Ibara ya 37(1) ya katiba ya JMT ipo wazi kabisa rais halazimiki kufuata ushauri wa mtu yoyote. Rais Samia hakupaswa kulalamika yeye kutosikilizwa . Ni

Umemaliza. Sitii neno zaidi.
 
Kwani Mama kwa sasa anaongozwa na katiba ipi, ya kwake binafsi au katiba aliyoikuta?

Na kama anaongozwa na katiba aliyoikuta ina maana basi haifai na ni swala lake sasa kuanzisha mchakato tupate nyingine ya kueleweka.

Hata hivyo ushauri sio lazima ufuatwe, ni either uupokee or uachane nao.
Ushauri ni kama vile vinashabihiana na ombi, linaweza kukubaliwa au kukataliwa na hakuna mtu atakukazia shingo.

Mama aache mambo ya kulalamika, kama mapungufu yapo achukue hatua, JPM amekwisha lala, hana nafasi ya kujitetea.
 
Kweli kabisa.
 
Sasa hata kama katiba inasema hakuna ulazima wa rais kusikiliza ushauri wa mtu,wewe kama mtu mwenye akili timamu,unaona hilo jambo ni zuri?
Na inapaswa kuwa hivo! Ata ww huwezi kuchukua ushauri wa kila mtu! Ndo maana umepewa utashi mwisho wa siku utasikiliza na utaamulia kama ushauri uliopewa unafaa au haufai!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo maneno yasiwepo kwenye katiba mpya
 
Mbona yeye na madelu hawajasikiliza malalamiko ya wananchi kuhusu kuwabambika tozo na utitiri wa kodi (double na triple taxation) ambayo ni kinyume cha sheria.......apige kimya tu asijifanye malaika kuna mauozo mengi tu wameshayafanya, wasijifiche kwenye kichaka cha marehemu......​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…