Huyu trafiki kumkaribia hivi Rais sio hatari?

Mkuu nimekumbuka baadhi ya trainings hizi ni halisi. Tunaweza kuwachukulia poa ila kumbe ni hatari. Pitia picha mojamoja hapa uone wanavyoivishwa




Hii sio muvi ni mafunzo halisi.
Cheki hapa wakila mazoezi ya pumzi
 
Sema bosi wake alimkata jicho la onyo baada ya saluti jicho lililokuwa linamwambia we mpumbavu uliamkia kilabuni nini?
 
Binafsi namuombea mama yetu maisha marefu,aishi miaka>100.
Kwani nadhani ana maadui wengi ndani ya chama chake, CCM.
HAKUNA ATAKAYEWEZA KUMDHURU RAIS WETU MPENDWA.


AMEN.
 
Sawa sawa Mkuu
 
Binafsi namuombea mama yetu maisha marefu,aishi miaka>100.
Kwani nadhani ana maadui wengi ndani ya chama chake, CCM.
HAKUNA ATAKAYEWEZA KUMDHURU RAIS WETU MPENDWA.


AMEN.
Yesu pamoja na kumtegemea mungu aliuwawa itakuwa uyo
 
Mpaka hii leo bado sijaona Kikosi Bora cha Ulinzi cha Rais kama cha Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kikifuatiwa na kilichokuwa cha Hayati Rais Mkapa na kilichokuwa kinajitahidi kwa Siku za karibuni ni cha Hayati Rais Dkt. Magufuli ila vilivyobakia vyote ( hasa hiki cha Rais Samia ) naona kima mapungufu mengi na hata huko nyuma nilishawahi kuja na 'thread' kama mbili hivi hapa hapa za Kulizungumzia kwa 'angles' tofauti. Hongereni nyote mlioona kuna tatizo mahala fulani kwani mpo sahihi tena 99.9%.

Na sasa ni Kazi ya Wahusika ( PSU ) Kuliangalia hili japo cha Kushukuru tu ni kwamba kwa Tanzania na Watanzania tulivyo Mheshimiwa Rais Samia hana sana Tishio na Maadui ni ngumu Kujipenyeza kwa Tanzania hasa kutokana na Uimara wa Idara ya TISS ambayo inafanya ( inatekeleza ) Majukumu yake vyema na Kiuweledi kabisa hasa Kiusalama ( Kiunjagu ) nchini.
 
BWANA asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure!

Haiti Jovenel Moise kala NJUGU.
 
Huku kusimama barabarani ni kiki za kishamba sana za mwendazake. Magari yanazuiwa kupita masaa mawili eti Rais anaongea na watu wake. Wakati huu wa covid delta hii mikusanyiko isitishwe
 
mimi napingana na wewe kamanda ivi askari aliyeingia chuo cha uaskari kweli afanye utopolwa kama ule...huku akiwa anajua ile principle ya 100/100/100.... izo 100 ni idara mbali mbali za ulinzi ikianza na msalaba mwekundu/uokoaji/polisi/kisha jeshi....
 
Kiongozi hata hiyo salute yenyewe umeiona inavyopigwa aisee, salute inapigwa huku mtu anatembea baada ya kubana matako arif.

Huyu mwamba ametisha aisee...!
hiyo saluti ya kubana matako ndio kwanza naisikia kwako...matako yanabanwaje ama ulikuwa unamaanisha kuibana mikono kiunoni...?
 
Kweli kuna yeyote duniani anaweza kumdhuru mama yetu? Kuna yeyote ana uthubutu wa kunyanyua mkono na kumdhuru mama? Hamna kabisa
Wako wengi tuu humu humo ndani.Sababu wanailalamikia katiba,iliyoru&su tuu mtu kuchukua nchi kirahisi
 
ata mimi nilikuwa nina swali kama lako...kwa nilivyo muona cheo chake hakupaswa kabisa kumfuata bwana mkubwa pale...eti amsalute...ili hiyo salute imsaidie nini..sasa
 
Huyu askari kweli? Kweli kweli askari huyu?? Mbona nidhamu sifuri? Hata kiongozi wake kamshangaa saluti yenyewe ya kilevi tu
 
Unaonaje ukamjaribu yule mlinzi aliyevaa high heels then uje utusimulie kitakachokupata km yupo fit na high heels au kavaa za mtoko
 
Acha petty issues kashughulike na sheria mahakamani. Nenda jukawaa la Sheria , toà elimu huko. Acha viti vidogo kama hivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…