishi wa kikuhani (1975-2000)

Alianza masomo ya seminari kuu mwaka 1975, kupadirishwa, na kufanya kazi ya utumishi wa kutoa huduma za kikanisa hadi mwaka 2000. Hivyo, amekuwa sehemu ya Kanisa Katoliki kwa kipindi cha miaka ipatayo 25.

Alisoma Diploma ya Filosofia katika Seminari ya Ntungamo huko Bukoba (1975-76); na Stashahada ya Teolojia katika Seminari ya Kipalapala huko Tabora (1977-81). Amefanya kazi kama Paroko Msaidizi katika Parokia ya Ntungamo huko Ngara (1982); na kama Mmisionari katika Parokia ya Munchen huko Ujerumani (1982-84).

Alipata Elimu ya Kilimo katika Chuo cha Kilimo Uyole huko Mbeya (1985-87); na kurudi kufanya kazi kama Paroko Msaidizi katika Parokia ya Bushangaro huko Karagwe (1987-97). Pia amehudumu kama Paroko katika Parokia ya Bushangaro huko Karagwe (1998).

Kisha alikwenda kusoma Diploma ya Haki za Binadamu Katika Chuo cha Copenhagen huko Denmark (1999); na kurudi kufanya kazi kama Paroko Msaidizi katika Parokia ya Buziku huko Biharamulo (1999-2000).

Mgogoro wa Privatus na Askofu Niwemugizi

Mwaka 2000 ulizuka mgogoro kati ya Padre Privatus na mkubwa wake wa kazi, Askofu Severine Niwemugizi. Kutokana na mgogoro huu, Privatus alisimamishwa kutoa huduma na kuamuliwa kuondoka jimboni Rulenge na kwenda kuishi nyumbani kwa wazazi wake Bukoba alikozaliwa.

Wakati huo alikuwa ametumikia kanisa kwa miaka ipatayo 20, na wazazi wake wote walishakufa. Pia, mfumo wa utawala wa Kanisa Katoliki haitoi kiinua mgongo kwa padre au sista anayeachishwa kazi. Aidha, hakuna utaratibu wa kuchangia mifuko ya pensheni ya Taifa kwa ajili ya padre au mtawa aliyeachishwa au kuacha kazi.

Hivyo, pamoja na kulitumikia kanisa kwa miaka ipatayo 20, ghafla Privatus alijikuta ni sawa na mwanafunzi aliyemaliza Chuo ambaye hubeba begi lake kurudi nyumbani. Alijikuta njia panda.

Alimua kumwomba rafiki yake mmoja, Askofu Benson Bagonza, wa KKKT Dayosisi ya Karagwe, ampangishie nyumba ya kuishi kwa muda. Akawa anatafakari afanye nini kama njia ya kupata mkate wa kila siku katika mazingira haya mapya. Askofu Bagonza alikubali kumsaidia.

Lakini, baadaye, Privatus aliamua kuondoka Karagwe na kwenda kuishi nje ya Jimbo la Rulenge. Alihamia huko wilaya ya Magu, mkoani Mwanza. Huko alipokelewa kwa ukarimu na Kaya ya Kisukuma, familia ya Mwalimu Mkina. Siku zikasonga mbele akiwa hapo anatafakari jinsi ya kupata mkate wake wa kila siku. Yalikuwa ni majira ya majaribu makubwa kwake.

Wakati akitafakari hayo, Askofu Niwemugizi aliamua kufungua kesi dhidi yake katika mahakama ya Kanisa akimtuhumu kwa makosa kadhaa. Kwa mujibu wa nakala ya barua aliyonionyesha kulikuwepo na tuhuma kama sita hivi. Nakumbuka tuhuma mbili.

Kwanza ni tuhuma ya kuvunja kiapo cha mapdre kuhusu maisha ya useja. Na pili, ni tuhuma kuhusu tabia ya kuhimiza watu kutumia kondomu kama kingamimba na kingamagonjwa kinyume cha mafundisho rasmi ya Kanisa Katoliki.

Kwa mujibu wa sheria za Kanisa Katoliki, Askofu anapofanya maamuzi ya kisheria lazima ashauriane na mwanasheria mwingine mmoja. Niwemugizi aliamua kushauriana na mwanasheria mwenzake, Padre Charles Kitima.

