I want to die a judge

Kwa shilingi 3000 tu unaipata hadithi hii mpaka mwisho kabisa sehemu ya 100

Lipia kupitia namba
0621567672
0745982347

Jina FEBIANI BABUYA

Lakini kwa wale ambao wanahitaji kujiunga na group langu la WhatsApp ni shilingi 3000 tu kwa mwezi, namba za malipo ni hizo hizo[emoji2768].

Muda ni wako sasa

Wasalaam

Bux the story teller
 
Habari, ni matumaini yangu mpo wazima wa afya kabisa.

Leo ni siku nyingine njooni msome hadithi huku mkiburudika na ofa ambazo hazielezeki kirahisi.

1. ULIMWENGU WA WATU WABAYA kipande kimoja ni shilingi mia tu za kitanzania (100).

2. I WANT TO DIE JUDGE...kipande kimoja shilingi mia tu za kitanzania, lakini pia leo GEREZA LA HAZWA Leo natoa ofa ya Pekee.

3. GEREZA LA HAZWA.....Leo kipande kimoja kinauzwa 100 badala ya 150 hii ni kwa leo tu, ipo mpaka 82 kwa sasa.

Namba za malipo ni zile zile
0621567672
0745982347

Zote jina ni FEBIANI BABUYA, natuma Kote WhatsApp na kwa wale wa simu ndogo natuma messenger Facebook.

Njoo uburudike na kalamu yangu.
 
No hiyo mwisho ni 100 sema niliona kama watu hawaitaki hivi nikaibwaga
Siyo watu hawaitaki tatizo unaiweka mara moja kwa mwezi hata mzuka unapotea ww kama mwandishi unaechepukia inatakiwa uweke mara kwa mara maliza hata riwaya moja humu ikutambulishe usiweke mbele pesa wakati bado hujatambulika vizur ukiisha tambulika utakuwa unaweka kidogo kidogo kama hivo
Ni ushauri tu
 
Hakika. Kuomba muendelezo kila mara Wakati kaileta mwenyewe inachosha.
 
Hakika. Kuomba muendelezo kila mara Wakati kaileta mwenyewe inachosha.
Sana unajua laiti angekuwa mwandishi mkubwa wala hata isingekuwa shida mm binafsi nanunua sana riwaya za wandishi wengi humu akiwemo singanojr sababu tayar wameshajijengea jina ila kwa yeye ambae bado inatakiwa ajenge jina kwanza
 

Hii sio hadithi ya kwanza kuileta humu, kuna hadithi ilisha isha kabisa kurasa zote 76 mpaka final humu humu, unfortunately kuna changamoto ambazo ni ngumu kwa wewe kuziona kupitia hichi nacho kifanya nazo kutana nazo. Shukrani kwa ushauri pia
 
Hii sio hadithi ya kwanza kuileta humu, kuna hadithi ilisha isha kabisa kurasa zote 76 mpaka final humu humu, unfortunately kuna changamoto ambazo ni ngumu kwa wewe kuziona kupitia hichi nacho kifanya nazo kutana nazo. Shukrani kwa ushauri pia
Inaitwaje?
 
Mkuu FEBIANI BABUYA ni kigezo gani unakitumia kujua kwamba watu wahaitaki hii riwaya?

Mkuu FEBIANI BABUYA ni kigezo gani unakitumia kujua kwamba watu wahaitaki hii riwaya?[emoji28]
Kaka sidhani kama ni salama sana kuweka kila kitu public, waandishi wadogo kuna changamoto nyingi sana tunakumbana nazo huku chini unfortunately msomaji yeye anajali kusoma na kusema tu waandishi wadogo wana tamaa ya pesa, nikiona mtu anaongea hivi huwa nasikitika sana na kuwasikitikia mno wale ambao nao wananitafuta na kuniomba ushauri kuhusu kuandika. Anyway inaendelea kuanzia leo
 
STORY: I WANT TO DIE JUDGE (NATAKA KUFA HAKIMU)
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
SEHEMU YA HAMSINI NA TATU

TULIPO ISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI.......

“Ni swali gumu sana kwa sababu watu hao wakinihitaji huwa wananifuata mwenyewe na hajawahi kuja mtu mmoja mara mbili kila anavyokuja mtu huwa anakuwa ni mwingine kwahiyo sijawahi kumkariri kwani wanabadilika sana hawamtumii mtu mmoja”

“Sasa wewe hizo taarifa huwa unazirudishaje kwa hao watu wanao kuagiza?”

ENDELEA...............................

“Kukiwa na taarifa za mhimu huwa wanakuja wao wenyewe kuzichukua na wanaondoka kwa sasa sijawahi kufanya nao mawasiliano ya simu kabisa”

“Kwahiyo nikihitaji kukutana nao inabidi niende moja kwa moja kwenye kampuni yao?”

“Pale uwe makini sana kama utaenda kwa sababu ile ni kampuni kama kampuni zingine na shughuli zinazo fanyika pale ni za halali hivyo kama ukienda kichwa kichwa utafunguliwa mashtaka serikalini kwa sababu wanapewa kipaumbele sana na serikali kwani ni watu wanao jitoa sana kwenye jamii huwezi ukajua chochote kinacho endelea hapo hata kama ukifanya kazi miaka kumi ndio maana mimi mwenyewe mpaka leo huwa sijui kampuni ndani yake kuna nini mpaka tunalipwa pesa nyingi sana namna hii kazi yangu napewa taarifa kuzituma na kurudisha majibu basi kwa mwezi naingiziwa milioni hamsini” maelezo yake the spy yalikuwa kama masiara sana ili huo ndio uliokuwa uhalisia watu wanafanya kazi kwa weledi sana siku hizi hauwezi kupewa kila kitu cha mhimu kinacho endelea ndani ya kampuni ni watu wachache sana wanaweza kuzipata taarifa nyeti za kampuni husika. Catherine aligundua kijana huyo hakuwa anahusika moja kwa moja kwenye hayo matukio ni njaa tu ndiyo ilikuwa inamsumbua japo alishangaa sana kazi nyepesi kama hiyo mtu analipwa milioni hamsini za kitanzania na namna jinsi makampuni yanavyolipa pesa ndogo alijawa na hamu ya kuwajua sana hao watu.

“Pole sana kwa nilicho kifanya kwa marafiki zako”

“Mambo ya kawaida tu hayo”

“Kwanini unajiita the spy?”

“Kwa sababu kazi yangu haina utofauti sana na wapelelezi unajua mtu mwenye taarifa za mhimu ndiye huwa ana maana kubwa kuliko hata watu wanaozitaka taarifa hizo ina maana yeye akiamua kuzivujisha au kupotea nazo inakuwa ni hatari sana”

“Vipi hauna familia labda huko kwenu”

“Familia ipo tena kubwa tu”

“Kwanini usiache hizi kazi ukaishi na familia?”

“Wanajua kila kitu kwenye maisha yangu na hicho ndicho kitu ambacho huwa wanawashinda watu wengi sana wanautumia udhaifu wako kwa ajili ya kukufanya uzifanye kazi zao kwa usahihi ukienda nao kinyume tu familia yako yote hakuna mtu wanamuacha wanaweza wakamuua kila mtu. Hivyo nikisema niache kazi kwa hawa watu lazima nitajiingiza kwenye hatari kubwa sana, huwa nawatumia familia yangu pesa nyingi sana ambazo kiufupi zimebadilisha sana maisha ya nyumbani saivi baba na mama yangu wanaishi kwenye nyumba nzuri, kaka zangu wote na dada zangu nimewafungulia biashara, wadogo zangu wote wanasoma shule za gharama kwa pesa ninazo zipata na wana furaha kubwa sana sasa angalia mwenyewe nikiacha kazi maana yake ile furaha yote ya familia inaenda kutoweka nitaonekana mwanadamu wa hovyo sana hata mbele za mwenyezi MUNGU kwa kuiua familia yangu kwa mikono yangu mimi mwenyewe.” Catherine alishusha machozi kwa kumuonea huruma kijana huyu, “siku zote maisha yanakupa somo la kuto mchukulia mtu poa kwa sababu ya mwonekano wake au kwa sababu ya udhaifu wake fulani mdogo ambao huenda wewe unauona machoni pake ila maisha yana mafunzo mengi sana mwanangu jitahidi sana kuwa mtu wa watu, pesa ziko kwa watu, maisha wanayaishi watu, dunia ni watu, amani ni watu kuna kufa na kutoweka duniani fanya mambo makubwa ya kuinufaisha jamii ili uje ukumbukwe na watu” ni jioni moja anakumbuka maneno hayo alikuwa anaambiwa na baba yake baada ya kutoka kuapishwa kuwa komando wa nchi ya Cuba baba yake alimuasa sana asiweze kutumia nguvu yake vibaya kwa sababu ya kuwatesa watu, nguvu yake itumike kwenye kuwalinda watu, aitumie kwenye kutetea amani ya watu, ilete furaha kwa watu na hayo ndiyo maisha ambayo anapaswa kuyaishi mwanadamu yeyote yule sehemu yoyote anayokuwepo.

Kijana Ismail waweza kumuita the spy alikuwa ni mfano wa kuigwa kwa vijana wote wengi wa rika lake, mjini alikuwa akiishi maisha ya kawaida sana wengi wakimjua kama dereva bajaji na mzee wa mishe mishe mjini ambapo aliwaunganisha wenzake wengi sana kuweza kuwapatia mishe za kuingizia chochote kilichofanya mikono yao kwenda kinywani kila siku na walimshukuru sana kwa hilo, hakuja mjini kuishi maisha ya starehe ambayo vijana wengi wakipata pesa kidogo tu wanaenda kuzitupa huko, alikuwa halali usiku kucha lakini familia yake nzima ilikuwa inaishi maisha mazuri sana huku usiku aking’atwa na mbu kila siku na hivi ndivyo mwanaume anavyo takiwa kuwa, Ismail alikuwa na kila sifa ya kuwa baba bora wa familia Catherine alijikuta akimsikitia sana kijana huyo alikuwa akistahili kuishi maisha bora sana lakini kuna neno linaitwa dunia ambalo ndani yake kuna wanadamu hawa ndio viumbe ambao wamnafanya wenzao kupitia kwenye mazingira magumu sana kama haya. Hakuwa na haja ya kuendelea kumtesa tena alimfungulia kamba alizo mfunga kisha alifungua koti lake na kutoa dawa fulani ya unga unga alimwagia eneo ambalo alikuwa ameizamisha nondo kikatili sana, Ismail aliyafumba macho yake yakitoka machozi kwa maumivu makali sana ya dawa hiyo ambayo alikuwa amewekewa, alishangaa kidonda kinaanza kukauka.

“Hiyo dawa utaitumia mara tatu kuweka hapo baada ya wiki moja mguu wako utakuwa umepona kabisa na hiyo alama itakuwa imetoka hapo, kumbuka tu kuwa mtu mwema siku zote siku moja nitarudi na kukutafuta nikiwa na mwanaume wa ndoto zangu goodbye the spy” dunia ilimjaza ujinga ila leo watu ambao wapo duniani walikuwa wanampa somo la maisha, licha ya kufunguliwa pale the spy alibaki amekaa kwa muda mrefu sana akiwaza na kuwazua namna mwanamke huyo alivyokuwa mrembo lakini alikuwa anatisha sana kukutana naye, alikuwa anapigania penzi lake la dhati na kijana huyo aliahidi atamuombea afanikishe hiyo safari yake salama japo alijua wazi safari hiyo lazima ingekuwa ngumu sana kwa upande wake, mpaka kunakucha asubuhi na mapema ndio muda ambao alitoka humo ndani.






DERISHRAWAR PRISON
Mponda street Vingunguti

“Mitaa maarufu sana ndani ya jiji la Dar es salaam ambayo inasifika sana kwa uchinjaji wa nyama hususani nyama ya Ng’ombe, kuna mhindi mmoja alikuwa akigeuza macho yake huku na huku kuona kama kuna mtu yeyote alikuwa anamfuatilia alivyo jiridhisha hakukuwa na mtu yeyote yule nyuma yake alikatiza kwenye maeneo ya machinjioni hayo alipanda ukuta akatokezea upande wa pili akawa anashuka njia moja ambayo ilikuwa imekunja kwenye kichochoro kimoja ambacho kilikuwa kimekomea sehemu na mbele yake kulikuwa na nyumba nzuri ya kawaida kwa mtu mwenye maisha yake ambayo sio ya wasiwasi sana. Aliruka kwenye fensi ya hiyo nyumba akafika mlangoni na kutoa funguo yake kwenye mfuko akafungua na kuufunga mlango huo ndani, sebule haikuwa na kitu chochote kile hata kimoja lilikuwa ni jambo la kushangaza sana kwa sababu nyumba kama hiyo ilitarajiwa kuwa na samani za kutosha ndani yake. Alipitiliza moja kwa moja chumbani ambako nako kulikuwa na kitanda kimoja tu,godoro na komputa ndogo ya mkononi kuna pafyumu aliitoa kwenye begi lake akaipulizia kwenye kila eneo ambalo alikuwa amewahi kushika akiwa ndani ya nyumba hiyo ambayo ilikuwa ni ya kwake mwenyewe lakini alikuwa akiingia kwa machale sana na alionekana hiyo sehemu huwa anafika mara chache sana mhindi huyu ambaye hakujulikana kipi kilikuwa kimemsibu mpaka awe na wasiwasi sana namna hiyo.

Baada ya kumaliza hakufunga sehemu yoyote zaidi ya kuweka laptop yake kwenye begi kisha kitandani akamwagia tindikali, lilikuwa ni suala la sekunde tu kitanda na godoro vyote vilimomonyoka, akavaa kofia yake kichwani ambayo ilimsaidia kuuficha uso wake kwa kiasi fulani kisha akatoka humo ndani alionekana kuwa na haraka kupita kiasi, wakati anatembea kuelekea sehemu ambayo alipita mara ya kwanza kuingia humo ndani mbele yake aliona kuna mtu amekaa ile sehemu akiwa anaizungusha bastola kwenye mkono wake.

“Mbona mapema namna hiyo ndugu yangu unahitaji kuikimbia mpaka nyumba yako wakati unajua kabisa kuna wageni wanakuja, haya nipe sababu inayokufanya nyumba yako mwenyewe unaingia kwa machale sana namna hii haufungui hata mlango” sauti ambayo ilionekana wazi haikuwahi kuwa ya mapenzi ilimtoka mwanaume ambaye alikuwa amekaa hapo chini akiwa anaizungusha bastola yake.

“Hapa ni kwangu sasa wewe inakuhusu nini hata nisipo pitia mlangoni?” aliongea kwa ujasiri mhindi huyu na kiswahili chake kilicho pinda pinda kiasi.

“Hujanijibu swali unaniuliza swali naomba begi lako hilo kisha uende na usije ukarudi tena kwenye ardhi ya nchi hii” mwanaume huyo aliongeza tena akiwa ameangalia chini bastola yake bado ilikuwa ipo kwenye mikono yake.

“Sio kirahisi hivyo ndugu yangu”

“Kwa sababu unajua ulicho kifanya sio, sasa utaileta kwa lazima” Mwanaume huyo alinyanyuka na kuanza kumsogelea huyo mhindi ambaye taratibu alianza kurudi nyuma hatua zake zilikoma ghafla baada ya kugundua nyuma kulikuwa na watu ni kweli walikuwa wapo wanaume wawili ambao walikuwa wakipokezana sigara nao muda huo walisimama mmoja wao akaizima sigara hiyo. Kilichokuwa kimebakia kwenye mkono wake ilikuwa ni kujitetea tu basi vinginevyo asingeweza kutoka kwenye hilo eneo akiwa bado ni mzima wa afya, aliihesabu miguu yake kwa makadirio ya kuwafikia watu waliokuwa nyuma yake, hesabu zake zilienda sawa na alidhihirisha kweli hesabu duniani chimbuko lake ni kwenye bara la Asia kwenye nchi hiyo inayosifika sana kwenye mapenzi duniani naizungumzia India hapa sio China. Aliwafikia watu wale baada ya kujigeuza na kuwapatia maumivu ya vifua kisha kuna sindano ndogo aliwachoma wakiwa wananyanyuka hawakuendelea tena kusimama walilala chini kwa usingizi mzito, mwanaume aliyekuwa na bastola mbele yake alikuwa amesimama tu anamuangalia anacho kifanya bastola yake ikiwa mkononi, mhindi huyu aliogopa sana kwani kama angefanya hata kosa la sekunde tu risasi hizo zilikuwa tayari ni sehemu ya maisha yake kuwa mafupi hakuna namna angeweza kuzikwepa.

“Nakupatia nafasi ya mwisho ya kuishi nairusha hii bastola hewani ambapo itaenda umbali wa mita hamsini kupanda juu ni nzito sana hii bastola ni tofauti na za kawaida kama ikirudi chini hapa ukiwa bado haujadondoka chini basi mimi mwenyewe nakupa ruhusa ya kwenda nchini kwenu India na hilo begi japo lina kitu cha hatari sana ila nakupa hiyo nafasi itumie vizuri” mwanaume huyo maelezo yake yaliendana na vitendo vya moja moja mkono wake ulikunjwa misuli iliyoshiba sana ilituna kwenye mikono hiyo akiwa ameishikilia bastola nzito mno ambazo huwa ni adimu sana kuzipata duniani na huwa zinatengenezwa maalumu kwa ajili ya watu maalumu pia ilirushwa hewani ikawa inapandisha juu haikuonekana tena mhindi alikuwa anatapika damu chini ujio wa mtu huyo hata hakuuona amekuja sangapi alishangaa tu begi lake lipo pembeni nayeye yupo chini anavuja damu alijinyanyua kwa sarakasi nzuri bahati mbaya sana kwake alikutanishwa na goti la kiuno hakuwa na uhakika kama atakuwa na uwezo wa kusimama tena, mguu mpana na mnene uliokuwa umejaa kwenye buti moja ambalo lilikuwa limesafishwa sana ulijaa usoni kwake alianza kuona kama kuna nyota zinapita hewani hakuelewa nini kinacho endelea alikuja kushituka risasi zinazama kwenye mwili wake mifupa ya kwenye miguu ilikuwa imevunjwa kwa risasi hizo nzito pamoja na mikononi, kiunoni alipigwa risasi moja.

DERISHRAWAR PRISON ni gereza la namna gani, linamhusu nani, huyu Mhindi ni nani, kwanini aishi kwa machale kwenye nyumba yake mwenyewe hili begi ambalo linamhatarishia maisha yake Lina nini hasa ndani yake kikubwa cha namna hii????......53 inafika mwisho usikose mwendelezo bado hujaijua michezo ya akili✍️

Bux the story teller
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…