ID ya Kidukulilo nimeiacha baada ya Kuibuka Matapeli huko Mitandaoni. Natumia Bill Lugano (Billionaire Lugano)

ID ya Kidukulilo nimeiacha baada ya Kuibuka Matapeli huko Mitandaoni. Natumia Bill Lugano (Billionaire Lugano)

Anachonifurahishaga huyu mtu,akishaandika post take hana muda wa kujibizana na mtu.
Huwa anasoma comments huku akiwa anapulizwa na kiyoyozi hapo Hyatt regency [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nmekuwa nikipokea Malalamiko sana kutoka kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki wakisema kuna watu wamekuwa wakiomba Funds kwa ajili ya Taasisi zao kwa kutumia jina langu la Kiduku Lilo.

Kwanza watu wangu walikuwa wanashangaa kuwa nini kimetokea mpaka naomba nichangiwe Usd 50,000 eti za kusaidia watu wenye uelewa hafifu na wenye mtindio wa kiuchumi. Maskini.

Jamaa zangu wengi na mashirika wamekuwa wakituma hizo pesa bila kuuliza. Lakini kuna jamaa yangu alinipigia simu leo akiwa Norway na kuuliza vipi hali yako kiuchumi mpaka unafikia kuomba utumiwe USD 25,000 Umekumbwa na nini? Ndo nikaona isiwe Shida. Kwa sasa Ntatambulika kama Bill Lugano. Hapo nimetumia jina moja la kibantu ambalo nilipewa kama kutunza asili ya Ubantu.

Huwa nawaambia mzazi wangu mmoja ana asili ya Tanzania. Mwingine ni Foreigner. So hapo walinipa majina moja la kizungu la Bill na lingine la Kibantu Lugano.

Karibuni sana wadau. Nipo hapa Hyatt Hotel napunga upepo tu weekend hii. Nikitafakari mambo mbalimbali. Nikichoka naenda zangu kulala.nlishachukua chumba. Waswahili hapo wakichukua chumba ni mpaka wawe na msichana. Si lazima.
Kumbe juzi niliyemtumia hela sio wewe ilikua kama $36,000
 
Ni wivu tu, unaonekana kuwa na chuki kwa jamaa na wivu. Hivi kuna mtu anaandika mambo ya kipumbavu ya kitoto kama wewe humu JF? Bill Lugano is very bright na wengi tuna mpenda. Hana ugomvi na mtu, hana matusi na mtu. Ana malezi mazuri si kama wewe ambaye ulichoandika tu hapa kinaonesha hukulelewa vyema. Bill Lugano ni the Don. Ana pesa wewe una matusi. Ana akili wewe una funza kichwani. Anafahamu mambo wewe unafahamu michambo...
Ila jf [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Gentamycine pamoja na kubadilisha ID akili imebaki ile ile...[emoji23][emoji23][emoji23] Ya kipumbavuh na wivu. Huyu Bill ndo habari ya mjini. Kwa wanaume watafutaji na wenye malezi mema. Sisi tunafuata madini aliyo nayo.... Huwa hana ugomvi na mtu. Wewe ulishadharaulika mpaka ukaamua kubadili ID ila akili ikabaki ni ile ile kisoda kichwa ndoo. Watu wameendelea kukudharau. Mwenzio mwanaume kabadili ID na taarifa katoa. Wewe sasa ..... Umebadili kimya kimya ila watu wakisoma wanaona hizi akili za kichokoraa mbona ni za gentamycine [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji119][emoji119]
 
Nawashukuru ndugu zangu Watanzania wenye Mtizamo Chanya na wapenda maendeleo. Kwa nini mimi nikisema nina pesa watu wanachukia? Wanataka niseme Sina ili ndo wafurahi? Why? Sijawahi pata muda wa kubishana na mtu kwa jambo ambalo mimi ndo nalifahamu. Kwa nini nibishane?

Nikisema mimi nina gari Range Rover 2, GMC,BMW,JEEP,MERCEDES BENZ na kuna jingine nataka ninunue mwaka huu. Wewe ukasema sina. Halafu mimi najua ninayo hayo magari inaniathiri nini? Nikisema ninayo halafu wewe ukasema sina na mimi kweli sina hilo pia linakuathiri nini wewe?

Mara ya mwisho nimebishana na mtu ilikuwa mwaka 2012 nlimwambia hakuna usafiri wa Toyota unafika thamani ya Mil 250 za Kitanzania akanambia upo. Nikamwambia nampa Mil 2 ya voucher akinionesha tu kwenye mtandao.akanionesha. basi nikampa Mil 2 na 200,000 sababu alitumia data kusearch hiyo info. Nikagundua mimi kutokujua kitu haimaanishi kuwa hakipo. Nliacha kubisha siku hiyo. Maisha ni Darasa Endelevu na kila siku tunajifunza.

So nilijifunza kila mtu ana haki ya kuamini anachoamini. Huwa sina sababu ya kuchukia. Niliwahi chukia tu siku moja Traffic aliponipiga faini sababu ya speed akaandika tsh 30,000 nikamuuliza ana uhakika ni tsh 30,000 na si 300,000 akasema ni tsh 30,000. Nikamwambia aache kuomba rushwa kijanja kwa kosa lile fain haiwezi kuwa chini ya 300,000 sitaki kumpa rushwa nataka nichangie mapato. Nikatoa 300,000 nikampa nikaondoka zangu nikimwacha aandike kosa ajuavyo yeye.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji119]
 
Tajiri asiye na makuu. Mpole na mnyenyekevu. Matajiri wengine hawataki kabisa kujiunga JF na pia kushare na vijana mawazo yao. Ila Jamaa kajitolea bado kuna watu wanamchukia.
[emoji16][emoji16]
 
Anachonifurahishaga huyu mtu,akishaandika post take hana muda wa kujibizana na mtu.
Matajiri wengi ndio tulivyo tuna Mambo mengi ya kufanya so hatuwezi kupoteza muda wetu kwaajili ya kubishana [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Hivi huyu hakukojoa kitandani kweli?
 
Nimekuwa nikipokea malalamiko sana kutoka kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki wakisema kuna watu wamekuwa wakiomba Funds kwa ajili ya Taasisi zao kwa kutumia jina langu la Kiduku Lilo.

Kwanza watu wangu walikuwa wanashangaa kuwa nini kimetokea mpaka naomba nichangiwe Usd 50,000 eti za kusaidia watu wenye uelewa hafifu na wenye mtindio wa kiuchumi. Maskini.

Jamaa zangu wengi na mashirika wamekuwa wakituma hizo pesa bila kuuliza. Lakini kuna jamaa yangu alinipigia simu leo akiwa Norway na kuuliza vipi hali yako kiuchumi mpaka unafikia kuomba utumiwe USD 25,000 Umekumbwa na nini? Ndo nikaona isiwe Shida. Kwa sasa Ntatambulika kama Bill Lugano. Hapo nimetumia jina moja la kibantu ambalo nilipewa kama kutunza asili ya Ubantu.

Huwa nawaambia mzazi wangu mmoja ana asili ya Tanzania. Mwingine ni Foreigner. So hapo walinipa majina moja la kizungu la Bill na lingine la Kibantu Lugano.

Karibuni sana wadau. Nipo hapa Hyatt Hotel napunga upepo tu weekend hii. Nikitafakari mambo mbalimbali. Nikichoka naenda zangu kulala, nilishachukua chumba. Waswahili hapo wakichukua chumba ni mpaka wawe na msichana. Si lazima.
Kiduku Lilo katika sura nyingine
 
Back
Top Bottom