Hatimaye, Askofu Niwemugizi alimtafuta Askofu Mkuu wa Metropolitani ya Kanda ya Ziwa Viktoria na wakakubaliana kuunda Mahakama ya Kanisa ya Kanda (Metropolitan Church Tribunal) iliyojumuisha Majimbo ya Rulenge, Bukoba na Mwanza, yaani hadi Magu alikukuwa anaishi Privatus.

Kwa mujibu wa Sheria za Kanisa, mara nyingi, Mahakama ya Kikanda ni mahakama ya rufaa (second instance court). Kwa mfano, inaweza kutumika kama mahakama ya mwanzo pale jimbo linapokuwa linashitakiwa.

Kwa mujibu wa maelezo ya Privatus, mahakama hii ya Kikanda ilipokea mashitaka dhidi yake kutoka kwa Askofu Niwemugizi wa Jimbo la Rulenge, bila mashtaka hayo kuanzia kwenye Mahakama ya Mwanzo (first instance court) iliyopaswa kuanzishwa jimboni Rulenge .

Hatimaye mahakama ya Kanda ilipokea utetezi wa maandishi kutoka kw Privatusi wenye mapingamizi ya awali yaliyoeleza dosari hizi za kisheria. Lakini bado, mahakama hii iliamua kuendeleza kusikiliza kesi dhidi ya Privatus. Kwa mujibu wa maelezo ya Privatus hakupewa wito wenye hadhi ya kisheria ili aweze kufika na kujitetea katika mahakama hiyo.

Hatimaye, bila yeye kuwepo, mahakama hiyo iliamua kusiliza kesi upande mmoja na kumtia hatiani Privatus. Hukumu hii ilipelekwa kwa Papa. Kwa mujibu wa gazeti la Kiongozi, toleo namba moja la mwaka 2009, Papa Yohanne Paulo II alikubaliana na hukumu hiyo.

Hatimaye Papa alifanya uamuzi wa kumondoa Privatus kutoka katika daraja la upadre tarehe 14 Septemba 2008, kwa kutumia hati ya Kipapa yenye kumbukumbu namba 4182/08. Baadaye kidogo, uongozi wa Kanisa ulipeleka hati ya Papa kwenye televisheni ya Taifa, kuisoma na kuionyesha wazi kwa umma wote.

Mnamo 26 Aprili 2017, miaka tisa baada ya kuvuliwa upadri, Privatus alifunga ndoa na Rose Birusya. Ndoa hiyo ilifungwa katika Kanisa la Mtakatifu Petro, jijini Dar es Salaam, katika misa iliyoongozwa na Padri Stefano Kaombe.

Kusudi aweze kufunga ndoa hiyo ilibidi kwanza aombe kuondolewa katika daraja la upadre. Kwa mujibu wa taratibu za Kanisa mchakato huo huanza baada ya mhusika kuandika barua kwa Papa kupitia kwa Balozi wa Papa.

“Kabla sijaandika barua hiyo, niliambiwa na Paroko kwamba tayari Balozi wa Papa anayo barua ya Padre Privatus aliyemwandikia Papa ili kuomba kibali cha kuoa tangu siku zile nilipoondolewa kwenye rosta ya upadre,” aliwahi kutamka Privatus.

Hivyo, Privatus aliamua kuitumia barua hiyo kukamilisha azima yake ya kufunga ndoa, na paroko alikubaliana naye. Privatus amekufa anaamini kwamba barua hiyo iliandikwa na Askofu Niwemugizi.

Mgogoro huu kati ya Padre Privatus na Askofu Niwemugizi unaweza kueleweka kama ukiwekwa ndani ya mraba unaounganisha Mtaguso wa II wa Laterani (1139), Mtaguso wa Trent (1545-63), Toleo Jipya la Sheria za Kanisa Katoliki (1983), na Waraka wa Papa Paul VI uitwao “Humanae Vitae (1968).”

Mwaka 1139 Papa Innocent II alitunga kanuni iliyopiga marufuku mapadre kufunga ndoa. Mwaka 1563 Papa Pius IV, kupitia Mtaguso wa Trent (1545-63), ulitunga kanuni iliyopiga marufuku walei kupadirishwa. Waraka wa “Humanae Vitae (1968)” ulipiga marufuku matumizi ya kingamimba kama vile kondomu, vidonge na kitanzi.

