IGP kwenye suala la Lissu chutama, umatusononesha sana Watanzania kwa kumshambulia mhanga kwa maneno badala ya kutafuta wahalifu

IGP kwenye suala la Lissu chutama, umatusononesha sana Watanzania kwa kumshambulia mhanga kwa maneno badala ya kutafuta wahalifu

Hata sisi tunaotumia vidonge vya ukimwi yupo tunaishi japo vidonge vyenyewe tunasaidiwa.
Hata vilema wanahaki kutumia vyoo wanavyotumia wenye maungo sawasawa kama hakuna msaada ya mahitaji ya mlemavu.
Tunaishi huku tunaongeza damu kwa kipindi ila hutanijua kama mlemavu wa damu chafu.
Tunatembea huku figo zilishafeli.
Tunatembea huku tumefungiwa betri yakusukuma moyo.
Tunatembea kwakuwa Mungu hajataka tuwe wake.
Mwambieni arudi Tanzania Jiwe keshakufa na aache uwongo. We endeleaaa kumeza njugu zako tu.
 
Ndugu IGP Sirro

Nimesikiliza mahojiano yako uliyofanya na mwanahabari mmoja hapa nchini ,katika mahojiano yako umeonyesha bila chembe ya shaka kuwa hauna interest ya kufuatilia, kuchunguza na hatimaye kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu walitenda tendo baya na la kinyama kabisa la kutaka kutoa roho ya Ndugu Tundu Antipass Lissu. Ndugu IGP umetusikitisha sana kwa sababu hizi zifuatazo:

1. Mosi, Unamshutumu Mhanga badala ya wewe kudeal na Wahalifu waliotekeleza jaribio la mauaji:
Ndugu Sirro, nimekusikia maneno yako uliyotoa kwenye kile chombo cha habari, umesema kuwa Lissu ni mkaidi, ukasema eti hakutoa ushirikiano wowote katika kipindi cha kampeni ulipomuita ili umhoji kuhusiana na tukio la shambulio lake. Ndugu Sirro nataka nikukumbushe tu kuwa hata wakaidi wanaowajibu wa kutii sheria bila shuruti. Sasa naomba uueleze umma huu wa Watanzania kwa kuwa Lissu alikataa kutoa ushirikiano katika kuhojiwa Je mlimchukulia sheria gani?, Maana kosa alilotendewa Lissu ambalo ni jaribio la mauaji ni kosa dhidi ya Jamhuri na siyo kosa la madai kumhusu Lissu binafsi. Kwa kweli ndugu Sirro, sababu uliyoitoa ya Jeshi la polisi kutofanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa ndugu Lissu ni sababu nyepesi sana inayotufanya tuanze kuwa na mashaka na jeshi la Polisi, Je Jeshi lako lina kitu gani cha kuficha katika shambulio lile?, Je wewe binafsi una kitu gani cha kuficha katika shambulio. Tueleze sisi wananchi tujue, maana nyie ndo mna dhamana ya ulinzi wa mali na raia. Majibu yako yanaacha wasiwasi mwingi sana

2. Hoja yako kuwa Lissu hajawahi kuripoti popote juu ya kushambuliwa kwake ina walakini:
Ndugu Sirro, usitake kutwambia kuwa kila Jinai ya wazi lazima aliyetendewa jinai ndo akaripoti. Ndugu Sirro, Lissu alikaa kwenye coma zaidi ya wiki moja na amekaa hospitali takriban mwaka mzima, na mpaka leo hii anaendelea bado na operesheni za kujitibia (imebaki moja), Ndugu Sirro je Jeshi la Polisi lilikuwa linangoja mhanga apone ndo muanze uchunguzi?, Je mhanga angekufa maana yake ni kwamba na uchunguzi wa tendo la jinai ndo ungeishia palepale?.
Ndugu Sirro kwa nini Jeshi la polisi halijafungua jalada la upelelezi wa suala hilo, Je shahidi wa hilo tukio ni mmoja tu yaani yeye?, kwa nini hamjamuita dereva wake popte alipo kumhoji, na kama ni suspect kwa nini hamkutumia Interpol kumtafuta ili kumhoji?, Mbona hamjahoji majirani, hata wabunge waliokuwa na mheshimiwa Lissu siku hiyo mbona hamkuwaita kuchukua maelezo yao?, Sirro tueleze wewe na Jeshi la Polisi mnajua nini na mnaficha nini?

