Poise
JF-Expert Member
- May 31, 2016
- 7,633
- 7,912
Anayedhani yuko salama asikilize vizuri clip ya mama Aquilina akimwambia prof Ndalichako kwamba alikuwa akisikia kwenye vyombo vya habari watu wanauawa na polisi lakini hakutegemea hata siku moja kwamba hilo litatokea kwa mmoja Wa wanafamilia wake. AJIDHANIAYE AMESIMAMA AANGALIE ASIANGUKE.
Leo hii kuna matukio makubwa mawili yanafanyika ambayo yametokana na athari za maandamano yaliyofanyika siku ya Ijumaa Februari 16, 2018.
Tukio la kwanza ni la kuagwa kwa mwili wa Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilin linalofanyika chuoni hapo; Tukio la Pili ni la Wafuasi wa Chadema waliokamatwa siku ya maandamano wakipandishwa Mahakamani.
Katika matukio yote mawili hatukumuona Mwenyekiti Mbowe aliyekuwa akiongoza maandamano haramu yasiyo na kibali ambayo yalisababisha madhara yote haya. Hajui pasipo kuitisha maandamano yasiyo na kibali pasingetokea madhara tunayoyaona leo?
Bado najiuliza, Mwenyekiti hajahudhulia msiba wa Akwilina kwa sababu hajaguswa nao? Ama sio wa muhimu kwake? Ama shida zetu sio zake? Inauma sana!
Kama haitoshi wale Wafuasi waliokamatwa wamekwenda Mahabusu kwa kukosa dhamana ya Tsh. Milioni 1.5 tu. Kweli wanakwenda Mahabusu kwa sababu wamekosa dhamana ya Tsh. Milioni 1.5?
Jambo la kushangaza, hakukuwepo hata kiongozi mmoja toka Chadema ambaye alikwenda Mahakamani kuwa nao bega kwa bega. Wanakwenda mahabusu kizembe kwa kuwasikiliza Wanasiasa ambao leo hii wamewatelekeza!!
Wamejikuta kwenye matatizo lakini wale waliosababisha wao wapate matatizo hawapo nao pamoja. Inauma sana!
Ninapofikia hapa nakumbuka ule msemo wa Rais Mstaafu Mzee Kikwete aliosema "Akili za kuambiwa, changanya na za kwako".
Hili ni funzo kwetu sote, tunapoambiwa na Wanasiasa tukafanye jambo ambalo tunajua tutakuwa matatani kisheria tuwe makini kuchanganya na akili zetu maana shida zitakazotupata zitakuwa ni zetu na si zao, mateso yatakuwa kwetu na si kwao.
Narudia tena kuwasihi, akili za kuambiwa changanya na za kwako.
*Na Thadei, Mwanaharakati Mpambanaji*
Bila bila
Mkuu,
Poise, huwa sishabikii vyama.vya siasa.
Jiulize, NEC na DED wa Kinondoni umewaona kwenye msiba wakisindikiza Akwilina!?
Au umewaona katika mahakama ya kisutu wakisomewa mashitaka ya kuwa chanzo kikuu cha kifo cha Akwilina B!?
Acha kufanya propaganda za kiuchwara mbuzi kwenye mambo yasiyohitaji siasa.
Tanzania, tatizo lake ni
CCM. CCM must go...
Kagame. Kagame must be stopped visiting Tanzania.
(Maana, amefanywa kuwa waziri na mshauri wa serikali ya ccm ndiyo matokeo yake hayo)
Management ya NEC na DED wa Kinondoni watumbuliwe wafungwe. Ndiyo wauaji polisi ilikuwa ni chaneli tu ya kuua ila.NEC, DED na CCM ndiyo wauaji.
Mwisho,
We need an immediate justice for our daughter Akwilina B.
R.I.P Binti, Akwilina A. B.
Ndoto zako zote zimezimwa ghafula kama vile mshumaa uzimwavyo.
Daima tutakukumbuka Binti, Kristo Yesu akuangazie mwangaza wake wa milele. Amina.