Na mwaka 1983 Sheria za Kanisa (CIC 290-293) ziliweka utaratibu wa kisheria wa kumwondoa mtu katika daraja la makleri na kumweka katika daraja la walei. Hadi leo kuna ukuta unaotenganisha sakramenti ya makleri (upadirisho) na sakramenti ya walei (ndoa).

Lakini, kwa mujibu wa sheria za Kanisa, ukuta huu una mlango unaofunguka kuelekea upande mmoja wa walei, na hivyo kuwaruhusu makleri kugeuka walei. Lakini bado walei waliofunga ndoa hawaruhusiwi kugeuka makleri.

Privatus alisema na ameandika sana kwamba, ni kweli kwamba aliwahi kuteleza na hivyo kukiuka kiapo cha useja. Lakini aliendelea kusema kwamba tayari alikwisha kutubu, tena kwa Askofu Niwemugizi.

Lakini, “Askofu Niwemugizi alitumia siri zangu alizizipata kupitia zoezi la kuendesha sakramenti ya kitubio kunitia hatiani, jambo ambalo ni kinyume na sheria za kanisa,” alilalamika Privatus kupitia maandiko yake kadhaa. Fungu la 983(1) la sheria za kanisa Katoliki (1983) lahusika.

Kuhusu marufuku dhidi ya matumizi ya kinga mimba, Privatus alikuwa anakosoa kwa hoja fundisho lifuatalo:

“This particular doctrine [that ‘each and every marital act must of necessity retain its intrinsic relationship to the procreation of human life’] … is based on the inseparable connection, … which man on his own initiative may not break, between the unitive significance and the procreative significance which are both inherent to the marriage act.” (Pope Paul VI, 1968: Humanae Vitae, No. 12).

Privatus alipenda kusema kuwa hoja ifuatayo haina ukweli wowote: “the unitive significance and the procreative significance … are both inherent to [every instance of] the marriage act”; thus, “each and every marital act must of necessity retain its intrinsic relationship to the procreation of human life”.

Kwa maoni ya Privatus, hoja hii inachanganya maembe na machungwa, kwa kuanzia kwenye dokezo linaongelea maumbile kwenda kwenye hitimisho linalongelea maadili.

Yaani, ni hoja inayopingana na kanuni ya kimantiki iitwayo “no ought from is principle,” yaani “NOFI principle.” Amekufa akiwa ameushikilia msimamo huu kwa uthabiti.

Kwa mtazamo wake, “contraception is extrinsically evil.” Yaani, uharamu wa kitendo cha kutumia kingamimba unategemea aina ya kingamimba iliyotumika na mazingira husika.

Maisha ya utafiti (2003-2018)

Kwa kipindi cha miaka 20 Privatus amekuwa anatafuta mkate wake wa kila siku kwa fanya kazi kama mtafiti asiyeajiriwa, yaani “daiwaka.” Kupitia utafiti huu ameandika au kushiriki katika uandishi wa ripoti zaidi ya 20, zinazohusu masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii hapa Tanzania.

Kazi za uandishi na makala

Mbali na kutafiti na kuandaa ripoti za kitafiti, Privatus alikuwa mwandishi wa vitabu na makala zaidi ya 1000 kwa lugha za Kiswahili, Kiingereza na Kijerumani.

Makala za Kijerumani zilichapishwa na gazeti liitwalo “Gemainde Heuite,” la Ujerumani. Makala za Kiswahili zilichapishwa kupitia magazeti ya Rai, Raia Mwema Tanzania Daima, na Uwazi.

Vitabu alivyoandika na kuchapisha ni pamoja na: Maisha yangu Wito wangu; Ubikira; Pambazuko gizani; Maswali 40, majibu 40 ya January Makamba; Maisha yangu Baada ya Miaka 70.

Pia kuna vitabu ambavyo ameandika lakini ameaga dunia kabla havijachapishwa. Vitabu hivyo ni: wasifu wenye jina “Mawazo, Matendo na Matunda ya Askofu Christopher Mwoleka” pamoja na riwaya iitwayo “Sista Kobulongo Maria Mtawa wa Karonga.”

