ICC yakiri kupokea rasmi malalamiko kutoka Tanzania juu ya ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi uliopita

Uchaguzi wa Kenya na machafuko yale ya wazi wazi akina Ruto na Kenyata kesi ikaota mbawa, ifikie mda viongozi wa chama wawe responsible na mambo wanayo yafanya, kiufupi upinzani bara ulijifia 2015.
 
Ndiyo mkuu, ulidhani dunia nzima ikianza asubuhi basi kote ni asubuhi?

Kwingine mchana kwingine usiku.
Nilikuwa sijui mkuu. Kwani huko kwenu sasa ni saa ngapi? Hapa ni saa nne asubuhi!
 
Dua la kuku halimpati mwewe.
 
Wengi mnapiga kelele kujitutumua kwenye hii issue lakini nawaona mnahangaika tu.
 
ICC hawapokei na kushighulikia barua za individuals

Zitto kaandika peke yake akiwa kajifungia ndani na Maria Sarungi naye kajiandikia peke yake !!!
Sheria ipi inayosema hivyo? tuwekee hapa tuione. Usiwadanganye wajinga wenzio, kama wangekuwa hawapokei, wasingekiri wameshapokea.

Mimi ninafahamu wanapokea malalamiko ya individuals, tena mwenyewe unaweza kuandika malalamiko yako, au ukipenda unaweza kuwakilishwa na mwanasheria.
 
Ukiangalia hili suala kwa mtazamo wa kitanzania utaona serikali ipo matatani lakini ukiangalia kwa mtazamo wa kidunia Tanzania haipo hata top 10 kwenyenchi zinazovunja haki za binadamu. Hii kesi itakuwa upuuzi mtupu. Tanzania inahitaji chama mbadala chenye watu wenye akili za kutaka na kupenda maendeleo na siyo utoto.
 
Huna ujualo, wacha kupiga porojo hapa, weka sheria tuisome.
 
Mkuu tupe kidogo insight ya hii Rome Statute. Ni makosa gani au ya aina gani ICC wanashughulika nayo. Itasaidia sana kufunga huu mjadala
 
Watu wanaangalia ushahidi uliowasilishwa mezani unaowatia hatiani, hii hoja yako ya "kidunia" ni ya hovyo kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…