3. Sirro haukutimiza ahadi yako, uliwaahidi wanasiasa waliokimbia nchi warudi utawapa ulinzi sasa umebadilika:
Mara baada ya uchaguzi mkuu, ulitoka kwenye vyombo vya habari ukiwaambia wanasiasa waliokimbia nchi kufuatia sintofahamu za baada ya uchaguzi kuwa warejee nchini utawapa ulinzi maalum, lakini juzi wakati ukiongea na mwandishi wa habari ulibadili kauli, ukasema hakuna cha ulinzi maalum na kwamba hao wanasiasa ni kama watanzania wengine tu, ukasema kuwa hata watanzania wengine huwa wanashambuliwa na majambazi n.k. Ndugu Sirro, Je unafahamu mtu aliyesurvive risasi 16 atakuwa na hali gani katika kuhofia usalama wake hasa ukizingatia kuwa alitamka mara nyingi kuwa anafuatiliwa na watu kabla ya shambulio lake lakini Jeshi la polisi liliamua kukaa kimya tu?- Je Ndugu Sirro unataka kutwambia kuwa haimo katika utendaji wa jeshi la polisi kufanyia kazi vitisho, na kauli zenye viashiria vya jinai kutendeka mpaka mtu aripoti polisi?, kama ni hivyo basi jeshi hilo chini yako litakuwa jeshi la ajabu sana!. Kwa hiyo leo kiongozi wa serikali akisema kuwa kuna kitisho dhidi yake hamtofanya lolote mpaka akaripoti polisi?-Sasa inakuwaje mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaita press conference kueleza kufuatiliwa na watu wasiojulikana na kuhofia maisha yake lakini jeshi la polisi lipolipo tu?- Tuambie Sirro, Jeshi lako linajua nini katika hili sakata?

4. Jinai haifi, wananchi tunataka tujue kwa nini Jeshi la polisi halifanyi uchunguzi juu ya tukio la jaribio la mauaji la ndugu Lissu:
Ndugu Sirro, maelezo uliyotoa kwenye vyombo vya habari juu ya hatua ya jeshi la polisi kutofanya lolote juu ya jaribio la mauaji ya ndugu Lissu ni maelezo mepesi sana, hayajasheheni sababu kuntu za kipolisi, za kiupelelezi na kwa kweli za kisheria. Sasa tunataka tujue ni lini jeshi la polisi litafungua jalada la upelelezi wa tukio la kumpiga risasi ndugu Lissu?, tunataka kuona wito wa kisheria wa kipolisi wa kuita mashahidi ili tuone kweli uchunguzi umefanyika, wahalifu wanafikishwa katika mkono wa sheria na haki inatendeka. Tunapotaka hivi hatumaanishi kuwa matukio yaliyowakumba wengine yasifanywe, lakini uchunguzi wa tukio fulani hauzuii uchunguzi wa tukio jingine. Ndugu IGP tunaomba majibu

5. Mwisho kabisa ndugu IGP naomba ufahamu yafuatayo:
Sisi watanzania tuliumizwa sana na tukio la kinyama alilofanyiwa mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, tulilia naye, tulimuombea Kwa Mwenyezi Mungu amponye. Ukatili ule uliofanywa juu yake wa kumpiga risasi zote zile utadhani watu walitaka kuua Chatu ni ukatili usio na mithili. Kila nikiufikiria ukatili roho yangu inagumia. Sisi Watanzania tuna haki ya kujua akina nani walihusika ili mkono wa sheria uwe juu yao. Ndugu Sirro unavyopiga chenga au kujivutavuta katika kufanya uchuhunguzi wa hili suala, na kadri unavyoongea kwa nguvu nyingi kulifunika ndivyo nasi tunakuwa tukufikiria vibaya sana. Tafadhali usistaafu huku damu ya Lissu iliyomwagika bila hatia pale Dodoma ikiwa inakulilia kudai haki yake. Wewe hapo ulipo unaweza kuamua uchunguzi wa hili suala ufanyike ili tujue umetimiza wajibu wako, na ukishindwa unawe mikono kama Pilato tujue. Ndugu Sirro, Watanzania tuna interest ya kujua juu ya jinai ile kwa sababu inahusu maslahi ya viongozi wetu tunaowachagua, kama mkiwaachia wahalifu kwenda free basi watarudia tena hayo matendo huko mbeleni, ndiyo maana sisi watanzania tunataka mfanye uchunguzi, wahalifu wajulikane na sheria ichukue mkondo wako!