Wakati wa uhai wake, Privatus alinambia kuwa anataka wasifu wa Mwoleka uchapwe na Pius Ngeze, wakati alitaka riwaya ya Mtawa wa karonga ichapwe na Elieshi Lema.

Kazi za ustawi wa jamii

Mbali na kazi za utafiti, Privatus alifanya kazi za kustawisha jamii, akiwa kama mshauri, au mjumbe wa Bodi au mwanachama wa taasisi mbalimbali zipatazo 15.

Taasisi hizo ni pamoja na: Edmin Education Centre; PESENET; SODT; KADENVO; DAC; European Community; USAD; KDCU; TGNP; SNV; HakiElimu, GEMSAT na Mkamilishano.

Hoja zake tutaendelea kuzichunguza sisi tuliobaki hai. Apumzike kwa amani Privatus.
Niliwahi kumpokea kwangu na mkewe Rose nilipokuwa naishi Kimara. Alinielezea misimamo yake mingi kwa hoja na nilimkubalia baadhi. Mingine tulikubaliana kutofautiana kwa heshima na kuendelea kuheshimu tofauti zetu.

Aidha, nilimshirikisha kazi ya ushauri niliyoipata CHADEMA ya kuwaandalia sera za chama zilizokuja kuzinduliwa 2004 baada ya Freeman Mbowe kupata uenyekiti. Alipenda sana harakati na mabadiliko ya kisiasa. Poleni wote kwa kumpoteza mtu mwenye fikra huru na pevu!

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
mfumo wa ajabu sana mtu kutubu kwa binadamu mwenzake
huu siyo mfumo wa kiKiristo ni wa kipagani
Mungu ana mgogoro na sisi kwa sababu ya dhambi. Dhambi inaelezewa katika Biblia kuwa uvunjaji wa sheria ya Mungu (1 Yohana 3: 4) na uasi dhidi ya Mungu (Kumbukumbu la Torati 9: 7; Yoshua 1:18). Mungu huchukia dhambi, na dhambi husimama kati yetu na Yeye. "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!" (Warumi 3:10). Wanadamu wote ni wenye dhambi kwa sababu ya dhambi tuliyorithi kutoka kwa Adamu, pamoja na dhambi tunayofanya kila siku. Adhabu tu ya dhambi hii ni kifo (Warumi 6:23), si kifo cha kimwili tu bali kifo cha milele (Ufunuo 20: 11-15). Adhabu ya haki kwa dhambi ni Jahannamu ya milele
"Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu" (1 Timotheo 2: 5).
Huu utaratibu wa kutubu kwa binadamu wenzetu ni kinyume na maandiko ambayo yanasema binadamu wooote, wakiwemo watawa wa madaraja yote( maaskofu,mapadre na papa mwenyewe ni binadamu wa kawaida mbele ya Mungu)
Yesu anawakilisha wale ambao wamemtegemea Yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Anatupatanisha, kama vile wakili anayemtetea mteja wake, akimwambia hakimu, "Hakimu, mteja wangu hana hatia ya mashtaka yote dhidi yake." Hiyo ni kweli kwetu pia. Siku moja tutakuna na Mungu, lakini tutafanya hivyo tukiwa tumekwisha samehewa dhambi kabisa kwa sababu ya kifo cha Yesu kwa niaba yetu. "Mwanasheria mtetezi" alichukua adhabu kwa ajili yetu!
Naam

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Simjui vizuri Padre Karugendo wala Askofu Niwemugizi. Ila nahisi kuna tatizo kubwa somewhere. Hizi kazi zinachukuliwa for personal glory instead of leading the shepherds to the lord. It is veru strange for a person to use confession against a person who confesses. That is what is termed as sin against the Holy Ghost. kama ni kweli, kuna shida kubwa sana.
 
Hii kesi nimeanza kuisikia tangu nikiwa darasa la sita mkuu, (I've been a seminarian since std 6 FYI).

Nimefuatilia pande zote mbili na kusoma baadhi ya machapisho yao kwenye magazeti mbalimbali. Zaidi zaidi nimesikia hadi maoni ya baadhi ya members of clergy kuhusu hii issue. Kiufupi bado ilikua na mixed feelings sana.

Unaposema nmesikiliza upande mmoja unakosea sana.

Anyway hio ni view yangu khs hio issue, naheshimu view yako pia.

