Ifahamu Sifongo iliotiwa Siki aliyopewa Yesu akiwa Msalabani

Duuh kumbe ilikuwa sumu? Ngoja namm niongeze kufanya utafiti zaidi wa hili
 
Ndiyo.
 
Tafsiri ya neno sifongo uliyoandika hapa si sahihi kwani sifongo si sumu wala kimiminika...

Sifongo ni kitu laini kama mayavuyavu chenye tundutundu na kinachofyonza vitu viowevu kama vile maji au mafuta au ambacho hutumika sana kusugulia mwili wakati wa kuoga.

Mathalani linaweza kuwa dodoki ama sponji ama tambara laini
 
Basi mimi miaka yote Nadhani "sifongo" ni kinywaji cha kuburudisha kutoa kiu! Kumbe ni simu! Nilishasikia kuwa Nyingo ya mamba ni simu hatari na mfupa wa nyoka ukichoma hata kama nyoka alikufa kitambo sana bado una madhara makubwa kwa binadamu.
Acha matumizi ya TECNO
 
And don't patronize me kwa kuuliza ninajua hiki au kile!! We jibu tu hoja kwa hoja.

Yaliyompitia Ayubu dunia inaona kama mateso lakini yeye mwenyewe aliona ni fursa ya kutubu na kuongeza ibada!
Sasa kama huwezi kunihakikishia unajua contradiction ni nini, nawezaje kuendelea kukupa hoja zilizojikita kuonesha uongo wa hoja za kuwepo Mungu kwa contradiction?

Umeoingea kuhusu Ayubu.

Nimekuuliza swali hujajibu.

Nauliza tena.

Mungu wako alishindwa kuumba ulimwengu ambao una mafunzo bila mateso?

Hujajibu swali hili.
 
Mungu wako alishindwa kuumba ulimwengu wenye mafundisho bila mateso?
 
Mungu wako alishindwa kuumba ulimwengu wenye mafundisho bila mateso?

Ulimwengu ya mafundisho bila ya mateso pia ipo, watu wengi wanaishi maisha yao vizuri bila kujua shida - lakina kuna mambo mengine unayashika vizuri ukiyapitia mateso na changamoto. A father with an obese child might put him through a harsh regime of strict diet, rigid exercises and strict discipline. This doesn't mean that the father is punishing the child, it's more out of his concern for the welfare of the child. It's same with God, at times he takes extreme measures to bring his creation on the right track! Zote dhiki na faraja zinatoka kwa Mungu na sisi tukiwa na dhiki tunapiga magoti na kutubu na tukiwa na faraja pia tunapiga magoti na kushukuru! Kwako wewe Mungu ni sawa akileta faraja, lakini hafai akileta dhiki!

I must admit it's a total wastage of time kujadiliana na wewe!!!! Hii hoja ya kuwepo kwa Mungu imeshajadiliwa na wadau wengi humu na wengi wamekushinda. Lakini kila unapoona unatapatapa basi unaleta baseless, irrelevant arguments - eti unajua maana ya hii au kile?? Umesoma kitabu hiki? (safuher)kasome halafu njoo kujadili na mimi! Unajua square root ya mbili? (zurri) Hata sijui inaconnection gani na uwepo wa Mungu? Ya kushangaza baada ya kupigwa buti na hoja nzito za wadau, bado unajitokeza na hoja zile zile zilizochoka na zisizonamshiko. Well, you can fool some of the people some of the time, but you can't fool all the people all the time. While we can't deny you your right to express yourself but we can certainly choose to ignore you, and that's what I've decided to do!!
 
Unajibu swali ambalo sijauliza, wakati nililouliza hujajibu.

Sijauliza kama ulimwengu wa mafundisho bila mateso upo.

Pia, huo unaousema upo huna ushahidi wala uthibitisho kama upo.

Unaposema ulimwengu wa mafunzo bila mateso upo, kwa sababu watu wengi wanaishi Maisha yao vizuri bila kujua shida, hujaelewa swali langu na wala hujaelewa shida ni nini.

1. Hujaelewa swali langu ni nini, kwa sababu unafikiri kwamba, kukiwa na watu wengi wanaishi bila mateso, katika ulimwengu ambao watu wengi wanaishi bila mateso, basi una ulimwengu usio na mateso.

Hapo umekosa uelewa wa set theory, kwamba, ukiondoa mateso yote ya ulimwengu, ukambakisha mbu mmoja tu anayesababisha malaria, basi ulimwengu mzima umeingiliwa na mateso, na huwezi kusema huu ulimwengu hauna mateso.

2. Hujaelewa mateso ni nini, kwa sababu mtu yeyote ni lazima akutane na mateso katika ulimwengu.

Ataugua, atafiwa na anaowapenda, atakuwa na njaa, atashindwa kwenda anapotaka kwenda, ataonewa, atakabiliwa na mawazo kuhusu kifo, atakutana na majanga ya asili ,atatamani asichoweza kupata, atapata asichotaka kupata, atakufa.

Hakuna mtu hata mmoja atakayeepuka mateso haya ya dunia.


Kwangu hata ukisema habari za peponi ni hadithi tu. Na wewe hujathibitisha vinginevyo.

Nakuuliza kuhusu ulimwengu huu tuuonao na kuujua wote.

Mungu wako alishindwa kuuumba ulimwengu huu uwe na mafunzo bila mateso?

Yani unamfananisha Mungu na baba anayehitaji kumshurutisha mwanawe vikali ili mtoto aepuke unene uliozidi kiasi?

Unaelewa huyu baba hana control kuhusu ulimwengu, na Mungu unayemsema ana control zote kuhusu ulimwengu?

Unaelewa huyu baba ana excuse ya kusema ninemuamrisha mwanangu afunge kwa sababu nampenda, namtaka afunge ili apunguze uzito.Sina control juu ya process ya kupunguza unene zaidi ya za kiutu. Mtoto atasikia njaa, lakini kusikia njaa kutamsaidia kupunguza uzito. Sina jinsi ya kumfanya apunguze uzito bila kusikia njaa.

Unaelewa Mungu muweza yote hapo anaweza kumfanya mtu apungue uzito bila kufunga, indeed angeweza kuumba ulimwengu ambao uzito uliopita kiasi hauwezekani kabisa kuwepo?

Sasa kama Mungu aliweza kuumba ulimwengu ambao haiwezekani mtu kuwa na uzito uliozidi kiasi, kwa nini hajaumba hivyo na kaumba vinginevyo mpaka anashurutisha waja wake kufunga ili tu wapungue uzito?

Mungu wako alishindwa kuuumba ulimwengu huu uwe wa mafunzo bila mateso?
 
Mungu mwenye sifa ya upendo wote hawezi kuwa na kiburi.

Kinuri na upendo haviwezi kukaa pamoja, hizi ni sifa zinazoji contradict.

Mungu wako ni wa kutungwa, na amefanywa kuwa egotistic.

Kiburi ni weakness, si sifa ya uungu. Si sifa ya intelligence.

Jibu lako linaonesha huyo Mungu katungwa na watu wanaooenda kiburi.

Hayupo katika uhalisia.
 
Wahubiri dini kwa sasa wana kazi ngumu sana. Maana watu wanatoka kwenye imani na kutaka fact. Ile hali ya kupokea kila wanachoambia inakwenda kuisha, maana watu wanahoji kila kitu.

Na huu utandawazi, wallah kazi wanayo haswa ndugu zetu katoliki.
 
Yesu wenu ni dhaifu sanaaaaa
Aliweza kufufua wafu alishindwaje kungoa vimisumari viwilii..akaamza kulia..

Hivi wafia dini haya maswali mbona hampendi kujiiuliza..?!
 
Unaweza kuweka aya yenyewe hapa tuisome tuone kama Allah hakusema kwamba atawafanya mioyo yao iwe migumu na kuwaziba masikio na macho yao?

Tuwekee wewe ili usije ukakataa baadae,kisha upewe tafsiri ya aya husika.
 
Mkuu umechanganya desa kidogo. Katika kiswahili Sifongo ni aina ya kitu kinachonyonya kimiminika kinaweza kuwa kama dodoki au godoro. Siki ni aina ya asidi ambayo yaweza kuwa sumu au la. Kwa kawaida siki ni chachu hivyo ukiiweka kwenye vidonda huleta maumivu. Inavyoonekana walikusudia kumsababishia maumivu kwani wakati huo Yesu alikuwa na vidonda sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo mdomoni. Ilibidi watumie kitu kama dodoki/godoro(sifongo) sababu wasingeweza kumnywesha kwa kikombe pale juu msalabani.Jaribu siku moja ukiwa na vidonda mdomoni chukua ndimu ule!
Kwamba siki ile ilikuwa sumu sijaona sehemu iliyofafanua hivyo.
 
