If you want long lasting relationship, usiguse simu ya mpenzi wako

hhaahha aisifiye mvua?......
 
Unajua matokeo huwa hayana maumivu sana
 
Kuna siku niligusa cm ya demu wangu duuuhh alikuwa mkali na alinuna cku nzima eti ananiuliza kwanini unagusa cm yangu kwani tumekubaliana hivyo?nikakaa kimya nilipo mchunguza nikagundua anavibwana ila nilimuweka sawa na sasa tuko pouwaa.
 
Kuna siku niligusa cm ya demu wangu duuuhh alikuwa mkali na alinuna cku nzima eti ananiuliza kwanini unagusa cm yangu kwani tumekubaliana hivyo?nikakaa kimya nilipo mchunguza nikagundua anavibwana ila nilimuweka sawa na sasa tuko pouwaa.

Kwa hiyo alishagawa uroda kwa hivyo vibwana vyake na wewe ukamsamehe mkasonga mbele na mapenzi yenu na sasa hivi kila kitu mswano?
 
Mimi ndio maana nina formula yangu ambayo so far sijapata wa kunibishia
Kuficha simu=Cheating

Hakuna explanation yoyote ya msingi. Ukiona mwenza wako anaficha simu jua tu mko kwenye open relationship. Watu wanazungumzia privacy kwa nini privacy iwe kwenye simu tu na usiseme wife tuwe tunalala vyumba tofauti kwa ajili ya privacy; ni simu tu?

Eti wengine wanakuja na weak points kama "simu imesajiliwa jina la nani?' Eh ni vingapi tumesajili majina yaso yetu na tunashare. Na kabla ya mambo ya kusajili simu?

Wewe sema tu wife/ honey usishike simu yangu nina vimeo;
kuwa muwazi.
Kwa hiyo alishagawa uroda kwa hivyo vibwana vyake na wewe ukamsamehe mkasonga mbele na mapenzi yenu na sasa hivi kila kitu mswano?
 
Mimi ndio maana nina formula yangu ambayo so far sijapata wa kunibishia
Kuficha simu=Cheating

Hakuna explanation yoyote. Ukiona mwenza wako anaficha simu jua tu mko kwenye open relationship

Uko sawa kabisa Nyumba Kubwa! Mtu kwa nini uifiche simu kwa mpenzi wako halafu uchi unamwachia auone? Uchi na simu kipi kilicho cha faragha zaidi?

Hapo jibu ni dhahiri kabisa. Kama mtu huna cha kuficha kwenye simu yako basi hautakuwa na wasiwasi wowote ule endapo mwenzako ataiangalia. Zaidi ya hapo kama utakuwa unaing'ang'ania na kusema eti simu yako ni yako na sijui nini nini kingine lazima kutakuwa na ulakini.

Asiye na cha kuficha hataificha!
 
Mie napenda sana kushika simu ya mume but najizuia coz sipendi nijiumize roho, nikishika lazima nitakuwa na maswali mengi kwa kila msg ,itamkosesha raha hata kama hakuna kitu kibaya maswali lazima nitauliza tu mengi,siitaki hii presha naacha tu simu akae nayo mwenyewe
 
Hii theory kuwa "simu ni private property" iko pioneered na wanaume. Afu nasikitika kuna wanawake/wasichana wana support hii theory wakati in most cases ni victims. Kuna ka mfumo dume kwenye hii theory. Mwanaume gani utamwambia upuuzi wa usishike simu yangu akubali. Ni sisi wanawake ndio tunajifanya watu wa kuelewa sana.
 


Si unaona Gaga hapo juu anasema eti hataki kujiumiza 'roho' (moyo). Hapo mi ndo sielewi kabisa kwa sababu kama mwenzako hafanyi chochote kibaya maumivu ya moyo yatatoka wapi?

Kwa maneno mengine attitude kama hiyo ya Gaga ni inaruhusu mwenzake kufanya chochote ili mradi yeye asijue tu kwa sababu akijua ataumia 'roho' (moyo)!
 
Mi na wewe tuko pamoja kabisa [sijui kwanini ckukuoa mimi!] kuepusha migogoro isiyo maana just avoid upekuzi sana
 
nyumba kubwa na nyani ngabu mmesema maneno ya msingi sana thanks ukiona mtu anafanya hayo ana agenda zisizo rasmi period tusilete maneno ya kujustfy uovu wetu maana mwisho wa siku haulipi.
<br />
<br />
 
mwanaharakati
 
Sina uharakati wowote lakini habari ndio hiyo. Kama unasema simu inasababisha kuvunja relationship nadhani hata wewe unakubaliana na mimi. Kwani simu ina nyundo ya kuvunja uhusiano. Tusisingizie simu ni kukosa uaminifu ndio kunakovunja uhusiano na si simu. Simu inakukamatisha tu. Yaani niguse simu tu ndoa ivunjike?

mwanaharakati
 
Mfano mzuri nilikuwa nashika simu ya hubby wangu kila anapoishia usingizini na kusoma sms zote na sometimes kuzijibu na kuwatukana wote waliotuma sms zisizoeleweka.Niligombana na watu hata wasiohusika huku wezi wenyewe wakiwa ni wajanja na hawatumi sms,enzi zile ambako hatukuwa tukisajili ndio walikuwa wanatuma sms itakayokurusha roho kwan wanajua utawaka na hutampata mtu.Ila baada ya kuamua kuacha kushika simu yake miaka minne sasa nina amani kubwa ajabu.
 
Kweli kabisa, kuchunguza chunguza huku unajipa presha.
 
Hahahaaaaa uchi acha auone but simu yake siitaki wala sitaki kuangalia simu yake, kwanza jiulize unaangalia ina maana una wasiwasi nae mara kwa mara
 
Ni ukosefu wa heshima kushikashika simu na kuchunguza wakati mwingine unapaniki kumbe hata hakuna kitu chochote, kuna dada alimtukana mwanamke kumbe mkwewe katumia simu ingine embu ona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…