Ila nikuulize swali, kwa nn kesi ilirushwa step?, kwa nn the late hakusikilizwa kwa namna inavyopaswa?, Barua yake ya kuomba idhini ya kufungwa ndoa iliandikwa na nani na kupelekwa kwa balozi bila the late kujua?

Na kumbuka Papa kiukweli hatoi hukumu, yeye anaidhinisha tu hukumu, coz kama unajua structure ya katoliki nadhan unafahamu kwamba majimbo yanaruhusiwa kujiendesha independently kwa baadhi ya mambo, then wanaomba tu idhinisho la papa. Na papa aliidhinisha kitu ambacho amepelekewa tu na hao wasaidizi wake, hivyo kama ilitumiwa chuki basi Fr Karugendo alikua hana cha kufanya ila kusubiri tu hukumu coz wakubwa ndio wanaamua Papa aone nini na nini?

Kama nilivyosema sina authority yyt kujudge hii issue ila kwa view yangu hii ilikua ni unfair play.

Kama Fr Karugendo alitolewa kwa kosa la adultery basi na bishop ilibidi awe responsible, au watoe ushahidi kwamba nje ya kitubio cha Fr Karugendo nini zaidi kilifanya authority ijue kama Fr Karugendo alifanya hilo kosa?

Double standards, Autocracy ndio matatizo huko RC.
Sawa.

Unamaanisha uongozi wa juu wa Kanisa Katoliki hupokea tu report na kunifanyia kazi bila verification yoyote!!?

Kwa mujibu wa andiko, adultery ni moja kati ya makosa sita aliyoshitakiwa nayo. Ukiwa mtu uliyefuatilia hii case kwa ukaribu kama ulivyosema, je, makosa yote sita alisingiziwa?
 
Mkuu kosa la padre kufundisha kinyume na mafundisho ya kanisa adhabu yake sio direct excommunication, cannon law haisemi hivyo.

Kutokana na nilichofundishwa Iko hivi, kwanza muhusika anapelekwa kwenye kamati maalum ili akili kama kweli alikosea au la, (huko Fr Karugendo hakufikishwa) refer kesi ya Martin Ruther uone mfano wa hii kesi in action.

Kama mhusika atakomalia msimamo wake kwa hoja ambazo hazina mashiko ndipo atapewa excommunication, lkn kama akikubali baada ya majadiliano kuwa alikosea basi hatopewa excommunication.

Usiangalie mambo juujuu hivyo mkuu


Haihitaji PHD kuona hio kesi ilipindishwa.
Hakuna sehemu nimesema Fr. Karugendo alikuwa excommunicated lest asingeruhusiwa hata kufunga hiyo ndoa. Ninaongelea abuse ya Sakramenti ya Kitubio kama ingefanywa na Askofu Niwemugizi angekuwa excommunicated right away.
 
mfumo wa ajabu sana mtu kutubu kwa binadamu mwenzake
huu siyo mfumo wa kiKiristo ni wa kipagani
Mungu ana mgogoro na sisi kwa sababu ya dhambi. Dhambi inaelezewa katika Biblia kuwa uvunjaji wa sheria ya Mungu (1 Yohana 3: 4) na uasi dhidi ya Mungu (Kumbukumbu la Torati 9: 7; Yoshua 1:18). Mungu huchukia dhambi, na dhambi husimama kati yetu na Yeye. "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!" (Warumi 3:10). Wanadamu wote ni wenye dhambi kwa sababu ya dhambi tuliyorithi kutoka kwa Adamu, pamoja na dhambi tunayofanya kila siku. Adhabu tu ya dhambi hii ni kifo (Warumi 6:23), si kifo cha kimwili tu bali kifo cha milele (Ufunuo 20: 11-15). Adhabu ya haki kwa dhambi ni Jahannamu ya milele
"Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu" (1 Timotheo 2: 5).
Huu utaratibu wa kutubu kwa binadamu wenzetu ni kinyume na maandiko ambayo yanasema binadamu wooote, wakiwemo watawa wa madaraja yote( maaskofu,mapadre na papa mwenyewe ni binadamu wa kawaida mbele ya Mungu)
Yesu anawakilisha wale ambao wamemtegemea Yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Anatupatanisha, kama vile wakili anayemtetea mteja wake, akimwambia hakimu, "Hakimu, mteja wangu hana hatia ya mashtaka yote dhidi yake." Hiyo ni kweli kwetu pia. Siku moja tutakuna na Mungu, lakini tutafanya hivyo tukiwa tumekwisha samehewa dhambi kabisa kwa sababu ya kifo cha Yesu kwa niaba yetu. "Mwanasheria mtetezi" alichukua adhabu kwa ajili yetu!
Wewe ni kasuku hujui maandiko matakatifu
 