MTOA MADA UMEDANGANYA KWA HERUFI KUBWA KABISA

SIFONGO
Kwa luga rahisi Sifongo ni kitu kinachoweza kufyonza maji kama sponji vile ama taulo chochote kinachoweza kufyonza unyevunyevu au kimiminika huitwa sifongo ila kiwe kimewekwa maalum kwa kazi hiyo maana hata tambala la deki lina tabia hiyo ila haliwezi kuitwa Sifongo

SIKI
Kwa lugha rahisi naweza sema ni kimiminika kinachotengenezwa kwa ajili kuongeza ladha katika chakula hutengenezwa kwa kutumia matunda kama ndimu limao nk ama kwa kutumia nazi
Huchachuliwa kwanza kama haina uchachu
Siki inaweza kutumika kama dawa pia kwa kuwekwa katika vidonda nk


Hizo ndio maana sahihi za Sifongo Na Siki Labda mwingine anaweza kuongeza zaidi ila mtoa mada umeongea uongo kabisaaa
 
Dah...ndo maana mungu anasisitiza kwa kusema NIJUENI VIZURI(sifa zangu) THEN NDO MNIABUDU.
Kiranga mungu sio THANOS au supermen.
Kiburi + upendo + contradict vyote kaumba yeye
Nnamaana situation yoyote ya vitu vyovyote kufanya contradiction ama kujicontradict katengeneza ama kaumba yeye..
Ubongo wa Binaadamu huawezi kuhandle kiburi na upendo ila kwa mungu inawezekana.
Kwa sababu yeye ndo muumba wa vitu vyote na Hali zote
 
Yohane 19:23-37
Yohane 19:23-37 BHN
Askari walipokwisha msulubisha Yesu, walizichukua nguo zake, wakazigawa mafungu manne, fungu moja kwa kila askari. Walichukua pia na kanzu yake; kanzu hiyo ilikuwa imefumwa kwa kipande kimoja tu, bila mshono. Basi, hao askari wakashauriana: “Tusiipasue, ila tuipigie kura itakuwa ya nani.” Jambo hilo lilifanyika ili yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: “Waligawana mavazi yangu, na nguo yangu wakaipigia kura.” Basi, ndivyo walivyofanya hao askari. Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene. Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake, “Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao.” Halafu akamwambia yule mwanafunzi, “Tazama, huyo ndiye mama yako.” Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake. Kisha, Yesu aliona kwamba yote yalikuwa yametimia; na, ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia, akasema, “Naona kiu.” Hapo palikuwa na bakuli limejaa siki. Basi, wakachovya sifongo katika hiyo siki, wakaitia juu ya ufito wa husopo, wakamwekea mdomoni. Yesu alipokwisha pokea hiyo siki, akasema, “Yametimia!” Kisha akainamisha kichwa, akatoa roho. Ilikuwa Ijumaa, siku ya Maandalio. Kwa hiyo, kusudi miili isikae msalabani siku ya Sabato, maana siku hiyo ya Sabato ilikuwa siku kubwa, Wayahudi walimwomba Pilato miguu ya hao waliosulubiwa ivunjwe na miili yao iondolewe. Basi, askari walikwenda, wakaivunja miguu ya yule mtu wa kwanza na yule wa pili ambao walikuwa wamesulubiwa pamoja na Yesu. Lakini walipomfikia Yesu, waliona kwamba alikwisha kufa, kwa hivyo hawakumvunja miguu. Lakini askari mmoja alimtoboa ubavuni kwa mkuki, na mara ikatoka damu na maji. ( Naye aliyeona tukio hilo ameshuhudia ili nanyi mpate kuamini. Na hayo aliyosema ni ukweli, tena yeye anajua kwamba anasema ukweli). Jambo hilo lilitendwa ili Maandiko Matakatifu yatimie: “Hapana hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.” Tena Maandiko mengine yanasema: “Watamtazama yule waliyemtoboa.”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…