IGP SIRRO KABLA HUJASTAAFU TANATAKA KUONA UKITENDA HAKI KATIKA DHULMA HII MBAYA KABISA ILIYOWAHI KULIKUMBA TAIFA LETU
Nakubaliana na wewe.
Simon Sirro anatakiwa achutame sana, na wala asijidanganye kuwa CCM itatawala milele.
Wakati Tundu Lissu anapigwa risasi nyingi nyingi, Kamera ya CCTV nyumbani kwa Waziri Kalemani ilikuwepo na tunaambiwa iling'olewa kesho yake.
Sirro anasemaje kuhusu hilo?
Waandishi wa Habari wetu Tanzania nao wanalo tatizo kubwa la kujitayarisha kufanya mahojiano.
Mwandishi alitakiwa aliulize hili ili tusikie Sirro anavyojiuma ulimi.
 
Naomba uongeze hii kwa hisani;
6.IGP Sirro katika mahojiano yale alisema kwa kujiamini kwamba Lissu anatumia madhira yaliyompata kujinufaisha. Swali kwake atueleze ni kwa vipi binadamu anaweza kujilengesha apigwe risasi zaidi ya 10 mwilini ili apate "political mileage" kama alivyoiita inayomwezesha kupata misaada na kinga kwa wazungu?
Hii kauli ni kauli ya ajabu sana, very insensitive, illogical na imebeba ukatili wa hali ya juu
 
Acha mawazo
Kufa kwaja na Mama yako anaanza Julia now
acha mawazo utapata magonjwa makubwa yasiyo na tiba alafu tulia uwandike kinacho eleweka kwani kuna kitu umekalia kinakutekenya
 
Kwa nn humlaumu Lisu abaye aliitwa na IGP kwa ajili ya mahojiano juu ya tukio lake lkn yeye kwa maksudi akapuuza??!!!
IGP alitumia busara zaidi sio kwamba alishindwa kutumia nguvu kumlazimisha Lisu, lkn aliona isiwe tabu, siku Lisu mwenyewe akijisikia atatoa ushirikiano.
ifike mahali tufahamu pia kuwa hata IGP ni binaaadamu kama ulivyo wewe, anaweza kukasirika pindi utakapo muonyesha dharau, hakuna anaye penda kudharauliwa.
Sasa unamuonyesha dharau IGP halafu tena unamtaka achunguze tukio lako, ahh!! jamani!!! hata aibu hatuna?!
hata mm ukinidharau nakupuuzia tu.
Lisu na Dereva wake ni wahanga wa tukio la kushambuliwa hivyo baada ya kunusurika na baada ya kuitwa mara kadhaa na IGP walipaswa watii wito na kutoa ushirikiano na sio vinginevyo.
Hata wewe leo hii ukiibiwa lazima utoe ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kufanikisha mambo mengine ya kisheria.
Lisu ni shahidi namba moja na dereva wake ni shahidi namba mbili, ni watu muhimu sana ktk kufanikisha upelelezi, hata mm huwa najiuliza kwa nn Lisu na dereva wake walikataa kwenda polisi kutoa maelezo?
 
1. Mosi, Unamshutumu Mhanga badala ya wewe kudeal na Wahalifu waliotekeleza jaribio la mauaji:
Ndugu Sirro, nimekusikia maneno yako uliyotoa kwenye kile chombo cha habari, umesema kuwa Lissu ni mkaidi, ukasema eti hakutoa ushirikiano wowote katika kipindi cha kampeni ulipomuita ili umhoji kuhusiana na tukio la shambulio lake. Ndugu Sirro nataka nikukumbushe tu kuwa hata wakaidi wanaowajibu wa kutii sheria bila shuruti. Sasa naomba uueleze umma huu wa Watanzania kwa kuwa Lissu alikataa kutoa ushirikiano katika kuhojiwa Je mlimchukulia sheria gani?, Maana kosa alilotendewa Lissu ambalo ni jaribio la mauaji ni kosa dhidi ya Jamhuri na siyo kosa la madai kumhusu Lissu binafsi. Kwa kweli ndugu Sirro, sababu uliyoitoa ya Jeshi la polisi kutofanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa ndugu Lissu ni sababu nyepesi sana inayotufanya tuanze kuwa na mashaka na jeshi la Polisi, Je Jeshi lako lina kitu gani cha kuficha katika shambulio lile?, Je wewe binafsi una kitu gani cha kuficha katika shambulio. Tueleze sisi wananchi tujue, maana nyie ndo mna dhamana ya ulinzi wa mali na raia. Majibu yako yanaacha wasiwasi mwingi sana
mtu alikataa kutoa ushirikiano halafu akatoroka ulitaka asaidiweje yaani suala lake anatakiwa atoe maelezo ili polisi wachukue hatua yeye kakimbia haleti ushirikiano asaidiweje ni unafiki tu huo
 
mtu alikataa kutoa ushirikiano halafu akatoroka ulitaka asaidiweje yaani suala lake anatakiwa atoe maelezo ili polisi wachukue hatua yeye kakimbia haleti ushirikiano asaidiweje ni unafiki tu huo

Isaidiwe Jamhuri, kosa la jinai ni kosa dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!
 
Kwahiyo we unatakaje?

Alafu tabia ya kipumbavu ya kusema sisi watanzania tuliumia sana unakosea ina manisha umenijumuisha na mimi.Ukwel ni kuwa sikuumia kabisa angekufa tu.Jiseme nafsi yako.
Kuna mtu alikifa badaya yake.
Vipi hapo
 
Ndugu IGP Sirro

Nimesikiliza mahojiano yako uliyofanya na mwanahabari mmoja hapa nchini ,katika mahojiano yako umeonyesha bila chembe ya shaka kuwa hauna interest ya kufuatilia, kuchunguza na hatimaye kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu walitenda tendo baya na la kinyama kabisa la kutaka kutoa roho ya Ndugu Tundu Antipass Lissu. Ndugu IGP umetusikitisha sana kwa sababu hizi zifuatazo:

1. Mosi, Unamshutumu Mhanga badala ya wewe kudeal na Wahalifu waliotekeleza jaribio la mauaji:
Ndugu Sirro, nimekusikia maneno yako uliyotoa kwenye kile chombo cha habari, umesema kuwa Lissu ni mkaidi, ukasema eti hakutoa ushirikiano wowote katika kipindi cha kampeni ulipomuita ili umhoji kuhusiana na tukio la shambulio lake. Ndugu Sirro nataka nikukumbushe tu kuwa hata wakaidi wanaowajibu wa kutii sheria bila shuruti. Sasa naomba uueleze umma huu wa Watanzania kwa kuwa Lissu alikataa kutoa ushirikiano katika kuhojiwa Je mlimchukulia sheria gani?, Maana kosa alilotendewa Lissu ambalo ni jaribio la mauaji ni kosa dhidi ya Jamhuri na siyo kosa la madai kumhusu Lissu binafsi. Kwa kweli ndugu Sirro, sababu uliyoitoa ya Jeshi la polisi kutofanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa ndugu Lissu ni sababu nyepesi sana inayotufanya tuanze kuwa na mashaka na jeshi la Polisi, Je Jeshi lako lina kitu gani cha kuficha katika shambulio lile?, Je wewe binafsi una kitu gani cha kuficha katika shambulio. Tueleze sisi wananchi tujue, maana nyie ndo mna dhamana ya ulinzi wa mali na raia. Majibu yako yanaacha wasiwasi mwingi sana

2. Hoja yako kuwa Lissu hajawahi kuripoti popote juu ya kushambuliwa kwake ina walakini:
Ndugu Sirro, usitake kutwambia kuwa kila Jinai ya wazi lazima aliyetendewa jinai ndo akaripoti. Ndugu Sirro, Lissu alikaa kwenye coma zaidi ya wiki moja na amekaa hospitali takriban mwaka mzima, na mpaka leo hii anaendelea bado na operesheni za kujitibia (imebaki moja), Ndugu Sirro je Jeshi la Polisi lilikuwa linangoja mhanga apone ndo muanze uchunguzi?, Je mhanga angekufa maana yake ni kwamba na uchunguzi wa tendo la jinai ndo ungeishia palepale?.
Ndugu Sirro kwa nini Jeshi la polisi halijafungua jalada la upelelezi wa suala hilo, Je shahidi wa hilo tukio ni mmoja tu yaani yeye?, kwa nini hamjamuita dereva wake popte alipo kumhoji, na kama ni suspect kwa nini hamkutumia Interpol kumtafuta ili kumhoji?, Mbona hamjahoji majirani, hata wabunge waliokuwa na mheshimiwa Lissu siku hiyo mbona hamkuwaita kuchukua maelezo yao?, Sirro tueleze wewe na Jeshi la Polisi mnajua nini na mnaficha nini?