Hakuna contraceptive ambayo ni 100% effective.
Kwanini tusitumie ambayo ni more effective than the other. Ni hesabu gani inatumika kutumia yenye 86% effectiveness kuliko yenye 99% effectiveness.
 
Hukumu ya kuvuliwa daraja la upadre kwa Karugendo haikunishangaza, alikuwa anaandika sana kupinga msimamo wa mwajiri wake kuhusu matumizi ya kondomu.

Naamini hakuonewa, nilimsoma na kusikia misimamo yake alipohojiwa na redio moja ya kimataifa.

Vv
 
Kwanini tusitumie ambayo ni more effective than the other. Ni hesabu gani inatumika kutumia yenye 86% effectiveness kuliko yenye 99% effectiveness.
Logically, kama zote hazipo 100% efficient then hakuna ambayo ni salama.
 
Nilichojifunza hapa ni kwamba, Askofu Niguwemizi roho yake inaendeshwa na shetani himself and yet anavaa joho la Uaskofu

Pia nimejifunza kwamba Kanisa Katoliki halimtumaini Mungu wa KWELI bali binadamu anayeitwa Papa.

Tatu nimegundua kwamba Kanisa Katoliki hujivika joho la demokrasia nchi mbalimbali wakati ndani ya Kanisa hilo hawaitambui demokrasia

Nne. Hawa watoto wa mapadri tunaoishi nao mitaani hatima yao ipoje kupitia misimamo ya kipagani ya Kanisa?
Huyo Askofu is an offspring of a devil. Ndio maana shetani mwenzake alimpa wakati mgumu.
 
Unamaanisha uongozi wa juu wa Kanisa Katoliki hupokea tu report na kunifanyia kazi bila verification yoyote!!?
Mkuu naona niliposema kwamba hao viongozi wa juu ndio wanaamua papa aone nini kwenye ripoti haukunielewa. Isitoshe the late alisema kwamba hakupewa chance rasmi ya kujitetea hivyo walikua huru ku-mould hizo ripoti watakavyo. Hata ungefanyika utafiti haohao viongozi ndio wanaoorganize hizo tafiti.


Kwa mujibu wa andiko, adultery ni moja kati ya makosa sita aliyoshitakiwa nayo. Ukiwa mtu uliyefuatilia hii case kwa ukaribu kama ulivyosema, je, makosa yote sita alisingiziwa?
Sijakataa kwamba the late alifanya makosa, pitia maandiko yangu khs hii issue utagundua hilo. Ninachosema ni unfair play ilochezwa na huo uvunjifu wa kanuni za kitubio.

Kutumia confession za Fr kwenye kesi na kuandika ile barua ya kuomba kufunga ndoa bila idhini yake wewe kwako unaona hio kitu iko fair?

Ndio maana nikasema RC kuna autocracy fln kwenye level ya majimbo ambayo inazaa double standards, hizi issue zinaanzia kwenye malezi humo seminarini ndg na kuu na watu wanakua nazo hadi ukubwani.
 
