Huyu Sallam kumbe ndio kila kitu kwa Diamond

m
mbona seven sio hata mdau mkubwa wa mziki tanzania
 
m

mbona seven sio hata mdau mkubwa wa mziki tanzania
Umeonae watu wanataka kubadilisha juu kwa juu! Seven si mdau mkubwa ,yupo wadau wanataka pindisha mambo! Mi nahisi ni mawinguni& associates
 
Umeonae watu wanataka kubadilisha juu kwa juu! Seven si mdau mkubwa ,yupo wadau wanataka pindisha mambo! Mi nahisi ni mawinguni& associates
kweli maana sallam anasema amekatisha ndoto za wasanii wengi na akimtaja hatutoamini
 
aliongea nae kila kitu kwa lugha gani?!
 
Nimemkubali muhojiwaji Na ninampenda Diamond sana. Nyimbo zake zimeniburudisha, nielimisha, niadibisha, n.k
"Kumbe mjinga ni mimi, ninayelea wenzangu wanachukua..."
"Nataka kesho twende tukamuone mama..."
 
Ruge si alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na uyu dada(7)??
 
Ni kweli huyu ni jembe..sio akina fella
Hivi huwezi kuisifia A bila kuiponda B? Napata shida na fikra kama hizi.

Btw niwaulize wadau kuhusu huyo jamaa aliyekuwa analeta figisu huko kwenye TV stations kubwa, nia yake ninini hasa je, Ni roho mbaya tu za kutaka kusababishiana umaskini. Au ni ile unambania mtu kwa kudhani bila wewe hawezi kufika popote na hata akijaribu atakurudia tu kudumb down hapo ndipo utamsaidia kwa masharti magumu. Nia ya kumbana kwenye music ni ipi? Bado sipati majibu.
 

Babu tale na felaa majingu na uswahili mwingi
 
Hapa jamaa ameniongezea kaelimu kidogo kwamba kuna baadhi vitu ni lazima ulazimishe.
Ina maana hajawahi kukutana na msemo maarufu.. '' If U don't ask U don't get it ''..
 
Kuna story nyingi Ni very interesting na Sallama hakugusia, labda vile hakuulizwa, na unaweza kuona jamaa alivyokua Professional manager, ilikua safari ya Marekani juzi Kati, Uwanja wa Ndege....Kanye west anakua interesting na raba ambayo Diamond kavaa, anamuomba Diamond aipige picha ile Raba yake, Sallama na Diamond na wengine wote walikua busy na Simu, so Diamond anampa go ahead Kanye ya kupiga picha, bila kumwangalia usoni, Kanye anapiga picha then, then anamshukuru Diamond Ia hamjui, then Diamond anajibu huku anamtizama Kanye usoni, anamtambua anakua kama kapagawa..... Ana shout kidogo "Ohhh! Kanye!" Diamond anasimama kupiga story na Kanye! Kina Sallama nao wanaachana na Simu zao na kusikiliza story, (point iko hapa).... Diamond anaonekana Ana papala, Sallama anamwambia Diamond.....Babu hapo Hamna kuomba Colabo (ndicho Diamond alitaka kufanya) Cha msingi omba contact basi! Nadhani alimwelekeza kwa kiswahili....... So Diamond anaomba Contact, anatambulisha crew yake, anaomba kupiga picha na Kanye, Wanaagana! Tusubiri kazi toka kwao, coz nimejifunza jamaa anajaribu kumfundisha Diamond majukumu yake kama msanii Ni yapi, then kama Manager Ni yapi, so nadhani Sallama yupo na maongezi na Management ya Kanye kwa sasa, wakifikia muafaka, wasanii watapewa taarifa! Like Oya!!! Jiandae mwanangu mwezi ujao Colabo na Kanye!!
 

Marekani alikuwa na Babu Tale sio Salaam..

Na Tale ndio aliongea na Kanye licha ya ubovu wa lugha unaosemwa na watu..
 
Kwakweli hata mimi. Baadae nilijikuta naishia na hitimisho kwa kuukubali ule msemo maalufu "kuzaliwa bongo form six".
Babu Tale na Fella? Haikuwahi kuniingia akilini kabisa!

Fella kaishi South Africa miaka mingi
halafu Fella ndo aliemwambia Diamond lazima Salaam awepo
so Fella bado muhimu ingawa hata mimi najiuliza maswali sipati majibu
 
Graduates wa huko SAUT na PR zao wanashindwa na jamaa kwenye maswala ya Events Management and Connections making kweli shule sio kila kitu..kama nimekwaza mtu halikua lengo langu
 
Huyu Jamaa hafanani na Watanzania japo ni Mtanzania. Yupo straight sana kwny majibu yake!
 
Sawa lakini Hao hawana ubavu wa kupasukua ukututa Mpaka wawekewe Ufa kwanza
Ndugu huwafahamu vizuri Fella na Tale... jamaa local music industry wanaijua sana tena sana... narudia tena sana! Hata huu urahisi wa Sallam kwa Mondi umetokana na kazi kubwa ambayo ilifanywa na hivi vichwa... don't underestimate these big boys!

Mafanikio makubwa ya Sallam yanatokana na collective force ya hawa jamaa bila kumsahau Diamond mwenyewe! Remember, kabla Sallam hajafanya kazi na Diamond alikuwa na Mr. Nice but very few people know about this! Hata hivyo, hawakufika popote kv hapakuwa na team aliyokutana nayo WCB!
 
m

mbona seven sio hata mdau mkubwa wa mziki tanzania
Mdau mkubwa sana tena sana labda umeanza kumfahamu miaka ya karibuni na kama ni tangu zamani basi hukuwa ukimfuatilia. Naweza kuthubutu ameaanza kitambo kuliko Fella ambae ni mkongwe....
 
daaaaahh pcha tafadhar kwa aliyenayo au utamburisho wake zaid, mana nnashauku naye sana.
Mtoto(co kwa umri) mmoja hivi, mkalii kwa vigezo vyangu! Kwanza muziki anaujua na anaujua toka kitambo... yaani c mtu ambae alikuja kui-feel muziki baada ya kuingia kwenye entertainment or media industry but since yuko young girl!

Alivyoanza kufanya kazi na Kiba niliamini angemfikisha mbali sana c tu kwa sababu muziki aliufahamu bali alikutana nae wakati keshaufanyia kazi muziki kwenye media mbali mbali ambazo ni infortainment media in Africa including Clouds na kuwa na connection nyingi sana pengine kuliko hata huyu Sallam by the time!

Kinyume chake ni kama ameshindwa kumfikisha Kiba pale nilipotarajia. Hata hivyo, ana tatizo moja ambalo nadhani linachangia! Labda aache cku hizi lakini zamani ilikuwa ni FULL uzungu... yaani Mchaga Mzungu! Huu muziki wetu ni wa mtaa... hauhitaji uzungu kupitiliza!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…