3. Sirro haukutimiza ahadi yako, uliwaahidi wanasiasa waliokimbia nchi warudi utawapa ulinzi sasa umebadilika:
Mara baada ya uchaguzi mkuu, ulitoka kwenye vyombo vya habari ukiwaambia wanasiasa waliokimbia nchi kufuatia sintofahamu za baada ya uchaguzi kuwa warejee nchini utawapa ulinzi maalum, lakini juzi wakati ukiongea na mwandishi wa habari ulibadili kauli, ukasema hakuna cha ulinzi maalum na kwamba hao wanasiasa ni kama watanzania wengine tu, ukasema kuwa hata watanzania wengine huwa wanashambuliwa na majambazi n.k. Ndugu Sirro, Je unafahamu mtu aliyesurvive risasi 16 atakuwa na hali gani katika kuhofia usalama wake hasa ukizingatia kuwa alitamka mara nyingi kuwa anafuatiliwa na watu kabla ya shambulio lake lakini Jeshi la polisi liliamua kukaa kimya tu?- Je Ndugu Sirro unataka kutwambia kuwa haimo katika utendaji wa jeshi la polisi kufanyia kazi vitisho, na kauli zenye viashiria vya jinai kutendeka mpaka mtu aripoti polisi?, kama ni hivyo basi jeshi hilo chini yako litakuwa jeshi la ajabu sana!. Kwa hiyo leo kiongozi wa serikali akisema kuwa kuna kitisho dhidi yake hamtofanya lolote mpaka akaripoti polisi?-Sasa inakuwaje mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaita press conference kueleza kufuatiliwa na watu wasiojulikana na kuhofia maisha yake lakini jeshi la polisi lipolipo tu?- Tuambie Sirro, Jeshi lako linajua nini katika hili sakata?

4. Jinai haifi, wananchi tunataka tujue kwa nini Jeshi la polisi halifanyi uchunguzi juu ya tukio la jaribio la mauaji la ndugu Lissu:
Ndugu Sirro, maelezo uliyotoa kwenye vyombo vya habari juu ya hatua ya jeshi la polisi kutofanya lolote juu ya jaribio la mauaji ya ndugu Lissu ni maelezo mepesi sana, hayajasheheni sababu kuntu za kipolisi, za kiupelelezi na kwa kweli za kisheria. Sasa tunataka tujue ni lini jeshi la polisi litafungua jalada la upelelezi wa tukio la kumpiga risasi ndugu Lissu?, tunataka kuona wito wa kisheria wa kipolisi wa kuita mashahidi ili tuone kweli uchunguzi umefanyika, wahalifu wanafikishwa katika mkono wa sheria na haki inatendeka. Tunapotaka hivi hatumaanishi kuwa matukio yaliyowakumba wengine yasifanywe, lakini uchunguzi wa tukio fulani hauzuii uchunguzi wa tukio jingine. Ndugu IGP tunaomba majibu

5. Mwisho kabisa ndugu IGP naomba ufahamu yafuatayo:
Sisi watanzania tuliumizwa sana na tukio la kinyama alilofanyiwa mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, tulilia naye, tulimuombea Kwa Mwenyezi Mungu amponye. Ukatili ule uliofanywa juu yake wa kumpiga risasi zote zile utadhani watu walitaka kuua Chatu ni ukatili usio na mithili. Kila nikiufikiria ukatili roho yangu inagumia. Sisi Watanzania tuna haki ya kujua akina nani walihusika ili mkono wa sheria uwe juu yao. Ndugu Sirro unavyopiga chenga au kujivutavuta katika kufanya uchuhunguzi wa hili suala, na kadri unavyoongea kwa nguvu nyingi kulifunika ndivyo nasi tunakuwa tukufikiria vibaya sana. Tafadhali usistaafu huku damu ya Lissu iliyomwagika bila hatia pale Dodoma ikiwa inakulilia kudai haki yake. Wewe hapo ulipo unaweza kuamua uchunguzi wa hili suala ufanyike ili tujue umetimiza wajibu wako, na ukishindwa unawe mikono kama Pilato tujue. Ndugu Sirro, Watanzania tuna interest ya kujua juu ya jinai ile kwa sababu inahusu maslahi ya viongozi wetu tunaowachagua, kama mkiwaachia wahalifu kwenda free basi watarudia tena hayo matendo huko mbeleni, ndiyo maana sisi watanzania tunataka mfanye uchunguzi, wahalifu wajulikane na sheria ichukue mkondo wako!