mfumo wa ajabu sana mtu kutubu kwa binadamu mwenzake
huu siyo mfumo wa kiKiristo ni wa kipagani
Mungu ana mgogoro na sisi kwa sababu ya dhambi. Dhambi inaelezewa katika Biblia kuwa uvunjaji wa sheria ya Mungu (1 Yohana 3: 4) na uasi dhidi ya Mungu (Kumbukumbu la Torati 9: 7; Yoshua 1:18). Mungu huchukia dhambi, na dhambi husimama kati yetu na Yeye. "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!" (Warumi 3:10). Wanadamu wote ni wenye dhambi kwa sababu ya dhambi tuliyorithi kutoka kwa Adamu, pamoja na dhambi tunayofanya kila siku. Adhabu tu ya dhambi hii ni kifo (Warumi 6:23), si kifo cha kimwili tu bali kifo cha milele (Ufunuo 20: 11-15). Adhabu ya haki kwa dhambi ni Jahannamu ya milele
"Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu" (1 Timotheo 2: 5).
Huu utaratibu wa kutubu kwa binadamu wenzetu ni kinyume na maandiko ambayo yanasema binadamu wooote, wakiwemo watawa wa madaraja yote( maaskofu,mapadre na papa mwenyewe ni binadamu wa kawaida mbele ya Mungu)
Yesu anawakilisha wale ambao wamemtegemea Yeye mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Anatupatanisha, kama vile wakili anayemtetea mteja wake, akimwambia hakimu, "Hakimu, mteja wangu hana hatia ya mashtaka yote dhidi yake." Hiyo ni kweli kwetu pia. Siku moja tutakuna na Mungu, lakini tutafanya hivyo tukiwa tumekwisha samehewa dhambi kabisa kwa sababu ya kifo cha Yesu kwa niaba yetu. "Mwanasheria mtetezi" alichukua adhabu kwa ajili yetu!
Bahati mbaya tunamsema mtu ambaye sasa hayupo,lakini kuna njia nyingi za kukata rufaa hadi kwa Baba mtakatifu kama umeonewa na Karugendo ni mtaalamusheria mbobezi.Nashangaa alivyonyamaza na kubaki akilalamika huko Magu.mtu akisha kufa na lake halipo kuendelea na mada hii ni kupoteza muda na tutakuwa hatumtendei haki marehemu.
 
Huyu askofu aliyemuondolea sakramenti ya upadrisho, angepigwa chini mara moja na mkuu wa Vatican.
 
Mkuu naona niliposema kwamba hao viongozi wa juu ndio wanaamua papa aone nini kwenye ripoti haukunielewa. Isitoshe the late alisema kwamba hakupewa chance rasmi ya kujitetea hivyo walikua huru ku-mould hizo ripoti watakavyo. Hata ungefanyika utafiti haohao viongozi ndio wanaoorganize hizo tafiti.



Sijakataa kwamba the late alifanya makosa, pitia maandiko yangu khs hii issue utagundua hilo. Ninachosema ni unfair play ilochezwa na huo uvunjifu wa kanuni za kitubio.

Kutumia confession za Fr kwenye kesi na kuandika ile barua ya kuomba kufunga ndoa bila idhini yake wewe kwako unaona hio kitu iko fair?

Ndio maana nikasema RC kuna autocracy fln kwenye level ya majimbo ambayo inazaa double standards, hizi issue zinaanzia kwenye malezi humo seminarini ndg na kuu na watu wanakua nazo hadi ukubwani.
Una uhakika gani kuwa alitumia maungamo kumhukumu. Huyo mwendazake alikuwa mjanja, alitafuta namna ya kumsulubu askofu wake (ili naye aingizwe hatiani). Waliopitisha hukumu walisikiliza pande zote ndio wakahukumu. Kosa lake kubwa ni kwenda kinyume na mafundisho ya kanisa, tena wazi wazi, redioni na magazetini. Ushahidi upo. Ungekuwa mfuatliaji wa mambo, ungekumbuka alipohojiwa na redio moja ya nje, na akajibu bila chenga. Akiwa arusha. Nadhani alikuwa anaganga njaa
 
Bahati mbaya tunamsema mtu ambaye sasa hayupo,lakini kuna njia nyingi za kukata rufaa hadi kwa Baba mtakatifu kama umeonewa na Karugendo ni mtaalamusheria mbobezi.Nashangaa alivyonyamaza na kubaki akilalamika huko Magu.mtu akisha kufa na lake halipo kuendelea na mada hii ni kupoteza muda na tutakuwa hatumtendei haki marehemu.
Uongo mwingi Sana wameweka hapa. Hizo mahakama wanazosema mbona zipo miaka nenda Rudi. Eti mahakama za kanda zilindwa kwa ajri ya Priva. Fanya utafiti kabla ya kusema. Watu wengine wana chuki zao binafsi
 
kwahiyo padri alitafuna mtu akaenda kutubu kwa baba askofu, baba askofu akaamua kumuangamiza kwa kitubio[emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom