Asante mkuuujumbe mzito, wauawaji hawawezi kujichunguza. ukiuwa mmoja wetu ni kama umetuwa wote. siasa sio uadui
Yaani sana hawajemtendea haki marehemu leo hii ni kama wao ndugu wamempiga risasi nyingine kumaliza kabisa. shame kwa wote waliohusika katika hili. na siongelei serikali tu hata vyama sio sehemu yao.Hapo wa kulaumiwa ni wazazi na Ndugu wa Marehemu kwa kukubali kuingia kwenye huu mtego wa Serikali kujiingiza kwenye Mazishi ya huyu Binti. ili kujijengea Heshima na kuonyesha hisia zao kwa hiki kitendo cha binti yao kuuawa kwa makusudi na hawa polisi wangekataa Jambo hili na wao kumzika huyu Binti kwa gharama zao wenyewe. kwa hiki kinachotokea wamejidhalilisha aisee.
maandamano yapo kwenye katiba muulize huyu muuwaji wenu aliyetoa ruhusa ya kuuwawa watanzania kuchinjwa nk nk nkLeo hii kuna matukio makubwa mawili yanafanyika ambayo yametokana na athari za maandamano yaliyofanyika siku ya Ijumaa Februari 16, 2018.
Tukio la kwanza ni la kuagwa kwa mwili wa Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilin linalofanyika chuoni hapo; Tukio la Pili ni la Wafuasi wa Chadema waliokamatwa siku ya maandamano wakipandishwa Mahakamani.
Katika matukio yote mawili hatukumuona Mwenyekiti Mbowe aliyekuwa akiongoza maandamano haramu yasiyo na kibali ambayo yalisababisha madhara yote haya. Hajui pasipo kuitisha maandamano yasiyo na kibali pasingetokea madhara tunayoyaona leo?
Bado najiuliza, Mwenyekiti hajahudhulia msiba wa Akwilina kwa sababu hajaguswa nao? Ama sio wa muhimu kwake? Ama shida zetu sio zake? Inauma sana!
Kama haitoshi wale Wafuasi waliokamatwa wamekwenda Mahabusu kwa kukosa dhamana ya Tsh. Milioni 1.5 tu. Kweli wanakwenda Mahabusu kwa sababu wamekosa dhamana ya Tsh. Milioni 1.5?
Jambo la kushangaza, hakukuwepo hata kiongozi mmoja toka Chadema ambaye alikwenda Mahakamani kuwa nao bega kwa bega. Wanakwenda mahabusu kizembe kwa kuwasikiliza Wanasiasa ambao leo hii wamewatelekeza!!
Wamejikuta kwenye matatizo lakini wale waliosababisha wao wapate matatizo hawapo nao pamoja. Inauma sana!
Ninapofikia hapa nakumbuka ule msemo wa Rais Mstaafu Mzee Kikwete aliosema "Akili za kuambiwa, changanya na za kwako".
Hili ni funzo kwetu sote, tunapoambiwa na Wanasiasa tukafanye jambo ambalo tunajua tutakuwa matatani kisheria tuwe makini kuchanganya na akili zetu maana shida zitakazotupata zitakuwa ni zetu na si zao, mateso yatakuwa kwetu na si kwao.
Narudia tena kuwasihi, akili za kuambiwa changanya na za kwako.
*Na Thadei, Mwanaharakati Mpambanaji*
R.I.P"Mimi ninasafiri (alikuwa akienda Bagamoyo), lakini sijajua nitarudi lini. Unajua ninapambana na maisha, nataka nitoke, lakini pia nataka niwasaidie wazazi wangu (wazazi wake ni wakulima na wafugaji), kwa hiyo niombee tu kwani na wewe pia utanufaika na mafanikio yangu.”
Maneno yake ya mwisho kwa ndugu yake na dada yake.
Painful. So much painful.
Wameenda mahabusu kwa muda gani mkuu!? Dah! Inasikitisha sana, haswa kama wana familia zinazowategemea maishani.Leo hii kuna matukio makubwa mawili yanafanyika ambayo yametokana na athari za maandamano yaliyofanyika siku ya Ijumaa Februari 16, 2018.
Tukio la kwanza ni la kuagwa kwa mwili wa Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilin linalofanyika chuoni hapo; Tukio la Pili ni la Wafuasi wa Chadema waliokamatwa siku ya maandamano wakipandishwa Mahakamani.
Katika matukio yote mawili hatukumuona Mwenyekiti Mbowe aliyekuwa akiongoza maandamano haramu yasiyo na kibali ambayo yalisababisha madhara yote haya. Hajui pasipo kuitisha maandamano yasiyo na kibali pasingetokea madhara tunayoyaona leo?
Bado najiuliza, Mwenyekiti hajahudhulia msiba wa Akwilina kwa sababu hajaguswa nao? Ama sio wa muhimu kwake? Ama shida zetu sio zake? Inauma sana!
Kama haitoshi wale Wafuasi waliokamatwa wamekwenda Mahabusu kwa kukosa dhamana ya Tsh. Milioni 1.5 tu. Kweli wanakwenda Mahabusu kwa sababu wamekosa dhamana ya Tsh. Milioni 1.5?
Jambo la kushangaza, hakukuwepo hata kiongozi mmoja toka Chadema ambaye alikwenda Mahakamani kuwa nao bega kwa bega. Wanakwenda mahabusu kizembe kwa kuwasikiliza Wanasiasa ambao leo hii wamewatelekeza!!
Wamejikuta kwenye matatizo lakini wale waliosababisha wao wapate matatizo hawapo nao pamoja. Inauma sana!
Ninapofikia hapa nakumbuka ule msemo wa Rais Mstaafu Mzee Kikwete aliosema "Akili za kuambiwa, changanya na za kwako".
Hili ni funzo kwetu sote, tunapoambiwa na Wanasiasa tukafanye jambo ambalo tunajua tutakuwa matatani kisheria tuwe makini kuchanganya na akili zetu maana shida zitakazotupata zitakuwa ni zetu na si zao, mateso yatakuwa kwetu na si kwao.
Narudia tena kuwasihi, akili za kuambiwa changanya na za kwako.
*Na Thadei, Mwanaharakati Mpambanaji*