IGP SIRRO KABLA HUJASTAAFU TANATAKA KUONA UKITENDA HAKI KATIKA DHULMA HII MBAYA KABISA ILIYOWAHI KULIKUMBA TAIFA LETU
Yeye na makonda ndio walimpiga Lisu shaba.
Mnategemea aseme nini
 
Kwa nn humlaumu Lisu abaye aliitwa na IGP kwa ajili ya mahojiano juu ya tukio lake lkn yeye kwa maksudi akapuuza??!!!
IGP alitumia busara zaidi sio kwamba alishindwa kutumia nguvu kumlazimisha Lisu, lkn aliona isiwe tabu, siku Lisu mwenyewe akijisikia atatoa ushirikiano.
ifike mahali tufahamu pia kuwa hata IGP ni binaaadamu kama ulivyo wewe, anaweza kukasirika pindi utakapo muonyesha dharau, hakuna anaye penda kudharauliwa.
Sasa unamuonyesha dharau IGP halafu tena unamtaka achunguze tukio lako, ahh!! jamani!!! hata aibu hatuna?!
hata mm ukinidharau nakupuuzia tu.
Lisu na Dereva wake ni wahanga wa tukio la kushambuliwa hivyo baada ya kunusurika na baada ya kuitwa mara kadhaa na IGP walipaswa watii wito na kutoa ushirikiano na sio vinginevyo.
Hata wewe leo hii ukiibiwa lazima utoe ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kufanikisha mambo mengine ya kisheria.
Lisu ni shahidi namba moja na dereva wake ni shahidi namba mbili, ni watu muhimu sana ktk kufanikisha upelelezi, hata mm huwa najiuliza kwa nn Lisu na dereva wake walikataa kwenda polisi kutoa maelezo?
Kwani Lissu hakuripoti kwa afande Mroto Dodoma ?! Ni siku aliofuatilia maendeleo ya kesi, hiyo na gari lake . Mroto akasema hawana cha kusema na kama ni gari asubiri kwanza lifanyiwe maandalizi !!. Sasa ulitaka aripoti mara ngapi ?! Ikiwa pale ndiko alikoshambuliwa !!
 
Kwani Lissu hakuripoti kwa afande Mroto Dodoma ?! Ni siku aliofuatilia maendeleo ya kesi, hiyo na gari lake . Mroto akasema hawana cha kusema na kama ni gari asubiri kwanza lifanyiwe maandalizi !!. Sasa ulitaka aripoti mara ngapi ?! Ikiwa pale ndiko alikoshambuliwa !!
Well said.

Kama Lissu kavunja sheria kwa kutoripoti zipo njia za kisheria za kudeal naye kwa kosa hilo, lakini hii haiondoi wajibu wa jeshi la Polisi kuchunguza jinai ile ya Risasi 16 kutaka kuutoa uhai wake!.
 
Siro, kwa reaction yako uliyoionesha juzi, any reasonable man, conclusion atakayofikia Ni kuwa kuna irresistible inference kuwa ulihusika katika Jambo hili la kumpiga Lisu risasi in one way or another.
Halafu ukijua hivyo?
 
Naomba uongeze hii kwa hisani;
6.IGP Sirro katika mahojiano yale alisema kwa kujiamini kwamba Lissu anatumia madhira yaliyompata kujinufaisha. Swali kwake atueleze ni kwa vipi binadamu anaweza kujilengesha apigwe risasi zaidi ya 10 mwilini ili apate "political mileage" kama alivyoiita inayomwezesha kupata misaada na kinga kwa wazungu?
Binadamu anaweza mengi hasa kuumiza mguu ambao upo upande wa dereva na kuacha mguu ulio upande wa dirisha! Pia kuhakikisha risasi haipigi kichwa au other vital organs. Ndio hivyo, na pia kupeleka dereva nje asiweze kutoa ushahidi. Hivi wewe hayo hikuyafikilia!
 
Kwahiyo we unatakaje?

Alafu tabia ya kipumbavu ya kusema sisi watanzania tuliumia sana unakosea ina manisha umenijumuisha na mimi.Ukwel ni kuwa sikuumia kabisa angekufa tu.Jiseme nafsi yako.

-gmfoq8.jpg
 
Ww sio mtanzania
Kwahiyo we unatakaje?

Alafu tabia ya kipumbavu ya kusema sisi watanzania tuliumia sana unakosea ina manisha umenijumuisha na mimi.Ukwel ni kuwa sikuumia kabisa angekufa tu.Jiseme nafsi yako.
 
Back
Top Bottom